Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Ubinafsishaji: Mkapa alikosea?

    Report Post
    Page 2 of 4 FirstFirst 1234 LastLast
    Results 21 to 40 of 73
    1. BAK
      #1
      BAK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2007
      Location : Mfaranyaki
      Posts : 26,586
      Rep Power : 44962
      Likes Received
      8327
      Likes Given
      8306

      Default Ubinafsishaji: Mkapa alikosea?

      Mkapa ajuta

      • Ahuzunishwa wageni kuhodhi uchumi

      na Mwandishi Wetu | Tanzania Daima~Sauti ya Watu

      RAIS mstaafu, Benjamin Mkapa, amesema anajutia kitendo chake cha kuliingiza taifa katika ubinafsishaji wa rasilimali bila ya kujiandaa kikamilifu na mabadiliko hayo.

      Mkapa alitoa majuto hayo katika mkutano ulioandaliwa na Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) uliofanyika Zanzibar wiki iliyopita katika Hoteli ya Zamani Kempinski na kuhudhuriwa na aliyekuwa Rais wa Afrika Kusini, Thabo Mbeki.

      Mbali ya Mbeki, viongozi wengine waliohudhuria mkutano huo ni Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara), Pius Msekwa na mwanasiasa mkongwe nchini, Kingunge Ngombale - Mwiru.

      Mmoja ya wajumbe waliohudhuria mkutano huo ambaye alizungumza na Tanzania Daima Jumapili kwa sharti la kutokutajwa jina lake, alisema Mkapa alikiri kuwa sera ya ubinafsishaji haijamsaidia kwa kiwango kilichotarajiwa Mtanzania na badala yake wamegeuka wageni katika rasilimali zao.

      Chanzo hicho kilidokeza kuwa Mkapa alibainisha kuwa kukubali kwake sera hiyo kulikuwa na lengo zuri la kuwafanya Watanzania waondokane na lindi la umaskini kupitia uwekezaji utakaofanywa katika rasilimali zao.

      “Alituambia sera ya ubinafsishaji inamuumiza mno, kwani alipoikubali hakutarajia kama ingeweza kuwafanya wageni wawe na sauti katika rasilimali za taifa kuliko wazawa kama ilivyo sasa,” kilisema chanzo hicho.


      Chanzo hicho kilibainisha kuwa Mkapa alifikia hatua ya kudai kuwa kama angepata nafasi ya kuwa kiongozi tena wa taifa hili angerekebisha sera ya ubinafsishaji haraka ili walau Watanzania waanze kufaidi rasilimali za nchi yao, badala ya kuwa mashuhuda wa wageni wanaoendelea kuneemeka na rasilimali za nchi.

      Alisema tatizo kubwa lililopo katika nchi za Afrika ni kutumia baadhi ya mambo wanayotakiwa kuyafanya na wafadhili au mifuko ya fedha, bila kuyafanyia tathmini ya kina ili kujua kama hayataleta madhara katika siku za usoni.

      “Mkapa alionyesha kujutia uamuzi alioufanya kwenye uwekezaji na aliweka wazi kuwa kama angeruhusiwa kurudi katika nafasi hiyo, basi jambo la kwanza kulirekebisha ni ubinafsishaji,” kilisema chanzo hicho.

      Mkapa katika utawala wake alibinafsisha mashirika mengi ya umma, ikiwemo Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa bei ya chini, kitendo ambacho kilizua malalamiko mengi kutoka kwa wananchi, pia alibinafsisha Shirika la Ndege Tanzania (ATC) na mengine mengi, kiasi cha kuzua malalamiko mbalimbali ndani na nje ya nchi.


      Aidha, katika utawala wake pia alilalamikiwa kwa kuwapendelea wawekezaji wa kigeni kuliko wazalendo, hasa katika sekta ya madini na kuingia mikataba mibovu ambayo hadi sasa imekuwa mzigo mkubwa kwa taifa, sambamba na wawekezaji hao kupata misamaha ya kodi kwa kigezo cha kuwavutia.

      Kuingia mikataba mibovu huku ndiko kulikomfanya Rais Jakaya Kikwete kuunda kamati ya kupitia mikataba ya madini na kutoa ushauri wa namna bora ya kushughulikia sekta hiyo.


      Majuto hayo ya Mkapa yanakuja huku kukiwa na shinikizo kubwa kutoka kwa baadhi ya wabunge na wananchi wakitaka afutiwe kinga yake ili aweze kushitakiwa kwa matumizi mabaya ya madaraka yake akiwa ikulu.

      Katika utawala wake, Mkapa anadaiwa kutumia madaraka yake kuanzisha miradi mbalimbali inayomhusu, ama kwa kupitia familia yake au ndugu zake, ukiwemo ule wa makaa ya mawe wa Kiwira, ambao hivi karibuni wamiliki wake wametajwa hadharani kwa mara ya kwanza.

      Chagizo la kutaka kutolewa kinga limezidi kupata kasi baada ya waliokuwa mawaziri wake, Basil Mramba (Fedha) na Daniel Yona (Nishati na Madini) na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Uchumi, Gray Mgonja, kufikishwa mahakamani kwa kosa la kulisababishia taifa hasara ya sh bilioni 11 kwa kutoa msamaha wa kodi kwa Kampuni ya M/S Stewart.

      Kinga ya Mkapa inaweza kuondolewa kama Bunge litapiga kura ya kutaka kutengua kinga hiyo, lakini ni lazima hoja hiyo iungwe mkono na theluthi mbili ya wabunge wote.
      Last edited by Silencer; 25th January 2009 at 06:53.
      nick mgongolwa likes this.
      Let your graceful words fly out into the World, carried on winds of courage, imagination and joy. Let them inspire others to step into action

    2. Miaka 50

    3. #21
      JokaKuu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st July 2006
      Posts : 6,820
      Rep Power : 2967
      Likes Received
      2424
      Likes Given
      3501

      Default re: Ubinafsishaji: Mkapa alikosea?

      wandugu,

      ..mashirika ya umma yaliuawa na wa-Tanzania wenyewe. matokeo yake yakawa ni mzigo kwa walipa kodi wa Tanzania.

      ..ubinafsishaji mimi nauchukulia kama TACTICAL RETREAT. kwamba ni hatua ya kurekebisha makosa na kujipanga upya.

      ..baada ya kuondokana na mzigo wa kutoa ruzuku kwa mashirika ya umma, na kuongeza bidii ktk kukusanya kodi, serikali sasa imeweza kutoa mchango mkubwa zaidi ktk miradi ya maendeleo kwa mfano ujenzi wa barabara.

      ..kwa upande mwingine sera ya ubinafsishaji siyo "maandiko matakatifu" yanayokataza serikali kuanzisha makampuni ya umma kama itaamua.

      ..naamini leo hii wa-Tanzania tuna nafasi nzuri zaidi ya kuanzisha makampuni ya umma, na kuyasimamia yasilitie taifa hasara na kuwa mzigo kwa wananchi.

    4. #22
      Capitol Hill's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th October 2007
      Location : U.S.A
      Posts : 747
      Rep Power : 741
      Likes Received
      34
      Likes Given
      119

      Default re: Ubinafsishaji: Mkapa alikosea?

      Binafsi nafikiri hii statement imekuja too late. Kwa kawaida viongozi wanapoondoka madarakani kwenye exit interviews zao na wanahabari au katika kuaga wananchi wao, huwa wana assess mafanikio yao na mapungufu yao. Lakini katika kujenga legacy zao huwa wanataja mafanikio zaidi kuliko mapungufu. Kwa kesi ya Mkapa, angeweza kuwaita journalists aliowahi kuwakandia na kuwaachia mwamuulize maswali. Hakuwa na hiyo courage. Yeye alikuwa yuko radhi kufanya interview na Riz Khan aliyekuwa CNN kuliko hawa local reporters wetu ambao pia nakiri wengi wao wanahitaji "msasa". Lakini that should have been a start.

      Pia alikuwa na venues nyingine. Kuna hotuba ya Rais, angeweza kusema naondoka na nina furaha kukabidhi utawala wa nchi kwa successor wangu kutoka kwenye chama changu, na mambo niliyoyafanya yanayonifanya nitoke kifua mbele ni x,y, na z. Na yale ambayo natamani ningeweza kuyafanya kwa ufanisi zaidi ni a,b, na c. Still he couldn't do that.

      Vile vile angeweza kutumia Sherehe za kiserikali kama za Muungano, Mei Mosi, na Uhuru kufikisha ujumbe...lakini aliona watanzania hawajui chochote na hawana haki ya ku muuliza maswali so pale criticism ilipoanza yeye akajificha na kukimbia nje ya nchi kwa excuses za kuwa mediator wa mgogoro wa Kenya na other international affairs. Lakini baada ya wananchi kuanza kupiga debe sana na hayo madebe kuwa echoed na actions za associates wake kufikishwa mahakamani, then he sees the need to speak about the weakness of his administration. Nafikiri ni too little, too late.
      FAIL EARLY, FAIL FAST, FAIL FORWARD

    5. #23
      Capitol Hill's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th October 2007
      Location : U.S.A
      Posts : 747
      Rep Power : 741
      Likes Received
      34
      Likes Given
      119

      Default re: Ubinafsishaji: Mkapa alikosea?

      Quote By JokaKuu
      wandugu,

      ..mashirika ya umma yaliuawa na wa-Tanzania wenyewe. matokeo yake yakawa ni mzigo kwa walipa kodi wa Tanzania.

      ..ubinafsishaji mimi nauchukulia kama TACTICAL RETREAT. kwamba ni hatua ya kurekebisha makosa na kujipanga upya.

      ..baada ya kuondokana na mzigo wa kutoa ruzuku kwa mashirika ya umma, na kuongeza bidii ktk kukusanya kodi, serikali sasa imeweza kutoa mchango mkubwa zaidi ktk miradi ya maendeleo kwa mfano ujenzi wa barabara.

      ..kwa upande mwingine sera ya ubinafsishaji siyo "maandiko matakatifu" yanayokataza serikali kuanzisha makampuni ya umma kama itaamua.

      ..naamini leo hii wa-Tanzania tuna nafasi nzuri zaidi ya kuanzisha makampuni ya umma, na kuyasimamia yasilitie taifa hasara na kuwa mzigo kwa wananchi.
      Swali kwako mkuu wangu, katika hii trial and error taifa la Tanzania limeingia hasara kiasi gani? Je tukifanya cost benefit analysis ya huu uwekezaji..tukachukua mashirika yote makubwa, je tuko better off leo hii, au ni bora tungeendelea kuyafadhili kwa fedha za Serikali na hivyo kuendelea kulibebesha taifa mzigo mzito wakati tukijifunza kutoka kwa wenzetu Benchmark (nchi zilizofanya ubinafsishaji successfully) na kufanya feasibility studies ya namna ya kuingia kwenye zoezi la ubinafsishaji?

      Nafikiri Administration iliyajua haya na these people did not do their homework. Hawakuwa na plan ambayo ilikuwa ni yenye manufaa kwa umma wa waTanzania. Plan yao ilikuwa ni ya wao (wachache) ku get wealthy quickly na kuachia regimes nyingine zije zi clean messy walizoziacha.
      FAIL EARLY, FAIL FAST, FAIL FORWARD

    6. #24
      Mkandara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd March 2006
      Location : T dot
      Posts : 13,770
      Rep Power : 7662
      Likes Received
      4929
      Likes Given
      4509

      Default re: Ubinafsishaji: Mkapa alikosea?

      FMES,

      Mkuu, wapo watu hutubu madhambi yao wakiwa mahututi kitandani (kina Nyerere) na wengine hutubu madhambi yao wakiwa kanisani (Mkapa)..wote wametubu mkuu wangu pamoja na kwamba makosa na madhambi yao hayalingani..hivyo tutawahukumu kulingana na makosa yao wengine watasameheka na wengine watakiona cha moto..

      Mkuu hapo juu nimeandika kwamba Nyerere hawezi kujutia Ujamaa kwa sababu objectives zake ni ktk kujenga society yetu (restoration of Africa's humanist and egalitarian principles of our society) kuondokana na adui wetu watatu.. UJINGA, UMASKINI na MARADHI based upon human dignity, respect and social justice kulingana na mazingira yetu..

      Mkuu ktk hotuba yake mwaka 1984 kabla ya kung'atuka, Nyerere mwenyewe ndiye aliye abolish strategic political functions ambazo zilikuwa primarily distributive badala ya kuwa productive..forceful applied badala ya re-asserts itself in a modern technical world - market economy..

      Lakini pamoja na kukubali kufungua milango alituonya kuwa uchumi wa haki ni lazima uendane na social development, na hatuwezi kufikia hayo ikiwa hakuna real socialisation of productive and distributive processes..Kwa hiyo Ujamaa bado upo pale pale..makosa yake sio malengo ya Ujamaa isipokuwa zile means to achieve the same ends!

      Ukitaka nakala zake nadhani watembelee HAKI ELIMU, hawa wana hotuba nyingi sana za mwalimu..
      Exploration of reality

    7. #25
      Field Marshall ES's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 27th April 2006
      Posts : 13,740
      Rep Power : 0
      Likes Received
      329
      Likes Given
      208

      Default re: Ubinafsishaji: Mkapa alikosea?

      - Mkuu Bob, nimekusikia sana nilichouliza ni kwamba unasema kuna mahali Mwalimu alikubali hadharani mbele yetu wananchi kuwa Ujamaa wake ulishindwa? Alisema exactly that au?

    8. FemaTV & Radio

    9. #26
      Mkandara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd March 2006
      Location : T dot
      Posts : 13,770
      Rep Power : 7662
      Likes Received
      4929
      Likes Given
      4509

      Default re: Ubinafsishaji: Mkapa alikosea?

      Jokakuu,
      Ubinafsishaji wa Mkapa ni sawa na yule Model - Miss Brazil aliyekatwa miguu na mikono kujaribu kumponya lakini matokeo yake amekufa..
      Leo hii wataalam wa maradhi yake wanasema hapakuwepo na haja ya kukatwa miguu wala mikono, maradhi yake yaliwezekana kabisa kutibiwa bila kumwondoa viungo!..
      Exploration of reality

    10. #27
      Mkandara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd March 2006
      Location : T dot
      Posts : 13,770
      Rep Power : 7662
      Likes Received
      4929
      Likes Given
      4509

      Default re: Ubinafsishaji: Mkapa alikosea?

      FMES,
      Kwani Mkapa kasema mbele yetu hadharani!..
      Exploration of reality

    11. #28
      JokaKuu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st July 2006
      Posts : 6,820
      Rep Power : 2967
      Likes Received
      2424
      Likes Given
      3501

      Default re: Ubinafsishaji: Mkapa alikosea?

      Quote By Capital Hill

      Swali kwako mkuu wangu, katika hii trial and error taifa la Tanzania limeingia hasara kiasi gani? Je tukifanya cost benefit analysis ya huu uwekezaji..tukachukua mashirika yote makubwa, je tuko better off leo hii, au ni bora tungeendelea kuyafadhili kwa fedha za Serikali na hivyo kuendelea kulibebesha taifa mzigo mzito wakati tukijifunza kutoka kwa wenzetu Benchmark (nchi zilizofanya ubinafsishaji successfully) na kufanya feasibility studies ya namna ya kuingia kwenye zoezi la ubinafsishaji?
      Nafikiri Administration iliyajua haya na these people did not do their homework. Hawakuwa na plan ambayo ilikuwa ni yenye manufaa kwa umma wa waTanzania. Plan yao ilikuwa ni ya wao (wachache) ku get wealthy quickly na kuachia regimes nyingine zije zi clean messy walizoziacha.
      Capitol Hill,

      ..kwanini tuangalie cost-benefit analysis ya yaliyopita, badala ya ku-focus on the future?

      ..tatizo lingine wananchi mnafanya cost-benefit analysis ya matatizo ya zamani ktk mazingira ya leo hii.

      ..ninavyoelewa mimi tulikuwa na hali mbaya sana kiuchumi na kifedha na ndiyo maana tukalazimika kuyabinafsisha mashirika ya umma.

      ..serikali imefanya iliyofanya, na tumefika mahali taifa lina uwezo wa kuchangia kifedha ktk miradi mbalimbali ya maendeleo.

      ..kwa msingi wa hoja hiyo hapo juu ina maana tunaweza ku-invest tena kwenye makampuni ya umma kama kuna ulazima huo.

      ..hakuna haja ya kuendelea kulalamika. kinachopaswa kufanyika ni kuchukua hatua za kurekebisha mapungufu na matatizo yaliyotokana na ubinafsishaji.

      NB:

      ..hakuna hatua yoyote ile ya uchumi ambayo itafanikiwa by 100%. kwa msingi huo kazi ya kurekebisha pale tulipokosea, na kuboresha zaidi pale tulipopatia, inapaswa kuendelea as long as we exist as a nation.

    12. #29
      JokaKuu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st July 2006
      Posts : 6,820
      Rep Power : 2967
      Likes Received
      2424
      Likes Given
      3501

      Default re: Ubinafsishaji: Mkapa alikosea?

      Quote By Mkandara

      Jokakuu,
      Ubinafsishaji wa Mkapa ni sawa na yule Model - Miss Brazil aliyekatwa miguu na mikono kujaribu kumponya lakini matokeo yake amekufa..
      Leo hii wataalam wa maradhi yake wanasema hapakuwepo na haja ya kukatwa miguu wala mikono, maradhi yake yaliwezekana kabisa kutibiwa bila kumwondoa viungo!..
      Mkandara,

      ..haitoshi kumlaumu Mkapa tu bila kuchukua hatua za kurekebisha makosa aliyoyafanya.

      ..tunafahamu kwamba mikataba yetu ya madini ina matatizo makubwa. kitu cha ajabu hatuiirekebishi tumeishia kumlaumu Mkapa tu.

      ..tuendelee kumzomea Mkapa na mafisadi, lakini pia tutumie the same efforts and energy kuipigia mayowe na kuishinikiza serikali iliyoko madarakani irekebishe mikataba ya madini.

      NB:

      ..hivi unafahamu kwamba Kikwete alimtimua kazi CEO[mtu wa mkapa] wa PSRC[taasisi ya ubinafsishaji] na kuweka mtu wake, ambaye ameendeleza madudu[ubinafsishaji wa TRC] yaleyale kama ya mtangulizi wake???

    13. BAK
      #30
      BAK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2007
      Location : Mfaranyaki
      Posts : 26,586
      Rep Power : 44962
      Likes Received
      8327
      Likes Given
      8306

      Default re: Ubinafsishaji: Mkapa alikosea?

      Quote By Mkandara
      Jokakuu,
      Ubinafsishaji wa Mkapa ni sawa na yule Model - Miss Brazil aliyekatwa miguu na mikono kujaribu kumponya lakini matokeo yake amekufa..
      Leo hii wataalam wa maradhi yake wanasema hapakuwepo na haja ya kukatwa miguu wala mikono, maradhi yake yaliwezekana kabisa kutibiwa bila kumwondoa viungo!..
      Ni kweli kabisa. Kurekebisha makosa yaliyofanyika na Mkapa katika sera zake za ubinafsishaji na kuwaleta wageni 'wawekeze' hakutafanikiwa bila kuyajua kwa undani matatizo yaliyotufikisha hapa tulipo ili marekebisho hayo yaweze kuzaa matunda ambayo Watanzania tunayategemea na pia kutorudia tena matatizo ya awamu ya tatu au hata ya nne.
      Let your graceful words fly out into the World, carried on winds of courage, imagination and joy. Let them inspire others to step into action

    14. #31
      Mkandara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd March 2006
      Location : T dot
      Posts : 13,770
      Rep Power : 7662
      Likes Received
      4929
      Likes Given
      4509

      Default re: Ubinafsishaji: Mkapa alikosea?

      Jokakuu,

      Swala la Mkapa kumlaumu litaendelea kuwepo, lakini binafsi nimemkubali tu pale alipoonyesha kwamba swala la mikataba yote ikiwa ni pamoja na madini inaweza kurekebishwa tofauti na viongozi au Kikwete alkivyokuwa akidai..

      Kwa hiyo hii ni hatua nzuri alochukua na nadhani imetokana na majuzi Bush alipokuwa akihojiwa amekubali baadhi ya makosa ktk Utawala wake, hivyo akaona umuhimu wa yeye pia kukubali makosa.... unajua tena sisi kwa kuiga.

      Tofauti inakuja tu kwamba wenzetu waliyaona haya mapema na wakamchagua mtu ambaye anaweza kurekebisha, wakati sisi ndio kwanza utawala mzima umeziba masikio na kusema kelele za mlangoni haziwazuii kulala..Hizi sio kelele tu ila mjenzi wa nyumba hiyo ametuhadharisha hatari iliyopo sio ya kelele za watu ila Uimara wa nyumba nzima...

      Ni mwanzo mzuri sana kiuchumi, na Mkapa mwenyewe ataendelea kulaumiwa kama Bush na utawala wake.
      Exploration of reality

    15. #32
      Capitol Hill's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th October 2007
      Location : U.S.A
      Posts : 747
      Rep Power : 741
      Likes Received
      34
      Likes Given
      119

      Default re: Ubinafsishaji: Mkapa alikosea?

      JokaKuu,

      nilichokuwa nasisitiza pale juu ni fact kwamba Serikali haiku plan vyema ubinafsishaji. Kama wangekuwa wamefanya kazi nzuri ya ku plan basi hii mikataba inayowanyonga watanzania ingeweza kuwa avoided. Lakini zoezi zima liliruhusu mianya ya rushwa na watu wachache wakataka kujinufaisha kwa haraka zaidi bila kujali effects za hiyo mikataba waliyoingia kwa niaba ya Taifa, miaka 10, 20 baadae.

      Naamini kama Mkapa and his regime wangechukua muda ku study zoezi zima la uwekezaji na kufanya mambo kwa uwazi, hali ingekuwa better kuliko sasa hivi. Sisemi kwamba tungekuwa tumefanikiwa 100% hapana, lakini kwa kiasi kikubwa tatizo la mikataba miref
      u, isiyo na manufaa kwa Serikali lingekuwa sio la magnitude kubwa kama sasa hivi.
      FAIL EARLY, FAIL FAST, FAIL FORWARD

    16. #33
      bm21's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th May 2008
      Location : Britain
      Posts : 777
      Rep Power : 718
      Likes Received
      2
      Likes Given
      15

      Thumbs up Re: Mkapa Ajuta: Ahuzunishwa na wageni kuhodhi uchumi

      Quote By Mzee Mwanakijiji
      zamani tulikuwa tunasema "gia ya kuingilia".. naamini hii ni mojawapo.., ya pili itakuwa ni kusikitikia wafanyakazi wa umma kujinufaisha kutokana na nafasi zao na atasikitika sana hawakuweza kusimamia maadili kwani waliamini kila mmoja ni mzalendo..

      Ha Ha ha mkulu mwanakijiji hii inahuhuzunisha vile vile inafurahisha. lakini pamoja na IMF na WB study nyingi za ndani zilikuwa zinaonyesha mashirika ya uma hayaperform na mapendekezo yakitolewa yabinafsishwe. Nakumbuka nilikuwa nafanya dissertation yangu kama partial fulfilment ya shahada yangu ya uchumi Bongo miaka hiyo na mpaka paper nyingi za Profs. wa bongo pia zilikuwa zikizumgumzia swala hilo hilo la ubinafsishaji. Pengine Mkapa kwa kusikiliza ushauri wakitaalam akaamua kutekeleza hilo.

      Kosa kubwa hapa ni namna zoezi la ubinafsishaji lilivyofanyika maana haukuwa ubinafsishaji bali redistribution ''come and take''. Hapo dnipo alipolikoroga sijui kama ilikuwa kwa kutojua au maksudi kutimiza mission fulani. nakwa hili nadhani PSRC pia inabidi iwajibike kwani ilipaswa kuwa na utaratibu endelevu wa kufanya ubinafsishaji na si kubinafsisha hata visivyobinafsishwa.

      May be muungwana anamaanisha kujutia hili ''Dramatugical!!!!!!!!!!!!!''

    17. #34
      Kidatu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th June 2008
      Posts : 1,430
      Rep Power : 1475
      Likes Received
      134
      Likes Given
      758

      Default re: Ubinafsishaji: Mkapa alikosea?

      Ya kweli haya ama Mkapa anatania?. Arudishe kiwira kwanza kwa watanzania ndipo tutaamini kwamba anajutia alichokifanya.

    18. #35
      Pasco's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 22nd September 2008
      Posts : 9,839
      Rep Power : 7368
      Likes Received
      6152
      Likes Given
      22273

      Default re: Ubinafsishaji: Mkapa alikosea?

      Quote By Bubu Ataka Kusema
      Pasco ni kweli ni hearsay, lakini tunaweza kufuatilia ili kuhakikisha je, kulikuwa na kikao kilichofanyika Z'bar kilichoandaliwa na UVCCM. Je, Thabo Mbeki hivi karibuni alikuwa Z'bar? kwa shughuli ipi? na je alihudhuria kikao cha UVCCM kilichofanyika Z'bar hivi karibuni? Je, Mkapa alikuwa Z'bar hivi karibuni? kwa shughuli ipi? Tukipata majibu ya maswali hayo ama tunaweza kuukaribia ukweli au kuzidi kuwa mbali nao.

      Sasa majina ya baadhi ya waliohudhuria kikao hicho yamewekwa hadharani. Basi ni wajibu wao kukanusha habari hii kama Mkapa hakutamka maneno hayo. Kukaa kwao kimya kuhusiana na habari hii ni ufisadi wa aina yake.
      Kwa vile news break imetolewa leo, naamini UVCCM watafanya Press Conference kesho na kukanusha hakuna kitu kama hicho kwenye mkutano wao. Kwa vile kilikuwa ni kikao cha siri, watasema Tanzania Daima ni waongo na story itaishia hapo.

      Kati ya marais wetu, hakuna rais sturborn kama Mkapa. Huyu jamaa hata kama kweli aliyasema hayo, he is too sturborn to addmit mistakes. Kwa waliowahi kuiona Hard Talk ya Mkapa na Tim Sebastian kwenye BBC watakumbuka alikasirika na kuvimba kama anataka kupigana. Kisa aliulizwa swali kuhusu ubinafsishaji was a mistake. Leo siamini ni Mkapa huyo huyo kaja kukubali eti "It was a mistake. Leys wait for the reaction"

      By the way, nimeipitia Katiba yetu na kugundua Mkapa hana kinga kwa hayo aliyotenda. Ibara ya 46 imempa kinga. Ibara ya 46.A (2)(a) imeiondoa kinga na kusema rais anaweza kushtakiwa kama amevunja katiba au kama amekiuka maadili ya uongozi.

      Hii maana yake Mkapa hajaburutwa Kisutu kwa sababu wanamstahi tuu na sio sababu ya kinga.

    19. #36
      Pasco's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 22nd September 2008
      Posts : 9,839
      Rep Power : 7368
      Likes Received
      6152
      Likes Given
      22273

      Default re: Ubinafsishaji: Mkapa alikosea?

      Quote By Lole Gwakisa
      Mkuu Pasco , pamoja na kuwa inawezekana kuwa ni hearsay laikini habari imeandikwa na haijakanushwa.
      Lets wait and see.
      Hata hivyo inaelekea the sentiments are geunine hata kama hazikuwa for public consumption.
      Mkuu Gwakisa, kwa vile habari ni ya leo tusubirie kesho. Uwezekano wa Mkapa kuyasema haya kwenye closed meeting upo ila yakitoka nje, siyo Mkapa atayekanusha ni UVCCM watakanusha tena ni kesho tuu. Mkapa mwenyewe ni kiburi na jeuri, he is too sturborn to addmit his mistakes.

    20. #37
      Mtarajiwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th February 2008
      Posts : 443
      Rep Power : 661
      Likes Received
      1
      Likes Given
      0

      Default re: Ubinafsishaji: Mkapa alikosea?

      Quote By Field Marshall ES
      - Mkuu Bob, nimekusikia sana nilichouliza ni kwamba unasema kuna mahali Mwalimu alikubali hadharani mbele yetu wananchi kuwa Ujamaa wake ulishindwa? Alisema exactly that au?

      Kwenye hotuba/press conference,sikumbuki katika tukio gani nyerere alisema 'tulifanya makosa,tulifanya makosa,hatukuwa malaika sisi,tulichukua nchi tukiwa na wasomi wachache,kama kitoto kilichotupwa baharini kinatapatapa,hakina msaada...lakini sasa hawa wenzetu wanaacha kuendeleza yale mazuri tuliyoyafanya wanachukua mabaya..'
      Halafu aliulizwa sikumbuki kama na BBC au la na sikumbuki vizuri swali lilikuwaje lakini muulizaji alitaka kujua kama nyerere angeweza kurudi tena na kuongoza tanzania,nyerere akasema kama alishindwa na ujamaa wake kwa miaka zaidi ya ishirini itakuwa wakati huu wa kuongoza kwa vipindi vya miaka mitano mitano..
      Kitu kama hicho.Wanaokumbuka vizuri watatufahamisha.

    21. #38
      Pasco's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 22nd September 2008
      Posts : 9,839
      Rep Power : 7368
      Likes Received
      6152
      Likes Given
      22273

      Default re: Ubinafsishaji: Mkapa alikosea?

      Quote By Kuhani
      Pasco,

      Hiki ki-habari cha TanzaniaDaima ni udaku mtupu. Mkapa ana soo la kubinafsisha mgodi na partner in crime wake Daniel Yona ana kesi mahakamani kuhusiana na haya haya ma hanky-panky ya dealings za serikali na wawekezaji, hawezi kujitia kitanzi kukiri makosa saa hizi.

      Sio principle za journalism tu, hata za stori za mtaani haziendi hivyo. Hivi tukiwa tunamtafuta Juma atujibu kuhusu mali zetu halafu tunakuja kuambiwa kuna fulani kasema Juma kakiri kosa, hatutataka kujua huyo fulani anaesema Juma katubu ni nani, na nani mwingine alisikia wakati anatubu? Halafu alipokubali makosa alisema nini kuhusu mali zetu going forward? You know?

      Halafu ki-habari kina misrepresent ukweli kwa kusema pressure ya kumshitaki Mkapa imeongezeka. Kila kukicha tunasikia padri so and so mbunge huyu na yule wanasema let this Mkapa character alone, sasa hiyo pressure iko wapi? Na Pinda keshapayuka kwamba it's a complicated process.

      Kinga yenyewe walivyoiongelea ni misrepresentation tupu. Hakuna sehemu kwenye Katiba paliposema Wabunge wanaweza kuondoa kinga. Itabidili Wabunge waandike kipengele hicho cha Katiba upya, na hiyo ndio itahitaji theluthi mbili za wabunge, tena inabidi ipatikane kote Zanzibar na Bara separately.

      Halafu Pasco, notice kwamba kwenye misingi journalism, ilibidi pale kwenye paragraph ya kwanza, au ya pili at the latest, waseme kwamba wanaripoti based on stori ya kuambiwa na anonymous source. Walivyoiweka ni kama wao Tanzania Daima ndio wanaripoti wakati hawana uhakika. Wakishitakiwa watasema sisi tumeambiwa na mtu, lakini hapa wameitengeneza kuwa-fool unwary readers kama wana uhakika vile. Wadaku.

      Halafu, notice vi-taarifa ambavyo hawana uhakika hawatoi jina la mwandishi, wanavunja cardinal rule of journalism, inayotakiwa kuleta credibility na accontability.

      Eti gazeti linaripoti kwa kuambiwa na mjumbe mmoja, udaku, uzushi, vilaza wakutupwa nje ya press room.
      Mkuu Kuhani, heshima mbele.
      Yote uliyasema ni kweli tupu, naomba tuwasamehe waandishi wetu wa habari, fani imevamiwa, ila hata ikivamiwa, ma editor nao wamevamiwa?. Hii ilikuwa kazi ya editor ku double chech na cross check hiyo story ili aibalance hata kiuongo uongo kwa just a line, 'juhudi za kumpata Mkapa kuthibitisha hazijazaa matunda sambamba na kuwapata maofisa wa UVCCM hawakupatikana'. Hii ilitosha kubalance na kuwathibitishia wasomaji, this is developing story na itaendelea.

      Hili la kinga ya Mkapa kutoshitakiwa, nimethibitisha kwa katiba halipo. Yaani hana kinga!.
      Natafuta muda muafaka nilianike vizuri tuu in black and white. Kinga sio issue, Pinda nae hana lolote, angesema tuu wazi, Mkapa ni binadamu, kwa heshima za Kiafrika/Kitanzania, tunawaheshimu wakubwa na wazee, hivyo Mkapa tunamstahi kwa heshima tuu na sio ka mujibu wa kinga Katiba.

    22. #39
      Pasco's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 22nd September 2008
      Posts : 9,839
      Rep Power : 7368
      Likes Received
      6152
      Likes Given
      22273

      Default re: Ubinafsishaji: Mkapa alikosea?

      Quote By Mtarajiwa
      Kwenye hotuba/press conference,sikumbuki katika tukio gani nyerere alisema 'tulifanya makosa,tulifanya makosa,hatukuwa malaika sisi,tulichukua nchi tukiwa na wasomi wachache,kama kitoto kilichotupwa baharini kinatapatapa,hakina msaada...lakini sasa hawa wenzetu wanaacha kuendeleza yale mazuri tuliyoyafanya wanachukua mabaya..'
      Halafu aliulizwa sikumbuki kama na BBC au la na sikumbuki vizuri swali lilikuwaje lakini muulizaji alitaka kujua kama nyerere angeweza kurudi tena na kuongoza tanzania,nyerere akasema kama alishindwa na ujamaa wake kwa miaka zaidi ya ishirini itakuwa wakati huu wa kuongoza kwa vipindi vya miaka mitano mitano..
      Kitu kama hicho.Wanaokumbuka vizuri watatufahamisha.
      Mwalimu alikubali makosa alipotangaza Azimio la Arusha alisema itatuchukua miaka 30 kuujenga ujamaa. Baada ya miaka 20 akakubali tulikosea, akasema itachukua muda mrefu kuujenga ujamaa, hata hivyo akasisitiza, kuna makosa mengi tumefanya huko nyuma ila nanukuu"Kufanya kosa si kosa, kosa ni kurudia kosa". Mwisho wa kunukuu.

    23. #40
      W. J. Malecela's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 15th March 2009
      Posts : 4,511
      Rep Power : 0
      Likes Received
      2029
      Likes Given
      1819

      Default Ubinafsishaji: Why Mkapa was 1000% Right!

      Heshima mbele sana Wakuu wote JF, juzi nimeangalia kwa mshangao mkubwa sana the so called wasomi wetu wakiongozwa na Shivji, wakimshambulia Rais mstaafu Mkapa, kuhusu Ubinafsishaji, I mean let me say this:-

      - Mnyonge mnyongeni, lakini haki yake apewe, sijawahi kuwa a big fan wa siasa za Mkapa, lakini this one I must say with my clear mind kwamba he was 100% right, Shivji na wenzake wako not only wrong isipokuwa ni professionals cying babies, wamezoea kila Awamu huwapa ujumbe wa bodi na kamati kamati za mlo, sasa ikitokea aawamu kama ya Mkapa ikawanyima mlo, basi huanza kuiandama ile Awamu wee na vilio vyao vya machozi ya mamba, kumbe ni waongo wakubwa!

      - Mkapa was right kubinfsisha kwa the FACT ya kuyaondoa mashirika na viwanda vilivyokuwa vimeathirika na utawala unaofuata siasa za sera zilizoshindwa za Azimio la Arusha, utawala ulikuwa mbovu na uliokufa. Ili kujenga uchumi imara unahitaji kuwa na Capital, Markets, na Leadership, ambavyo vyote havikuwepo under mfumo wa Azimio la Arusha tulilokuwa nalo then, ambalo haliwa freindly na wageni kuja kuwekeza, kwa hiyo ilikuwa ni sawa kwa Mkapa, kuyauza na mengine kuwauzia wazawa ili yaweze kusimama na kuendelea tena. In the process Mkapa alibinafsisha mashirika na viwanda 330, 180 aliwauzia wazawa ambayo ni more than 50%, 23 tu aliwauzia wageni na 127 alitoa kwa ubia wa wageni na wazawa, matokeo yamekuwa Serikali kukusanya Shillingi Billioni 250 kwa mwezi kwa mashirika machache tu kama NBC, CRDB, TCC, na TBL as opposed to Shillingi Billion 10 tu zilizokuwa zikikusanywa kabla ya Mkapa kubinafsisha.

      - It is about time sasa Shivji na wenzake wakajitokeza kwenye nafasi za uongozi wa taifa ili tuone uwezo wao wa kufikiri kuliko kulia lia kwa kila awamu. Ni lini watajikita kwenye kutoa solutions badala ya kulaumu tu kila siku kwa sababu ya kukosa mlo? I mean hili taifa wengine tumechoshwa sana na hawa crying babies wasiokuwa na jipya zaidi tu ya kulilia defeated theories ambazo tumezijaribu na zimtufikisha hapa tulipo pabaya sana hili taifa.

      NINASEMA TENA KWENYE KUBINAFSISHA, MKAPA WAS RIGHT 100%, SHIVJI NA WENZAKE SHOULD APOLOGIZE KWA KUMSHAMBULIA MKAPA BILA SABABU KWENYE KIGODA!


      William.

      -
      bucho likes this.

    Page 2 of 4 FirstFirst 1234 LastLast

    Similar Topics

    1. Hawara wa zamani wa Ryan Giggs ajutia...
      By Rutashubanyuma in forum Celebrities Forum
      Replies: 2
      Last Post: 23rd December 2011, 07:31
    2. Ajutia kugawa namba ya simu
      By kilimasera in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 36
      Last Post: 18th January 2011, 03:15
    3. Mkapa vs kikwete
      By pcman in forum Tanzania 2010-2015
      Replies: 23
      Last Post: 23rd September 2010, 00:55
    4. Kikwete Vs. Mkapa
      By Mzee Mwanakijiji in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 9
      Last Post: 21st January 2008, 14:47

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...