Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Ukabila na umimi/usisi..........

    Report Post
    Results 1 to 6 of 6
    1. #1
      M'Jr's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 8th July 2011
      Location : Still cracking....................
      Posts : 2,843
      Rep Power : 3152
      Likes Received
      807
      Likes Given
      653

      Post Ukabila na umimi/usisi..........

      Katika siku za hivi karibuni dhana ya ukabila/udini na umimi imekuwa inachukua nafasi kubwa sana hasa baada ya msuguano wa kisiasa kuonekana unakuwa mkubwa hapa nchini. Nakumbuka katika hotuba kadhaa za baba wa taifa alikuwa akijaribu kukemea hili kwa nguvu sana hasa suala hili la udini na ukabila.

      Ukabila
      Katika hili ntatoa mifano michache ambayo inazungumzwa sana kwa kipindi hiki ili kuonyesha dhana ya ukabila inavyochukua nafasi katika siku za hivi karibuni. Nakumbuka katika uchaguzi wa mwaka 1995 kulizuka dhana ya ukabila ambayo ilienezwa ikikihusisha zaidi chama cha NCCR Mageuzi wakati huo kikiwa chini ya Mh. Lyatonga kuwa ni chama cha "wachaga" baadae dhana hiyo ikafutika hasa baada ya uchaguzi ule kumalizika lakini sasa imeibuka tena na kipindi hiki ikihusisha zaidi chama cha Chadema ambapo awali ilikuwa ikiita chama cha "wachaga" lakini sasa imepanuka zaidi na kukiita chama cha "Kaskazini" kinachonitia hofu kidogo hapa ni namna dhana hii inavyokuwa kwa kasi na wakati mwingine napata woga kidogo kuwa "watanzania tumeshafika hapo"

      Hivi tunapochagua kiongozi ni nini tunakuwa tunaangalia kutoka kwake? Je ni kabila lake, wapi anatoka au ni uwezo wake wa kufanya kazi? Inanisikitisha kidogo kwasababu ni dhana ambayo sasa inawaingia mpaka wasomi wakubwa ambao mi nilitegemea wangekuwa nguzo ya umoja na mshikamano wetu kama nchi.

      Udini
      Hivi majuzi baada ya tume ya katiba kutangazwa na kuapishwa niliendelea kusikia minong'ono kuwa "mbona waislam ni wengi kuliko wakristo" Dah hii nayo ikanifanya nitetemeke maana niliona sasa huku tunakokwenda siko na tena kigezo walichokuwa wanakitumia wenye hoja hiyo ni majina nikawa najiuliza hivi kwa mfano jina la "Jaji Augustino Ramadhani" unamuita mkristo au Muislam?

      Mi mtazamo wangu ni kwamba nafikiri bado tuna uwezo wa kurekebisha hili hasa kwa wanasiasa maana ukiangalia kwa kiwango kikubwa dhana hii inachangiwa na wanasiasa ambao wako tayari kufanya lolote ili kuwa bora wenzao huku wakiteketeza umoja na mshikamano tulionao watanzania. Mwisho nasema kwamba;

      "Yule anayewasema wenzie ni wakabila na wadini, yeye ndiye mkabila na mdini maana kama asingekuwa mkabila na mdini asingeona ukabila na udini bali uwezo wa kufanya kazi wa watu"
      Mr Rocky likes this.
      A hen is only an egg's way of making another egg

    2. RukaaJuu Final

    3. #2
      Mr Rocky's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th October 2007
      Location : Hungumalwa
      Posts : 9,208
      Rep Power : 46193
      Likes Received
      6554
      Likes Given
      5321

      Default Re: Ukabila na umimi/usisi..........

      Hizi ni dhana mbili wanazotumia watu waliofilisika kimawazo na kisera (kama alivyosema Nyerere R.I.P).

      Huwa hawana pa kuangukia na wanazichagua ili kupata huruma za watu kuwa unaona dini yetu haijawahi kumtoa kiongozi wa juu nichagueni au nipeni uongozi niwakomboe au kabila letu limedharauliwa sana nichagueni muone maendeleo; kabila letu ni dogo sana na hatuna sauti nipeni uongozi nilikomboe au kabila letu ni kubwa sana na sisi ndo tunatakiwa kutoa kiongozi kwa sasa. Ni dhana mufilisi na wanaziendeleza na kuzidakia bila kujua madhara yake kwenye vichwa vya watu

      Maana unapopandikiza mbegu hizo kwenye vichwa vya watu ipo siku wale unaowaambia kuwa wanaonewa watanyanyuka na kusema sasa imetosha tumeonea sana wacha tujikomboe.

      Kuna jeshi ambalo lipo tayari muda wowote kujitolea kufanya hayo wanayoyapandikiza vichwani mwa watu bila kutarajia
      M'Jr likes this.
      When you are in Love you can't fall asleep because reality is better than your dreams

    4. #3
      M'Jr's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 8th July 2011
      Location : Still cracking....................
      Posts : 2,843
      Rep Power : 3152
      Likes Received
      807
      Likes Given
      653

      Default Re: Ukabila na umimi/usisi..........

      Quote By Mr Rocky
      Hizi ni dhana mbili wanazotumia watu waliofilisika kimawazo na kisera (kama alivyosema Nyerere R.I.P).

      Huwa hawana pa kuangukia na wanazichagua ili kupata huruma za watu kuwa unaona dini yetu haijawahi kumtoa kiongozi wa juu nichagueni au nipeni uongozi niwakomboe au kabila letu limedharauliwa sana nichagueni muone maendeleo; kabila letu ni dogo sana na hatuna sauti nipeni uongozi nilikomboe au kabila letu ni kubwa sana na sisi ndo tunatakiwa kutoa kiongozi kwa sasa. Ni dhana mufilisi na wanaziendeleza na kuzidakia bila kujua madhara yake kwenye vichwa vya watu

      Maana unapopandikiza mbegu hizo kwenye vichwa vya watu ipo siku wale unaowaambia kuwa wanaonewa watanyanyuka na kusema sasa imetosha tumeonea sana wacha tujikomboe.

      Kuna jeshi ambalo lipo tayari muda wowote kujitolea kufanya hayo wanayoyapandikiza vichwani mwa watu bila kutarajia
      Mkuu kinachonitisha ni namna ambayo dhana hiyo imeanza kuongelewa na watu ambao mi nilitegemea wangekuwa mstari wa mbele kupingana nalo tena wanaongea wakiwa vifua mbele kabisa.

      Dah shame on them!
      Mr Rocky likes this.
      A hen is only an egg's way of making another egg

    5. #4
      Mr Rocky's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th October 2007
      Location : Hungumalwa
      Posts : 9,208
      Rep Power : 46193
      Likes Received
      6554
      Likes Given
      5321

      Default Re: Ukabila na umimi/usisi..........

      Quote By M'Jr
      Mkuu kinachonitisha ni namna ambayo dhana hiyo imeanza kuongelewa na watu ambao mi nilitegemea wangekuwa mstari wa mbele kupingana nalo tena wanaongea wakiwa vifua mbele kabisa.

      Dah shame on them!
      Mkuu sitaki kumhukumu mtu ila haya mambo yameanzia mbali.

      Na hizo dhana zinavyotumiwa sijui kama wanajua madhara yake. Kuna vijana ambao hawana kazi kwa wingi sana na ambao kwa sasa ni hatari sana iwapo watapata mtu ambaye atawapa wazo mbadala la kufanya.

      Ni dhana potofu ambazo ningetegemea hata viongozi wetu wa juu wazipigie kelele ila inaonekana na wao wanajihusisha kuziongelea
      M'Jr likes this.
      When you are in Love you can't fall asleep because reality is better than your dreams

    6. #5
      M'Jr's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 8th July 2011
      Location : Still cracking....................
      Posts : 2,843
      Rep Power : 3152
      Likes Received
      807
      Likes Given
      653

      Default Re: Ukabila na umimi/usisi..........

      Quote By Mr Rocky
      Mkuu sitaki kumhukumu mtu ila haya mambo yameanzia mbali.

      Na hizo dhana zinavyotumiwa sijui kama wanajua madhara yake. Kuna vijana ambao hawana kazi kwa wingi sana na ambao kwa sasa ni hatari sana iwapo watapata mtu ambaye atawapa wazo mbadala la kufanya.

      Ni dhana potofu ambazo ningetegemea hata viongozi wetu wa juu wazipigie kelele ila inaonekana na wao wanajihusisha kuziongelea
      Mr Rocky,

      Wakati mwingine nachukia siasa mkuu kwasababu inawabadilisha watu na kuwafanya kuwa wanyama wasio na utashi
      Mr Rocky likes this.
      A hen is only an egg's way of making another egg

    7. Miaka 50

    8. #6
      Mr Rocky's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th October 2007
      Location : Hungumalwa
      Posts : 9,208
      Rep Power : 46193
      Likes Received
      6554
      Likes Given
      5321

      Default Re: Ukabila na umimi/usisi..........

      Quote By M'Jr
      Wakati mwingine nachukia siasa mkuu kwasababu inawabadilisha watu na kuwafanya kuwa wanyama wasio na utashi
      M'Jr,

      Huwezi kuikimbia wala kuichukia maana ni kama maisha yetu ya kila siku hao wanasiasa ndio wanaoamua mustakabali wetu wakikaa kwenye viti vyao vya kuzunguka huwa ndio waamuzi wa nini kifanyike.

      Nafikiri tufike mahali hao wanaohubiri hayo mambo waambiwe kabisa usoni mwao kuwa hizo ni sera mufilisi na zimepitwa na wakati.

      Maana tukianza kujuana makabila hapa ni balaa; inawezekana mke wangu akawa mnyakusya na nikiwachukia wanyakyusa ina maana nianze na mke wangu kule ndani kitu ambacho hakitawekezekana kabisa
      When you are in Love you can't fall asleep because reality is better than your dreams

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...