Mkuu nitasisitiza kwamba bado hujanielewa. Taifa ni lazima liwe na dira yake kabla hujamfikia rais na vision yake kufikia yale yaliyokusudiwa. Mkuu dira ya rais inakuja tu ktk kutekeleza dira kubwa ya Kitaifa. JK leo ni kama CEO ambaye anaendesha shirika lakini mwenye mali ni sisi, hivyo lazima tuwe na vision ya Kitaifa kiasi kwamba kama CEO hakufikia malengo tunayoyataka tutamfukuza kazi na kumweka meneja mwingine. Sisi kama taifa hatuna malengo hayo tunamtegemea JK mwajiriwa wetu na CEO ndiye atueleze atajenga kitu gani.
Kwa mfano wakati wa Nyerere tulikuwa na Malengo ya kuondokana na mambo matatu nayo ni UJINGA, UMASKINI na MARADHI na kufikia mwaka 1990 tulibadilisha ama kwa kuongeza maadui wetu kufikia Nane - 8, kupitia Millenium development.. Hii ndio ilojenga DIRA ya Kitaifa naweza sema lakini ukweli ni kwamba tumefungiwa kanyaboya na IMF au hao wazungu na ndio maana Nyerere hata siku moja hakupenda kupangiwa jinsi gani tutaondokana na maadui hao ama kupata maendeleo yetu.. tulikuwa na dira yetu (compass) sisi wenyewe japokuwa wakati mbaya.
Sasa ukitazama mathlan Umaskini na maradhi, tunachokifanya ni kuukuza zaidi umaskini na maradhi kwa sababu tunapambana na adha zake (umachinga) badala ya kuwekeza ktk vyanzo vitakavyo ondosha umaskini na Maradhi. Na ndio maana nikasema mtoto aliye maskini hawezi kutafuta mbinu za kuondokana na umaskini kwa kuweka malengo ya toka mkononi hadi mdomoni, ila atatakiwa kufikiria atakuwa nani akikua halafu anapanga long term strategy ambayo itamlenga yeye kufanikiwa na sio umaskini kuondoka maana akifanikiwa yeye umaskini unaondoka automatically..Lakini kama ataweka malengo ya kuondokana na umaskini basi hata darasa la kwanza hataweza kulimaliza maana atakuwa akiuza vitu kimachinga barabarani (as short term strategy). Kwa hiyo tunaweza pata results lakini ni za muda mfupi tu.
Makosa yako wapi na kwa nini sisi maskini, labda nimjibu Ogah hapa..Picha kubwa inajionyesha kwamba Malengo yetu ni kufuta Umaskini lakini tunachofanya ni Umachinga, hivyo results tunazozipata ni za muda mfupi not sustainable, umaskini unaendelea kuwepo kama vijana wa kimachinga barabarani ambao wao wanaona wana ajira, wakiacha umachinga watakula wapi? watafanya nini?... lakini ukweli ni kwamba they are being used kuuza mali za mtu mwingine tajiri ambaye hana malengo ya kufuta umaskini maana yeye sii maskini..
Result oriented yetu ni ya kimachinga yaani kuweka mkate mezani na ndio maana wanasema mkakati huu wa millenium unalenga asilimia 33 ya maskini nchini wakitupa kazi ya Umachinga na toka 1990 hadi leo ni asimilia chini ya 2 wametoka ktk umaskini kama hawakuongezeka zaidi maana population imeongezeka maradufu. Na pia nikatoa mfano wa mh. Mkapa ktk kuyafilisi mashirika na viwanda vya Umma, mikataba mibovu, Kugawa madini yetu ili mradi tupate asilimia 3 ya ruzuku ambayo inachangia only 1.7% ya mfuko wa Taifa. Ukweli ni kwamba hata leo tukisimamisha uzalishaji wa dhahabu nchini haitakuwa na impact kubwa kwa sababu inachangia only asilimia 2 ya pato la taifa.
Tazama Elimu chini ya Millenium inalenga Achieve universal primary education.. Sasa kweli tumerudi kufikiria kusoma na kuandika kamam msingi wa dira ya Kitaifa wakati tumeshindwa kabisa kuwaandaa vijana wetu wachimbe gas, wachimbe madini, walime ukulima wa kisasa, wafungue viwanda na kadhalika, matokeo yake leo hii tuna vijana wengi waliomaliza darasa la 7, 12, 16 na University hawana kazi. Tena naweza sema walio fail kimasomo ni wengi kuliko waliofaulu na pia kati ya waliofaulu ni wengi hawana kazi kuliko wenye kazi. Hii yote haitokani na uongozi bora kwanza bali kukosa DIRA yetu sisi isipokuwa ya kufungiwa na IMF ambayo inatuweka kama machinga wanaouza vitu barabarani kwa masharti ya Mhindi mwenye duka Kariakoo..
Kama tungejiandaa ama kuwaandaa vijana wetu, rasilimali zetu na kwa kuitazama Tanzania tuitakayo mwaka 2015, toka 1990 leo hii tungekuwa tumefuta baadhi ya malengo yetu, na ukitazama kwa undani zaidi utagundua kwamba matatizo ndio yanazidi kuongezeka.. Haya ukitazama Maradhi, iwe Malaria au HIV yote tunapambana na maradhi yenyewe yanapotokea, kwa kugawa vyandarua na na madawa toka nje wakati hatupambani na vyanzo vya maradhi haya on spot. Maradhi kama Ukoma na utapia mlo yamerudi kwa kasi ya ajabu lakini hatupambani na na viini vyake ila kwa kupitia madawa ya ponya. Hatua zote za Millenium goals hazilengi DIRA nayofikiria mimi au wewe maana haiwezekani kabisa kitaifa ati Hospital hazina dawa wala vifaa vya kufanyia kazi namadaktari hawalipwi mishahara tosha lakini tunaendelea kudai tupo vitani.
Mwisho nachoweza kusema nadhani imefika wakati wadanganyika tusikubali kuendelea na Umachinga. Na binafsi yangu sioni mtu wala kiongozi mwenye guts za kusimama na kwaambia mataifa makubwa kwamba Umachinga basi, sisi tuna malengo haya na tutaweza kuyafikia kwa kufanya kdhaa wa kadhaa.. maana hii ndio dira yetu na compass tutakayotujmia kufika huko tunakotaka kwenda.. Ufisadi ni matokeo ya Umachinga kama wachinga wanavyoibiana ama kugombania wateja kama viongozi wetu na nafasi za ajira.. Kila mmoja wetu anatazama tumbo lake kwanza, tumepoteza UTU..
Follow Us Here