Na hata ukimsikia ktk majibu yake mengi hutumia maneno haya ya kujiamini yeye pekee kwa kila anachokifanya ama maamuzi anayochukua, kumbe Kisiasa ni makosa makubwa sana, na hasa kwa nchi za Kiafrika unajimaliza kisiasa. Ni sawa na mwanamke/mwanamme alokuwa kwenye ndoa anaamua kufanya atakavyo kwa sababu he/she think of their personal rights of being independent..Unapokuwa katika ndoa kuna mambo lazima uyaache na kuna marafiki inabidi uwaache. Huchaguliwi marafiki lakini unashauriwa kuwa makini single friends wanaokuvuta kwenda Nyumbani Lounge bila mwenza..
Hii ndio logic behind, kumnasua Zitto ktk kiza lakini hakuna ukweli wowote kwamba Zitto ni mla rushwa. tena naweza sema kuwa na mashaka na watu wengine ndani ya Chadema kuliko Zitto japokuwa kwa Bongo yetu sidhani kama kuna mtu hata mmoja ni MSAFI niseme SAINT - Hakuna, alikuwa Nyerer naye kisha kutoka.. Jamani tusidanganyane, hali ya maisha na mfumo uliopo leo hii TZ huwezi kumpasa mtu msafi kabisa kabisaaa ambaye akaingia uongozi au Ubunge kwa usafi na anategemea atabakia mbunge kwa usafi wake wakati nchi nzima ipo ndani ya bomba la majitaka (sewerage system)... Inawezekana kweli?..mimi nina mashaka..sasa haya ya kumsingizia Zitoo mla rushwa wakati sii kweli na anajaribu kuwafahamisha hamtaki kujua yeye afanyeje? mnataka Zitto avue nguo zake kuwaonyesha ukichaa ndio muweke imani naye...Tena amini maneno yangu ningekuwa Zitto ningwambia ile Hotel Dodoma yangu, Nina majumba Dar Kigoma na kwingineko, leteni ushahidi zimetokana na rushwa..
Katika haya ya RUSHWA ni lazima mfahamu ya kwamba CCM wanataka WanaChadema muendelee kumchukia ZItto, utengano wetu utaanzia kwake na sijui kama umenielewa uliposoma Utangulizi wa kichwa cha mada..Kama Chadema itamfukuza Zitto ama kuendelea kumsodolea kidole, itafika mahala aidha yeye kujitoa ama Chadema kumfukuza na nakuhakikishia Kama Zitto ataondoka Chadema kama wanavyotaka CCM.. Amini maneno yangu 2015 uchaguzi mkuu usikieni ktk magazeni na Tv.. Chadema itaporomoka kama CUF 2010 kumbuka hawakudhania kwamba itatokea hivyo hadi uchaguzi waliendelea kuamini wao ni mbadala..Na Zitto hawezi kuifanya kazi nje ya CDM huo ndio utakuwa mwisho wake kisiasa.. aamini maneno yangu atakuwa Mbatia au Jussa wa Chadema, kuingia Ubunge kwa hisani ya rais au baraza la wawakilishi..
CCM wanataka Chadema kisambaratike kupitia Zitto na inaonekana mnaumeza mtego wake nyote sii Zitto au wanaChadema... Mkae chini muulizane nini matatizo yetu, na kwa nini hatuishi kugombanishwa ukweli ni upi..Chadema njooni na mafaili yenu mlopewa kuhusu Zitto na Zitto aje na mafaili yake alopewa kuhusu Viongozi wengine wa Chadema halafu mtayatazame mlinganishe ukwlei ndio mtajua kwamba nyote mlikuwa mkilishwa uongo..
Follow Us Here