
By
Next Level
Ndugu yangu Kandambili your observation is quite right!
Employees wanalipa kodi kubwa sana kulinganisha na makundi mengine ya kijamii relative to their income.
Ukifanikiwa kuwa mjasiliamali na business yako ikatake off vizuri, ukaiendesha informally, unauwezekano wakulipa kodi ndogo sana kuliko ukiwa umeajiriwa!
Ngoja nitoe mfano mmoja hapa;
Nimemwajiri mtu X kwa ajili ya kutoa huduma fulani kwenye yangu na namlipa kwa mwezi Tshs 400,000/= (Gross income), mwajiriwa huyu nitamkata kwa kila mwezi Tshs 54,500 kama PAYE so kwa mwaka atakatwa Tsh 654,000!
Scenerio ya pili, sitaki kuajiri na mcontract mjasiriamali Y awe ananifanyia kazi ambayo X angeifanya, tunakubaliana niwe namlipa labda baada ya miezi sita Tshs 2,400,000 so kwa mwaka Tshs 4,800,000 kama fees excluding disbursements. Huyu mambo ya kodi anatakiwa kuhandle mwenyewe, so labda ataenda kukata TIN na kujisajili kama mfanyabiashara mdogo.
Kwa kuwa mapato /mauzo yake hayazidi Tshs 7,000,000 kwa mwaka....anatakiwa alipe Tshs 95,000 tu kwa mwaka kama kodi
Now linganisha Tshs 654,000 PAYE anayolipa mwajiriwa na Tshs 95,000 kwa mapato sawa utaona jinsi waajiriwa wanavyoumizwa.
Mfano mwingine; niko na jamaa zangu pale k/koo wanafanya biashara mbalimbali na wanamiliki majengo kadhaa pale.....mauzo yao kwa mwaka ni kati ya Tshs 100,000,000 to 1,000,000,000! Lakini kodi wanayolipa.....utashangaa kweli, hata Tshs 500,000 kwa mwaka haifiki na hii wanakadiriwa na TRA. Wakati mfanyakazi anayepata say Gross ya 5,000,000 kwa mwezi, tayari analipa zaidi ya 1 mil kama kodi kila mwezi!
So ukiwa kwenye informal sector kodi unalipa kidogo sana relative to your income compared to employees!
TRA na serikali wanatakiwa kupanua wigo wa kodi (tax base) ili kuyanusuru maisha ya wafanyakazi waliobebeshwa mzigo wa kodi kama punda! Waache uvivu wa kufikiria vyanzo vingine vya kodi kama vile Kodi za pango (rental taxes), waongeze kodi kule kwenye informal sector, including income inayopotea kule kny masherehe, madalali, MCs, Usafirishaji etc na pia kupunguza matumizi yasiyokuwa ya lazima kwa serikali!
Vinginevyo wote tutahamia huko kwenye informal sector, kwenye unafuu mkubwa sana wa kodi!
Follow Us Here