Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Je, wapinzani ni wakombozi?

    Page 4 of 26 FirstFirst ... 2345614 ... LastLast
    Results 61 to 80 of 509
    1. #1
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 29,518
      Rep Power : 46714
      Likes Received
      16434
      Likes Given
      8469

      Default Je, wapinzani ni wakombozi?

      Kuna baadhi ya watu ambao wanataka tuamini kuwa siku Tanzania ikichukuliwa na wapinzani basi matatizo yote ya Tanzania yatatoweka kama ukungu! Baadhi ya watu hawa, hawaishi kuonesha udhaifu wa chama tawala na serikali yake iliyoko madarakani. Ni watu hawa ambao kwao hakuna jema lolote, na hakuna kitu chochote kizuri ambacho kimewahi kufanywa na serikali iliyoko madarakani. Kwa watu hawa, ili kuweza kuona angalau kitu kizuri basi inabidi utumie darubini!!

      Baadhi ya watu hawa wameonesha uwezo mkubwa wa kuonesha matatizo na udhaifu wa chama tawala ambao hahuitaji darubini kuuona kwano ni dhahiri! Ni rahisi kwao kuonesha mapungufu ya masuala ya mikataba mbalimbali, tuhuma za rushwa n.k! Ni kwa sababu hiyo basi baadhi ya watu hawa pamoja na wapiga debe wengine wa upinzani wamefikia mahali pa kudai kwa ujasiri kuwa CCM na serikali yake havijafanya lolote la maana zaidi ya kutudidimiza kimaisha.

      Ukweli wa mambo ni kuwa hoja zao nyingi ni za msingi na mambo mengine ambayo wanayaonesha ni ya wazi ambayo hata mtu asiye mpinzani anaweza kuyaona! Kwa mtu yeyote anayeipenda nchi yetu hatuna budi kuwashukuru watu hao kwa moyo wao wa kizalendo na kujituma kufichua maovu na ufisadi! Siyo jukumu la watu hao peke yao na vyama vyao kuonesha ubaya, upotofu, na ubovu wa serikali iliyoko madarakani! Si vibaya kabisa kwa wao kwa kutumia mwanga kama wa kurunzi kuangazia umma na kuonesha kuwa baadhi ya viongozi au wafanyakazi wa serikali ni wabadhirifu, wanatumia madaraka yao vibaya, na baadhi yao wamefanya vitendo ambavyo vinapakana kabisa na usaliti kama siyo uhaini dhidi ya jamhuri yetu.

      Viongozi hawa walioko upinzani na wapambe wao wamejitahidi miaka nenda rudi tangu kurudishwa kwa mfumo wa vyama vingi kuiamsha Tanzania ili wananchi waelewe kuwa kuna chaguo jingine na kuna chama mbadala wa CCM. Walijaribu kwa mafanikio makubwa kwenye uchaguzi wa 1995 na kutokana na mvuto wa mmoja wa wapinzani hao aliyewahi kuwa madarakani basi watu waliamua kuachana na CCM na kujiunga na upinzani wakitumaini kuwa hapo "wamefika nyumbani" kwani CCM imewachosha! Lakini katika chaguzi mbili zilizofuata baadaye (2000 na 2005) vyama hivi vimeendelea kufanya vibaya licha ya majina yao na itikadi zao kueleka zaidi!

      Pamoja na kudidimia kwa vyama hivyo kwenye sanduku la kura, viongozi wao bado wanapita kunadi sera zao wakiangazia udhaifu na ubovu wa CCM kuwa ni sababu ya wananchi kuwaamini kuwa wapinzani ndio mbadala wa uhakika wa chama tawala, na hivyo wananchi waanze kuwaamini kwa kuwapa madaraka!

      Swali kubwa na la msingi ambalo kila Mtanzania hana budi kujibu ni kuwa, je wapinzani wakipewa madaraka ya nchi leo hii (siyo kupewa kama hisani bali kutwaa kwa nguvu ya kura) matatizo ya Tanzania yatatoweka ghafla? Je wapinzain wakiwa Ikulu hospitali zetu zote zitakuwa za kisasa, wanafunzi wote watakwenda shule, mishahara italipwa kwa wakati n.k n.k? Je wapinzani wakitwaa madaraka ina maana umasikini wa Tanzania utatoweka ndani ya mwaka mmoja?

      Kama mifano ya wapinzani kuchukua madaraka katika nchi jirani inaonesha lolote, basi mtu yeyote mwenye akili timamu ambaye anadhania kuwa endapo wapinzani watachukua madaraka basi maisha ya mwananchi wa kawaida yatakuwa ahuei na yatabadilika kwa ghafla mtu huyo adhanie tena! Ni mabadiliko gani ya kimaisha wananchi wa Kenya wameyapata baada ya NARC kuingia madarakani? Vipi kule malawi baada ya chama cha MDC kuingia madarakani watu wa Bulawayo, Lilongwe, Blantyre, na Karonga maisha yao yamebadilika vipi? Je wapinzani walipochukua madakaraka huko Zambia, maisha ya watu wa Lusaka, Copper Belt, na Capri Mposhi yamebadilika vipi?

      Wapinzani wameendelea kudai kuwa CCM imejaa watu wafisadi wasioipenda nchi yao, wenye kutumia madaraka yao vibaya, je wao wakiingia madarakani na kujaza nafasi zote za utawala kuanzia Rais hadi mwenyekiti wa kijiji watatuhakikishia vipi kuwa hakuna mtu kati mamia ya watumishi hao atakayekula rushwa au kutumia madaraka yake vibaya? Je tuna uhakika gani kuwa vyama vya upinzani vitaweza kumsimamia kila polisi, kila mwalimu, kila meneja, kila Mkurugenzi, kila mwenyekiti wa bodi n.k na kuhakikisha hakuna hata mmoja wao atakayemziba raia kibao hadharani au ambaye atafyatua bunduki yake na kumlipua mpiga debe?

      Kama kweli wapinzani wataahidi kufanya haya yote na kutokosea kabisa, kutoharibu hata mara moja, na wakiahidi kuondoa kero zote na matatizo yote yanayoikabili Tanzania huku viongozi wake wote (Rais hadi mwenyekiti kata wa kijiji cha Mkata) wakiwa waadilifu wasiomezwa na ulafi, wasiolewa madaraka wakitumikia nchi yao kwa mapenzi makubwa, basi Tanzania lazima iwachague wapinzani!! Kwani kwenye vyama vya upinzani hakuna binadamu wote ni Malaika, na wote hawajali matumbo yao wala mifuko yao!! Ni katika vyama hivyo yule Musa Nabii yupo, na ni yeye ndiye atakayetutoa utumwani!! Kama kweli vyama vya upinzani vitafanya mambo hayo yote basi ndugu zangu Watanzania, inawezekana mkombozi yupo katikati yetu na hatujamgundua!!

      Kwa kuelewa hulka za binadamu bila kujali itikadi zao na mitazamo yao kutegemea wapinzani kuwa wakombozi wa Tanzania kwa vile tu ni Watanzania wanaotoka Chadema, TLP, CUF, NCCR, au vyama vingine ni mategemeo ambayo yatapeperuka kama unyasi upeperushwavyo na upepo, ni kama umande unavyopukutika kwenye majani asubuhi inapofika! Manabii wa upinzani wako wapi watutabirie?
      Profesa and Mgibeon like this.
      [email protected]
      Tunapotaka kubadilisha watawala si kwa sababu tunataka kubadilisha sura; bali kubadilisha utawala! Yaani, tunataka kubadilisha jinsi tunavyotawaliwa siyo tu sura za wanao tutawala M. M. Mwanakijiji

    2. RukaaJuu Final

    3. #61
      Mkandara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd March 2006
      Location : T dot
      Posts : 13,770
      Rep Power : 7663
      Likes Received
      4929
      Likes Given
      4509

      Default

      Mwanasiasa,
      Well said.. Baabu kubwa kuhusu katiba umenipa shibe.
      Vipi, Chadema wamepisha tayari mchakato huu?..
      Exploration of reality

    4. #62
      Lunyungu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th August 2006
      Location : Malampaka
      Posts : 8,026
      Rep Power : 2563
      Likes Received
      788
      Likes Given
      28

      Default

      Kwako Mzee MKJJ
      Tukiwa tunapambana kujua namna gani Wapinzani wanaweza kuongezeka Bungeni wewe una madai kwamba hawakubaliki kwa Watanzania mimi nasema wanakubalika ila matumizi mabaya ya madaraka na wizi wa kura wa CCM ndiyo chanzo kikubwa hadi wao wana dorora soma hii report ni ya siku nyingi kidogo lakini haya haya yalitokea 2005 Oct japokuw watu hawakufa .


      http://www.hrw.org/reports/2002/tanzania/

    5. #63
      Kitila Mkumbo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th February 2006
      Posts : 3,919
      Rep Power : 6962
      Likes Received
      1066
      Likes Given
      35

      Default

      Quote By Mkandara
      Mwanasiasa,
      Well said.. Baabu kubwa kuhusu katiba umenipa shibe.
      Vipi, Chadema wamepisha tayari mchakato huu?..
      Kwa kweli sina uhakika kama umewahi kupitiwa kama chama. Ila najua wanachama wengi hasa viongozi wana subscribe na huu mchakato. CCM wao walishaukataa kwa kusema kuwa una mlolongo mrefu na kwamba katiba ya sasa inatosheleza isipokuwa inahitaji mabadiliko ya hapa na pale!
      A Struggle Without Casualties is No Struggle-Steve Biko

    6. #64
      Mkandara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd March 2006
      Location : T dot
      Posts : 13,770
      Rep Power : 7663
      Likes Received
      4929
      Likes Given
      4509

      Default

      Mwanasiasa,

      Nadhani utaona kuwa nimekuwa very fair ktk mjadala mzima na pengine naweza kukushukuru sana wewe.
      1. Swala la matumizi ya helikopta wakati wa uchaguzi nimelikubali kutokana na maelezo marefu ya ndugu J J. Mnyika. Sirudi huko tena ila tunasonga mbele na hili jipya la matumizi ya helikopta tena, jambo ambalo limewakimbiza baadhi ya wanachama.
      2. Elimu, Afya na Ustawi wa Jamii umechukua 5 zangu pamoja na kwamba hukunieleza zaidi jinsi gani utaweza kugawa bugdet ya serikali.. Unapoongeza fedha wizara fulani ni lazima upunguze matumizi wizara fulani. Je, ni zipi zinazotegemea kupungua budget yake na kwa nini?
      3. Swala la kubadilisha katiba umenipa dawa safi iliyopimwa! ila tu hukugusia upande wa Zanzibar!..
      4. Majimbo?... bado kabisa
      5. Swala la ndoa na Conservative.... bado!
      Hadi hapa nadhani tupo pamoja na yote haya ni ktk kuelimishana.
      Last edited by Mkandara; 14th January 2007 at 04:55.
      Exploration of reality

    7. #65
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 29,518
      Rep Power : 46714
      Likes Received
      16434
      Likes Given
      8469

      Default

      Lunyungu, sijasema wapinzani hawakubaliki, nimesema hawajajifanya waonekane wanahitajika (relevance). Ndio maana swali la msingi la mada hii hapa ni "Wapinzani ni Wakombozi"? Ni mpaka wafanye watu wawaone kweli wanawahitaji wasitarajiekupata viti vingi bungeni. Jinsi gani wanajifanya kuwa wanahitajika?

      Kwa maoni yangu, siyo kwa kuonesha mapungufu ya CCM au serikali yote, kwani kila mtu anayajua na matatizo ya wananchi chini ya serikali ya CCM ni dhahiri. Huhitaji kuwa mwanasayansi kuweza kuyafahamu.

      Mimi na wengine ambao tunaangalia kutoka nje (ya CCM na Upinzani) bado hatujaona mvuto wa upinzani zaidi ya kuipinga CCM. Upinzani lazima uwe zaidi ya kupinga na kukosoa, lazima wawe wanatuonesha kuwa wanaweza kuongoza na kutawala. Hadi hivi sasa binafsi sijawa impressed kuwa Tanzania inaweza kuwapa uongozi wa nchi wapinzani na matatizo yetu yatakwisha. Matatizo ya Kenya yamekwisha sababu NARC wako madarakani? Je, matatizo ya Zambia yamekwisha? vipi Malawi? Wapinzani watafanya nini zaidi kuliko kile ambacho kinaweza kufanywa au kimefanywa na CCM.
      [email protected]
      Tunapotaka kubadilisha watawala si kwa sababu tunataka kubadilisha sura; bali kubadilisha utawala! Yaani, tunataka kubadilisha jinsi tunavyotawaliwa siyo tu sura za wanao tutawala M. M. Mwanakijiji

    8. Miaka 50

    9. #66
      dondola's Avatar
      Member Array
      Join Date : 14th November 2006
      Posts : 50
      Rep Power : 651
      Likes Received
      3
      Likes Given
      0

      Default

      Quote By Mzee Mwanakijiji
      Mimi na wengine ambao tunaangalia kutoka nje (ya CCM na Upinzani) bado hatujaona mvuto wa upinzani zaidi ya kuipinga CCM. Upinzani lazima uwe zaidi ya kupinga na kukosoa, lazima wawe wanatuonesha kuwa wanaweza kuongoza na kutawala. Hadi hivi sasa binafsi sijawa impressed kuwa Tanzania inaweza kuwapa uongozi wa nchi wapinzani na matatizo yetu yatakwisha. Matatizo ya Kenya yamekwisha sababu NARC wako madarakani? Je, matatizo ya Zambia yamekwisha? vipi Malawi? Wapinzani watafanya nini zaidi kuliko kile ambacho kinaweza kufanywa au kimefanywa na CCM.
      Vyema kabisa! Hawawezi kufanya kitu kwa vile hawajaelimika, na jamii nayo haijaelimika. Na hili ni tatizo la sub-sahara nzima. Kuna watu wanaongelea faida za upinzani kwa kulinganisha na Republican-Democrats au Labour-Conservatives, etc, sio vyema kulinganisha namna hiyo kwani Republicans+Democrats etc, ni watu walewale wanaoelewa wajibu wao, jamii ileile iliyoelimika. Sasa kwa hawa wapinzani wetu wanaogombea ruzuku au tuwaonao kila kukicha wakirudi CCM ili kuongeza ulaji, ni wapinzani kweli?

      Kwa mazingira ya sub-saharan Africa ya leo, 'wapinzani wa kweli' ni wale walioamua kujikita kwenye kuelimisha jamii kwa NGO kama za Elimu, afya, wanaojenga mashule na hospitali, etc. Kwani ni kupitia huko ndio jamii itaelimika na kuweza kujua nini inahitaji kwa mustakabali wake kuliko hawa matapeli fisadi wanaopigana vikumbo kuingia ikulu.
      Thin line between creativity and madness

    10. #67
      Lunyungu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th August 2006
      Location : Malampaka
      Posts : 8,026
      Rep Power : 2563
      Likes Received
      788
      Likes Given
      28

      Default

      Vikwazo je toka kwa Serikali zilizoko madarakani ? Maana wakijua wanapigwa bao wana anza kubadili sheria .It has happened in Tanzania the last 3 years ama mimi nakosea kukumbuka?

    11. #68
      dondola's Avatar
      Member Array
      Join Date : 14th November 2006
      Posts : 50
      Rep Power : 651
      Likes Received
      3
      Likes Given
      0

      Default

      Quote By Lunyungu
      Vikwazo je toka kwa Serikali zilizoko madarakani ? Maana wakijua wanapigwa bao wana anza kubadili sheria .It has happened in Tanzania the last 3 years ama mimi nakosea kukumbuka?
      Ni kweli wanawekewa vikwazo (e.g. HakiElimu), ila kuwekewa kwao vikwazo ni uthibitisho tosha kuwa wao ndio wapinzani wenyewe ambao jamii zetu zinawahitaji sasa. Kama watu wanaweza kupaza sauti kushinikiza serikali kwenye mambo kama ya kulilia ruzuku, kuibiwa kura n.k. Hizo sauti zingetakiwa haswa ziishinikize serikali ili wapinzani wa kweli wanaowekeza kwenye maendeleo ya jamii wafanye kazi zao bila vikwazo.
      Thin line between creativity and madness

    12. #69
      Mkandara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd March 2006
      Location : T dot
      Posts : 13,770
      Rep Power : 7663
      Likes Received
      4929
      Likes Given
      4509

      Default

      Dondola,
      Kwa mazingira ya sub-saharan Africa ya leo, 'wapinzani wa kweli' ni wale walioamua kujikita kwenye kuelimisha jamii kwa NGO kama za Elimu, afya, wanaojenga mashule na hospitali, etc. Kwani ni kupitia huko ndio jamii itaelimika na kuweza kujua nini inahitaji kwa mustakabali wake kuliko hawa matapeli fisadi wanaopigana vikumbo kuingia ikulu.[
      Hii ndiyo Miujiza ya Mussa na Yesu... sijui kwa nini inaonekana kuwa lugha ngumu sana.

      Lunyungu,
      Hata Manabii wetu hawakukuta barabara ya lami.. walihenya na kupambana na kilai ufedhuli wa Binadamu pamoja na kwamba wao walikuwa Mitume. Msitegemee kabisa kuwepo kwa ulaini.. Siasa kama Dini ni mchezo mchafu ingawa malengo yake ni kuwakomboa haohao binadamu.
      Exploration of reality

    13. #70
      Nyangumi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th January 2007
      Posts : 593
      Rep Power : 752
      Likes Received
      5
      Likes Given
      1

      Default

      Dondola amegusia kitu sahihi kabisa.Mie naami si wanamageuzi wote ni wabovu lakini wanafukikwa na kuchafuliwa na wanamageuzi koko.hivyo basi sehemu kubwa ya watanzania wanashindwa kuwakubali ipasavyo. Upinzani lazima pia usisahau kuwa watanzania wengi wana uvivu wa kufikiri, ukiongeza na umaskini ambao unafanya watumie 99.9% ya muda wao kufikiri jinsi gani ya kuishi, wanahitaji kuwa approached na mbinu zilizokomaa. Wanahitaji kuonyeshwa tofauti kati ya CCM na upinzani kwa vitendo na si kwa maneno .Mfano; Pesa alizotumia M/kiti wa Chadema zingetumika kununua matrekta na pembejeo nyingine za kilimo na tumia katika vijiji watakavyoviteua na kuwa kama miradi ya Chadema kuwalimia wananchi kwa gharama nafuu na kisha kuwatafutia masoko ya mazao yao kwa bei nafuu.Tofauti watakayoiona katika kipato chao itasaidia kuwafanya waamini nini watafanyiwa.Pia upinzani kwa ujumla uelekeze nguvu ktk kuchukua majimbo na si urais.Hizi mbinu za wizi wa kura hazitafua dafu pale watanzania watakapokuwa tayari kuupokea upinzani kwa kishindo.
      Last edited by Nyangumi; 15th January 2007 at 20:47.

    14. #71
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 29,518
      Rep Power : 46714
      Likes Received
      16434
      Likes Given
      8469

      Default

      Nyangumi, hicho ndicho CCM imejaribu kufanya.. nacho ni kushika hatamu na utamu wa nchi!! Wao wanajenga, wao wananunua, wanalima na kuvuna!! Mwananchi wa kawaida hahitaji kufanyiwa kila kitu. Tunachohitaji ni kujengewa mazingira mazuri ambapo soko linatuamulia nani afanye nini. Nimeshaeleza toka huko nyuma ni nini wapinzani wafanye. La kwanza, wawe majasiri kusema:

      a. Upinzani ukichukua madaraka itaundwa tume huru itakayochunguza mali zote ambazo viongozi waliopita walichuma wakiwa madarakani na kuoanisha na mapato yao. Wale itaoonekana mapato yao hayawiani na mali zao basi mali zao zitafilisiwa! Wasema watalifanya hilo ndani ya miezi sita ya mwanzo ya utawala wao.

      b. Wapinzani wawaambie wananchi kuwa kila kijana wa Kitanzania aliyefaulu kwenda chuo Kikuu Serikali itagharimia nusu ya ada zao na matumizi. Anayepata daraja la kwanza kila mhula analipiwa 75% Wanaoenda shahada ya uzamili watalipiwa 75% na wa shahada ya Udaktari 100% Hii ni kuonesha kuwa upinzani unatilia maanani elimu. Na kwenye hilo la Elimu Wapinzani waseme chini ya uongozi wao, Elimu ya Msingi hadi ya Sekondari (O'Level) itakuwa ni ya bure!

      Pia waamue kusema kuwa yeyote anayetaka kusomea Udaktari (Utibabu) analipiwa gharama zote! (nafikiri CCM inafanya kitu kama hiki).

      c. Wapinzani waweke wazi kuwa pindi wakichaguliwa, watasitisha mara moja mikataba yote ya Nishati na Madini na kurenegotiate na kampuni yoyote ambayo inataka kuendelea kufanya kazi Tanzania. Katika kufanya hivi wawaambie wananchi kuwa Serikali hiyo mpya itawachunguza viongozi wote waliohusika na mikataba hii na wale ambao walinufaika kwa namna yoyote ile watafikishwa mahakamani kwa ufujaji wa mali ya umma.

      d. Wapinzani wawahakikishie wananchi kuwa Watadumisha Muungano wetu na umoja wetu wa kitaifa! Hakuna mabadiliko yoyote ya mfumo au utendaji kazi wa Muungano yatakayofanywa pasipo ridhaa ya wananchi.

      Hayo ni machache ya kuanzia!
      [email protected]
      Tunapotaka kubadilisha watawala si kwa sababu tunataka kubadilisha sura; bali kubadilisha utawala! Yaani, tunataka kubadilisha jinsi tunavyotawaliwa siyo tu sura za wanao tutawala M. M. Mwanakijiji

    15. #72
      Nyangumi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th January 2007
      Posts : 593
      Rep Power : 752
      Likes Received
      5
      Likes Given
      1

      Default

      Hayo ni sahihi Mwanakijiji,lakini yanaingia kwa watu walikwenda shule.Tunapokuja kwa watanzania ambao sehemu kubwa wanaishia darasa la saba hiyo kwao inakuwa ngumu.Nakupa mfano.Kuna mbunge mmoja wa CCM kule KIbondo,(nimemsahau jina)alichofanya alitafuta soko la kahawa la wananchi wake. Pili, pesa anayopewa ya shangingi na baadhi ya posho zake kwenye hospitali.Wananchi kule walikwishasema hawataki mtu mwingine na huyo ni mbunge wao wa maisha.Akihama chama nao wanamfuata.

    16. #73
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 29,518
      Rep Power : 46714
      Likes Received
      16434
      Likes Given
      8469

      Default

      Nyangumi, akifa je nao watajiua? Kiongozi anayefanya hivyo ameshindwa kuongoza!!
      [email protected]
      Tunapotaka kubadilisha watawala si kwa sababu tunataka kubadilisha sura; bali kubadilisha utawala! Yaani, tunataka kubadilisha jinsi tunavyotawaliwa siyo tu sura za wanao tutawala M. M. Mwanakijiji

    17. #74
      Nyangumi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th January 2007
      Posts : 593
      Rep Power : 752
      Likes Received
      5
      Likes Given
      1

      Default

      Akifa watampata atakayewafaa.Hata Yesu aliwalisha samaki na mikate watu waliokuja kumsikiliza.Hivyo aliwaweka fiti kimwili ili waweze ku-concentrate kwenye mahubiri yake.

    18. #75
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 29,518
      Rep Power : 46714
      Likes Received
      16434
      Likes Given
      8469

      Default

      yeah.. baada ya kula akawaambia nenda mkavue samaki!!!
      [email protected]
      Tunapotaka kubadilisha watawala si kwa sababu tunataka kubadilisha sura; bali kubadilisha utawala! Yaani, tunataka kubadilisha jinsi tunavyotawaliwa siyo tu sura za wanao tutawala M. M. Mwanakijiji

    19. #76
      Nyangumi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th January 2007
      Posts : 593
      Rep Power : 752
      Likes Received
      5
      Likes Given
      1

      Default

      Sio kweli.Ila kwa huyu mbunge, baada ya wananchi kupata matibabu aliwaambia nendeni mkalime,mimi nitawatafutia soko la zuri la mazao yeni lisilo na ulaji wa vyama vya ushirika.Zaidi kibondo wanalisha Mwanza na Shinyanga na Kagera.

    20. #77
      Mkandara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd March 2006
      Location : T dot
      Posts : 13,770
      Rep Power : 7663
      Likes Received
      4929
      Likes Given
      4509

      Default

      Mzee Mwanakijiji,

      Mzeee chagua mji!...haya ndiyo maneno napenda kuyasikia toka kwa Freeman!..
      Atachukiwa na wengi lakini sio walalahoi na hawa ndio wapiga kura!

      Unajua mzee siku hizi kuna masoko yameanzishwa yanaitwa Fair Trade?..Sidhani kama wakulima wa Bongo wameisha yashitukia... kahawa inanunuliwa kwa bei nzuri kuliko ile ya soko la dunia na hivi sasa makampuni mengi sana yamejiingiza kununua kahawa hizi kuzisaidia nchi maskini na hasa za Afrika. Tim Hortons, Starbucks ni mojawapo zilizojiunga ktkmashirika haya ya Fair trade... wenzetu nchi kama Kenya na Ethiopia wameisha ingia. Globalexchange ni moja ya wanunuzi wakubwa wa kahawa toka nchi maskini moja kwa moja toka kwa wakulima.
      Kwa hiyo Chama kama Chadema (chenye wasomi) kinatakiwa kutafuta vitu kama hivi na kuwapa wakulima somo ama ushauri wa bure.
      Exploration of reality

    21. Dua
      #78
      Dua's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th November 2006
      Posts : 3,534
      Rep Power : 1365
      Likes Received
      9
      Likes Given
      0

      Default

      Mkandara

      Hawa Starbuck wana ugomvi mkubwa sana na Ethiopia, CEO wa Starbuck alikwenda Addis ili kuweka makubaliano ya kumiliki nembo ya kahawa na hakuna suluhisho mpaka alipoondoka kwa sababu Ethiopia wamekataa udhalimu wa hii kampuni.

      Sakata hili bado halijapata ufumbuzi................

      Nitajaribu kupata hiyo story kutoka hapa UK
      Dua la kuku halimpati mwewe

    22. Dua
      #79
      Dua's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th November 2006
      Posts : 3,534
      Rep Power : 1365
      Likes Received
      9
      Likes Given
      0

      Default

      Starbucks in Ethiopia coffee row

      Starbucks says it has programmes in place to help farmers
      US coffee chain Starbucks is denying Ethiopia earnings of £47m ($88m) a year, according to Oxfam.
      The UK charity says Starbucks asked the National Coffee Association (NCA) to block the country's bid to trademark three types of coffee bean in the US.

      Oxfam says poor farmers would have benefited from the move but the NCA says there is no economic case to support the charity's claims.

      Starbucks denies initiating opposition to the trademark application.

      'Backwards step'

      The Ethiopian government filed its applications to trademark its most famous coffee bean names - Sidamo, Harar and Yirgacheffe - in US courts last year.

      This particular scheme is going to hurt the Ethiopian coffee farmers economically

      Robert Nelson
      NCA

      Oxfam claims that Starbucks flagged up the application to the NCA - of which the firm is a leading member.

      The NCA then filed its opposition at the US Patent and Trademark Office.

      Oxfam's Phil Bloomer said the charity had worked with Starbucks in the past and appealed to the firm to "act responsibly".

      "Their behaviour on this occasion is a huge backwards step and raises serious questions about the depth of their commitment to the welfare of their suppliers," he said.

      Berhanu Kebede, Ethiopia's ambassador to the UK, said in a statement that the international community should support the country's efforts to ensure farmers got a fair reward for their hard work.

      "This campaign has a pivotal role in redressing the unfairness of the international trading system," he said.

      'Reduce demand'

      Starbucks' senior vice-president of coffee procurement, Dub Hay, denied approaching the NCA to oppose the Ethiopian move.

      "We did not get the NCA involved - in fact it was the other way around, they contacted us."

      Robert Nelson, head of the NCA, backed Mr Hay's claim, adding that his organisation opposed the Ethiopian move for economic reasons.

      "For the US industry to exist, we must have an economically stable coffee industry in the producing world," he said.

      "This particular scheme is going to hurt the Ethiopian coffee farmers economically."

      He claimed that the Ethiopian government was being badly advised, and the move would price them out of the market.

      The trademark move would also reduce demand for the country's coffee, he said.

      Oxfam said the NCA and Starbucks should not dictate to Ethiopia how best to sell its products.
      Link ya hii news iko hapa:http://news.bbc.co.uk/1/hi/world/africa/6086330.stm
      Dua la kuku halimpati mwewe

    23. #80
      Mkandara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd March 2006
      Location : T dot
      Posts : 13,770
      Rep Power : 7663
      Likes Received
      4929
      Likes Given
      4509

      Default

      Dua, hilo sakata nimelisikia toka kwa rafiki yangu mchumi Mu-ethiopia!...
      Sasa hapa ndio pima akili ya mwafrika utajua kuwa mengi tunafanya kuiga tu.
      Wewe mnagombana na kampuni kubwa kwa sababu ya nembo tu. Pili, KULA ya tradefair inakwenda moja kwa moja kwa mkulima haipitii viongozi waserikali yaani hapo hakuna 5%.. mwafrika anatafuta njia za kupinga. Tazama kahawa ya Columbia pamoja na kupewa majina mengi na kutumika kwa kila kampuni duniani yenye trademark zao jinsi inavyotamba!.
      Tena basi Starbucks waliipamba kahawa ya Ethiopia kishenzi na wazungu leo wanaamini kabisa kuwa kahawa ilivumbuliwa Ethiopia kutokana na matangazo ya Starbucks!..
      Wee unajua kabisa kuwa waafrika hatujui kujitangaza wala fedha hiyo hatuna kwani kutangaza tu kwa mwaka ni budget nzima ya nchi.
      Leo umepewa nafasi ya kuendelea kuzalisha wewe kisha mtu atumie jina lake kuitangaza mali yako mswahili unaona umeibiwa hali China wanatumiwa na makampuni yote duniani kutengeneza vitu kwa majina, trademark na kadhalika. Ethiopia wamesajili kweli majina ya hizo kahawa zao lakini kahawa bila matangazo na mkono wa mzungu huwezi kuuza America..Utakuja nambia kama baada ya miaka kumi ijayo hukusikia wenyewe wananyoosha mikono tena basi safari hii Starbuck atakuwa akimiliki mashamba yenyewe!.. Maskini siku zote jeuri sana lakini NJAA humfanya akala matumbo yake kama fisi.
      Starbuck sasa hivi wanaonekana waongo kwa kuwalemba ethiopia kwa miaka yote na kuna watu wanaanza ku-question. http://www.poorfarmer.blogspot.com/
      Last edited by Mkandara; 16th January 2007 at 05:20.
      Exploration of reality

    Page 4 of 26 FirstFirst ... 2345614 ... LastLast

    Similar Topics

    1. Je, wapinzani ni wakombozi?
      By Mzee Mwanakijiji in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 494
      Last Post: 24th July 2011, 12:29
    2. Ukombozi kutoka kwenye Makucha ya Wakombozi Wetu.
      By Kakalende in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 0
      Last Post: 20th April 2008, 12:55
    3. Hawa Wachina Ni Wakombozi Wa Africa Au?
      By Field Marshall ES in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 26
      Last Post: 2nd March 2008, 14:13

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...