Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Nassari Backlash on Sera ya Majimbo- It seems CCM CADRE ARE SCARED TO DEATH!

    Report Post
    Results 1 to 11 of 11
    1. #1
      George Maige Nhigula Jr.'s Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th March 2008
      Posts : 464
      Rep Power : 667
      Likes Received
      142
      Likes Given
      235

      Default Nassari Backlash on Sera ya Majimbo- It seems CCM CADRE ARE SCARED TO DEATH!

      Ndugu wana Jamii ya wazalendo,

      Ni dhahiri kabisa sera ya majimbo ya chadema yenye lengo la kurejesha mamlaka kwa wananchi, na kuondoa mamlaka ya wateule wachache kama wakuu wa mikoa na wilaya ambao wamekuwa wakiteuliwa kwa kulipana fadhila na kupeana ulaji bila ya kuwa na ridhaa ya wananchi na uwajibikaji wa moja kwa moja kwa wananchi imekuwa tishio kubwa kwa makada wengi wa chama cha mapinduzi. ambao wengi wao wamekuwa wakisubiri na kujipanga kupata ulaji wa chee bila kuwa na uwajibikaji wowote kwa wananchi.

      Wimbi tunaloliona kwa viongozi na makada wengi wa ccm kujitokeza na kutumia statement ya Nassari Joshua ambayo ilikuwa poorly phraised! na ambayo mwenyekiti wa chama Taifa Mh. Freeman Mbowe kuitolea ufafanuzi pale pale NMC na kuweka kumbukumbu sawa kuwa huo sio msimamo wa chama. Hii inaonesha kuwa wana ccm wengi wamepata kisingizio cha kuibeza na kuiponda sera ya majimbo ambayo ndiyo njia sahihi ya kuleta uwajibikaji na usimamizi wa rasilimali zetu vizuri.

      Hii sio bahati mbaya kwa makada wa ccm to tie statement ya Nassari(Dogo Janja) Na Sera nzuri ya majimbo, kwani sisi sote tunajua kuwa wana ccm wengi hawaitaki sio kwa sababu ni sera mbaya la hasha! bali inakwenda kuondoa ulaji wa kupeana ukuu wa wilaya na mkoa ambao wengi wamekuwa wakipigana vikumbo kwa kujipendekeza au kufanya kila hila ili wateuliwe.

      Hali kadhalika sera ya majimbo itahamisha mamlaka mengi kutoka serikari kuu na kurejesha majimboni ambako watanzania ndio wanaishi, na watanzania wenyewe watapata fursa ya kuwachagua ma governor na leutenant governor, hivyo uwaziri hautakuwa na deal tena na wizara zitabaki kuratibu sera tu! kwa nani hajui kuwa watu wengi wanakimbilia kugombea ubunge ccm ili wawe mawaziri?

      Hivyo lazima watanzania tugundue nia ovu ya chama cha mapinduzi kuipiga mbao sera ya ya majimbo kwa mwamvuli wa kuepuka mgawanyiko wa nchi, hicho ni kisingizio ambacho hakina msingi, mbona hivi sasa tuna mikoa zaidi ya 25 na hakuna mgawanyiko sasa tukigawa majimbo ambayo yatakuwa yanajumuisha zaidi ya mikoa mitatu, huo mgawanyiko utatoka wapi?

      Ningependa sana kuona makamanda hususani viongozi wakuu wa chama wakaipigania sera hii kwa kutoa elimu kwa umma inayoeleweka, siyo hivi sasa walivyoiacha hewani ina ning'inia bila base na facts za kutosha, la sivyo kwa mwendo huu wa magamba kuposha wananchi wakati wao magamba wanajua fika kuwa SERA YA MAJIMBO ndo mwisho wa ulaji na vyeo vya kupeana.

      TUIPIGANIE SERA YA MAJIMBO KWA MAENDELEO YA NCHI YETU, UWAJIBIKAJI NA KUREJESHA MAMLAKA KWA WANANCHI,TUSIKENGEUSHWE NA DOGO JANJA BACKLASH!
      "We cannot walk alone, we must pledge once more to march into the future. Let us keep that promise and in the words of Scripture hold firmly, without wavering to the hope that we confess."

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      Uwezo Tunao's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th November 2010
      Posts : 6,873
      Rep Power : 2289
      Likes Received
      1138
      Likes Given
      1479

      Default Re: Nassari Backlash on Sera ya Majimbo- It seems CCM CADRE ARE SCARED TO DEATH!

      MJADALA NA UTOAJI MAONI HATA YALE YASIOKIPENDEZA CCM NI SHARTI KUPEWA UHURU WOTE UNAOSTAHILI BILA BUGHUDHA WALA VITISHO NDIPO KATIBA MPYA UTAKAPOWEZA KUPATIKANA KWA MURUA NA USHWARI

      Kama swala dogo tu la Mhe Nassari kusaidia kuibua mjadala mzito kitaifa ndio kama hivi inaonyesha kukitetemesha CCM hadi mfupa wa mwisho mwilini, je mijadala mizito ya Katiba Mpya tunayokusudia kuanzisha kote nchini hivi karibuni sasa chama hiki huenda kinapanga kufunga wangapi ili maoni yao yasisikike umbali wa pua zao wenyewe?

      Waheshimiwa Wana-CCM mliosalia katika jumba hilo hapo Chimwaga, napenda niseme hivi; Swala la katiba mpya lisiposhughulikiwa kwa akili zilizotulia, utaifa uliokomaa na busara zisizo mawaa;

      ... kuna uwezekano mkubwa taifa likapigwa dhoruba na mawimbi makali kushoto kulia bila kumletea mtu na au upande wowote mavuno ya kheri huko tuendako.

      Hili ni letu sote tukalifnyie kazi bila hila wala itikadi ndipo tupate kufika salama kama jamii moja wenye sababu zote kushikamana katika HAKI, MAJADILIANO, USHIKISHWAJI KWA KILA HATUA, NA UWAZI.

    4. #3
      Uliza_Bei's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th February 2011
      Posts : 794
      Rep Power : 576
      Likes Received
      112
      Likes Given
      45

      Default Re: Nassari Backlash on Sera ya Majimbo- It seems CCM CADRE ARE SCARED TO DEATH!

      Ninaota jimbo kubwa na tajiri la kusini nyanda za juu-mbeya,iringa na rukwa linafuata sukumaland-mwanza,shinyanga na tabora. Wakwe.re mtakula jeuri yenu

    5. #4
      Hofstede's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th July 2007
      Posts : 3,604
      Rep Power : 21341
      Likes Received
      981
      Likes Given
      988

      Default Re: Nassari Backlash on Sera ya Majimbo- It seems CCM CADRE ARE SCARED TO DEATH!

      Hakuna Nassari backlush wala explosion. CCM wameona wameshindwa na sasa wanaanza witch-hunt. Sera ya majimbo si kuigawa nchi kwani nchi iliisha unganishwa na Mwalimu. Sera ya majimbo ni njia pekee ya kuongeza mwendokasi wa maendeleo. Mtu mmoja kukaa magogoni akiendesha nchi kwa remote control ni sababu kubwa sana kufanya viongozi wa chini kutokuwa kuwa wabunifu. Kila wanalolifanya wanajiuliza mara mbilmbili je litamfurahishwa 'bwana mkubwa' ?

      CCM wanaposhindwa kuzishikia bango kauli za kina Jusa Ladhu na kuanza kum-demonise kijana mdogo asiye na uzoefu kwenye siasa ni dalili za disperate na hazitawasaidia na wimbo la mawazo ya kimageuzi lililojikita miongozi mwa majority ya watanzania.

      Hizi kelele zao ni sawa na mtu mwenye 'terminal desease who takes painkillers' while waiting for the death in peaceful manner.
      Jasusi, KOMBESANA and Uwezo Tunao like this.

    6. #5
      Idimi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th March 2007
      Location : Ikwiriri
      Posts : 4,666
      Rep Power : 13623
      Likes Received
      838
      Likes Given
      319

      Default Re: Nassari Backlash on Sera ya Majimbo- It seems CCM CADRE ARE SCARED TO DEATH!

      Tatito ni kwamba sera ya majimbo inakuwa misinterpreted na CCM. Hivi kwa nini wasiwaulize waziwazi CMD kwamba hiyo sera ikoje na inafanyaje kazi? Mbona majimbo ya Marekani yana sheria zinazotofautiana kidogo lakini bado Marekani ni moja?
      A successful man is one who makes more money than his wife can spend. A successful woman is one who can find such a man!
      [email protected]

    7. Miaka 50

    8. #6
      Bitabo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th September 2011
      Posts : 1,375
      Rep Power : 661
      Likes Received
      447
      Likes Given
      261

      Default Re: Nassari Backlash on Sera ya Majimbo- It seems CCM CADRE ARE SCARED TO DEATH!

      Sera ya majimbo itapunguza wizi wa fedha za wananchi maana makusanyo yote yanakuwa controlled na uongozi wa jimbo kabla ya kuwasiliana na serikali kuu. Sasa CCM wamezoea kuzichota hazina ambako ndo kapu la fedha zote.
      Wakilifikiria hili, wanaamua kuwaongopea watanzania.
      Yana mwisho lakini
      KOMBESANA likes this.
      Uovu wa siku moja, unaondoa wema wa MWAKA MZIMA

    9. #7
      Kobello's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th February 2011
      Posts : 2,946
      Rep Power : 1659
      Likes Received
      1107
      Likes Given
      191

      Default Re: Nassari Backlash on Sera ya Majimbo- It seems CCM CADRE ARE SCARED TO DEATH!

      Quote By Bitabo
      Sera ya majimbo itapunguza wizi wa fedha za wananchi maana makusanyo yote yanakuwa controlled na uongozi wa jimbo kabla ya kuwasiliana na serikali kuu. Sasa CCM wamezoea kuzichota hazina ambako ndo kapu la fedha zote.
      Wakilifikiria hili, wanaamua kuwaongopea watanzania.
      Yana mwisho lakini
      Kama Nigeria, Congo ..... majimbo siyo dawa ya uwajibikaji. Ni njia ya waliokosa kura kupata mamlaka through divide and rule. Tupo wengi tunaopinga hili, let the ballotbox speak.
      Keeping quiet is a war crime.

    10. #8
      Zakumi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2008
      Location : Mtoni
      Posts : 3,975
      Rep Power : 1346
      Likes Received
      893
      Likes Given
      374

      Default Re: Nassari Backlash on Sera ya Majimbo- It seems CCM CADRE ARE SCARED TO DEATH!

      Kinachowasumbua ni kutaka kuendeleza failed legacies za Nyerere. Kwanini kushindwa kwa majimbo tutumie mifano ya Congo na Nigeria tu?Nchi karibu zote zilizoendelea zina Majimbo. Kwaninj basi msitaje hizo nchi?
      JokaKuu likes this.

    11. #9
      JokaKuu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st July 2006
      Posts : 6,819
      Rep Power : 2966
      Likes Received
      2421
      Likes Given
      3495

      Default Re: Nassari Backlash on Sera ya Majimbo- It seems CCM CADRE ARE SCARED TO DEATH!

      Quote By Zakumi
      Kinachowasumbua ni kutaka kuendeleza failed legacies za Nyerere. Kwanini kushindwa kwa majimbo tutumie mifano ya Congo na Nigeria tu?Nchi karibu zote zilizoendelea zina Majimbo. Kwaninj basi msitaje hizo nchi?
      Zakumi,

      ..mimi naogopa nchi hii kuwa na serikali 13.

      ..serikali 3[znz,tgk,muungano], halafu hayo majimbo 10 yanayopendekezwa.

      ..I will be interested kumsikiliza mtu atakayekuja na idea ya kupunguza ukubwa wa serikali tuliyonayo, na wakati huohuo kuifanya iwe more efficient.

      ..mambo haya ukiwaachia wanasiasa wayazungumze basi siku zote watakuja na mbinu za kujiongezea ulaji tu.

    12. #10
      Mkandara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd March 2006
      Location : T dot
      Posts : 13,770
      Rep Power : 7662
      Likes Received
      4929
      Likes Given
      4509

      Default Re: Nassari Backlash on Sera ya Majimbo- It seems CCM CADRE ARE SCARED TO DEATH!

      Nadhani swala hili kila mmoja wetu atalitazama kwa sura ya kutumia mifano ya nchi nyinginezo ama kutumia vitabu (elimu) lakini nadhani ni bora zaidi tujitazame sisi wenyewe tulipo kisha tutazame faida na athari zake na jinsi gani zinaweza kurekebishwa ama kuondolewa maana lengo ni kusonga mbele ktk maendeleo.

      Serikali ya Majimbo ni sera ya Chadema ambayo kwa bahati mbaya sana inatazama nchi nyinginezo. Kuna Uzuri wake na ubaya wake lakini kabla hatuja hukumu lolote ni vizuri zaidi kujipima sisi wenyewe. Tusimame mbele ya kioo na kujitazama who we are, where we at, na wapi tunataka kwendaKujitazama kiooni na kujitambua kabla ya maamuzi kufanye nini?

      Kuna kijana hapo juu kazungumza na kueleza majimbo yatakayo endeleo na majimbo ambayo yataachwa nyuma..tena kwa kusisitiza WAKWERE watakula jeuri yao. Je, hii ndio sura halisi ya Mdanganyika? Hivi kwelitunataka mgao sawa wa keki ya taifa ama tunataka kuchagua kundi la watu gani wanaostahili kupata kipande kikubwa cha keki hiyo..

      Hii ni hatari kubwa sana kisiasa yaani mfumo unaundwa ili kuwadhalilisha wengine na hasa Wakwere sijui kwa sababu ya JK ambaye hakuuweka mfumo huu, naye kaukuta na atauacha.. Ikiwa sera ya Majimbo inatokana na hisia za watu kuona majimbo fulani hayafaidiki na keki ya Taifa hivyo solution ni kuunda majimbo ambayo yatawapa nafasi kubwa ya kufaidika na mali zao.. Hapa yanajitokeza maswali mengi magumu zaidi.

      1. Hoja kubwa ya Muungano kuhusu Mafuta.. mathlan Mafuta yamepatikana Tanga, haya mafuta yatakuwa ya serikali ya muungano ama yatakuwa ya jimbo hilo hata kama mkopo umetolewa kwa Tanzania?.. Maana tukumbuke jimbo pekee haliwezi kuchukua dhamana ya kupewa mikopo mikubwa ya kimataifa unayohusu rasilimali za kitaifa kama hizi..Miradi ilokwisha wenkezwa kama Buzwagi, Songos, Makaa ya mawe na kadhalika itakuwa mali ya nani?.. ikiwa tunalipa watanzania wote deni lake.

      2. Uongozi wa haya Majimbo utafanyika vipi, Je kiongozi wa jimbo moja anaweza kwenda kugombea jimbo jingine japokuwa yeye ni mkazi wa Dar?..Kutokana namfumo uliopo viongozi wengi wanaishi majimbo wasiyowakilisha na wana Uhuru wa kuhama na kuendelea na nyadhifa zao. Je, mfumo wa Majimbo utawalazimu viongozi kuishi ktk majimbo yao? ni uhalali upi utatumika kumkubali mgombea kuwa mkazi au raia wa jimbo husika ikiwa leo Tanzania kila mtu anagombea anapotaka, kuishi anapotaka na kupewa transfer kona zote za Jamhuri.. Ni vigezo gani vitatumika kutenganisha jimbo haddi jimbo.

      Binafsi yangu pamoja na kwamba kuna haja kubwa sana ya kuondoa mfumo huu uliopo ambao unategemea serikali kuu kuepeleka maendeleo mikoani. Ni mfumo dume, mfumo unaowalazimisha wananchi wapiga kura kuchagua chama tawala laa sivyo watakosa maendeleo. Na hii imetumika sana toka tumeingia demokrasia na kwa bahati mbaya sana watu wameshindwa kuelewa kwamba mikoa yote ambayo haikuwachagua CCM toka 1995 ndio mikoa iliathirika zaidi.

      Kusini ambako kulikuwa ngome ya CUF wameathirika sana hadi majuzi ndio tunaona maendeleo yakisogezwa sogezwa. Mikoa ya Nyanda za juu na hasa Kilimanjaro imefaidika tu kwa sababu kuna viongozi wengi Wachanga ndani ya serikali ya CCM ambao wameshinda nafasi tofauti za kiutawala, hivyo kwa kutumia mapenzi yao ya asili kwa mkoa wao ndio tumeona mabadiliko haswa wakati Mbowe alipogombea Urais, wakazoa baadhi ya majimbo...

      Hakika Wabunge wa vyama vya Upinzani wana wakati mgumu sana ktk mfumo huu, hawa wanalazimika kupiga magoti kuiomba serikali ipeleke maendeleo majimboni mwao na sii kwamba fedha tayari ziko alllocated ktk majimbo hayo bali Waziri ndiye mweye kiroba chote na hutazama wapi na afanye nini au laa halazimiki.. He can easly explain tomorrow kwa nini sehemu fulani hawakufanikiwa maadam ktk umaskini huu sababu ziko nyingi. Bila mbunge kumbembeleza na kumlamba miguu Waziri au Naibu hutoka mtupu na haijalishi kuna umuhimu gani kwa wananchi wake..

      This is Sonething has to be done against Bureaucracy.. Na ushauri wangu baada ya kuwasoma Wadanganyika na hasa uongozi ulochoka na dhaifu. hakuna njia zaidi ya kupeleka madaraka mikoani. Acha mikoa ichague wakuu wake wa mikoa, wabunge, madiwani, Mameya na viongozi wote wa Halmashauri na serikali za mitaa ambao watawajibika kwa mkuu wa mkoa Regional Commision ambaye atakuwa kama Gawana na mwakilishi wa chama kilichoshinda. Uongozi wa serikali hii utatokana na nusu au zaidi ya pato la kodi walizokusanya ktk mkoa kila mwaka.. na nusu nyingine itapelekwa ktk serikali kuu ambayo itahudumia miradi na madeni ya Kitaifa ktk maendeleo.

      Na serikali kuu itawajibika kuepeleka maendeleo mikoani kutokana na pato la uwekezaji ktk miundombinu na miradi ya Kitaifa hivyo Mafuta yaliyopatikana Tanga itajulikana kwamba nusu ya pato lake litakwenda mfuko wa Taifa na kuingia ktk miradi ya kitaifa na kulipa madeni..Lakini umuhmu wa mfumo huu ni kuufanya mkoa unaozalisha zaidi kufaidika na rasilimali yake tofatui na kuwepo majimbo kutatulazimisha kesho mkoa wa Tanga kutaka kujitenga na jimbo kwa sababu wao ndio wenye Mafuta na wanaendesha uchumi wa jimbo..Sii rahsi kwa Tanga kujitoa ktk serikali kuu kwa sababu haina uhuru kamili wa Kitaifa..

      Kuiga serikali za Majimbo kuna athari zake maana ikumbukwe tu kwamba wenzetu waliunda majimbo yao kama sisi tulivyounda muungano wetu na Zanzibar.. majibmo hayo yalikuwa huru na yenye mamlaka kamili yakaungda UMOJA ili kujenga nguvu kubwa ya kiuchumi tofauti na sisi tunataka kuunda majimbo kwa kuigawa nchi vipande japokuwa tuna UMOJA hivyo tutauondoa UMOJA wetu.

      Kwa akili za Wadanganyika hii itakuwa mwanzo wa Ukabila, Udini na hata vita maana hili la Zanzibar tu na halali ya kuwepo majimbo mawili inatushinda..Kama hatuna solution na swala la Muungano itakuwaje rahisi tukate majimbo na uwapa mamlaka kamili ya kuunda serikali na bunge?..
      Last edited by Mkandara; 9th July 2012 at 22:19.
      Exploration of reality

    13. #11
      Sangarara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th September 2011
      Posts : 3,306
      Rep Power : 1198
      Likes Received
      1182
      Likes Given
      1557

      Default Re: Nassari Backlash on Sera ya Majimbo- It seems CCM CADRE ARE SCARED TO DEATH!

      Quote By Mkandara
      Nadhani swala hili kila mmoja wetu atalitazama kwa sura ya kutumia mifano ya nchi nyinginezo ama kutumia vitabu (elimu) lakini nadhani ni bora zaidi tujitazame sisi wenyewe tulipo kisha tutazame faida na athari zake na jinsi gani zinaweza kurekebishwa ama kuondolewa maana lengo ni kusonga mbele ktk maendeleo.

      Serikali ya Majimbo ni sera ya Chadema ambayo kwa bahati mbaya sana inatazama nchi nyinginezo. Kuna Uzuri wake na ubaya wake lakini kabla hatuja hukumu lolote ni vizuri zaidi kujipima sisi wenyewe. Tusimame mbele ya kioo na kujitazama who we are, where we at, na wapi tunataka kwendaKujitazama kiooni na kujitambua kabla ya maamuzi kufanye nini?

      Kuna kijana hapo juu kazungumza na kueleza majimbo yatakayo endeleo na majimbo ambayo yataachwa nyuma..tena kwa kusisitiza WAKWERE watakula jeuri yao. Je, hii ndio sura halisi ya Mdanganyika? Hivi kwelitunataka mgao sawa wa keki ya taifa ama tunataka kuchagua kundi la watu gani wanaostahili kupata kipande kikubwa cha keki hiyo..

      Hii ni hatari kubwa sana kisiasa yaani mfumo unaundwa ili kuwadhalilisha wengine na hasa Wakwere sijui kwa sababu ya JK ambaye hakuuweka mfumo huu, naye kaukuta na atauacha.. Ikiwa sera ya Majimbo inatokana na hisia za watu kuona majimbo fulani hayafaidiki na keki ya Taifa hivyo solution ni kuunda majimbo ambayo yatawapa nafasi kubwa ya kufaidika na mali zao.. Hapa yanajitokeza maswali mengi magumu zaidi.

      1. Hoja kubwa ya Muungano kuhusu Mafuta.. mathlan Mafuta yamepatikana Tanga, haya mafuta yatakuwa ya serikali ya muungano ama yatakuwa ya jimbo hilo hata kama mkopo umetolewa kwa Tanzania?.. Maana tukumbuke jimbo pekee haliwezi kuchukua dhamana ya kupewa mikopo mikubwa ya kimataifa unayohusu rasilimali za kitaifa kama hizi..Miradi ilokwisha wenkezwa kama Buzwagi, Songos, Makaa ya mawe na kadhalika itakuwa mali ya nani?.. ikiwa tunalipa watanzania wote deni lake.

      2. Uongozi wa haya Majimbo utafanyika vipi, Je kiongozi wa jimbo moja anaweza kwenda kugombea jimbo jingine japokuwa yeye ni mkazi wa Dar?..Kutokana namfumo uliopo viongozi wengi wanaishi majimbo wasiyowakilisha na wana Uhuru wa kuhama na kuendelea na nyadhifa zao. Je, mfumo wa Majimbo utawalazimu viongozi kuishi ktk majimbo yao? ni uhalali upi utatumika kumkubali mgombea kuwa mkazi au raia wa jimbo husika ikiwa leo Tanzania kila mtu anagombea anapotaka, kuishi anapotaka na kupewa transfer kona zote za Jamhuri.. Ni vigezo gani vitatumika kutenganisha jimbo haddi jimbo.

      Binafsi yangu pamoja na kwamba kuna haja kubwa sana ya kuondoa mfumo huu uliopo ambao unategemea serikali kuu kuepeleka maendeleo mikoani. Ni mfumo dume, mfumo unaowalazimisha wananchi wapiga kura kuchagua chama tawala laa sivyo watakosa maendeleo. Na hii imetumika sana toka tumeingia demokrasia na kwa bahati mbaya sana watu wameshindwa kuelewa kwamba mikoa yote ambayo haikuwachagua CCM toka 1995 ndio mikoa iliathirika zaidi.

      Kusini ambako kulikuwa ngome ya CUF wameathirika sana hadi majuzi ndio tunaona maendeleo yakisogezwa sogezwa. Mikoa ya Nyanda za juu na hasa Kilimanjaro imefaidika tu kwa sababu kuna viongozi wengi Wachanga ndani ya serikali ya CCM ambao wameshinda nafasi tofauti za kiutawala, hivyo kwa kutumia mapenzi yao ya asili kwa mkoa wao ndio tumeona mabadiliko haswa wakati Mbowe alipogombea Urais, wakazoa baadhi ya majimbo...

      Hakika Wabunge wa vyama vya Upinzani wana wakati mgumu sana ktk mfumo huu, hawa wanalazimika kupiga magoti kuiomba serikali ipeleke maendeleo majimboni mwao na sii kwamba fedha tayari ziko alllocated ktk majimbo hayo bali Waziri ndiye mweye kiroba chote na hutazama wapi na afanye nini au laa halazimiki.. He can easly explain tomorrow kwa nini sehemu fulani hawakufanikiwa maadam ktk umaskini huu sababu ziko nyingi. Bila mbunge kumbembeleza na kumlamba miguu Waziri au Naibu hutoka mtupu na haijalishi kuna umuhimu gani kwa wananchi wake..

      This is Sonething has to be done against Bureaucracy.. Na ushauri wangu baada ya kuwasoma Wadanganyika na hasa uongozi ulochoka na dhaifu. hakuna njia zaidi ya kupeleka madaraka mikoani. Acha mikoa ichague wakuu wake wa mikoa, wabunge, madiwani, Mameya na viongozi wote wa Halmashauri na serikali za mitaa ambao watawajibika kwa mkuu wa mkoa Regional Commision ambaye atakuwa kama Gawana na mwakilishi wa chama kilichoshinda. Uongozi wa serikali hii utatokana na nusu au zaidi ya pato la kodi walizokusanya ktk mkoa kila mwaka.. na nusu nyingine itapelekwa ktk serikali kuu ambayo itahudumia miradi na madeni ya Kitaifa ktk maendeleo.

      Na serikali kuu itawajibika kuepeleka maendeleo mikoani kutokana na pato la uwekezaji ktk miundombinu na miradi ya Kitaifa hivyo Mafuta yaliyopatikana Tanga itajulikana kwamba nusu ya pato lake litakwenda mfuko wa Taifa na kuingia ktk miradi ya kitaifa na kulipa madeni..Lakini umuhmu wa mfumo huu ni kuufanya mkoa unaozalisha zaidi kufaidika na rasilimali yake tofatui na kuwepo majimbo kutatulazimisha kesho mkoa wa Tanga kutaka kujitenga na jimbo kwa sababu wao ndio wenye Mafuta na wanaendesha uchumi wa jimbo..Sii rahsi kwa Tanga kujitoa ktk serikali kuu kwa sababu haina uhuru kamili wa Kitaifa..

      Kuiga serikali za Majimbo kuna athari zake maana ikumbukwe tu kwamba wenzetu waliunda majimbo yao kama sisi tulivyounda muungano wetu na Zanzibar.. majibmo hayo yalikuwa huru na yenye mamlaka kamili yakaungda UMOJA ili kujenga nguvu kubwa ya kiuchumi tofauti na sisi tunataka kuunda majimbo kwa kuigawa nchi vipande japokuwa tuna UMOJA hivyo tutauondoa UMOJA wetu.

      Kwa akili za Wadanganyika hii itakuwa mwanzo wa Ukabila, Udini na hata vita maana hili la Zanzibar tu na halali ya kuwepo majimbo mawili inatushinda..Kama hatuna solution na swala la Muungano itakuwaje rahisi tukate majimbo na uwapa mamlaka kamili ya kuunda serikali na bunge?..
      Mkandara
      Kabla sijachangia, kuna makosa nikisema kwamba, umefanya tasmini kwa kuangalia vitu vilivyoko kwenye majimbo badala ya watu walioko kwenye majimbo?

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...