Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Ubinafsishaji: Mkapa alikosea?

    Report Post
    Page 3 of 4 FirstFirst 1234 LastLast
    Results 41 to 60 of 73
    1. BAK
      #1
      BAK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2007
      Location : Mfaranyaki
      Posts : 26,617
      Rep Power : 44968
      Likes Received
      8366
      Likes Given
      8346

      Default Ubinafsishaji: Mkapa alikosea?

      Mkapa ajuta

      • Ahuzunishwa wageni kuhodhi uchumi

      na Mwandishi Wetu | Tanzania Daima~Sauti ya Watu

      RAIS mstaafu, Benjamin Mkapa, amesema anajutia kitendo chake cha kuliingiza taifa katika ubinafsishaji wa rasilimali bila ya kujiandaa kikamilifu na mabadiliko hayo.

      Mkapa alitoa majuto hayo katika mkutano ulioandaliwa na Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) uliofanyika Zanzibar wiki iliyopita katika Hoteli ya Zamani Kempinski na kuhudhuriwa na aliyekuwa Rais wa Afrika Kusini, Thabo Mbeki.

      Mbali ya Mbeki, viongozi wengine waliohudhuria mkutano huo ni Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara), Pius Msekwa na mwanasiasa mkongwe nchini, Kingunge Ngombale - Mwiru.

      Mmoja ya wajumbe waliohudhuria mkutano huo ambaye alizungumza na Tanzania Daima Jumapili kwa sharti la kutokutajwa jina lake, alisema Mkapa alikiri kuwa sera ya ubinafsishaji haijamsaidia kwa kiwango kilichotarajiwa Mtanzania na badala yake wamegeuka wageni katika rasilimali zao.

      Chanzo hicho kilidokeza kuwa Mkapa alibainisha kuwa kukubali kwake sera hiyo kulikuwa na lengo zuri la kuwafanya Watanzania waondokane na lindi la umaskini kupitia uwekezaji utakaofanywa katika rasilimali zao.

      “Alituambia sera ya ubinafsishaji inamuumiza mno, kwani alipoikubali hakutarajia kama ingeweza kuwafanya wageni wawe na sauti katika rasilimali za taifa kuliko wazawa kama ilivyo sasa,” kilisema chanzo hicho.


      Chanzo hicho kilibainisha kuwa Mkapa alifikia hatua ya kudai kuwa kama angepata nafasi ya kuwa kiongozi tena wa taifa hili angerekebisha sera ya ubinafsishaji haraka ili walau Watanzania waanze kufaidi rasilimali za nchi yao, badala ya kuwa mashuhuda wa wageni wanaoendelea kuneemeka na rasilimali za nchi.

      Alisema tatizo kubwa lililopo katika nchi za Afrika ni kutumia baadhi ya mambo wanayotakiwa kuyafanya na wafadhili au mifuko ya fedha, bila kuyafanyia tathmini ya kina ili kujua kama hayataleta madhara katika siku za usoni.

      “Mkapa alionyesha kujutia uamuzi alioufanya kwenye uwekezaji na aliweka wazi kuwa kama angeruhusiwa kurudi katika nafasi hiyo, basi jambo la kwanza kulirekebisha ni ubinafsishaji,” kilisema chanzo hicho.

      Mkapa katika utawala wake alibinafsisha mashirika mengi ya umma, ikiwemo Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa bei ya chini, kitendo ambacho kilizua malalamiko mengi kutoka kwa wananchi, pia alibinafsisha Shirika la Ndege Tanzania (ATC) na mengine mengi, kiasi cha kuzua malalamiko mbalimbali ndani na nje ya nchi.


      Aidha, katika utawala wake pia alilalamikiwa kwa kuwapendelea wawekezaji wa kigeni kuliko wazalendo, hasa katika sekta ya madini na kuingia mikataba mibovu ambayo hadi sasa imekuwa mzigo mkubwa kwa taifa, sambamba na wawekezaji hao kupata misamaha ya kodi kwa kigezo cha kuwavutia.

      Kuingia mikataba mibovu huku ndiko kulikomfanya Rais Jakaya Kikwete kuunda kamati ya kupitia mikataba ya madini na kutoa ushauri wa namna bora ya kushughulikia sekta hiyo.


      Majuto hayo ya Mkapa yanakuja huku kukiwa na shinikizo kubwa kutoka kwa baadhi ya wabunge na wananchi wakitaka afutiwe kinga yake ili aweze kushitakiwa kwa matumizi mabaya ya madaraka yake akiwa ikulu.

      Katika utawala wake, Mkapa anadaiwa kutumia madaraka yake kuanzisha miradi mbalimbali inayomhusu, ama kwa kupitia familia yake au ndugu zake, ukiwemo ule wa makaa ya mawe wa Kiwira, ambao hivi karibuni wamiliki wake wametajwa hadharani kwa mara ya kwanza.

      Chagizo la kutaka kutolewa kinga limezidi kupata kasi baada ya waliokuwa mawaziri wake, Basil Mramba (Fedha) na Daniel Yona (Nishati na Madini) na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Uchumi, Gray Mgonja, kufikishwa mahakamani kwa kosa la kulisababishia taifa hasara ya sh bilioni 11 kwa kutoa msamaha wa kodi kwa Kampuni ya M/S Stewart.

      Kinga ya Mkapa inaweza kuondolewa kama Bunge litapiga kura ya kutaka kutengua kinga hiyo, lakini ni lazima hoja hiyo iungwe mkono na theluthi mbili ya wabunge wote.
      Last edited by Silencer; 25th January 2009 at 06:53.
      nick mgongolwa likes this.
      Let your graceful words fly out into the World, carried on winds of courage, imagination and joy. Let them inspire others to step into action

    2. RukaaJuu Final

    3. #41
      Albedo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th February 2008
      Posts : 4,978
      Rep Power : 1573
      Likes Received
      1077
      Likes Given
      555

      Default Re: Ubinafsishaji: Why Mkapa was 1000% Right!

      Mkapa alisubiri Nyerere Kafa akagawa NBC kwa Makaburu usifikiri hatujui Mkuu
      "SISI SOTE NI NDUGU TATIZO NI CCM" Chris Lukosi kada wa CCM


    4. #42
      Albedo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th February 2008
      Posts : 4,978
      Rep Power : 1573
      Likes Received
      1077
      Likes Given
      555

      Default Re: Ubinafsishaji: Why Mkapa was 1000% Right!

      Akasubiri Nyerere Kufa AKAJIBINAFSISHIA KIWIRA bwa ha ha haaa
      "SISI SOTE NI NDUGU TATIZO NI CCM" Chris Lukosi kada wa CCM


    5. #43
      Albedo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th February 2008
      Posts : 4,978
      Rep Power : 1573
      Likes Received
      1077
      Likes Given
      555

      Default Re: Ubinafsishaji: Why Mkapa was 1000% Right!

      Nilimuona Mkapa akilia Baada ya Kubanwa juu ya Sera zake Mbovu za "UGAWAJI" Alizoziita "UBINAFSISHAJI"
      "SISI SOTE NI NDUGU TATIZO NI CCM" Chris Lukosi kada wa CCM


    6. #44
      NewOrder's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Posts : 275
      Rep Power : 889
      Likes Received
      109
      Likes Given
      93

      Default Re: Ubinafsishaji: Why Mkapa was 1000% Right!

      Uchambuzi wako ni wa jumla sana. Hebu usiishie tu kusema hatukuwa na mitaji, masoko na uongozi. Ni matusi kusema kuwa hatukuweza kutafuta mitaji ya kuinua uzalishaji sukari, hatukuwa na soko la sukari (sasa kuna sukari hata kutokoa nje, ni soko hili hili unalizungumzia??) na eti hatukuwa na uongozi. This is an insult!! Kumekuwa na professionals toka enzi za uhuru!!

      Hebu toa takwimu (statistics) za vitu unavosema. Haitoshi kusema alikuwa sahihi 100%. Toa takwimu za usahihi wake ukiinganisha na malengo na matarajio. Kufanikiwa asilimia 10% au 20% si kitu cha kushangilia. Sema difference ya ubinafsishaji imekuwa na ukubwa gani.

      It's no time for sentiments and emotions, provide data!
      TELO likes this.

    7. #45
      Keil's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd July 2007
      Posts : 2,381
      Rep Power : 1090
      Likes Received
      756
      Likes Given
      292

      Default Re: Ubinafsishaji: Why Mkapa was 1000% Right!

      Tuweke record sahihi:

      Katika kumbukumbu zangu sijawahi kusikia Prof. Shivji ameteuliwa kuwa Mwenyekiti au Mjumbe wa Bodi ya Mashirika ya Umma. Kama kuna mtu anafahamu, then naomba atuwekee hapa ili asije kubebeshwa mzigo ambao si wake.

      Prof. Shivji hakuwahi kuiva na Nyerere, japo kuna mambo mengi ambayo alikuwa anakubaliana nae. Kosa la kwanza la Shivji ilikuwa ni claim kwamba Tanzania kuna Classes pale alipoandika "Silent Class Struggles in Tanzania". Nyerere alijua kwamba anajenga nchi isiyo na matabaka, lakini Shivji alipinga wazi. Utetezi wake ni kwamba that was an academic paper na haihusiani na mambo ya siasa.

      Utawala wa Mwinyi, sikusikia Shivji akipewa uongozi, na hata awamu ya Mkapa ndiyo kabisa.

      Kwa hiyo sikubaliani na hoja kwamba Shivji anampinga Mkapa kwa kuwa alinyimwa ulaji.
      Jasusi, Albedo and Gad ONEYA like this.

    8. Miaka 50

    9. #46
      Mtazamaji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th February 2008
      Location : global village
      Posts : 5,979
      Rep Power : 1775
      Likes Received
      1323
      Likes Given
      2661

      Default Re: Ubinafsishaji: Why Mkapa was 1000% Right!

      Quote By W. J. Malecela

      NINASEMA TENA KWENYE KUBINAFSISHA, MKAPA WAS RIGHT 100%, SHIVJI NA WENZAKE SHOULD APOLOGIZE KWA KUMSHAMBULIA MKAPA BILA SABABU KWENYE KIGODA!


      William.

      -
      Tatizo Mkuu unashindwa kutofautisha mambo . Hata Nyerere mweneywe alijua na alikubali kuwa ubinafisaji wa njia fulani ni muhimu.

      Wanachsema na kupigia kelele kina SHIVJI sio ubinafisaji pekee bali ni utaratibu wa ubinafishaji TBL kiwanda cha pombe ndio moja ya mifano inayotumika kuoyesha uznuri wa Ubinfassishaji

      Lakni vipi viwawada kama mfano vya kusindikiza ngozi (Mwanza Tanneries,Morogoro Tannnriesetc ) amabvyo
      • vimeuzwa kwa bei chee
      • Waliovinunua kwa mgongo wa ubinifsiahaji wametumia kupata mikopo tena humu humu nchini na hawajaviendeleza wamefanya maghala
      • Vingine ndio vimetumia hata kwenye Kagoda


      Ubinafsishaji haikuwa kosa . Kosa lingine ni conflict of interest. Pale wale wanaobinafisha wanataka wawe na "Hisa" Kwenye vitu wanavyouza.

      Yaani umempa mkapa 100% umesahau japo kuondoa 10% ya Kiwira ?????!!!!!!! Ebu Tuambie Mkapa alikuwa sawa kujiuzia Kiwira.
      Gad ONEYA likes this.
      Tazama michezo live katika gym nayotumia kukuzia misuli ya IT- http://teknohama.x10.mx/live-sports/


    10. #47
      engmtolera's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st October 2010
      Posts : 3,610
      Rep Power : 1332
      Likes Received
      780
      Likes Given
      655

      Default Re: Ubinafsishaji: Why Mkapa was 1000% Right!

      wewe bwana william kiukweli unamatatizo ya kifikra,nadhani unahitaji uachane na mambo ya siasa na uendelee na maswala ya ubaharia nayasema haya kutoka moyoni kabisa.

      sera ya ubinafsishaji ilikuja kutoka nje na hili lilikuwa ni shinikizo kutoka mashirika ya kipesa duniani,
      tanzania pasi hata kujiandaa na sera hii tuliamuwa kuipokea kichwakichwa na kufanya uuzaji wa mashirika ya umma na si ubinafsishaji tena.

      Tanzania tulikuwa na viwanda 12 vya kubangua korosho kabla ya ubinafsishaji,lakini kwa sasa ni kiwanda kimoja tu ndicho kinafanya kazi na 11 vimegeuzwa ni matunzio ya wanyama

      Tanzania hatukutakiwa kuuza viwanda,bali serikali ilitakiwa kushiriki ktk uwekezaji huo kwa kumiliki hisa kama walivyo fanya Zimbambwe na hata uchina.
      tulikuwa na viwanda pale Tanga na morogoro wakati huo wa azimio la arusha,lakini baada ya kuviuza viwanda hivyo,kwa tanga baadhi vimekufa na watu kukosa ajira na morogoro baadhi vimebadirishwa matumizi na havifanyi kazi

      vile vya tumbaku viliuzwa kwa wa USA wakati haohao wa USA kule Zimbambwe kiwanda kama hicho cha tumbaku hawakuuziwa bali serikali ya zimbambwe nayo inamilika hisa.

      vile vya miwa kilombero na mtibwa inajulikana nani mmiliki hata wewe unawaelewa,haiingii kichwani kwanini serikali ilishindwa kumili viwamda hivyo wakti baada ya kujiuzia baadhi ya viwanda vimedumu hadi leo hii,kama vingekuwa havina faida nadhani wasingejiuzia

      william

      nina mengi sana lakini nashindwa kuyaweka kwani nakuona bado uu mdogo sana ktk mambo ya kisiasa,historia na hata uchumi unatakiwa ukae chini usome zaidi,na si kusoma tu yakupasa uelewe pia

      unajua bwana,umenikumbusha ile sera ya MCKENZIE kutoka USA aliykuja Tanzania na kuishauri serikali iwapunguze wafanya kazi wake kuepusha gharama,tukachukua wazo,bila kujiandaa,mwisho wa siku tukajikuta tumepunguza wasomi wetu na hatukuajipa nafasi ya kufikiria madhara ya mda mrefu.

      nalifananisha hilo la MCKENZIE na hili la uuzaji wa viwanda vyetu.hatukujipa nafasi ya kujiandaa na kuweka njia sahihi ama mipango sahii ya jinsi tutakavyo binafsisha viwanda vyetu

      hivi william nini maana ya kubinafsisha?
      Last edited by engmtolera; 25th April 2012 at 21:26.
      Chuma Chakavu likes this.
      "The person who says it cannot be done should not interrupt the person doing it."

    11. #48
      JATELO1's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st October 2011
      Posts : 1,015
      Rep Power : 901
      Likes Received
      81
      Likes Given
      39

      Default Re: Ubinafsishaji: Why Mkapa was 1000% Right!

      Quote By W. J. Malecela
      Heshima mbele sana Wakuu wote JF, juzi nimeangalia kwa mshangao mkubwa sana the so called wasomi wetu wakiongozwa na Shivji, wakimshambulia Rais mstaafu Mkapa, kuhusu Ubinafsishaji, I mean let me say this:-

      - Mnyonge mnyongeni, lakini haki yake apewe, sijawahi kuwa a big fan wa siasa za Mkapa, lakini this one I must say with my clear mind kwamba he was 100% right, Shivji na wenzake wako not only wrong isipokuwa ni professionals cying babies, wamezoea kila Awamu huwapa ujumbe wa bodi na kamati kamati za mlo, sasa ikitokea aawamu kama ya Mkapa ikawanyima mlo, basi huanza kuiandama ile Awamu wee na vilio vyao vya machozi ya mamba, kumbe ni waongo wakubwa!

      - Mkapa was right kubinfsisha kwa the FACT ya kuyaondoa mashirika na viwanda vilivyokuwa vimeathirika na utawala unaofuata siasa za sera zilizoshindwa za Azimio la Arusha, utawala ulikuwa mbovu na uliokufa. Ili kujenga uchumi imara unahitaji kuwa na Capital, Markets, na Leadership, ambavyo vyote havikuwepo under mfumo wa Azimio la Arusha tulilokuwa nalo then, ambalo haliwa freindly na wageni kuja kuwekeza, kwa hiyo ilikuwa ni sawa kwa Mkapa, kuyauza na mengine kuwauzia wazawa ili yaweze kusimama na kuendelea tena. In the process Mkapa alibinafsisha mashirika na viwanda 330, 180 aliwauzia wazawa ambayo ni more than 50%, 23 tu aliwauzia wageni na 127 alitoa kwa ubia wa wageni na wazawa, matokeo yamekuwa Serikali kukusanya Shillingi Billioni 250 kwa mwezi kwa mashirika machache tu kama NBC, CRDB, TCC, na TBL as opposed to Shillingi Billion 10 tu zilizokuwa zikikusanywa kabla ya Mkapa kubinafsisha.

      - It is about time sasa Shivji na wenzake wakajitokeza kwenye nafasi za uongozi wa taifa ili tuone uwezo wao wa kufikiri kuliko kulia lia kwa kila awamu. Ni lini watajikita kwenye kutoa solutions badala ya kulaumu tu kila siku kwa sababu ya kukosa mlo? I mean hili taifa wengine tumechoshwa sana na hawa crying babies wasiokuwa na jipya zaidi tu ya kulilia defeated theories ambazo tumezijaribu na zimtufikisha hapa tulipo pabaya sana hili taifa.

      NINASEMA TENA KWENYE KUBINAFSISHA, MKAPA WAS RIGHT 100%, SHIVJI NA WENZAKE SHOULD APOLOGIZE KWA KUMSHAMBULIA MKAPA BILA SABABU KWENYE KIGODA!


      William.

      -
      Nilifikiri una exposure na angalao elimu hivyo ungeweza kutueleza kwa kina ni kwa jinsi gani Mkapa alikuwa right 100%, na badala yake umeishia kutuletea figure za ku-cut and paste kutoka kwenye hoja za Mkapa. Umekuwa wa jumla jumla na bila kuelezea impact za hizo ubinafsishaji katika uchumi wetu. Unageneralize issues as usual kama wazee wa CCM. Sasa nimefarijika kwasababu ya wewe kukosa ubunge wa EAC, kwani kuna wanatakiwa wenye uelewa wa issues na siyo mbumbumbu wa masuala ya ubinafsishaji kama ulivyo sasa. Pia lazima ukumbuke kule watu wanakwenda kujenga hoja based on Issues na siyo kwenda kuongea kuongea umbea kisa unaongea Kiingereza.

      Umenibore sana kwa argument zako, kwani nyinyi ndiyo mnaoishia kuuza nchi kama wanavyofanya wenzako mdani ya serikali na chama. Nilitegemea umejiandaa lkn mmmmmmmmmh, yaani tofauti yako wewe na Lusinde hata sioni.

      Vipi, what is your area of competency? may be is not about trade and privatization.

    12. #49
      TIQO's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th January 2011
      Posts : 4,593
      Rep Power : 6851
      Likes Received
      1037
      Likes Given
      131

      Default Re: Ubinafsishaji: Why Mkapa was 1000% Right!

      Mkuu nyamaza kimyaa watu tuna machungu na sera za kupe huyo
      Mwisho wa Ubaya Aibu.

    13. #50
      W. J. Malecela's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 15th March 2009
      Posts : 4,511
      Rep Power : 0
      Likes Received
      2029
      Likes Given
      1819

      Default Re: Ubinafsishaji: Why Mkapa was 1000% Right!

      Quote By Mtazamaji
      Tatizo Mkuu unashindwa kutofautisha mambo . Hata Nyerere mweneywe alijua na alikubali kuwa ubinafisaji wa njia fulani ni muhimu.

      Wanachsema na kupigia kelele kina SHIVJI sio ubinafisaji pekee bali ni utaratibu wa ubinafishaji TBL kiwanda cha pombe ndio moja ya mifano inayotumika kuoyesha uznuri wa Ubinfassishaji

      Lakni vipi viwawada kama mfano vya kusindikiza ngozi (Mwanza Tanneries,Morogoro Tannnriesetc ) amabvyo
      • vimeuzwa kwa bei chee
      • Waliovinunua kwa mgongo wa ubinifsiahaji wametumia kupata mikopo tena humu humu nchini na hawajaviendeleza wamefanya maghala
      • Vingine ndio vimetumia hata kwenye Kagoda


      Ubinafsishaji haikuwa kosa . Kosa lingine ni conflict of interest. Pale wale wanaobinafisha wanataka wawe na "Hisa" Kwenye vitu wanavyouza.

      Yaani umempa mkapa 100% umesahau japo kuondoa 10% ya Kiwira ?????!!!!!!! Ebu Tuambie Mkapa alikuwa sawa kujiuzia Kiwira.
      - Kiwanda cha TBL kilikuwa kikiendeshwa kwa hasara, kodi ilikuwa Sillingi Billioni 1 tu kulinganisha na baada ya kuuzwa kinatoa kodi ya karibu Shillingi Billioni 40 kwa mwezi, Kiwira naomba uniambie ipi bora kujiuzia yeye na kutoa ajira na kodi kwa taifa au sasa kurudi kwenye serikali na kukaa bila kazi wala faida?

      William.

    14. #51
      JATELO1's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st October 2011
      Posts : 1,015
      Rep Power : 901
      Likes Received
      81
      Likes Given
      39

      Default Re: Ubinafsishaji: Why Mkapa was 1000% Right!

      Quote By W. J. Malecela
      - Usingeweza kukopeshwa Capital wakati huna uchumi, Soviet walishaanguka so hawakuwa tena na nguvu ya kusaidia anybody, mengine ni ya kawaida mtu anapokuwa hana hoja si unajua who you are dealing with by now right!

      William.
      kama bado unatetea huu upuuzi, sasa tuambie nini mafanikio ya hicho alichofanya Mkapa katika uchumi wa Tanzania?

    15. #52
      TIMING's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th April 2008
      Location : Roaming...
      Posts : 20,086
      Rep Power : 12252
      Likes Received
      6015
      Likes Given
      6851

      Default Re: Ubinafsishaji: Why Mkapa was 1000% Right!

      William J. Malecela....

      KUna kitu kimoja tunaambiwa kila siku kwamba when you plan something, always wend mawazo yako kwenye mwisho wa initiative, aangalia watakani, wafikaje huko na pia una nini

      If the unbinafsishaji ulikua right, basi ungekuja na preparations na sio kukurupuka; nafananisha habari yako na kile kisa cha abunuwasi ambaye baada ya kushiba sana, alikwenda kufukia chakula kilichobaki akiamini kwamba hataumwa njaa tena

      Hebu tukutane pale Tanganyika Packers ili tuongee tukiwa kwenye moja ya sites zilizoathiriwa na unplanned privatization

      MY ADVICE, FOR THE Nth TIME.... SOMA WILLIAM, HATA KAMA HAIKUA CULTURE YAKO BEFORE RETURNING HOME, KUBWABWAJA BILA UPEO NI NGUMU MKUU
      zumbemkuu likes this.
      .....Ana sifa zote, nzuri na mbaya!!!

    16. #53
      Albedo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th February 2008
      Posts : 4,978
      Rep Power : 1573
      Likes Received
      1077
      Likes Given
      555

      Default Re: Ubinafsishaji: Why Mkapa was 1000% Right!

      Quote By W. J. Malecela
      - Kiwanda cha TBL kilikuwa kikiendeshwa kwa hasara, kodi ilikuwa Sillingi Billioni 1 tu kulinganisha na baada ya kuuzwa kinatoa kodi ya karibu Shillingi Billioni 40 kwa mwezi, Kiwira naomba uniambie ipi bora kujiuzia yeye na kutoa ajira na kodi kwa taifa au sasa kurudi kwenye serikali na kukaa bila kazi wala faida?

      William.
      Sio Kujiuzia ni Kujipa
      "SISI SOTE NI NDUGU TATIZO NI CCM" Chris Lukosi kada wa CCM


    17. #54
      W. J. Malecela's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 15th March 2009
      Posts : 4,511
      Rep Power : 0
      Likes Received
      2029
      Likes Given
      1819

      Default Re: Ubinafsishaji: Why Mkapa was 1000% Right!

      Quote By TELO
      kama bado unatetea huu upuuzi, sasa tuambie nini mafanikio ya hicho alichofanya Mkapa katika uchumi wa Tanzania?
      - Leo Serikali inakusanya Shillingi Billioni 250 za kodi kwa mwezi kutoka mashirika manne tu CRDB, NBC, TBL na TCC as opposed na zile Shillingi Billioni 10 tu, kabla ya kubinafsishwa!

      William.

    18. #55
      Jasusi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th May 2006
      Posts : 10,625
      Rep Power : 2893
      Likes Received
      3844
      Likes Given
      12242

      Default Re: Ubinafsishaji: Why Mkapa was 1000% Right!

      Quote By W. J. Malecela
      - Kiwanda cha TBL kilikuwa kikiendeshwa kwa hasara, kodi ilikuwa Sillingi Billioni 1 tu kulinganisha na baada ya kuuzwa kinatoa kodi ya karibu Shillingi Billioni 40 kwa mwezi, Kiwira naomba uniambie ipi bora kujiuzia yeye na kutoa ajira na kodi kwa taifa au sasa kurudi kwenye serikali na kukaa bila kazi wala faida?
      William.
      Kiwanda cha bia TBL na kiwanda cha sigara havijawahi kuendeshwa kwa hasara. Actually hata kuna wakati Mwalimu alisema kuwa serikali ilikuwa inategemea zaidi kiwanda cha bia kwa fedha za matumizi yake. Tatizo la kiwanda cha bia lilikuwa ni management na si hasara. Bia ilikuwa haiivi na supply ilikuwa haikidhi demand. Actually walichofanya Makaburu baada ya akina Mwinyi kuwauzia ni wali flood soko la bia Tanzania na bia zao Castle, na hapo ndipo walipopata fedha za kukarabati mitambo ya TBL. Kaburu hakuweka hata senti tano ya Afrika kusini katika TBL wakati wa ubinafsishaji. Hii inaonyesha jinsi soko la bia Tanzania lilivyokuwa kubwa. Hata kama kilitoa kodi ya bilioni moja wakati huo. Hakikuendeshwa kwa hasara na kilisaidia kuendeshea matumizi ya serikali na faida ilikuwa inaingizwa serikalini.

      Eniwei, umeshakumbatia uwekezaji na ubinafsishaji sitaki kukuondoa huko. Lakini ukweli hubaki pale pale.
      Keil likes this.

    19. #56
      TIMING's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th April 2008
      Location : Roaming...
      Posts : 20,086
      Rep Power : 12252
      Likes Received
      6015
      Likes Given
      6851

      Default Re: Ubinafsishaji: Why Mkapa was 1000% Right!

      Quote By W. J. Malecela
      - Mimi ninasoma namuona mtu anaandika bila kusoma, ninampotezea maana nikimjibu wenye akili watashangaa sana!

      William.
      Sina cha kuongeza mkuu maana umenijibu, na it is simple and clear.... you are not ready, you are a sorry dude flipping around desperately kupayuka mada ambazo hujafanyia research za kutosha


      One can understand situation yako mkuu, umehonga ukaliwa pesa na ukashindwa; unajaribu kutafuta mileage kwenye platforms za kisiasa, ila huna upeo; umeishia kuchanganyikiwa na kuzidi kufunga macho na masikio lakini unataka watu wakusome na kukuelewa

      KWA JINSI ULIVYOKUJA NA KASI YA KUANZISHA THREAD, UNAKARIBIA KUFANANANA NA MALARIA SUGU, ALIKUA NAYE ANAKUJA NA HOJA HIVIHIVI, UBISHI, HOJA JUU-JUU NA MAJIBU YALIYOPELEA

      ALL THE BEST
      .....Ana sifa zote, nzuri na mbaya!!!

    20. #57
      sosoliso's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th May 2009
      Location : Mwembekiuno
      Posts : 2,817
      Rep Power : 17959
      Likes Received
      1607
      Likes Given
      1542

      Default Re: Ubinafsishaji: Why Mkapa was 1000% Right!

      Naona mkuu umeamua kuja kivingine sasa..!
      Nadhani Professor Shivji hakuwa anapinga sera za ubinafsishaji.. Kikubwa ni (na ambacho hata Mkapa mwenyewe alikiri na kujivua lawama) ufuatiliaji wa hivyo viwanda na mashirika yalivyouzwa.. Jee wanunuzi waliviendeleza kwa mikataba ile waliokubalina na serikali..? Na jee serikali ilifuatilia kujua viwanda walivyoviuza vinatumika kama mkataba unavyosema..? Na suala jingine ni uuzwaji wa bei za kutupa za viwanda, mashirika ya umma na mabenki..
      Cijui unajaribu kutengeneza au ku-achieve nini kwa ur last 2 posts bt ushauri mdogo tu.. angalia zicije zika-backfire na kukuharibia huko mbele ya safari..
      Jasusi likes this.

    21. #58
      engmtolera's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st October 2010
      Posts : 3,610
      Rep Power : 1332
      Likes Received
      780
      Likes Given
      655

      Default Re: Ubinafsishaji: Why Mkapa was 1000% Right!

      Quote By W. J. Malecela
      - Kiwanda cha TBL kilikuwa kikiendeshwa kwa hasara, kodi ilikuwa Sillingi Billioni 1 tu kulinganisha na baada ya kuuzwa kinatoa kodi ya karibu Shillingi Billioni 40 kwa mwezi, Kiwira naomba uniambie ipi bora kujiuzia yeye na kutoa ajira na kodi kwa taifa au sasa kurudi kwenye serikali na kukaa bila kazi wala faida?

      William.
      nilicho kuja kukigundua ni kwamba hawakutaka kuvisimamia viwanda vyetu ili iwawie rahisi kujiuzia,maana ktk hivyo wanavyomiliki usimamizi wake ni wa hali ya juu,tofauti na ilivyokuwa mwanzo

      angalia kapunga,dakawa,yaani ukienda dakawa unaweza kulia,nyerere alitaka eneo lile liwe la utafiti akajenga chuo na kunamajengo mazuri sana,akatengeneza shamba na vifaa vyote vya kilimo vikawekwa pale,lakini mwisho wa siku wanasiasa wakabadirisha matumizi,wakauziana na mwisho wa siku wakataka kupanda jatropha kapunga eneo ambalo lilikuwa likizarisha mpunga na kuwalisha hadi wachina(naima hili hulijui waulize wazee wakueleze kuwa tanzania tuliwahi peleka chakula cha msaada china kutoka kapunga na dakawa),lakini sasa hivi ndio hao watatu duniani kwa kuomba omba

      william hizi post usiwe unazileta ni kubwa sana kwako ktk kuzitengenezea hoja
      Jasusi and Keil like this.
      "The person who says it cannot be done should not interrupt the person doing it."

    22. #59
      Elisha Ray's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th March 2012
      Posts : 262
      Rep Power : 414
      Likes Received
      64
      Likes Given
      51

      Default Re: Ubinafsishaji: Why Mkapa was 1000% Right!

      Quote By W. J. Malecela
      Heshima mbele sana Wakuu wote JF, juzi nimeangalia kwa mshangao mkubwa sana the so called wasomi wetu wakiongozwa na Shivji, wakimshambulia Rais mstaafu Mkapa, kuhusu Ubinafsishaji, I mean let me say this:-

      - Mnyonge mnyongeni, lakini haki yake apewe, sijawahi kuwa a big fan wa siasa za Mkapa, lakini this one I must say with my clear mind kwamba he was 100% right, Shivji na wenzake wako not only wrong isipokuwa ni professionals cying babies, wamezoea kila Awamu huwapa ujumbe wa bodi na kamati kamati za mlo, sasa ikitokea aawamu kama ya Mkapa ikawanyima mlo, basi huanza kuiandama ile Awamu wee na vilio vyao vya machozi ya mamba, kumbe ni waongo wakubwa!

      - Mkapa was right kubinfsisha kwa the FACT ya kuyaondoa mashirika na viwanda vilivyokuwa vimeathirika na utawala unaofuata siasa za sera zilizoshindwa za Azimio la Arusha, utawala ulikuwa mbovu na uliokufa. Ili kujenga uchumi imara unahitaji kuwa na Capital, Markets, na Leadership, ambavyo vyote havikuwepo under mfumo wa Azimio la Arusha tulilokuwa nalo then, ambalo haliwa freindly na wageni kuja kuwekeza, kwa hiyo ilikuwa ni sawa kwa Mkapa, kuyauza na mengine kuwauzia wazawa ili yaweze kusimama na kuendelea tena. In the process Mkapa alibinafsisha mashirika na viwanda 330, 180 aliwauzia wazawa ambayo ni more than 50%, 23 tu aliwauzia wageni na 127 alitoa kwa ubia wa wageni na wazawa, matokeo yamekuwa Serikali kukusanya Shillingi Billioni 250 kwa mwezi kwa mashirika machache tu kama NBC, CRDB, TCC, na TBL as opposed to Shillingi Billion 10 tu zilizokuwa zikikusanywa kabla ya Mkapa kubinafsisha.

      - It is about time sasa Shivji na wenzake wakajitokeza kwenye nafasi za uongozi wa taifa ili tuone uwezo wao wa kufikiri kuliko kulia lia kwa kila awamu. Ni lini watajikita kwenye kutoa solutions badala ya kulaumu tu kila siku kwa sababu ya kukosa mlo? I mean hili taifa wengine tumechoshwa sana na hawa crying babies wasiokuwa na jipya zaidi tu ya kulilia defeated theories ambazo tumezijaribu na zimtufikisha hapa tulipo pabaya sana hili taifa.

      NINASEMA TENA KWENYE KUBINAFSISHA, MKAPA WAS RIGHT 100%, SHIVJI NA WENZAKE SHOULD APOLOGIZE KWA KUMSHAMBULIA MKAPA BILA SABABU KWENYE KIGODA!


      William.

      -
      Kimsingi nakubaliana na wewe mkuu kwamba ubinafsishaji ulikuwa sahihi. Lakini nionavyo mimi tatizo lilikuwa kwamba kulikuwa na element ya wizi na mtandao wa wizi mkubwa tu which came with the whole idea of privatisation. Kama hawa watu-Mkapa and co wangekuwa really genuine na kufuatilia the whole issue closely then tusingekuwa na matatizo yaliyopo lakini ilikuwa ni wizi uliojificha na ndio maana yameibuka matatizo ambayo ni lazima yatokee tu kutokana na hawa jamaa kuwa dishonest!! So kama viongozi wenyewe ni wezi unategemea nini kutoka kwa watu wengine? Si watakuwa hivyo hivyo tu na kuishia kula na hao hao viongozi na kuifikisha nchi pabaya kama ilivyo sasa? Hawa watu wasingekuwa wezi tusingekuwa na hali tuliyonayo. Wanaiba and yet wako mitaani wanatesa na kutubeza kama vile they were born into a royal family of some sort. And they don't care at all!!! Their days are numbered and the medicine is boiling in the kitchen ready to treat these cancerous creatures as they can not heal themselves! Sasa jamaa (Che Nkapa) alivoona anasakamwa pale kigodani akaja kwa hasira na swali "kwani toka 2005 kuna kiwanda gani kimeanzishwa?"
      engmtolera likes this.

    23. #60
      W. J. Malecela's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 15th March 2009
      Posts : 4,511
      Rep Power : 0
      Likes Received
      2029
      Likes Given
      1819

      Default Re: Ubinafsishaji: Why Mkapa was 1000% Right!

      Quote By Elisha Ray
      Kimsingi nakubaliana na wewe mkuu kwamba ubinafsishaji ulikuwa sahihi. Lakini nionavyo mimi tatizo lilikuwa kwamba kulikuwa na element ya wizi na mtandao wa wizi mkubwa tu which came with the whole idea of privatisation. Kama hawa watu-Mkapa and co wangekuwa really genuine na kufuatilia the whole issue closely then tusingekuwa na matatizo yaliyopo lakini ilikuwa ni wizi uliojificha na ndio maana yameibuka matatizo ambayo ni lazima yatokee tu kutokana na hawa jamaa kuwa dishonest!! So kama viongozi wenyewe ni wezi unategemea nini kutoka kwa watu wengine? Si watakuwa hivyo hivyo tu na kuishia kula na hao hao viongozi na kuifikisha nchi pabaya kama ilivyo sasa? Hawa watu wasingekuwa wezi tusingekuwa na hali tuliyonayo. Wanaiba and yet wako mitaani wanatesa na kutubeza kama vile they were born into a royal family of some sort. And they don't care at all!!! Their days are numbered and the medicine is boiling in the kitchen ready to treat these cancerous creatures as they can not heal themselves! Sasa jamaa (Che Nkapa) alivoona anasakamwa pale kigodani akaja kwa hasira na swali "kwani toka 2005 kuna kiwanda gani kimeanzishwa?"
      - Then tukubaliane kwamba sera ya kuuza mashirika na viwanda ilikuwa sawa kimsingi, sasa waetekelezaji nini kosa la Mkapa kwa hoja yako mkuu? Je tulitegemea Rais wa Jamhuri aache kazi zake wka taifa akasimamie ubinafsishaji?

      - I mean ninakubaliana na wewe kwamba kuna makosa makubwa yaliyotokea kwenye the process, lakini still the outcome bado no progressive sio kama the process isingfanyika!

      William.

    Page 3 of 4 FirstFirst 1234 LastLast

    Similar Topics

    1. Hawara wa zamani wa Ryan Giggs ajutia...
      By Rutashubanyuma in forum Celebrities Forum
      Replies: 2
      Last Post: 23rd December 2011, 07:31
    2. Ajutia kugawa namba ya simu
      By kilimasera in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 36
      Last Post: 18th January 2011, 03:15
    3. Mkapa vs kikwete
      By pcman in forum Tanzania 2010-2015
      Replies: 23
      Last Post: 23rd September 2010, 00:55
    4. Kikwete Vs. Mkapa
      By Mzee Mwanakijiji in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 9
      Last Post: 21st January 2008, 14:47

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...