Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Suluhu ya msongamano wa magari jijini Dar

    Report Post
    Page 2 of 18 FirstFirst 123412 ... LastLast
    Results 21 to 40 of 354
    1. #1
      Morani75's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st March 2007
      Location : Duniani
      Posts : 662
      Rep Power : 761
      Likes Received
      9
      Likes Given
      0

      Default Suluhu ya msongamano wa magari jijini Dar

      Wana JamiiForums wenzangu...

      Hii habari ninayoiweka ni kutoka kwenye gazeti la Guardian, 09/07/2007. Kwa kweli UCLAS wamekuja na mpango mzuri. Lakini kwa wale ambao wapo kwenye vyombo kama ERB, UDSM, DIT na vyuo vingine kwa pamoja na serikali na sekta binafsi ikiwemo Polisi, Ujenzi, TANROADS, Conslutants, SUMATRA, MUWADA etc wachangie mawazo. Wenzetu wa UCLAS kama mpo jumuisheni wadau wengine ili mpango wenu uwe maridhawa na utoe suluhu ya tatizo hili la usafiri.

      Wazee wa vyuo vikuu, jamani wanafunzi wakati wanafanya projects kwa nini wasipewe mwamsho wa kuweza chunguza na kutoa mapendekezo yao kuhusu suala hili...tayari UCLAS wameshatupa "skeleton" what we need now ni "flesh and blood". Congrats UCLAS but don't hide the info to yourself, share and improve it to cater for the need......

      The article is as below:

      UCLAS: Here is the major solution for Dar congestion

      2007-07-09 09:49:32
      By Pascal Shao



      The University College of Lands and Architectural Studies (UCLAS) has come with a cost effective and permanent solution on road traffic jams in Dar es Salaam.

      UCLAS Assistant Research Fellow, Hussein Rajab, told The Guardian that should the government take into account the said solution, traffic congestion in the city of Dar es Salaam would become history.

      He said: ``Most traffic congestions arise at the junctions. The only answer to traffic jams is to improve the intersections where vehicles converge. Improvement here means construction of either flyovers (overpass) or underpass lanes.

      ``Overpass or underpass is a permanent solution as vehicles will not meet at the junctions as the situation appears at the moment,`` he said.

      He said the lanes would facilitate movement of vehicles heading to final destinations without meeting at the junctions (where there are traffic lights).

      Rajab said the solution would be suitable for small vehicles rather than daladalas due to stoppages and heavy vehicles, as 80 percent of traffic to city centre is made up of small vehicles.

      He said that overpasses could be applicable at the junctions of Mwenge, Morocco, Ubungo, Tabata, Shekilango to mention a few, while the underpasses could be built at the slopes of Kawe Road, St Peter road junction etc.

      ``Construction of an overpass or underpass is a one time investment,`` he said.

      Rajab said expansion or adding more roads would not reduce traffic jams but would instead facilitate vehicles to meet at the junctions.

      He said that traveling on congested roads resulted in increased fuel consumption.

      He mentioned effects of traffic congestion as time wastage, environmental pollution, tear and wear and stress. He further mentioned other effects as difficulties in case of emergencies, noise as motorists try to divert to other quiet areas such as hospitals and schools.

      Dar es Salaam has been experiencing traffic jams, which normally occur during peak hours in the mornings and evenings, as most traffic is heading to and from the city centre due to most offices being located there.

      SOURCE: Guardian

      Hali ilivyo kwa Dar as at March, 2010:


      Ali Hassan Mwinyi road


      Morogoro road near Magomeni Mapipa


      Old Bagamoyo road near Shopper's plaza


    2. FemaTV & Radio

    3. #21
      Kibunango's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th August 2006
      Location : Tampere
      Posts : 6,804
      Rep Power : 44130
      Likes Received
      368
      Likes Given
      1428

      Default Re: Tatizo la Msongamano wa Magari Jijini Dar es Salaam

      Quote By mwafrika wa kike
      Najua huko saudi arabia unakoishi kuna restriction sana ya watu wa aina fulani kutoa maoni yao. Karibu sana kwenye free world ya JF!
      Ingependeza kutumia siku ya leo kwa kutoa au kuchangia vitu vya maana ili kuweza kusukuma gurudumu la maendeleo hapo bongo badala ya kuwa Hadija Kopa... kumbuka kesho huna jeuri ya kuwepo hapa na mipasho yako...
      Save Water Drink Beer. "Alcohol doesn't solve any problem,
      But, if you think again, neither does milk."
      Vituko Vya Zenj

    4. #22
      Quemu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th June 2007
      Posts : 1,079
      Rep Power : 828
      Likes Received
      27
      Likes Given
      16

      Default Re: Tatizo la Msongamano wa Magari Jijini Dar es Salaam

      Fly-overs ni wazo zuri. Lakini nina mashaka kama zitawezekana Tz kutokana na magari mengi kuwa vimeo.

      Fly-overs system inabidi iende sambamba na ukaguaji wa magari mara kwa mara. Asilimia kubwa ya magari bongo hayako kwenye hali mzuri kutokana na ukosefu wa regular check-up. Kwa hiyo nina wasiwasi tutakuwa tunapata ajali nyingi zinazotokana na magari yanayoshindwa ku-accelerate kwenye slope ya hizo fly-overs. Hebu imagine jinsi vipanya na malori yatakavyokuwa yanapoteza maisha ya watu kwa ku-flip baada ya kukwama kupanda kwenye hizo fly-overs? I mean, ikiwa tunashuhudia malori kadhaa kupinduka baada ya kushindwa kupanda kale kamlima ka pale junction ya Kawe, tuweza kuhimili fly-overs kweli?

      Kwa mtazamo wangu, njia mbili sambamba tunaweza kuzitumia kupunguza msongamano wa magari:

      1)Kutanua barabara - tuongeze idadi ya lanes kwenye major roads kutoka mbili mpaka nne kila upande. Then, tuzigawe hizo lanes mara 2. Lane 2 za kulia zinakuwa za high speed lanes kwa magari madogo. Na 2 za kushoto zinakuwa za dala dala na malori. Tusisahau kuwa foleni bongo zinasababishwa na madaladala. Kwa hiyo tu kizitengea lanes zake, tutaweza kutibu suala la foleni kwa kiasi kikubwa.

      2) Tuongeze idadi ya barabara - Tuna barabara chache sana Bongo. Tukitumia mfano uliouweka wa maeneo ya Mbezi Beach, Tegeta na kuendelea, utaona kuwa kuna njia mbili tu za kutoka na kuingia Mebzi Beach -Ali Hassan Mwinyi na ile inayoanzia Avocado Kawe mpaka barabara ya White Sand Hotel (bado inajengwa). Hii idadi ni ndogo ukizingitia idadi ya watu wanaoishi maeneo haya. Tegeta peke yake ina idadi ya watu wanaotesheleza kuitwa wilaya. Anyway, mkazi wa Mbezi Beach akitaka kwenda airport inabidi aje mpaka mwenge kupata access ya kwenda airport. Inabidi tujenge barabara kama mbili au tatu zinazounganisha Mabezi Beach na Mbezi Kimara? Tena wala zisiishie hapo, at least moja au mbili ziendelee all the way mpaka Pugu Road or something. Kuna ile barabara ya kupanga kule Goba, mpaka leo ujenzi wake bado wanaupiga danadana. Au vipi ile barabara ya Wazo Hill, kwa nini wasiendeleze zaidi. Yaani imeishia pale kwende kile kiwanda tu....kuendelea mbele ni mbonde tu.

      Kwenye fly-over hiyo, iwapo gari ingetaka kwenda Msasani kutokea Mwenge, kungekuwa na sehemu (mstari) maalum ya kuliwezesha gari hilo kuingia pole pole kwa kutumia utaratibu wa kisheria unaojulikana kama "yielding". Utaratibu huo ungetumika pia kwa wale ambao wangetaka kwenda Kinondoni kutokea Mwenge, hivyo kuwezesha magari kutembea kwa kasi zaidi bila kusimama, na hivyo kufanikiwa kuondoa kabisa tatizo la msongamano wa magari.
      Tukiondoa suala la fly-overs, nakubaliana na wewe kuhusu kuweka filters kwenye junctions. Tukiongeza lanes, ninaamini hizo filters zitafanya kazi vizuri sana.

      Kwa kifupi, mimi naona barabara zetu zibaki tu chini. Tunachotakiwa ni kuongeza barabara na lanes. Pia tuzitenganishe hizo lanes baina ya magari na daladala. Tukifanya hivi tutaweza kupunguza foleni kwa kiasi kikubwa.

    5. #23
      Kilongwe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th February 2008
      Location : Optical valley-China
      Posts : 382
      Rep Power : 729
      Likes Received
      50
      Likes Given
      5

      Default Re: Tatizo la Msongamano wa Magari Jijini Dar es Salaam

      Mmi naona tatizo ni kuwa mji wetu huduma muhimu zote zimerundikana sehemu moja,kila kitu posta,sasa inafanya kuwe na msongamano kuelekea sehemu moja..so tuangalie kugawa huduma ili tuweze angalau badala ya watu kila aibihu kudamkia posta kununua samaki wabichi basi wawe wananunuliwa tazara(mfano),na baadhi ya huduma nyingine..
      Sharing knowledge occurs when people are genuinely interested in helping one another develop new capacities for action; it is about creating learning processes.

    6. #24
      Masanja's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st August 2007
      Location : Benaco
      Posts : 1,646
      Rep Power : 937
      Likes Received
      157
      Likes Given
      0

      Default Re: Tatizo la Msongamano wa Magari Jijini Dar es Salaam

      Quote By kibunango
      Tatizo ni msongamano! Je wanaJF wanaushauri gani juu ya hilo.. sasa mdada tayali umekibilia kwenye kuhukumu... hapana shaka una uwalakini kuwepo hapa JF
      Kibunango, be real bana hapa tunajadili serious issue. Hivi wewe unaijua foleni ya Dar? alichokiandika MM ndo ukweli wenyewe. Watawala wetu hawajui kwamba wamepewa dhamana ya kulinda the general good ya wote.

      Kama wanavyosema wenzangu foleni Dar siyo kero tena limekuwa ni Jambo la kitaifa! Jiulize kama kuna mgonjwa TMJ anahitaji kukimbizwa Muhimbili..si atafia njiani? Ushauri, inabidi tuboreshe PUBLIC TRANSPORT, ukifanya hivi hata wanaonunua magari watapungua (wengi wananunua si kwa kupenda bali kuepuka adha za kusimama kwenye dala dala, ambazo hata kuzipanda mpaka uwe na nguvu!).

      Tanzania we cant afford shortcut, hata fly overs sina uhakika kama zinaweza kusaidia, kwa bara bara zipi?..mnaonaje tukikarabati hizo bara bara harafu tukaongea na serious investors tukajenga trams (treni) from my experience Europe wana vibara bara vidogo lakini trams zimerahisisha usafiri. Well hatuwezi kuwa Europe leo au kesho, but hey..we have to dare tufanye kitu ambacho kitatusaidia na generations nyingine zijazo!

      At times I wonder serikali inafaidika vipi na wasomi wake..kwa nini isiwatumie maprofesa kibao wa uhandisi...wakafikiria namna ya kutatua hili tatizo? mpaka Lowassa mwenye degree ya sanaa ndo anakuja kutupa ideas za kutumia bara bara efficiently? some body somewhere must not be doing his homework.. and you all know who!
      Silaha ya maskini ni elimu.

    7. #25
      Ogah's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Posts : 5,669
      Rep Power : 21814
      Likes Received
      735
      Likes Given
      3190

      Default Re: Tatizo la Msongamano wa Magari Jijini Dar es Salaam

      Quote By Bongolander
      Ogah you are right, lakini ukiangalia kwa layman analysis utaona kuwa ajali ndogondogo zimeongezeka, congestion haijapungua, imeanza hata kuleta confusion vichwani mwa madereva, na enforcement yake ni very mechanical. Inaonekana kama ni decision iliyofanyika ili kujitafutia political gains lakini haikutafitiwa kama inaweza kuendana na mazingira ya sasa.
      1.Congestion haijapungua - this can be evaluated and report should be made public.....moja ya main issue itakayoangaliwa ni "travel times" on different sections in relation to its respective Level of Service

      2.Confusion Vichwani mwa Madereva - Hapa ni Enforcement na hasa katika utoaji wa leseni za kuendesha magari.......Dar es salaam kuna "madreva" sio madereva. katika hili serikali inahitaji mabadiliko ya HALI YA JUU na hasa ukizingatia SAFETY ni kitu cha kwanza barabarani.

      3.Enforcement yake ni mechanical - nakubaliana na wewe zote soft and mechanical ni muhimu ziende pamoja........mind you the technology is very simple and not expensive either.

      4. Decision na political gains - you may assume that........but to me technical officers always ndio wa kuwapa policy makers idea ili kufanikisha malengo ya technicalities walizokubuhu nazo....sasa kama ilikuwa ni political gains.........mmmhhh interesting!!

    8. Miaka 50

    9. #26
      Kibunango's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th August 2006
      Location : Tampere
      Posts : 6,804
      Rep Power : 44130
      Likes Received
      368
      Likes Given
      1428

      Default Re: Tatizo la Msongamano wa Magari Jijini Dar es Salaam

      Quote By Masanja
      Kibunango, be real bana hapa tunajadili serious issue. Hivi wewe unaijua foleni ya Dar? alichokiandika MM ndo ukweli wenyewe. Watawala wetu hawajui kwamba wamepewa dhamana ya kulinda the general good ya wote.

      Kama wanavyosema wenzangu foleni Dar siyo kero tena limekuwa ni Jambo la kitaifa! Jiulize kama kuna mgonjwa TMJ anahitaji kukimbizwa Muhimbili..si atafia njiani? Ushauri, inabidi tuboreshe PUBLIC TRANSPORT, ukifanya hivi hata wanaonunua magari watapungua (wengi wananunua si kwa kupenda bali kuepuka adha za kusimama kwenye dala dala, ambazo hata kuzipanda mpaka uwe na nguvu!).

      Tanzania we cant afford shortcut, hata fly overs sina uhakika kama zinaweza kusaidia, kwa bara bara zipi?..mnaonaje tukikarabati hizo bara bara harafu tukaongea na serious investors tukajenga trams (treni) from my experience Europe wana vibara bara vidogo lakini trams zimerahisisha usafiri. Well hatuwezi kuwa Europe leo au kesho, but hey..we have to dare tufanye kitu ambacho kitatusaidia na generations nyingine zijazo!

      At times I wonder serikali inafaidika vipi na wasomi wake..kwa nini isiwatumie maprofesa kibao wa uhandisi...wakafikiria namna ya kutatua hili tatizo? mpaka Lowassa mwenye degree ya sanaa ndo anakuja kutupa ideas za kutumia bara bara efficiently? some body somewhere must not be doing his homework.. and you all know who!
      Kamanda Masanja, kama una ushabiki na MWK ni juu yako lakini penye ukweli lazima aambiwe....

      Nikirudi kwenye mada umezungumzia waandisi na wasomi wengine katika kero hii ya msongamano. Lakini umeshindwa kijua ni nini tatizo la msongamano jijini.

      Ni vema kwanza kujua tatizo ambalo limeleta kadhia hii, baada ya hapo ni rahisi kujadili namna ya kuondokana na tatizo hilo.

      Kwa maoni yangu tatizo hili linachangiwa na mambo yafuayo
      • Mipango Miji kwa ujumla
      • Ongezeko la waakazi wa jiji
      • uchumi


      Katika suala la Mipango Miji, Jiji la DSM leo lina Halmashauri tatu, lakini huduma muhimu zinapatikana katika halmashauri moja tu. Hii inasababisha waakazi karibia wote kwenda katika halmashuri moja kila siku hivyo kusababisha msongamano.

      Ni vema kutawanya huduma muhimu katka halmashauri zote, hii itapunguza msongamano kwa asilimia kubwa.
      Save Water Drink Beer. "Alcohol doesn't solve any problem,
      But, if you think again, neither does milk."
      Vituko Vya Zenj

    10. #27
      Mwafrika wa Kike's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th July 2007
      Posts : 5,840
      Rep Power : 1776
      Likes Received
      13
      Likes Given
      0

      Default Re: Tatizo la Msongamano wa Magari Jijini Dar es Salaam

      Quote By kibunango
      Ingependeza kutumia siku ya leo kwa kutoa au kuchangia vitu vya maana ili kuweza kusukuma gurudumu la maendeleo hapo bongo badala ya kuwa Hadija Kopa... kumbuka kesho huna jeuri ya kuwepo hapa na mipasho yako...
      Mhhh...

      jeuri hiyo utaileta wewe?
      Well Behaved Women Never Make History

      Mwafrika wa kike is now asking President Kikwete to resign his presidency effective immediately for the sake of our nation

    11. #28
      Kibunango's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th August 2006
      Location : Tampere
      Posts : 6,804
      Rep Power : 44130
      Likes Received
      368
      Likes Given
      1428

      Thumbs down Re: Tatizo la Msongamano wa Magari Jijini Dar es Salaam

      Quote By mwafrika wa kike
      Mhhh...

      jeuri hiyo utaileta wewe?
      Ama kweli ukubwa wa pua sio wingi wa kamasi
      Save Water Drink Beer. "Alcohol doesn't solve any problem,
      But, if you think again, neither does milk."
      Vituko Vya Zenj

    12. #29
      Ufunuo wa Yohana's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th October 2007
      Posts : 327
      Rep Power : 659
      Likes Received
      1
      Likes Given
      0

      Default Re: Tatizo la Msongamano wa Magari Jijini Dar es Salaam

      Mimi ktk utafiti wangu kwa suala la msongamano dar ni kuwa hatujafikia hatua hiyo ya kujenga fly-over. Dar kuna barabara nyingi mno za mitaani zimesaulika, hazifanyiwi ukarabati. Chukua mfano wewe ulikuwa unatoka Mbezi luguluni unaenda mbezi beach kitu gani kingekupeleka Ubungo kama kungekuwa na barabara inayounganisha mbezi luguluni na mbezi beach?

      Haya chukulia mtu yuko Manzese anataka kwenda kinondoni kuna barabara nyingi sana pembeni mwa morogoro road ambazo unaweza kuzitumia ili ufike kinondoni lakini itakubidi uende mpaka mapipa maana hizo barabara ni mbovu kupita maelezo. why kila mtu anataka atumie morogoro road? Au Alhasani mwinyi? believe me hizi barabara zikitengenezwa kwa kiwango cha lami hakuna mtu atakayeng'ang'ania kupita haya mabarabara makubwa. Fikiri mtu anaenda airport kutoka kibamba lazima apite ubungo unategemea usiwepo msongamano? Ukitengeneza hizi barabara hatutakuwa na msongamano kamwe.

      Pili office zetu tuangalie namna ya kuzi-alocate isiwe kila kitu Posta na kariakoo. yafaa kuanza kubuni maeneo mengine ya kujenga maofisi na sehemu za biashara kama supermakets pembeni mwa mji.Kwa sababu sasa hivi kila mtu akiamuka asubuhi ni posta, kariakoo, mjini na jioni nyumbani hii lazima kuwe na msongamano.

    13. #30
      Kilinzibar's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 6th March 2008
      Location : high way
      Posts : 131
      Rep Power : 598
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Tatizo la Msongamano wa Magari Jijini Dar es Salaam

      Zote points ila kwa ukweli ivi jamani hata daraja la feri limetushinda miaka nenda rudi sasa huku mitaani si ndio kabisa, barabara ya uhuru ndio usiseme
      ivi na hii ya bagamoyo rd morocco mwenge sasa kuna lane 3,mbili zimewekwa alama ya kwenda town sasa kwaio ni watu wa kutoka mwenge tuu ndio watumie au na ndio kuchanganyana tu!!!!!

    14. #31
      Ngereja's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th February 2007
      Posts : 652
      Rep Power : 760
      Likes Received
      148
      Likes Given
      17

      Default Re: Tatizo la Msongamano wa Magari Jijini Dar es Salaam

      MwanaH na wakuu wengine mliotangulia..... Hili swala la msongamano wa magari jijini kwa kweli limeongelewa sana humu jamvini......
      1. Tulianzia kwenye issue ya project iliyofanywa na wale wakuu wa pale Chuo cha Ardhi, siku hizi panaitwa UCLAS, they did a marvelous job.
      Kwanza ndugu Morani75 nikusahihishe kidogo tu. UCLAS kwa sasa inaitwa Chuo Kikuu cha Ardhi (Ardhi University).

      Nikirejea kwenye mjadala, tatizo kubwa la msongamano jijini Dar es salaam linatokana na mipango duni ya miundo mbinu ya barabara. Ni bahati mbaya kwamba waliosanifu barabara za jiji nadhani hawakutilia maanani ukuaji wa jiji na ongezeko la magari.

      Sasa nini kifanyike ili kuondoa tatizo japo inahitaji uwekezaji mkubwa
      1. Barabara zote zinazoingia na kutoka jijini zote zipanuliwe na ziwe dual carriage-way, hili lina athali zake kwamba bomoaboma itakuwa nyingi.
      2. Maeneo ya makutano ya barabara kuu zijengwe multi-level roads, nina maana kusiwe na traffic light. Wahandisi watanisaidia kuweka kiswahili sawa.
      3. Barabara zaidi ziimarishwe ili kuondoa tatizo la wasafiri kutumia barabara kuu tu wanapotaka kwenda mjini, kwa mfano, kupitia Makongo juu au changanyikeni kwenda maeneo ya mbezi hadi Tegeta.
      4. Katikati ya jiji barabara zipamgwe za kuingia tu na za kutoka, nin maana (one way traffic roads)

      ...Mengine nitaendelea baadaye.

    15. #32
      Kibunango's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th August 2006
      Location : Tampere
      Posts : 6,804
      Rep Power : 44130
      Likes Received
      368
      Likes Given
      1428

      Default Re: Tatizo la Msongamano wa Magari Jijini Dar es Salaam

      • Magari mengi yaingiayo ndani ya jiji ni machakavu
      • Barabara zote ndani ya Jiji zinatosha na nzuri
      • Ufungaji wa barabara za mitaa maarufu Jijini


      Iwapo kweli tunakata kuondokana na msongamano wa magari Jijini, ni vema kuangalia ubora wa magari ambayo yanaingia Tz. Kwa wengi hii ni lawama.

      Upo umuhimu wa kufunga kabisa barabara maarufu ndani ya jiji. Barabara hizo zitumike kwa waendao kwa miguu na wapanda baiskeli tu. Hii itasaidia watu kuacha magari yao majumbani na kutumia public transport kwenda ndani ya Jiji, Kimazingira ni wazo zuri huku kiafya ni jambo la msingi.

      Barabara zote za mjini na nzuri na wala hazihitaji kupanuliwa. kinachotakiwa hapa ni kuwepo kwa kodi ya matumizi ya barabara za mijini. Hii ni zaidi na kodi ya kuegesha gari.
      Save Water Drink Beer. "Alcohol doesn't solve any problem,
      But, if you think again, neither does milk."
      Vituko Vya Zenj

    16. #33
      Mwafrika wa Kike's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th July 2007
      Posts : 5,840
      Rep Power : 1776
      Likes Received
      13
      Likes Given
      0

      Default Re: Tatizo la Msongamano wa Magari Jijini Dar es Salaam

      Quote By kibunango
      Ama kweli ukubwa wa pua sio wingi wa kamasi
      Na huu ni usemi mpya huko kwenu?
      Well Behaved Women Never Make History

      Mwafrika wa kike is now asking President Kikwete to resign his presidency effective immediately for the sake of our nation

    17. #34
      vassil's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 13th April 2008
      Posts : 121
      Rep Power : 591
      Likes Received
      13
      Likes Given
      8

      Default Re: Tatizo la Msongamano wa Magari Jijini Dar es Salaam

      ukiangalia kiwango cha uchumi wa Tanzania na infrastructure ilivyo primitive tutakuwa tunajidanganya kufikiri serikali itaweza kujenga highway interchanges dar-es-salaam wameshindwa kumaintain barabara walizojenga kwa misaada na mikopo hawana uwezo wa kutatua tatizo hilo.

      Jambo pekee lililobakia ni ni kuwataka wananchi wenye pesa za kihalali na za mafisadi tuchange na mabepari wengine wa nje ya nchi tuanzishe tollroad authority na government ikaribishwe. Badala ya Lowassa na mafisadi wenzake kuchukua pesa Tanesco kwa capacity charges wangeweza kupata fedha kihalali kutoka kwa wenye magari,maisha yatakuwa bora haraka

    18. #35
      Quemu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th June 2007
      Posts : 1,079
      Rep Power : 828
      Likes Received
      27
      Likes Given
      16

      Default Re: Tatizo la Msongamano wa Magari Jijini Dar es Salaam

      Quote By kibunango
      • Magari mengi yaingiayo ndani ya jiji ni machakavu
      • Barabara zote ndani ya Jiji zinatosha na nzuri
      • Ufungaji wa barabara za mitaa maarufu Jijini
      Are you serious unaposema barabara zetu mzuri na zinatosha?

      Ni uzuri upi huo unaoungelea?

      Barabara bongo ni chache mno. Na isitoshe hizo chache ni mbaya na ndogo. Sasa sijui mzee unazumngumzia barabara zipi? Labda ungefafanua tafadhali..

      Quote By kibunango
      Iwapo kweli tunakata kuondokana na msongamano wa magari Jijini, ni vema kuangalia ubora wa magari ambayo yanaingia Tz. Kwa wengi hii ni lawama.

      Upo umuhimu wa kufunga kabisa barabara maarufu ndani ya jiji. Barabara hizo zitumike kwa waendao kwa miguu na wapanda baiskeli tu. Hii itasaidia watu kuacha magari yao majumbani na kutumia public transport kwenda ndani ya Jiji, Kimazingira ni wazo zuri huku kiafya ni jambo la msingi.
      Nakubaliana na wewe. Kuna umuhimu wa ki-set kiwango cha ubora cha magari yanayoingia nchini. Lakini hiyo haitatosha peke yake. Bado tunahitaji kufuatilia kwa karibu ubora wa magari yaliyo tayari nchini. Magari mengi ni vimeo vya kutupwa. Kwa kweli tutajichimbia kaburi wenyewe kama hatutaweka sawa ubora wa magari kwanza kabla hatufikiria kujenga hizo fly-overs.

      Suala la kufunga barabara downtown linawezekana, na litasaidia kupunguza foleni. Pale mjini tunaweza ku-implement shuttles (buses au trains) ambazo zita control mizunguko ndani ya downtown.

      Quote By kibunango
      Barabara zote za mjini na nzuri na wala hazihitaji kupanuliwa. kinachotakiwa hapa ni kuwepo kwa kodi ya matumizi ya barabara za mijini. Hii ni zaidi na kodi ya kuegesha gari.
      Again, are you serious? Kabisa una uhakika unaposema barbara zetu haziitaji upanuzi?

      Unapozungumzia kuwepo kwa kodi ya matumizi ya barabara unamaanisha tuzigeuze barabara zetu kuwa toll-roads? Huoni kama kufanya hivyo tutajishindilia wenyewe msumari wa gharama za maisha

      Binafsi, sidhani kama tunahitaji toll sytem kwenye major roads. Nitaunga mkono wazo la toll roads kama litahusishwa kwenye ujenzi wa private roads. Vinginevyo, bado hatujafikia hatua ya kutoza watanzania toll (directly)kwenye utumizi wa barabara. Nafikiri tunalipa kodi (inderectly) ya barabara. Si hivyo?

    19. #36
      Kibunango's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th August 2006
      Location : Tampere
      Posts : 6,804
      Rep Power : 44130
      Likes Received
      368
      Likes Given
      1428

      Default Re: Tatizo la Msongamano wa Magari Jijini Dar es Salaam

      Quote By QM
      Are you serious unaposema barabara zetu mzuri na zinatosha?

      Ni uzuri upi huo unaoungelea?

      Barabara bongo ni chache mno. Na isitoshe hizo chache ni mbaya na ndogo. Sasa sijui mzee unazumngumzia barabara zipi? Labda ungefafanua tafadhali..



      Nakubaliana na wewe. Kuna umuhimu wa ki-set kiwango cha ubora cha magari yanayoingia nchini. Lakini hiyo haitatosha peke yake. Bado tunahitaji kufuatilia kwa karibu ubora wa magari yaliyo tayari nchini. Magari mengi ni vimeo vya kutupwa. Kwa kweli tutajichimbia kaburi wenyewe kama hatutaweka sawa ubora wa magari kwanza kabla hatufikiria kujenga hizo fly-overs.

      Suala la kufunga barabara downtown linawezekana, na litasaidia kupunguza foleni. Pale mjini tunaweza ku-implement shuttles (buses au trains) ambazo zita control mizunguko ndani ya downtown.



      Again, are you serious? Kabisa una uhakika unaposema barbara zetu haziitaji upanuzi?

      Unapozungumzia kuwepo kwa kodi ya matumizi ya barabara unamaanisha tuzigeuze barabara zetu kuwa toll-roads? Huoni kama kufanya hivyo tutajishindilia wenyewe msumari wa gharama za maisha

      Binafsi, sidhani kama tunahitaji toll sytem kwenye major roads. Nitaunga mkono wazo la toll roads kama litahusishwa kwenye ujenzi wa private roads. Vinginevyo, bado hatujafikia hatua ya kutoza watanzania toll (directly)kwenye utumizi wa barabara. Nafikiri tunalipa kodi (inderectly) ya barabara. Si hivyo?
      Kamanda hebu rudi nyuma na tizama tatizo la msongamano wa magari hapo DSM. Magari mengi huwa yanaelekea sehemu moja tu ya Jiji hilo ambalo lina Halmashauri tatu kubwa. Napozungumzia utawanyaji wa huduma nina maana hata zile ofisi kubwa kubwa ndani ya jiji, ambazo zina wateja lukuki.

      Kufunga barabara za ndani ya jiji ni mojawapo ya hatua muhimu katika kuondoa tatizo la msongamano. Iwapo kutakuwepo na hatua za makusudi za kufunga barabara hizo, ina maana kuwa wengi wataacha magari yao majumbani na kutumia usafiri wa daladala.

      Kama barabara za bongo zitahitaji upanauzi basi ni vema kupanua barabara kwa ajili ya daladala na teksi. Na sio kupanua barabara kwa magari ya kawaida. Iwapo upanuzi wa lane utakuwa kwa ajili ya public transport hii ina maana ya kujenga ufanisi kwa daladala hivyo kutoa ushawishi mkubwa kwa watumiao magari binafsi kupanda daladala hizo.

      Kuna baadhi ya wajumbe wamezungumzia kuhusu "fly over" ujenzi wake iwapo utashirikisha kampuni binafsi hapana ujanja zaidi ya kulipia kodi katika matumizi ya hizo fly over. Na iwapo zitzjengwa ni vema zijengwe nje ya katikatika ya Jiji na zijengwe kwa lengo la kuunganisha Halmashauri hizo tatu pasipo kupitia katikati ya jiji.
      Save Water Drink Beer. "Alcohol doesn't solve any problem,
      But, if you think again, neither does milk."
      Vituko Vya Zenj

    20. #37
      Richard's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd October 2006
      Location : LANGLEY
      Posts : 2,272
      Rep Power : 1098
      Likes Received
      490
      Likes Given
      1680

      Default Re: Tatizo la Msongamano wa Magari Jijini Dar es Salaam

      Ni wazo zuri kabisa na linahitaji msaada wa kufikishwa kunakohusika.

      Lakini mimi nadhani ni bora kuanza kutatua tatizo la mifereji ya maji machafu kwanza kabla ya kulaza barabara yoyote ile.

      Sasa serikali inatumia vipi wasomi waliopo Tanzania kushiriki kujenga nchi ndio mjadala.

      La sivyo kuna siku mvua itakuja kunyesha na mji mzima itajaa maji kwa miezi na kutokee mlipuko wa magonjwa.

      Pesa zinazoibwa zingesomesha vijana wenzetu katika nchi zilizoendelea ambako ukiondoa mafuriko katika maeneo ya mabonde, sijawahi kuona maji yamekwama mahala fulani.

      Mungu ibariki Tanzania siku moja ibadilike.
      When thinking about my risk assessment, I always remember:
      HAZARD and the RISK .

    21. #38
      Quemu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th June 2007
      Posts : 1,079
      Rep Power : 828
      Likes Received
      27
      Likes Given
      16

      Default Re: Tatizo la Msongamano wa Magari Jijini Dar es Salaam

      Quote By kibunango
      Kamanda hebu rudi nyuma na tizama tatizo la msongamano wa magari hapo DSM. Magari mengi huwa yanaelekea sehemu moja tu ya Jiji hilo ambalo lina Halmashauri tatu kubwa. Napozungumzia utawanyaji wa huduma nina maana hata zile ofisi kubwa kubwa ndani ya jiji, ambazo zina wateja lukuki.
      Kibunango,
      Mbona decentralization ya offisi imeanza siku nyingi tu! Mabenki mengi (ndio biggest employer) yanafungua matawi kila kona ya jiji. Tanesco, post office, na telecommunication companies, kama Vodacom and the like, wana watawi kila sehemu. Idadi ya watu waneolekea downtown imepungua kwa kiasi kikubwa. kuna baadhi ya watu inabidi wapitie downtown kwenda na kurudi makazi. Hii yote inasababishwa na uchache wa barabara.

      Quote By kibunango
      Kama barabara za bongo zitahitaji upanauzi basi ni vema kupanua barabara kwa ajili ya daladala na teksi. Na sio kupanua barabara kwa magari ya kawaida. Iwapo upanuzi wa lane utakuwa kwa ajili ya public transport hii ina maana ya kujenga ufanisi kwa daladala hivyo kutoa ushawishi mkubwa kwa watumiao magari binafsi kupanda daladala hizo.
      Hii ndio mimi nazungumzia. Mawazo yangu ni kwamba tuongeze lanes ili baadhi ya hizo lanes ziwe kwa ajili ya daladala na malori tu. Tena kwa ishu ya malori, inabidi yakatazwe kutumia baadhi ya barabara.

      Unajua, Bongo magari sio mengi kama tunavyodhania. Kinachofanya yaonekane mengi ni uchache wa barabara. Pindi tukiziongeza na kuzitanua, hapo ndio tutakapoweza kuona ni kiasi gani tuna magari.

      Of course, watu wanaendelea kungiza magari kwa wingi. Kwa hiyo, haitachukua muda kabla idadi ya magari haija-tripple.

    22. #39
      MwanaHaki's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th October 2006
      Posts : 1,413
      Rep Power : 1003
      Likes Received
      156
      Likes Given
      91

      Default Re: Tatizo la Msongamano wa Magari Jijini Dar es Salaam

      Quote By kibunango
      Tatizo la msongamano ndani ya jiji linaweza kupungua kwa kuongeza au kweka kodi ya kuingia jijini. Sioni ulazima wa kila mwenye gari kuingia mjini wakati anaweza kupanda daladala..
      Apande daladala zipi? Hivyo vipanya vya kina Afande Kula Kula?
      Speaking Openly, without fear!

    23. #40
      MwanaHaki's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th October 2006
      Posts : 1,413
      Rep Power : 1003
      Likes Received
      156
      Likes Given
      91

      Default Re: Tatizo la Msongamano wa Magari Jijini Dar es Salaam

      Quote By UFUNUO WA YOHANA
      Mimi ktk utafiti wangu kwa suala la msongamano dar ni kuwa hatujafikia hatua hiyo ya kujenga fly-over. Dar kuna barabara nyingi mno za mitaani zimesaulika, hazifanyiwi ukarabati. Chukua mfano wewe ulikuwa unatoka Mbezi luguluni unaenda mbezi beach kitu gani kingekupeleka Ubungo kama kungekuwa na barabara inayounganisha mbezi luguluni na mbezi beach?

      Haya chukulia mtu yuko Manzese anataka kwenda kinondoni kuna barabara nyingi sana pembeni mwa morogoro road ambazo unaweza kuzitumia ili ufike kinondoni lakini itakubidi uende mpaka mapipa maana hizo barabara ni mbovu kupita maelezo. why kila mtu anataka atumie morogoro road? Au Alhasani mwinyi? believe me hizi barabara zikitengenezwa kwa kiwango cha lami hakuna mtu atakayeng'ang'ania kupita haya mabarabara makubwa. Fikiri mtu anaenda airport kutoka kibamba lazima apite ubungo unategemea usiwepo msongamano? Ukitengeneza hizi barabara hatutakuwa na msongamano kamwe.

      Pili office zetu tuangalie namna ya kuzi-alocate isiwe kila kitu Posta na kariakoo. yafaa kuanza kubuni maeneo mengine ya kujenga maofisi na sehemu za biashara kama supermakets pembeni mwa mji.Kwa sababu sasa hivi kila mtu akiamuka asubuhi ni posta, kariakoo, mjini na jioni nyumbani hii lazima kuwe na msongamano.
      Barabara inayotoka Mbezi Beach hadi Mbezi Luguruni [sic] ipo, lakini tatizo ni kwamba haiko kwenye hali nzuri. Kipindi kifupi kilichopita barabara hiyo, ambayo inapitia Goba hadi Mbezi Luis, iliweza kupitika kwa muda wa dakika 25 hadi 30, ingawa ni kwa uangalifu mkubwa kutokana na kuwapo kwa milima na mabonde na kona kali MNO! Lakini baada ya mvua zilizonyesha na zinazoendelea kunyesha, barabara hiyo imeharibika kiasi cha kupitika kwa shida sana au kutopitika kabisa kwenye sehemu nyingi.

      Nayapenda mawazo yako... nayapenda sana!
      Speaking Openly, without fear!

    Page 2 of 18 FirstFirst 123412 ... LastLast

    LinkBacks (?)


    Similar Topics

    1. Replies: 89
      Last Post: 11th April 2013, 16:57
    2. IBM (Tanzania) kupunguza msongamano wa magari katika Barabara za DSM!
      By Baba_Enock in forum Business & Economic Forum
      Replies: 31
      Last Post: 22nd March 2012, 12:19
    3. Replies: 1
      Last Post: 30th June 2011, 12:35
    4. Replies: 4
      Last Post: 15th June 2011, 18:40
    5. Replies: 47
      Last Post: 21st April 2009, 16:11

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...