Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Ushauri wangu kwa Zuberi Zitto Kabwe

    Report Post
    Page 7 of 10 FirstFirst ... 56789 ... LastLast
    Results 121 to 140 of 188
    1. #1
      Mkandara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd March 2006
      Location : T dot
      Posts : 13,770
      Rep Power : 7662
      Likes Received
      4929
      Likes Given
      4509

      Default Ushauri wangu kwa Zuberi Zitto Kabwe

      Mimi nikiwa mmoja wa watu ambao tumeweka matumaini makubwa kwa chama cha Chadema kuleta mageuzi nchini nina ushauri mdogo sana kwa Zitto kuhusu SIASA zake na misimamo yake ambayo ndiyo sababu na chanzo cha yeye kuwa bangusilo ktk kila tukio la Upinzani..

      Mheshimiwa Zitto amekuwa akisimama sana peke yake (independent) kwa fikra kwamba anaweza kuleta mabadiliko kupitia mwamvuli wa CCM. Hutumia sana maneno ya kwamba yuko huru na anafanya kile anbachokiamini yeye kuwa ndio haki na sahihi. Kwa fikra hizo amekuwa mstari wa mbele ktk tunzi za uwekezaji nchini wakati yeye kama mwanasiasa wa Upinzani hakutakiwa kabisa kugusa jambo hilo pasipo kuwepo makubaliano na ushirikiano wa vyama (Bipartisan) ktk kufuata sera (policies) zitakazo tumika..

      Siku zote mwanasiasa na hasa mbunge wa chama cha Upinzani unatakiwa kuwa kinyume cha maamuzi ya sera za chama tawala, napengine kutumia nafasi hiyo kuweka shinikizo kwa chama tawala wakubali kufuata sera za Upinzani lakini wewe binafsi huwezi kutumikiwa na sera zile zile ambazo ndizo sababu ilokufanya wewe usimame upande wa pili, fikra hizi ni kuonyesha immaturity ktk ulingo wa siasa!

      Nakushauri sana mkuu wangu achana na siasa za CCM inapofikia maswala ya kamati yako ya bunge. Kama mbunge wa Upinznai unachotakiwa ni kutafuta makosa ktk sera zao na kuweka wazi ubadhilifu unaofanyika laa sivyo hakuna sababu ya kuwa na upinzani maana sote tunakubaliana na sera za Chama tawala. Kazi yako ni kupinga sera hizo na sio kujaribu kurekebisha utekelezaji wa miradi ndani ya sera mbovu.. Siasa haijengwi hivyo mkuu wangu.

      Huwezi kurekebisha utekelezaji wa sera za CCM kwa kutumia kiti cha upinzani -HAIWEZEKANI isipokuwa utatumiwa muda wote na kuwa the weakest link kwao kumaliza upinzani, maana kinachowezekana kutekelezeka kinatokana na sera zenyewe ambazo wewe kama Mpinzani hukubaliani nazo.

      Brother, kitumikie chama chako, simama nyuma ya sera za chama chako na pingana na sera za chama tawala kama mpinzani na sii kutekeleza sera za chama Tawala kwa fikra zile zile zilizotufikisha hapa tulipo. Mtazame mwenzako January Makamba, he is smart kisiasa na siku zote husimama nyuma ya chama chake hata kama hakubaliani na mtu ndani ya chama. Mtazame Lowassa, he is smarter hata kama hakubaliwi na watu wengi nje ya CCM lakini ameendelea kujijenga ndani ya chama kuliko nje kwa sababu huko ndiko alikozaliwa - Hutaki yote haya Unaacha!
      Exploration of reality

    2. RukaaJuu Final

    3. #121
      Mkwawa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th June 2011
      Location : Kalenga
      Posts : 613
      Rep Power : 3564
      Likes Received
      694
      Likes Given
      388

      Default Re: Ushauri wangu kwa Zuberi Zitto Kabwe

      Mkandara,
      Sioni ubishani tulikuwa tunaelimishana na kufafanualiana habari na ushauri wako kwa kijana wetu ZZK. Ni wazi kila mtu anajinsi ya ufahamu na chanzo cha habari ikumbukwe tu ZZK ni mwanasiasa wa chama maarufu. Sioni kama watu wanachuki naye bali wengi wanampenda sana na wanamategemeo naye makubwa ndio maana wana hoji na kuhoji na kuhoji.

      Naona kuna wenye nia mbaya sana na CDM kwani wanapenyeza hata ambayo hayahusiki, Kama nia ni kumshauri usikatae na mawazo ya wengine, ZZK anafahamiana na wengi na kafanya kazi na wengi kwenye hii siasa yetu.

      Ushauri wako kwa upande ni mzuri na sehemu nyingine itabidi ZZK aamue mwenyewe.

      Mkubwa Mkandara lazima wote tukubali kuwa hakuna mtu alizaliwa anapenda fedha ila maisha na mahitaji ndio yanasukuma uhitaji wa fedha , sidhani kama kuna mtu anayependa kuwa masikini na sitaki kumwona mtu wa hivyo. Huwezi kuwa na uhakika na rushwa na kupenda fedha kwa mtu ila mtu mwenyewe.

      Wote tunaamini (imani) kwamba kijana ni safi ila sidhani kama ni sahihi kuchukua nafasi yake kumtetea mimi nikiwa kama mwana CDM na rafiki wa ZZK ningependa yeye mwenyewe ajitete kuliko kuwa kama CCM ambao huwa wanateteana hata kwenye ukweli. Kama ZZK ni msafi hakuna la kuogopa wala hakuna sababu ya kuogopa wanaojadili.

      CDM lazima ijengwe kwenye misingi ya uwazi na ukweli na ninamsifia ZZK kuweka wazi kwamba yeye yuko tayari kuchunguzwa na yeyote.

      Swala la makundi ndani ya CDM nafikiri ni fikra na baadhi ya watu kutaka kuwavuruga na kutengeneza makundi kwa hisia , ni kweli kuna wenye misimamo tofauti lakini sitegemei CDM viongozi wafikiri sawa hakuna zidumu fikra huku, kuna uwanja huru wa maoni na fikra.

      Misuguano hakuna mahala ambapo haipo ila bado haijawa tatizo ndani ya chama.
      Mkandara likes this.
      Nilijitoa mhanga kwa watu wangu; watoeni watawala wadhalimu na mafisadi kwa ustawi wa nchi yetu.

    4. #122
      Mkandara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd March 2006
      Location : T dot
      Posts : 13,770
      Rep Power : 7662
      Likes Received
      4929
      Likes Given
      4509

      Default Re: Ushauri wangu kwa Zuberi Zitto Kabwe

      Nicholas, For the last time nakwambia hivi soma tena mada yangu hakuna mahala nimezungumzia TUHUMA isipokuwa hali halisi ambayo Zitto anaifanya kusimamia sera za CCM pale anapoona anaweza kuleta mabadiliko through sera mbovu. Na nimeshauri ajipange na team yake kupinga sera mbovu za CCM badala ya kufikiria he can make them change what they stand for!..

      Maelezo hayo juu hayana kabisa TUHUMA za watu ama magazeti kwa sababu vitu vyote unavyomlaumu wewe ni tuhuma zinazo endeshwa na watu wasiompenda na wewe mmoja wapo maana huna facts. Nimekuuliza vizuri tu toka lini mtu anayetuhumiwa ndiye anatakiwa kujieleza ili kufuta tuhuma hizo wakati kisha sema sihusiki ktk vyombo vya habari. Mnasema anapenda rushwa nimesema sio kweli, naye kajibu hivyo hivyo lakini bado hamtaki kuamini..Well kama huna mafaili yake unakataa kitu gani sasa? It's my guess u have facts kuhusu Zitto na rushwa na tamaa mnayozungumzia!.

      Now, to declare ana nia ya kugombea Urais, sio kosa na nimekuuliza kosa gani?..hukujibu isipokuwa unarukia yale uyatakayo..japokuwa nina hakika akisema Dr.Slaa wakati wowote ule utamuunga mkono na wengine wote wanaomchambua Zitto kwa kauli ile kwa sababu mmezoea Usiri wa CCM kupitia CC na mafia yake. Labda niseme pia kutotangaza nia yake ya kugombea tena Urais inaweza kuwa ni makosa vile vile maana kuweka nia inawajenga wanachama nyuma yake badala ya hizi kelele mnazopiga humu. WE need a leader ktk harakati zozote zile, na ifahamike wazi nani anatuongoza ktk mapambano haya ili awe kioo chetu.. Kukosekana kwa kiongozi ndio maana kila mtu analoloma anavyotaka..

      Again unataka kuzungumzia scandals za Zitto anzisha mada yako nitakuja huko lakini hii inahusu mchango wake kwa chama katika kuzitangaza, kuzitetea na kuzinadi SERA za Chadema, na atashirikiana na CCM tu pale CCM na CDM wamekubaliana ushirika kwa muafaka wa kisera ktk utekelezaji wa mikakati ya maendeleo. Haya yote ni katika Ujenzi wa taifa kwa kutumia sera za chama chake kukosoa mabaya ya CCM badala ya kujitenga kutafuta Umaarufu.

      Kwa nini nimezungumzia KUTENGANA, ni kwa sababu kutengana kuna jumuisha pande mbili sisizo kubaliana. IT TAKES TWO TO TANGO, laa sivyo ingekuwa upande mmoja unanyenyekea. Na ukinisoma vizuri pale nilipoweka mafaili nimesema wazi kwamba jaribio lile lilishindikana kukisambaratisha chama isipokuwa kuharibu mahusiano kati ya Zitto na Mbowe. Nasema haya kwa sababu najua kilichofanyika na najua kwa kirefu Zitto ana habari zipi na Mbowe ana habari zipi na nimesema hizi zote zilipikwa kuhakikisha wana kigawanisha chama. They never showed up to deny this fact. WEWE pamoja na kuwepo CDM - HUJUI kitu na hujui minuso ndio maana unashindwa kuelewa mambo yanayokwenda chini ya ardhi.

      - Nimemaliza - HUTAKI UNAACHA!
      Last edited by Mkandara; 7th August 2012 at 07:17.
      Exploration of reality

    5. #123
      timbilimu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd September 2010
      Location : DSM
      Posts : 2,672
      Rep Power : 977
      Likes Received
      584
      Likes Given
      10

      Default Re: Ushauri wangu kwa Zuberi Zitto Kabwe

      Mengi yamesemwa hapa,natumaini imekua shule tosha kwa Zitto,wanasiasa vijana na kwa uongozi wa CDM. Umoja ni Nguvu na Utengano ni Udhaifu.
      Mkandara likes this.

    6. #124
      Ally Kanah's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th June 2011
      Posts : 780
      Rep Power : 559
      Likes Received
      37
      Likes Given
      35

      Default

      Quote By Mkandara
      Nicholas, For the last time nakwambia hivi soma tena mada yangu hakuna mahala nimezungumzia TUHUMA isipokuwa hali halisi ambayo Zitto anaifanya kusimamia sera za CCM pale anapoona anaweza kuleta mabadiliko through sera mbovu. Na nimeshauri ajipange na team yake kupinga sera mbovu za CCM badala ya kufikiria he can make them change what they stand for!..

      Maelezo hayo juu hayana kabisa TUHUMA za watu ama magazeti kwa sababu vitu vyote unavyomlaumu wewe ni tuhuma zinazo endeshwa na watu wasiompenda na wewe mmoja wapo maana huna facts. Nimekuuliza vizuri tu toka lini mtu anayetuhumiwa ndiye anatakiwa kujieleza ili kufuta tuhuma hizo wakati kisha sema sihusiki ktk vyombo vya habari. Mnasema anapenda rushwa nimesema sio kweli, naye kajibu hivyo hivyo lakini bado hamtaki kuamini..Well kama huna mafaili yake unakataa kitu gani sasa? It's my guess u have facts kuhusu Zitto na rushwa na tamaa mnayozungumzia!.

      Now, to declare ana nia ya kugombea Urais, sio kosa na nimekuuliza kosa gani?..hukujibu isipokuwa unarukia yale uyatakayo..japokuwa nina hakika akisema Dr.Slaa wakati wowote ule utamuunga mkono na wengine wote wanaomchambua Zitto kwa kauli ile kwa sababu mmezoea Usiri wa CCM kupitia CC na mafia yake. Labda niseme pia kutotangaza nia yake ya kugombea tena Urais inaweza kuwa ni makosa vile vile maana kuweka nia inawajenga wanachama nyuma yake badala ya hizi kelele mnazopiga humu. WE need a leader ktk harakati zozote zile, na ifahamike wazi nani anatuongoza ktk mapambano haya ili awe kioo chetu.. Kukosekana kwa kiongozi ndio maana kila mtu analoloma anavyotaka..

      Again unataka kuzungumzia scandals za Zitto anzisha mada yako nitakuja huko lakini hii inahusu mchango wake kwa chama katika kuzitangaza, kuzitetea na kuzinadi SERA za Chadema, na atashirikiana na CCM tu pale CCM na CDM wamekubaliana ushirika kwa muafaka wa kisera ktk utekelezaji wa mikakati ya maendeleo. Haya yote ni katika Ujenzi wa taifa kwa kutumia sera za chama chake kukosoa mabaya ya CCM badala ya kujitenga kutafuta Umaarufu.

      Kwa nini nimezungumzia KUTENGANA, ni kwa sababu kutengana kuna jumuisha pande mbili sisizo kubaliana. IT TAKES TWO TO TANGO, laa sivyo ingekuwa upande mmoja unanyenyekea. Na ukinisoma vizuri pale nilipoweka mafaili nimesema wazi kwamba jaribio lile lilishindikana kukisambaratisha chama isipokuwa kuharibu mahusiano kati ya Zitto na Mbowe. Nasema haya kwa sababu najua kilichofanyika na najua kwa kirefu Zitto ana habari zipi na Mbowe ana habari zipi na nimesema hizi zote zilipikwa kuhakikisha wana kigawanisha chama. They never showed up to deny this fact. WEWE pamoja na kuwepo CDM - HUJUI kitu na hujui minuso ndio maana unashindwa kuelewa mambo yanayokwenda chini ya ardhi.

      - Nimemaliza - HUTAKI UNAACHA!
      Basi wewe chukua hiii


      http://www.youtube.com/watch?v=pI_3S...e_gdata_player

    7. #125
      Avanti's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th August 2010
      Posts : 696
      Rep Power : 583
      Likes Received
      103
      Likes Given
      260

      Default Ni kweli imekuwa "SINA BEI" mwaka huu!

      Katika wabunge vijana niliokuwa nawavulia kofia ni pamoja na Mheshimiwa Zitto Kabwe, tunakumbuka jinsi awamu yake ya kwanza ya ubunge alivyokuwa akijenga hoja vizuri na hadi kuna wakati alifikia kusimamishwa ubunge kwa ajili ya ujasiri wa kusimamia msimamo wake. Lakini kwa sasa tumeona wabunge vijana wengi, wamekuja juu na tayari wanamfunika Zitto Kabwe. Najua Zitto Kabwe ameweza kufanya mambo mazuri na kuonesha mfano kuwa vijana wanaweza katika kuongozo lakini nakiri na ningependa sio Zitto tu, na wapenzi wake wengine wakiri kuwa Zitto kiasi amepwaya katika siasa mwaka huu. Mwaka huu nimeshuhudia Zitto akipotoka kwa baadhi ya mambo mfano:

      1. Wakati akisoma maoni ya upinzani kuhusu bajeti ya Serikali aliharibu na ndiyo maana alitoa nafasi kwa Gamba Mwigulu kuichana chana bajeti mbadala ya upinzani. Hapa hata yeye alikiri kufanya makosa.
      2. Alikurupuka kutaka kuingilia sakata la TANESCO ambalo tayari lilishaanza kufanyiwa kazi na mamlaka ingine, hii pia alijitetea sana na kuonekana kubadilika msimamo na hadi kutishia kwamba yeye yupo tayari kuachia ngazi ili ainusuru Kamati yake. Ikumbukwe kuwa wakati akisema watafanya uchunguzi alikuwa kama anaona TANESCO wanaonewa, baadaye akageuka eti hakuwa na maana hiyo.
      3. Amekuwa akituhumu kuna watu wanataka nafasi zake, ya Uenyekiti wa Kamati, Usaidizi Kuongoza Kambi ya Upinzania bungeni, na kuzengea ugombeaji wa Uraisi mwaka 2015.
      4. Amekuwa anatishia na kutaka kuogopwa, kumbuka hapa pia anatuhumiwa kumwandikia ujumbe wa simu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini kwamba yeye "hana bei".
      5. Ameshindwa kueleweka katika maelezo yake ya hivi karibuni alipojaribu kuelezea sakata la yeye kutajwa kufagiliwa njia ya uraisi 2015 pale ilipoandikwaa magazetini, n.k, kutokana na tamasha la wasanii lililofanyika Kigoma.
      6. N.K.

      And the list goes on and on....

      My advice: Zitto ajiangalie upya kwani inawezekana ndiyo anasererekea bondeni.
      Last edited by Avanti; 9th August 2012 at 11:46.

    8. Miaka 50

    9. #126
      Edson's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th March 2009
      Posts : 7,308
      Rep Power : 0
      Likes Received
      1799
      Likes Given
      433

      Default Re: Ni kweli imekuwa "SINA BEI" mwaka huu!

      lengo lako hasa ni nini?
      I'm Naturaly Evasive..

    10. #127
      Avanti's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th August 2010
      Posts : 696
      Rep Power : 583
      Likes Received
      103
      Likes Given
      260

      Default Re: Ni kweli imekuwa "SINA BEI" mwaka huu!

      Quote By Edson
      lengo lako hasa ni nini?
      Umeona? ni kujaribu kumrudisha Zitto kwenye form!

    11. #128
      andrews's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 28th March 2012
      Posts : 1,683
      Rep Power : 0
      Likes Received
      142
      Likes Given
      76

      Default Zito rudi CCM usiichafue CDM

      zito nakushauri urudi ccm na ukagombee ubunge kwa kupitia huko au vyama nipya vilivyoanzishwa na ccm kwa ajili ya kuikabili chadema ambavyo ni chauma ,adc na vingine wanavyovijua wao. nasema hayo sababu nyingi lakini nitasema chache.

      1.wakati viongozi wa juu wote wa chadema wanapambana kwa kutumia m4c zito haujaonekana hata kwenye mkutano mmoja ikiwa kama ni kutotaka kutamka maneno ya kuwaudhi waliokutuma kuichafua chadema.

      2.zito unapopeleka hoja yoyote bungeni inakuwa ya kujijenga binafsi na si kwa maslahi ya wanyonge wengi na wabunge wa upinzani hususani chama chako na hii ni pamoja na kutokutoka nje ya ukumbi wa bunge pale chadema wanapofanya hivyo kwa maslahi ya chama chao.

      3.umejisifu sana kuwa wewe ni muadilifu na unao uwezo wa kuwa rais wa nchi 2015 kwa hili umekosea maana njia uliyoitumia ni mbovu sana maana kuna vikao vya chama ambavyo ungevitumia kueleza hoja yako lakini kwa kutumia waandishi wa habari na bunge na vijana wako wa kigoma halitakusaidia kufika huko maana nyuma yake inaoonekana kuna baraka za bwana mkubwa ili muivuruge chadema.

      4.taarifa zisizo rasmi zinaonyesha urafiki wako wa karibu na jakaya na ridhiwani ni mashaka makubwa sana maana hakuna sehemu yoyote ambayo umemlaumu rais wa nchi kwa udhaifu wake bali amekutumia kumdhalilisha waziri mkuu kwa maslahi ya ikulu na si kwa upinzani unaposema serikali haiko makini bado unaficha kumtaja jakaya moja kwa moja sababu ya agenda zenu za siri ambazo wana ccm na wanachadema wengi wameliona.

      Umeingizwa kwenye orodha ya wala rushwa wabunge kwa makusudi tu kuichafua chadema na si vinginevyo na hili unalijua vizuri.sidhani kama kupitia chadema utafanikiwa ndoto zako maana chadema wako makini ndio maana hakuna kiongozi wa juu wa chama aliyejibu hoja zako za kuutaka uraisi kiurahisi ushauri wangu kwako utangaze adharani kujiunga kwako na kundi la shibuda nakutakia safari njema.m4c daima.

      Incredible likes this.

    12. #129
      Adharusi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd January 2012
      Location : Mtwara
      Posts : 504
      Rep Power : 470
      Likes Received
      66
      Likes Given
      295

      Default re: Zito rudi CCM usiichafue CDM

      Huyuu jamaa ni mbinafsi

    13. #130
      Wizzo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th November 2010
      Location : Arusha
      Posts : 432
      Rep Power : 516
      Likes Received
      79
      Likes Given
      34

      Default re: Zito rudi CCM usiichafue CDM

      pointi ya nne inalojiki...

    14. #131
      andrews's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 28th March 2012
      Posts : 1,683
      Rep Power : 0
      Likes Received
      142
      Likes Given
      76

      Default re: Zito rudi CCM usiichafue CDM

      amuulize waridi kabouru ccm ilimtumia lakini sasa imemtupa kigamboni asijidanganye hata siku moja nguvu aliyopata ni kutokana na ubora wa chadema ila akitaka kuondoka atuchie chadema yetu halafu aende ccm au cuf safari njema zito

    15. #132
      SAMRICH1's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th July 2011
      Posts : 1,236
      Rep Power : 643
      Likes Received
      206
      Likes Given
      129

      Default re: Zito rudi CCM usiichafue CDM

      pointi ya nne ni nzuri sana

    16. #133
      majebere's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd April 2012
      Posts : 2,210
      Rep Power : 0
      Likes Received
      322
      Likes Given
      111

      Default re: Zito rudi CCM usiichafue CDM

      Vijana acheni kutumika kwa hela ya mboga,mnakaa tumwa humu JF kila kukicha kumpaka matope zitto. Huu mzimu wa urais utawamaliza CDM.

    17. #134
      andrews's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 28th March 2012
      Posts : 1,683
      Rep Power : 0
      Likes Received
      142
      Likes Given
      76

      Default re: Zito rudi CCM usiichafue CDM

      mbona ccm mnamuogoga lowasa na huo ni mzimu wa urais au ufisadi nieleze vizuri

    18. #135
      ZeMarcopolo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th May 2008
      Posts : 7,194
      Rep Power : 5038
      Likes Received
      2435
      Likes Given
      2226

      Default re: Zito rudi CCM usiichafue CDM

      Arudi kwani kashawahi kuwa CCM?
      Watu wa CDM naona kama mnaanza kutengeneza chama ndani ya chama...
      "To greed, all nature is insufficient"

    19. #136
      andrews's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 28th March 2012
      Posts : 1,683
      Rep Power : 0
      Likes Received
      142
      Likes Given
      76

      Default re: Zito rudi CCM usiichafue CDM

      ananunuliwa kama akina mrema na wenzake

    20. #137
      KALYOVATIPI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th August 2011
      Posts : 1,184
      Rep Power : 591
      Likes Received
      136
      Likes Given
      0

      Default re: Zito rudi CCM usiichafue CDM

      Sitaki kuamini kama zzk unapakwa matope na wana cdm. hawa ni wafuasi wa nape kaka cdm bado tunakupenda na kila mwanachama wa cdm ana haki ya kuwa mwakilishi wa chama mahala popote pale bila ya kuingiliwa ilimradi asiende kinyume na katiba za chama

    21. #138
      andrews's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 28th March 2012
      Posts : 1,683
      Rep Power : 0
      Likes Received
      142
      Likes Given
      76

      Default re: Zito rudi CCM usiichafue CDM

      zito ana kiburi kwa kufikiri wale bongoflavour wake watampeleka ikulu unahitaji baraka za chama sio za kikwete

    22. #139
      Malunkwi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th January 2011
      Location : Dar es salaam
      Posts : 260
      Rep Power : 475
      Likes Received
      44
      Likes Given
      16

      Default Re: Zito rudi CCM usiichafue CDM

      Zito hakuwahi kuwa mwanachama wa ccm, hivyo kusema arudi ccm si sahihi ni bora ungesema ahamie ccm,
      Sisi sote ni watanzania hivyo kutofautiana ki-itikadi hakutenganishi utanzania wetu, si dhambi kuwa na urafiki na mtu eti kisa hamko chama kimoja.
      Zito bado ni Mwanasiasa safi na makini pale Chadema.

    23. #140
      JF-MBUNGE's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st May 2012
      Posts : 361
      Rep Power : 428
      Likes Received
      125
      Likes Given
      199

      Default Re: Zito rudi CCM usiichafue CDM

      Hata sie CCM wazalendo hatumtaki akihamia CCM sie tunaendaaa CDM....kijana kama huyu ndio anawakilisha vijana wa kisanii kwenye siasa za sasa kupitia mingongo ya vijana, uzalendo, na wandishi vijana wa mjini mjiniii.

    Page 7 of 10 FirstFirst ... 56789 ... LastLast

    User Tag List

    Tags for this Topic

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...