Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: WARIOBA na rekodi yake akiwa Waziri Mkuu

    Report Post
    Page 1 of 3 123 LastLast
    Results 1 to 20 of 46
    1. #1
      JokaKuu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st July 2006
      Posts : 6,915
      Rep Power : 2990
      Likes Received
      2548
      Likes Given
      3634

      Exclamation WARIOBA na rekodi yake akiwa Waziri Mkuu

      ..hii ni sehemu ya mahojiano ya Waziri Mkuu Mstaafu Sinde Warioba alipozungumza na gazeti la raia mwema.

      ..alianza hivi:

      "Mwaka 1985 hatukuwa na akiba ya fedha za kigeni. Tulikuwa tunashindwa hata kulipia meli moja ya mafuta. Sasa kama akiba yetu ikipungua, bei ya mafuta imepanda, bei ya vyakula imepanda, tukajikuta hatuna akiba ya fedha za kigeni, tunafanyaje? "


      Swali: Ulipata kuwa Waziri Mkuu. Kama leo ungeshika tena nafasi hiyo ni mambo gani ambayo ungeyashughulikia ambayo hukuyashughulikia?

      Jaji Warioba: Kwanza, kwanza kabisa, sina mawazo ya kuwa Waziri Mkuu kabisa. Hilo halipo. Na kwa msingi huo hata nisingefikiria nitafanya nini kwa sababu hayo wakati wetu umepita. Hali imebadilika.

      Wakati nikiwa Waziri Mkuu matatizo yetu yalikuwa tofauti kabisa na matatizo ya sasa. Wakati ule uchumi wetu ulikuwa umeporomoka. Ulikuwa haukuwi.

      Mfumuko wa bei ulikuwa mkubwa, asilimia 36, 37 na hatuna fedha za kigeni. Hatuna vitu madukani. Ni wakati ule wa bidhaa adimu, nchi haina chakula.

      Kwa hiyo, wakati ule jukumu letu kubwa lilikuwa kuirudisha nchi katika msingi ambao utatuletea maendeleo ya kiuchumi na kijamii, na tuliweka priorities zetu.

      Moja, ilifika tukasema tujitosheleze kwa chakula katika muda wa miaka mitatu. Tulifanikiwa vizuri sana, lakini tukapata tatizo la hifadhi. Ikabidi tujenge maghala kwa haraka sana, tumepata chakula kingi zaidi tukiweke wapi?

      Tukasema lazima tu stabilise hali ya mafuta katika kipindi kifupi. Tukaweza. Tukasema lazima tuteremshe mfumuko wa bei. Hatukufanikiwa sana, lakini haukuendelea kukua.

      Tumeukuta uko 36, tunatoka baada ya miaka mitano umekuwa 19. Tukasema haya yalikuwa ni mafanikio makubwa.

      Tukasema tuwe na sera za msingi na ndipo tulipoanza. Mnajua matatizo tuliyopata wakati ule, tulipunguza sana matumizi kwenye huduma za jamii, elimu, afya, maji tukatia kwenye huduma za uchumi. Tukaanza kujenga miuondombinu, hatukukamilisha.

      Vipindi viwili vya Rais Mkapa walikazania hii. Tukafika mahali unaweza kuona mafanikio fulani fulani. Mfumuko wa bei umepungua, miundombinu iliboreshwa sana, ukakuta huduma za jamii zimeboreshwa ikiwa ni shule na afya na nyinginezo.

      Kwa hiyo, sisi ilikuwa ni kuweka msingi ule. Na ndiyo ilikuwa jukumu letu. Tulijitahidi. Tulijitahidi na ndiyo kipindi hicho sasa uchumi umeanza kukua.

      Sasa hivi hali ni tofauti na siwezi ku-speculate kwa sababu haikuja mawazoni mwangu. Mimi nasema sasa ni mzee wa kushauri tu. Ya kufikiria ningekuwa Waziri Mkuu hata haimo, kwa hiyo hata sisemi ningefanya hiki na hiki hapana. Nakumbuka hali ilivyokuwa kule na tulifanya nini. Tulipata matatizo. Unajua hali ilikuwa mbaya sana kwenye afya?

      Tulikuwa na matatizo lakini tulivumilia hivyo kwa yale makubwa, na hasa chakula, maana hata mazao ya biashara miaka ile ndiyo tulifikia rekodi ya kuvuna pamba, na ilikuwa ni kwa kufanya kazi na wananchi.

      Swali: Kuna majuto? Ungetaka kufanya nini ambacho hukufanya?

      Jaji Warioba: Siwezi kusema na regret kwa sababu hali ilivyokuwa mazingira yenyewe ni kwamba unatamani tu kwamba aah kwa jitihada ungekuwa umefanikiwa mengi zaidi lakini haikuwezekana.

      Kwa kweli hali haikuwa nzuri sana. Kwamba matarajio yalikuwa miaka mitano tutakuwa tumefika hapa. Hatukuweza kufika huko, lakini tulijitahidi tulivyoweza.
      mooduke and KANJARA like this.


    2. #2
      Mtu wa Pwani's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th December 2006
      Posts : 4,265
      Rep Power : 1498
      Likes Received
      171
      Likes Given
      168

      Default Re: WARIOBA na rekodi yake akiwa Waziri Mkuu.

      naam wako wanaosema mzee ruhsa awamu yake hawajafanya kitu wajifunze between the lines
      Our job is not to make up anybody's mind, but to open minds and to make the agony of the decision-making so intense you can escape only by thinking. ~Author Unknown

    3. #3
      JokaKuu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st July 2006
      Posts : 6,915
      Rep Power : 2990
      Likes Received
      2548
      Likes Given
      3634

      Default Re: WARIOBA na rekodi yake akiwa Waziri Mkuu.

      ..huyu nafikiri alifanya kazi yake kwa kufuata sheria, bila makeke.

      ..pia inaelekea aliondoka na heshima zake. ndiyo maana hana uwoga kuizungumzia rushwa au kuwanyooshea kidole wala rushwa.

      ..najua kwa Tanzania si rahisi kukuta mwanasiasa asiye na mawaa, lakini kwa standards zetu, Sinde Warioba anaelekea kuwa msafi.

      NB:

      ..IS HE THE BEST PRIME MINISTER WE HAVE EVER HAD?

    4. #4
      Zitto's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd March 2007
      Posts : 1,196
      Rep Power : 38470
      Likes Received
      2517
      Likes Given
      18

      Default Re: WARIOBA na rekodi yake akiwa Waziri Mkuu.

      Quote By jokaKuu View Post
      ..huyu nafikiri alifanya kazi yake kwa kufuata sheria, bila makeke.

      ..pia inaelekea aliondoka na heshima zake. ndiyo maana hana uwoga kuizungumzia rushwa au kuwanyooshea kidole wala rushwa.

      ..najua kwa Tanzania si rahisi kukuta mwanasiasa asiye na mawaa, lakini kwa standards zetu, Sinde Warioba anaelekea kuwa msafi.

      NB:

      ..IS HE THE BEST PRIME MINISTER WE HAVE EVER HAD?
      He was one of the best Prime Ministers, not the best. Inabidi tuwapime hawa wazee kwa vigezo mahususi. JF inaweza kuanzisha thread maalumu ya kuangalia utendaji wa PMs wetu na kuweka vigezo kisha tukasema nani alikuwa bora kwenye nini na nini? Je tunaweza kuwapima bila kugusia marais wao?

      Njia nyingine tumwombe Warioba awe online kwa saa moja tumuulize maswali hapa jamvini. Kisha afuate SAS, EL, MP, etc. Tujaribu kuwatafuta. Ninaweza kumtafuta Salim na Warioba!
      Speaker and Mzee like this.

    5. #5
      Indume Yene's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th March 2008
      Location : Chumbani
      Posts : 2,169
      Rep Power : 4961
      Likes Received
      340
      Likes Given
      324

      Default Re: WARIOBA na rekodi yake akiwa Waziri Mkuu.

      Quote By Zitto View Post
      Njia nyingine tumwombe Warioba awe online kwa saa moja tumuulize maswali hapa jamvini. Kisha afuate SAS, EL, MP, etc. Tujaribu kuwatafuta. Ninaweza kumtafuta Salim na Warioba!
      Naamini itakuwa jambo la busara kama utaweza kufanikisha hilo. Tanzania bado tuna rasilimali ya Wazee wa Busara lakini cha kushangaza Mh. Kingunge anawaponda,.... mmmh.

      Mkuu Mwanakijiji naamini ingependeza kama nawe unaweza kupata nafasi ya kuongea na hawa wazee kwenye radio yako ili iwe na manufaa kwa Watanzania wengine maana kwa Bongo still hawa wazee watazidi kuwapiga madongo kutoka SISIEMU kutokana na misimamo yao.


    6. #6
      Jasusi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th May 2006
      Posts : 10,702
      Rep Power : 2912
      Likes Received
      3893
      Likes Given
      12476

      Default Re: WARIOBA na rekodi yake akiwa Waziri Mkuu.

      Indume,
      Achana na Kingunge. Yeye alishageuka kuwa kigeugeu. Baada ya kupata mshiko wa parking pale Dar basi lazima awaponde wenzake ambao hakuandamana nao kisiasa. He is a Judas.

    7. Dua is offline
      Dua
      #7
      Dua's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th November 2006
      Posts : 3,534
      Rep Power : 1369
      Likes Received
      9
      Likes Given
      0

      Default Re: WARIOBA na rekodi yake akiwa Waziri Mkuu.

      Quote By Zitto View Post
      He was one of the best Prime Ministers, not the best. Inabidi tuwapime hawa wazee kwa vigezo mahususi. JF inaweza kuanzisha thread maalumu ya kuangalia utendaji wa PMs wetu na kuweka vigezo kisha tukasema nani alikuwa bora kwenye nini na nini? Je tunaweza kuwapima bila kugusia marais wao?

      Njia nyingine tumwombe Warioba awe online kwa saa moja tumuulize maswali hapa jamvini. Kisha afuate SAS, EL, MP, etc. Tujaribu kuwatafuta. Ninaweza kumtafuta Salim na Warioba!

      Ha ha haaaa hiyo ndio itakuwa siku ya nyani kuteleza kutoka kwenye mti, hawawezi kuthubutu kuja hapa kwa saa moja kwani wanajua joto ya jiwe iko hapa. Hasa wale wanafiki maana wataumbuliwa.

      BTW wazo zuri jaribuni kuwakaribisha hapa halafu tupeane taarifa tuwahoji.
      Dua la kuku halimpati mwewe

    8. #8
      Kuhani's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd April 2008
      Posts : 2,985
      Rep Power : 1993
      Likes Received
      21
      Likes Given
      0

      Default Re: WARIOBA na rekodi yake akiwa Waziri Mkuu.

      Quote By jokaKuu View Post
      ..huyu nafikiri alifanya kazi yake kwa kufuata sheria, bila makeke.

      ..pia inaelekea aliondoka na heshima zake. ndiyo maana hana uwoga kuizungumzia rushwa au kuwanyooshea kidole wala rushwa.

      ..najua kwa Tanzania si rahisi kukuta mwanasiasa asiye na mawaa, lakini kwa standards zetu, Sinde Warioba anaelekea kuwa msafi.

      NB:

      ..IS HE THE BEST PRIME MINISTER WE HAVE EVER HAD?
      La hasha!

      Hapo umeongelea sifa moja tu, tena labda haifiki moja. Alikuwa msafi, alifuata sheria, hakula rushwa, na akaondoka na heshima yake. Kwa kifupi, Muadilifu.

      Muadilifu ni sifa. Na inaweza kuwa sio sifa. Unapokula kiapo cha madaraka, zaidi ya kufanya kazi zako, cha chini kuliko vyote unachoahidi ni kufuata sheria, kutokutuibia. Ukitimiza hilo unakuwa umekamilisha wajibu, tena wa chini kuliko wote. Unapotimiza wajibu hupigiwi ngoma. Unapofika kazini katika muda unaotakiwa kila siku hupewi malipo ya ziada, unapewa mshahara. Hata kama wenzako wanachelewa kila siku. Ukiingizia kampuni mapato kuliko ulivyo tarajiwa ndio unaweza kudai bonus, au overtime payment kama umefanya kazi muda wa ziada. Hutakiwi kupewa chereko kwa kuwa muadilifu, hata kama kama unalinganishwa na Wachafu, wakina Mkapa.

      Ndio maana nasema mazuri uliyo yataja hapo yanaweza yakawa au yasiwe sifa inayoweza kupima excellence - kwa sababu ni wajibu wa Waziri Mkuu kutokutuibia. Na kama ni sifa, ni sifa moja tu.

      Jokakuu, sijui kama unakumbuka enzi za Warioba lakini Mkuu aliondoka na sifa mbaya ya kushindwa katika Utekelezaji. Dhihaka mpaka zikaenea kwamba Mwinyi alipo fire baraza la Mawaziri, Warioba akauliza kama yeye pia yuko fired!

      Kwa hiyo, sio tu, hawezi kuwa the best, nadhani hata katika the best hayumo. Mawaziri wakuu wazuri kuliko wote nadhani ni Nyerere na Sokoine. Na watatu labda Salim.

      Ahsante.
      ``Nilidhani hapa kwenye JF we are above perceptions and we attempt to search for truth and only truth.´´ Dr.W.Slaa

    9. #9
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 29,624
      Rep Power : 46738
      Likes Received
      16734
      Likes Given
      8564

      Default Re: WARIOBA na rekodi yake akiwa Waziri Mkuu.

      Quote By Indume Yene View Post
      Naamini itakuwa jambo la busara kama utaweza kufanikisha hilo. Tanzania bado tuna rasilimali ya Wazee wa Busara lakini cha kushangaza Mh. Kingunge anawaponda,.... mmmh.

      Mkuu Mwanakijiji naamini ingependeza kama nawe unaweza kupata nafasi ya kuongea na hawa wazee kwenye radio yako ili iwe na manufaa kwa Watanzania wengine maana kwa Bongo still hawa wazee watazidi kuwapiga madongo kutoka SISIEMU kutokana na misimamo yao.
      Napenda sana kufanya mahojiano na hawa wazee, nilikuwa nimewaline up wengi tu.. but it cost money...!
      [email protected]
      The Best of Tanzanian Socio-Political Blogging - http://www.mwanakijiji.com

    10. #10
      Mpanda Merikebu's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 27th December 2007
      Posts : 185
      Rep Power : 627
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: WARIOBA na rekodi yake akiwa Waziri Mkuu.

      Quote By jokaKuu View Post
      ..huyu nafikiri alifanya kazi yake kwa kufuata sheria, bila makeke.

      ..pia inaelekea aliondoka na heshima zake. ndiyo maana hana uwoga kuizungumzia rushwa au kuwanyooshea kidole wala rushwa.

      ..najua kwa Tanzania si rahisi kukuta mwanasiasa asiye na mawaa, lakini kwa standards zetu, Sinde Warioba anaelekea kuwa msafi.

      NB:

      ..IS HE THE BEST PRIME MINISTER WE HAVE EVER HAD?
      He sure is one of the greatest...but the best? Maybe the best living PM. Sokoine had a caliber of his own. Salim, well, he didn't serve long enough to have a good analysis of his Premiership. Warioba ni muadilifu lakini nafikiri he should have stood up for himself when Mzee Ruksa was being led astray with the Dirias and KK!
      Emancipate yourself from mental slavery, none but ourselves can free our mind ~RNM

      Saa ya ukombozi ni sasa ~ Rev. C. Mtikila

    11. #11
      Nyani Ngabu's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 15th May 2006
      Location : Ikungulyabashashi
      Posts : 39,521
      Rep Power : 0
      Likes Received
      9766
      Likes Given
      696

      Default Re: WARIOBA na rekodi yake akiwa Waziri Mkuu.

      Quote By Mzee Mwanakijiji View Post
      Napenda sana kufanya mahojiano na hawa wazee, nilikuwa nimewaline up wengi tu.. but it cost money...!
      Unahitaji mchango..?

    12. #12
      Single D's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th February 2007
      Location : Duniani
      Posts : 467
      Rep Power : 723
      Likes Received
      2
      Likes Given
      5

      Default Re: WARIOBA na rekodi yake akiwa Waziri Mkuu.

      Huwa najiuliza kwa nini huyu Warioba hakuendelea kuwa waziri mkuu wa mzee Ruksa kwa kipindi cha miaka 10.

      Anaongea vitu vinaeleweka kuhusu Muafaka kuliko Babu wa Kilwa na Mgosi,Je Ruksa aliogopa kuwa huenda angeweza kugombea Urais awamu ambayo ilifuata kama kawaida ya wanaomaliza uwaziri mkuu hugombea U rais?Huyu jamaa ndo waziri wa kwanza kuundiwa wizara hii ya TAMISEMI ambayo iliundwa kipindi cha Ruksa.

      Hata kupata ubunge kule Bunda mkoani Mara kipindi fulani ilikuwa mbinde maana waliendeshana na Stephen Wassira alipokuwa amehamia NCCR-MAGEUZI.
      Naona baada ya kukosa U waziri mkuu kipindi cha pili,mambo yalimwendea kombo sana ktk duru za siasa.

      Hiki kichwa bado tunakihitaji kwa maendeleo ya Taifa hili
      'Without unity, there is no future for Africa' J.K.Nyerere,1997,Accra Ghana.

    13. #13
      Kitila Mkumbo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th February 2006
      Posts : 3,940
      Rep Power : 6971
      Likes Received
      1102
      Likes Given
      36

      Default Re: WARIOBA na rekodi yake akiwa Waziri Mkuu.

      Quote By jokaKuu View Post
      ..
      ..IS HE THE BEST PRIME MINISTER WE HAVE EVER HAD?
      I would like to think so; but I am not sure how he would behave if he were PM in the multiparty politics era.

    14. #14
      JokaKuu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st July 2006
      Posts : 6,915
      Rep Power : 2990
      Likes Received
      2548
      Likes Given
      3634

      Default Re: WARIOBA na rekodi yake akiwa Waziri Mkuu.

      Kitila Mkumbo,

      ..amezungumzia mabadiliko makubwa ktk KILIMO/CHAKULA na UCHUMI/FEDHA. hivi haiwezekani kwamba wanaostahili sifa hapo ni mawaziri wa sekta hizo mbili kuliko yeye Sinde Warioba?

      ..ile kashfa ya Rio-Degeneiro ilitokea akiwa bado Waziri Mkuu? baada ya hapo ndiyo mambo yalianza kwenda mrama ktk serikali ya Mzee Ruksa.

    15. #15
      Myujumi Juma's Avatar
      Member Array
      Join Date : 31st October 2007
      Posts : 25
      Rep Power : 600
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: WARIOBA na rekodi yake akiwa Waziri Mkuu.

      naomba niulize kama kumbukumbu zangu sio nzuri, ile ishu ya mwananchi gold ya benki kuu haimhusu?

    16. #16
      Jamco_Za's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th July 2007
      Posts : 1,239
      Rep Power : 857
      Likes Received
      20
      Likes Given
      0

      Default Re: WARIOBA na rekodi yake akiwa Waziri Mkuu.

      CCM ya wakati wao sio ya sasa, maana sasa hivi hakuna msafi hata mmoja ndo maana kikwete anapata tabu kupata mawaziri, kila mtu ana kashifa yake inayosubiri kuibuka. Wakati wa mkutano wa Rio de Geneiro yeye alishaachishwa uwaziri mkuu nafikiri waziri mkuu alikuwa Msuya, mwananchi gold sinauhakika.

    17. #17
      Pezzonovante's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st May 2008
      Posts : 648
      Rep Power : 697
      Likes Received
      33
      Likes Given
      7

      Default Re: WARIOBA na rekodi yake akiwa Waziri Mkuu.

      Quote By jokaKuu View Post
      ..huyu nafikiri alifanya kazi yake kwa kufuata sheria, bila makeke.

      ..pia inaelekea aliondoka na heshima zake. ndiyo maana hana uwoga kuizungumzia rushwa au kuwanyooshea kidole wala rushwa.

      ..najua kwa Tanzania si rahisi kukuta mwanasiasa asiye na mawaa, lakini kwa standards zetu, Sinde Warioba anaelekea kuwa msafi.

      NB:

      ..IS HE THE BEST PRIME MINISTER WE HAVE EVER HAD?
      JOKA KUU NILIKUWA NAJIULIZA HIVI KWA NINI WAZEE WENGINE WAKO KIMYA NCHI INALIWA WANALO JAMBO WAKISEMA TU WATAUMBULIWA WARIOBA HANA MAFINDOFINDO NDIYO MAANA ANA MA CONFIDANCE YA KUSEMA.

    18. #18
      JokaKuu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st July 2006
      Posts : 6,915
      Rep Power : 2990
      Likes Received
      2548
      Likes Given
      3634

      Default Re: WARIOBA na rekodi yake akiwa Waziri Mkuu.

      Quote By jamco
      Wakati wa mkutano wa Rio de Geneiro yeye alishaachishwa uwaziri mkuu nafikiri waziri mkuu alikuwa Msuya, mwananchi gold sinauhakika.
      jamco,

      ..cleopa msuya alikuwa waziri mkuu mwishoni mwa utawala wa mzee mwinyi. nafikiri kuanzia late 1994. mkutano wa Rio ulifanyika wakati wa waziri mkuu akiwa sinde warioba au john malecela. matumizi ktk mkutano ule yalikuwa ni kashfa kubwa kuliko ile ya safari ya sumaye marekani.

      ..hiyo kampuni ya mwananchi si inahusika na masuala ya kusafisha dhahabu. nadhani CCM wana hisa huko, na Sinde Warioba yuko kwenye bodi ya wakurugenzi.

    19. #19
      Mwikimbi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th March 2008
      Posts : 1,545
      Rep Power : 953
      Likes Received
      346
      Likes Given
      128

      Default Re: WARIOBA na rekodi yake akiwa Waziri Mkuu.

      pamoja na sifa zote hizo, tuliokuwa vyuo vikuu wakati ule akiwa pm naddhani mwaka 1989-1990, tutamkumbuka, alivyowateka akina matiko matare na kwenda kuwahoji kunako giza, nadhani anakumbuka vema alivyowashuhulikia wanafunzi wakati wule walipomchora mwnyi pale revoulinary square. atabaki kwetu kama mtu ambaye alijua maana ya state yaani...cohesive,...invisible, ..incognito,...inconquencocabl e....eheee, na kila aliyehoji kuhusu mwenye kwenda kucheza isambe pale uwanja wa taifa na bongo man wakati madaktari wakiwa wamegoma pale muhimbili montuary ikiwa inajaa, walikutana na definition ya state ya warioba...incognito, ehee.. invisible...endelea

    20. #20
      Lambardi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th February 2008
      Location : KITAANI ZAIDI
      Posts : 4,588
      Rep Power : 1813
      Likes Received
      666
      Likes Given
      0

      Default Re: WARIOBA na rekodi yake akiwa Waziri Mkuu.

      Nami Nakubali Kuwa Sokoine Na Julius Kidogo Na Salim....ingawa Hakukaa Sana...warioba Hapana..........

    Page 1 of 3 123 LastLast

    Similar Topics

    1. Tetesi: Waziri mkuu mstaafu Warioba na TTCL
      By bundas in forum Jamii Intelligence
      Replies: 12
      Last Post: 7th November 2012, 14:46
    2. Replies: 37
      Last Post: 22nd July 2012, 14:31
    3. Replies: 11
      Last Post: 16th October 2011, 17:08
    4. WARIOBA na rekodi yake akiwa Waziri Mkuu
      By JokaKuu in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 66
      Last Post: 24th July 2011, 09:36

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...