Ndugu wana JF,
Wakati tunaangalia kulia na kushoto ili kuifanya nchi yetu ipate viongozi yule ambaye kila mtu anamtaka , naona bado natatizwa na hiki kitu kinachoitwa ruzuku!
Ni kweli ruzuku itolewayo na serikali kwa vyama vya upinzani inaweza ikawa ni chachu ya mabadiliko nchini, lakini pia inaonekana kama ni chanzo cha matapeli wachache kuitumia vibaya, wengine kwa uroho tu, wengine wamekosa ajira na sababu nyingi zifananazo na hizo.
Napendekeza :
1. Ruzuku itolewe mwaka mmoja tu kwa vyama vinavyoanza;na kuwe na ufuatiliaji wa hali ya juu, juu ya matumizi ya hizo fedha au
2. Isitolewe kabisa, kwa sababu:
(a) Kila chama kizuri chenye sera nzuri kitakachowavutia wananchi ni dhahiri kitapata wanachama wazuri watakaohakikisha wanakitunza chenyewe na watu wake.
(b) Hali ya sasa hivi hata kama tutasema tunataka demokrasia ni dhahiri utitiri wa vyama hivi, unaleta
- Uadui kati ya wenyewe kwa wenyewe!
- Wengine kuona basi CCM iendelee tu maana vyama vingi vimeshajizolea umaarufu, aidha wataleta fujo na mara nyingi wanapigana kwa sababu ya fedha. N hii imeongeza hofu ya watu wengi kuwapigia kura hawa wapinzani.
- Kudhihirisha kuwa vyama vingi vinataka fedha tu, utavisikia wakati tunakaribia uchaguzi!!
Tukiwa na vyama ambavyo wananchi ndio wanaokiendesha, tutapata viongozi wanaowajali zaidi wananchi. Tutapata viongozi amabo hatima ya maamuzi yao ni kwa manufaa ya wananchi.
Kwa jinsi hii tutatengeneza akinaTsavangirai wetu akina Riala Odinga n.k
Viongozi wengi wa siasa hasa wapinzani , wawajabike wasiwajibike mwisho wa mwezi hela watapata tu.
Ni heri kupunguza vyama viwe vichache vya kiwananchi zaidi kuliko hali ya sasa. Afadhali hizo hela ziende mahospitalini n.k
Tukiangalia kwa undani sasa , hali hii ya kupewa ruzuku haitapelea vyama vya upinzani kushinda, sana sana tumeona migogoro ya ruzuku kila siku na watu kufanya ofisi za vyama kama vijiwe.
Pia kwa vyama vya siasa vikongwe, sijajua wana miradi gani, na wamewaza nini ili kupata income zao!
Naamini ubunifu wa kuoata hela kwa njia ya halali , ndio ubunifu huo utahitajika pindi watakaposhika nchi.
Naomba chama, haswa kile kinachoona kiko tayari kujiendesha kwa nguvu ya umma, kiwe cha kwanza kusema hatutaki ruzuku , hizo fedha ziende hospitalini!
Vyama vikishuka chini, vikawa havina hela na viongozi wake waanze kuishi maisha ya kulingana na fedha za wanachama, wala yasiyo ya kifahari. Hawa vingozi watakuwa viongozi wa kweli.
Baadhi ya vyama vya siasa tulivyonavyo kamanilivyopata kwenye wikipedia ni:
• Chama Cha Mapinduzi (Revolutionary State Party)
• Civic United Front (Chama Cha Wananchi)
• Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)
• Tanzania Labour Party
• United Democratic Party
• Chama cha Haki na Usitawi (CHAUSTA)
• Democratic Party (DP)
• Demokrasia Makini (MAKINI)
• Forum for the Restoration of Democracy (FORD)
• Jahazi Asilia
• National Convention for Construction and Reform-Mageuzi (NCCR)
• National League for Democracy (NLD)
• National Reconstruction Alliance (NRA)
• Popular National Party (PONA)
• Sauti ya Umma (SAU)
• Tanzania Democratic Alliance (TADEA)
• Progressive Party of Tanzania-Maendeleo (PPT-Maendeleo)
• Union for Multiparty Democracy (UMD)
• United People's Democratic Party (UPDP)
Naomba tujadili
wakatabahu
Waberoya
Update:
Msimamo wangu haujabadilika-2011 April
Msimamo wangu haujabadilika-2012 May

Reply With Quote




Follow Us Here