Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Vita vya Kagera: Nini chanzo? Kulikuwa na ulazima?

    Report Post
    Page 1 of 25 12311 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 481
    1. #1
      Zizou's Avatar
      Member Array
      Join Date : 13th December 2010
      Posts : 19
      Rep Power : 435
      Likes Received
      3
      Likes Given
      0

      Default Vita vya Kagera: Nini chanzo? Kulikuwa na ulazima?

      Wandugu, salam za mida hii.

      Natafuta hotuba ya "SABABU TUNAYO, NIA TUNAYO NA UWEZO TUNAO."


      Nataka kusikia hizo "sababu tunazo" na hoja ya Rais ya kwenda vitani kwa mapana na urefu, badala ya kumbukumbu ya mstari mmoja tuliyokaririshwa toka udogoni.


      Nitangulize ahsante.


    2. #2
      BRUCE LEE's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th December 2010
      Posts : 693
      Rep Power : 630
      Likes Received
      19
      Likes Given
      7

      Default re: Vita vya Kagera: Nini chanzo? Kulikuwa na ulazima?

      naskia kuna mkono wa waingereza na wamarekani, sina uhakika nahitaji maelezo kwa wanaojua zaidi. Amini alikua na silaha pamoja na jeshi lililojitosheleza zaidi yetu, je ilikuaje tukashinda?tulitumia satelite za nani ku target majeshi ya amini?na kwanini? Kuna siri nyingi wakubwa.

    3. #3
      CHESEA INGINE's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 7th November 2010
      Posts : 170
      Rep Power : 471
      Likes Received
      14
      Likes Given
      164

      Default re: Vita vya Kagera: Nini chanzo? Kulikuwa na ulazima?

      Nilisikia maneno, sina uhakika nayo kwamba ''hiyo ilikuwa njia ya kusambaza ukimwi afrika ya mashariki!" naomba kusahihishwa!

    4. #4
      Nonda's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th November 2010
      Location : Gongo La Mboto
      Posts : 5,987
      Rep Power : 1901
      Likes Received
      966
      Likes Given
      370

      Default re: Vita vya Kagera: Nini chanzo? Kulikuwa na ulazima?

      Mkuu,
      Utasikia sababu tano na domo, longo longo tu.
      Mpango ilikuwa ni kumrudisha Obote madarakani!

    5. #5
      kilimasera's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd December 2009
      Posts : 3,049
      Rep Power : 1104
      Likes Received
      184
      Likes Given
      257

      Default re: Vita vya Kagera: Nini chanzo? Kulikuwa na ulazima?

      Sababu ya kwanza ni utawala wa kidikteta wa idd amin uganda kubomoa daraja la mto kagera mtukula na maneno ya kebehi kwa baba wa taifa pia alitangaza kwamba kagera ni sehemu ya uganda na alichoma bendera ya taifa na ya chama cha mapinduzi hadharani vilevile alisema anataka jeshi lake lifike mpaka dar es salaam yaani liiteke dar jamaa alikua anajiamini sana kwasababu alikua anaona tu kwamba sisi watanzania ni wapole sana kumbe uwezo tunao na nguvu tunayo nadhani waganda mpaka leo wanatuogopa maana tulipiga mpaka tukatokezea ethiopia!
      Dawa kuchanana tu likes this.


    6. #6
      Waberoya's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd August 2008
      Location : Busia-Uganda
      Posts : 5,948
      Rep Power : 1746
      Likes Received
      1519
      Likes Given
      2835

      Default re: Vita vya Kagera: Nini chanzo? Kulikuwa na ulazima?

      Quote By kilimasera View Post
      sababu ya kwanza ni utawala wa kidikteta wa idd amin uganda kubomoa daraja la mto kagera mtukula na maneno ya kebehi kwa baba wa taifa pia alitangaza kwamba kagera ni sehemu ya uganda na alichoma bendera ya taifa na ya chama cha mapinduzi hadharani vilevile alisema anataka jeshi lake lifike mpaka dar es salaam yaani liiteke dar jamaa alikua anajiamini sana kwasababu alikua anaona tu kwamba sisi watanzania ni wapole sana kumbe uwezo tunao na nguvu tunayo nadhani waganda mpaka leo wanatuogopa maana tulipiga mpaka tukatokezea ethiopia!
      Kilimasera ukiona mdogo wakoa anampiga ngumi mwezio na mwenzi akarudishia mkorofi ni yule aliyeanza kurusha ngumi??

      Tafuta Literatures, uliza waganda, nenda kulia nenda kushoto......

      Uganda mpaka leo wanamkumbuka Amin! ambaye wewe unamwona dictator

      Amin aliua makumi
      Obote kaua maelfu
      Museven kaua makumi elfu.......


      Kwa kufupi mkuu, Nyerere alikuwa na mtu ambaye anatakwa sana na Amin..Mr.Obote,

      kwa kifupi ulikuwa mpango wa Nyerere kumuweka Obote madarakani!!! yale ya kagera n.k ni hasira za Amin, ukweli NYERERE NDIYE ALIKUWA MKOROFI!!!!!
      MUSSOLIN likes this.
      You are not supposed to be so blind with patrotism that you cant face reality. Wrong is wrong no matter who says it. Malcom X

    7. #7
      Easymutant's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd June 2010
      Posts : 1,076
      Rep Power : 674
      Likes Received
      153
      Likes Given
      68

      Default re: Vita vya Kagera: Nini chanzo? Kulikuwa na ulazima?

      Quote By CHESEA INGINE View Post
      Nilisikia maneno, sina uhakika nayo kwamba ''hiyo ilikuwa njia ya kusambaza ukimwi afrika ya mashariki!" naomba kusahihishwa!
      Sina uhakika na hili lakini nahisi uko very very wrong mkuu gharama ya ile vita ukilinganisha na hiyo sabu du! hapana kama nikusambaza ukimwi wangeweza ku2mia njia ambayo isingeinvolve mauaji kama yale na gharama kama hizo..
      KISS-Keep It Simple Stupid.........[email protected]



    8. #8
      kilimasera's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd December 2009
      Posts : 3,049
      Rep Power : 1104
      Likes Received
      184
      Likes Given
      257

      Default re: Vita vya Kagera: Nini chanzo? Kulikuwa na ulazima?

      Quote By Waberoya View Post
      Kilimasera ukiona mdogo wakoa anampiga ngumi mwezio na mwenzi akarudishia mkorofi ni yule aliyeanza kurusha ngumi??

      Tafuta Literatures, uliza waganda, nenda kulia nenda kushoto......

      Uganda mpaka leo wanamkumbuka Amin! ambaye wewe unamwona dictator

      Amin aliua makumi
      Obote kaua maelfu
      Museven kaua makumi elfu.......


      Kwa kufupi mkuu, Nyerere alikuwa na mtu ambaye anatakwa sana na Amin..Mr.Obote,

      kwa kifupi ulikuwa mpango wa Nyerere kumuweka Obote madarakani!!! yale ya kagera n.k ni hasira za Amin, ukweli NYERERE NDIYE ALIKUWA MKOROFI!!!!!
      kwa research za harakaharaka mie nadhani amin ndiye aliekua mkorofi man any way ngoja nipitie tena maana hizo nilizitoa kichwani na nikapitia faster literature zangu so wait nitakupa jibu ila kwa ile vita sidhani kama alikua mkorofi ni nyerere man!

    9. #9
      Sikonge's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th January 2008
      Location : Sikonge, Tabora
      Posts : 7,986
      Rep Power : 2362
      Likes Received
      2948
      Likes Given
      5799

      Default re: Vita vya Kagera: Nini chanzo? Kulikuwa na ulazima?

      Du haya majibu?

      Ukitaka kujua sababu hasa ni jaribu kuangalia mambo yafuatayo:

      1. Museven ilikuwaje akapigana vita ya kumg'oa Idd Amin?

      2. Akina Paul Kagame ilikuwaje wakapigana vita ya kumg'oa Amin?

      3. Ilikuwaje hao wawili na kundi lao wawe Tanzania kabla ya vita?

      4. Kwa nini walipatia mafunzo ya vita Tanzania na kufanya mazoezi ya kivita Msumbiji?

      5. .............................. .............................. .........................

      Sababu ya kuanza vita kamwe haiwezi kuwa ni MOJA tu. Lazima kulichangiwa na vitu vingi sana. Obote ni kipande tu kwani Mzeven na akina Kagame pamoja na vita kuisha, walibaki Tanzania. Hata mie kwa sasa sina uhakika wa sababu ngapi hasa zilisababisha.

      Kuhusu Unyama wa Idd Amini kulinganisha na Mseven, mhhh Tafadhalini wajamani. Nimekaa na jamaa wengi wa Uganda na wengine hadi leo nawasiliana nao na mmoja wao akiwa ni kijana aliyepigana na Mseven kama askari wa Mizinga. Wengi wanasema kuwa Idd Amin alikuwa mnyama sana. Tatizo lake ni kuwa aliuwa hata wasiotaka kujihusisha na siasa. Kila msomi alikuwa ni tishio lake kubwa sana.

      Mseven yupo zaidi kupigana na adui zake. Kama wewe hujihushi na siasa, basi huwezi kupambana naye. Obote pia alikuwa mnyama sana sana na ndiyo maana Amin alipoingia, watu walimshangilia sana. Ila na Amin akawa kama Kikwete kwa kuunguza imani kubwa aliyopewa na wananchi.

      Miaka ya 80 na 90 Waganda walikuwa wakichukia sana Kiswahili. Msifikiri akina Cameleon leo wakiimba Kiswahili basi mkafikiri imekuwa hivyo muda wote. Jamaa walikuwa wakidai kuwa "enzi za Amin ukisema Kiswahili basi Mageti yote yanafunguliwa na unapigigiwa saluti. Kisa ni kuwa Kiswahili kilitumika zaidi na Amini na jeshi lake." Hivyo ukisema Kiswahili tu, watu wanajua kuna mtu anaweza kupoteza maisha sasa hivi au kupigwa sana.

      Ila ukweli mwingine ni kuwa, SIASA za Uganda ni ngumu sana. Utaona mtu analalamika kuwa kaonewa na Mseven na mwisho wa siku ukaja shangaa kaishia mitini na kisa ni kwamba jamaa ni Mpelelezi wa upinzani. Waswidi waliachwa mitini na jamaa mmoja na familia yake. Jamaa alikuja kuomba hifadhi, mwisho akaleta hadi familia yake. Siku moja wameamka jamaa hayupo Sweden na familia yake. Wakaulizia mipakani hakuna data zozote. Walipoenda Kampala kumtafuta, siku moja kawapigia simu na kuwaambia anawaona kwenye Mkahawa na kuwa wasimfuatefuate zaidi. Jamaa (waandishi wa habari) wakasema SIASA ZA UGANDA NI KIBOKO.

      Ndiyo maana nasema "Kama kuna mtu anafahamu hasa sababu, basi huyo ni Mganda. Kama siyo basi ni Nyerere na wengine wachache. Wengine wote wanajua tu sababu kadhaa na siyo zote". Uganda mambo ni mazito sana na sijui yataisha lini. Hata ukiweka katiba mpya na uchaguzi huru, Uganda ni ngumu sana. Wakija zubaa, Uganda yaweza kuwa kama Somalia maana WAJUAJI WENGI SANA UGANDA.
      we gule likes this.
      Nguruwe pita leo sina Mkuki(By Malila wa JF).

    10. #10
      Shomy . I's Avatar
      Member Array
      Join Date : 4th January 2011
      Posts : 60
      Rep Power : 441
      Likes Received
      5
      Likes Given
      0

      Default re: Vita vya Kagera: Nini chanzo? Kulikuwa na ulazima?

      Vita ya Kagera na sababu za KIDINI. Nitafafanua. Idd amin alikuwa ni mmoja wa viongozi ambao ni mwiba kwa mataifa ya Marekani na Uingereza. Alikopa fedha WB kwa ajili ya maendeleo ya nchi na badala yake alijenga msikiti ambao unakadiriwa kuwa ni mkubwa ktk A.Mashariki. Na alikuwa mbioni kutangaza Uganda kuwa nchi ya kiislam kitendo kilichowakasirisha mabwana hao wa ulaya.

      Ilikuwa ngumu kwa wao kujiingiza 1kwa1 ktk kumuondoa madarakani na badala yake wakaamua kuitumia tz km walivyofanya kule NJUWANI huku wao wakiwa nyuma ya tz kwa kutoa silaha za kivita. Pia Nyerere alikabidhiwa eneo lote la A.Mash.kuusimamia ukristo na kuuendeleza. Hivyo ilikuwa ni lazma awajibike ipasavyo.

      Kwa kusema ukweli Tz hatukuwa na uwezo wa kumng'oa Idd Amin wala kule NJUWANI. Pia kuhusu kula nyama za watu, hakuna kitu km hicho hata hizo filamu wametengeza haohao(marekani na uingereza) ili kunakshi uongo wao watu waamin kile walichofanya. Mifano mingine ni sudani na angola (huu ni mjadala unaojitegemea).

      Nyerere hakuwa na 'UWEZO' wala 'NIA' Na huo ndio ukweli wenyewe mkuu.
      Last edited by Shomy . I; 23rd January 2011 at 22:43.

    11. #11
      Mtemakuni's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 18th September 2010
      Posts : 163
      Rep Power : 476
      Likes Received
      13
      Likes Given
      19

      Default re: Vita vya Kagera: Nini chanzo? Kulikuwa na ulazima?

      Watanzania tupende kuwa tunasoma historia na vitabu na kuanalyse mambo bila emotions. Wala tusitawaliwe na uswahiba au mapenzi just bcaz unampenda mtu bac kila anachofanya is right..!

      Kwa udadisi wangu na uelewa wangu na source zangu za information sababu za vita ya amini zilikua kuu mbili 1st Interest ya nyerere kumpandikiza washikaji zake obote na museveni though alizuga mwanzoni kwa kumpa lule..!

      2nd was interest ya wamarekani na waingereza kutokana na dini ya Amini, uhusiano wake na waarabu na kauli zake dhidi ya israel na baada ya kuteka ile ndege ya waisrael plan zilifanywa chap chap kwa kumuhusisha nyerere na kwasababu nyerere alikua na hiyo plan mambo yalikua mepesi akawezeshwa vita ikapigwa. Though china pia walitupa silaha soo hapa nyerere alitumia ucomunist wake pia kuget other helps...!

    12. #12
      kilimasera's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd December 2009
      Posts : 3,049
      Rep Power : 1104
      Likes Received
      184
      Likes Given
      257

      Default re: Vita vya Kagera: Nini chanzo? Kulikuwa na ulazima?

      Quote By Shomy . I View Post
      Vita ya Kagera na sababu za KIDINI. Nitafafanua. Idd amin alikuwa ni mmoja wa viongozi ambao ni mwiba kwa mataifa ya Marekani na Uingereza. Alikopa fedha WB kwa ajili ya maendeleo ya nchi na badala yake alijenga msikiti ambao unakadiriwa kuwa ni mkubwa ktk A.Mashariki. Na alikuwa mbioni kutangaza Uganda kuwa nchi ya kiislam kitendo kilichowakasirisha mabwana hao wa ulaya.

      Ilikuwa ngumu kwa wao kujiingiza 1kwa1 ktk kumuondoa madarakani na badala yake wakaamua kuitumia tz km walivyofanya kule NJUWANI huku wao wakiwa nyuma ya tz kwa kutoa silaha za kivita. Pia Nyerere alikabidhiwa eneo lote la A.Mash.kuusimamia ukristo na kuuendeleza. Hivyo ilikuwa ni lazma awajibike ipasavyo.

      Kwa kusema ukweli Tz hatukuwa na uwezo wa kumng'oa Idd Amin wala kule NJUWANI. Pia kuhusu kula nyama za watu, hakuna kitu km hicho hata hizo filamu wametengeza haohao(marekani na uingereza) ili kunakshi uongo wao watu waamin kile walichofanya. Mifano mingine ni sudani na angola (huu ni mjadala unaojitegemea).

      Nyerere hakuwa na 'UWEZO' wala 'NIA' Na huo ndio ukweli wenyewe mkuu.
      kwa mfano upo kwenye paper ya advanced level hilo shwali unakutana nalo na lina maksi 20 unafikiri mwalimu wako angekupa ngapi kwa point hiyo?
      Mbalamwezi and NAKAMO like this.

    13. #13
      IHOLOMELA's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd November 2010
      Location : New York
      Posts : 416
      Rep Power : 521
      Likes Received
      55
      Likes Given
      59

      Default

      Quote By Waberoya View Post
      Kilimasera ukiona mdogo wakoa anampiga ngumi mwezio na mwenzi akarudishia mkorofi ni yule aliyeanza kurusha ngumi??

      Tafuta Literatures, uliza waganda, nenda kulia nenda kushoto......

      Uganda mpaka leo wanamkumbuka Amin! ambaye wewe unamwona dictator

      Amin aliua makumi
      Obote kaua maelfu
      Museven kaua makumi elfu.......


      Kwa kufupi mkuu, Nyerere alikuwa na mtu ambaye anatakwa sana na Amin..Mr.Obote,

      kwa kifupi ulikuwa mpango wa Nyerere kumuweka Obote madarakani!!! yale ya kagera n.k ni hasira za Amin, ukweli NYERERE NDIYE ALIKUWA MKOROFI!!!!!
      umenena ukweli mtupu. Mie nilikuwa mji wa Mbarara siku moja nilipokwenda kutafta mahali pa kulala baada ya kujitambulisha kuwa ni Mtz walikataa kunipa rum kisa eti tajiri yao amepiga marufuku kulala watanzania kwani ni waongo sana na walimtia umackni wakat wa vita.

    14. #14
      Mrdash1's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st September 2010
      Posts : 1,379
      Rep Power : 1464
      Likes Received
      305
      Likes Given
      201

      Default re: Vita vya Kagera: Nini chanzo? Kulikuwa na ulazima?

      Quote By BRUCE LEE View Post
      naskia kuna mkono wa waingereza na wamarekani, sina uhakika nahitaji maelezo kwa wanaojua zaidi. Amini alikua na silaha pamoja na jeshi lililojitosheleza zaidi yetu, je ilikuaje tukashinda?tulitumia satelite za nani ku target majeshi ya amini?na kwanini? Kuna siri nyingi wakubwa.
      Mwaka 1977/78 wewe ulikuwa uzaliwa? Kuna sababu gani ya vita zaidi ya nchi kuivamia nchi ingine?

      Amini aliivamia Tanzania, akatangaza mpaka mpya kuwa ni mto kagara kiasi cha kilomita 25 hivi ndani ya mipaka ya Tanzania, wananchi watanzania wenzetu waliokuwa wanaishi maeneo yaliyotekwa walifanyiwa unyama na wengine kuuawawa bila makosa.

      Jina sahihi la vita ya kagera ni "Vita ya Ukombozi wa Kagara" Ndiyo maana Nyerere alipounganisha vita ya ukombozi na vita ya kumwondoa Amini Madarakani Uganda Umoja wa Mataifa haukumlaani kama ilivyo kuwa kwa G W Bush na Sadam Hussein. Actually, Waamerika walii copy Tanzania kama precedent ya nchi kumwondoa madarakani raisi wa nchi ingine wakati wa sakata la iraki huko UN.
      Ukweli wa vita ya kagera unaujua ila hapa umeuliza tu kiunaafiki, una ajenda yako mwenyewe ambayo unaona aibu kuiweka wazi.

      Kama ungekuwa siyo mnafiki ungeuliza ni kwa nini Amini alikimbilia Saudi Arabia au ni kwa nini Gadaffi alileta majeshi kumsaida Amini
      Mbalamwezi likes this.

    15. #15
      BRUCE LEE's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th December 2010
      Posts : 693
      Rep Power : 630
      Likes Received
      19
      Likes Given
      7

      Default re: Vita vya Kagera: Nini chanzo? Kulikuwa na ulazima?

      Wana jamvi nilifanya utafiti kuhusu vita hiyo,pia nikaandika makala yenye kurasa 50,mzee hamad hemed mtz mwenye asili ya kiarabu alikua huko wakati wa vita hiyo na anasema amin alipendwa sana na aliwapeleka maka kuhiji waislam wengi bure.

      Pia urafiki wake na gadaf pa 1 na mataifa ya uislam iliwaudhi wamarekani, pia kitendo cha kuwashinikiza wana diplomasia na viongozi wa uingereza walioenda uganda kumbeba juu na kuzunguka nae kampala kama walivyotumikishwa watu weusi kwenye biashara ya utumwa iliwauzi sana, hivyo nyerere akapewa dili la kumuangusha amin, mzee J Kenyata akamwambia amin dhidi ya mpango huo ndio amini akatangaza vita dhidi ya tz kwani alishajua mpango mzima nyerere na jesh lake masikini halikua hata sare za kutosha na wengine walikua wanafunga kudu kwa kukosa mikanda,alitumia rada na satelite za waingereza kumpiga amini, hakua na uwezo wala sababu ya msingi.

      Naishia hapa wengine waendelee.

    16. #16
      Sikonge's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th January 2008
      Location : Sikonge, Tabora
      Posts : 7,986
      Rep Power : 2362
      Likes Received
      2948
      Likes Given
      5799

      Default re: Vita vya Kagera: Nini chanzo? Kulikuwa na ulazima?

      Kwa nini isiwe ni kwa sababu ALIWAFUKUZA WAHINDI kwa kuwapa siku 90 wawe wameondoka wote Uganda?

      Yameanza yale ya Vipofu walioenda kumshika Tembo na kila mmoja akawa na story yake ya Tembo alivyo, kwa sababu kila mtu alishika kipande tu cha tembo.

      Kumbuka Wahindi wengi walienda UK na Canada.

      Pia Obote alikuwa na mpamgo wa kurudi madarakani akisaidiwa na akina Museven, Kagame na Tanzania.

      Angalieni film ya RISE AND FALL OF AMIN, iliyotengenezewa Kenya na huku Wakenya wakisaidia kutengeneza.

      Sikujuwa hata hili watu wataleta UDINI. Kaaazi kwelikweli. Hitler angelikuwa Muislaam .........
      Quote By BRUCE LEE View Post
      Wana jamvi nilifanya utafiti kuhusu vita hiyo,pia nikaandika makala yenye kurasa 50,mzee hamad hemed mtz mwenye asili ya kiarabu alikua huko wakati wa vita hiyo na anasema amin alipendwa sana na aliwapeleka maka kuhiji waislam wengi bure.

      Pia urafiki wake na gadaf pa 1 na mataifa ya uislam iliwaudhi wamarekani, pia kitendo cha kuwashinikiza wana diplomasia na viongozi wa uingereza walioenda uganda kumbeba juu na kuzunguka nae kampala kama walivyotumikishwa watu weusi kwenye biashara ya utumwa iliwauzi sana, hivyo nyerere akapewa dili la kumuangusha amin, mzee J Kenyata akamwambia amin dhidi ya mpango huo ndio amini akatangaza vita dhidi ya tz kwani alishajua mpango mzima nyerere na jesh lake masikini halikua hata sare za kutosha na wengine walikua wanafunga kudu kwa kukosa mikanda,alitumia rada na satelite za waingereza kumpiga amini, hakua na uwezo wala sababu ya msingi.

      Naishia hapa wengine waendelee.
      jouneGwalu likes this.
      Nguruwe pita leo sina Mkuki(By Malila wa JF).

    17. #17
      BRUCE LEE's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th December 2010
      Posts : 693
      Rep Power : 630
      Likes Received
      19
      Likes Given
      7

      Default re: Vita vya Kagera: Nini chanzo? Kulikuwa na ulazima?

      mwl nyerere aliwahi sema kua yeye kama binadam alikua na mazuri pia mabaya hivyo niwajibu we2 kufuata mazuri na kuyapuuza mabaya yake, hili la vita ni baya na alichemsha pia muungano na zanzbar pia alichemsha kwani wakati karume anataka kujitenga baada ya mkataba wa muda kumalizika nyerere huyohuyo anahusishwa na mipango ya kumuua karume ili kulinda mungano, na wanaoutaka zaidi ni ulaya na marekani ili kuudhibit uislam na tishio la ugaidi, wazenj wanalijua hilo sio siri.

    18. #18
      Zizou's Avatar
      Member Array
      Join Date : 13th December 2010
      Posts : 19
      Rep Power : 435
      Likes Received
      3
      Likes Given
      0

      Default re: Vita vya Kagera: Nini chanzo? Kulikuwa na ulazima?

      Nashukuru sana kwa michango hii wandugu.

      Sababu zilizotolewa zinaleta mantiki na baadhi nimewahi kuzisikia.

      Ambacho sijawahi kukisikia, na ambacho nimetaja kuwa nakiomba, kama kipo, ni hoja ya vita kupitia hotuba ya "Sababu Tunazo, Uwezo Tunao" iliyotolewa Agosti 18, 1978, na Hayati J. Kambarage Nyerere.

      Unaposema "sababu ni kuvamiwa, kwani hujui" hainisaidii. Si kila unapovamiwa unaamkia vitani. Yapaswa, katika diplomasia za vita, uonyeshe, kama ambavyo nasikia Rais alifanya, kuwa njia nyingine zimeshindikana.

      Hiyo hoja ya Rais ndio ninayoitafiti. Kuna mtu anayo?

    19. #19
      Wa Ndima's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th August 2010
      Posts : 1,388
      Rep Power : 735
      Likes Received
      223
      Likes Given
      645

      Default re: Vita vya Kagera: Nini chanzo? Kulikuwa na ulazima?

      Nyerere alikuwa mkorofi, ni yeye mwenyewe aliyebomoa daraja la Kagera kutafuta chokochoko za kumpiga Idd Amini. Alifanya hivi kumuingiza rafiki yake Obote madarakani kama mnakumbuka kipindi kile Obote alikuwa Dar. Ametuingiza kwenye umasikini wa kutosha kwa kutufungisha mkanda mpaka leo. Nachukia sana vita vile....
      Mzee Kijana and Kaptula like this.


    20. #20
      JokaKuu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st July 2006
      Posts : 6,915
      Rep Power : 2990
      Likes Received
      2548
      Likes Given
      3634

      Default re: Vita vya Kagera: Nini chanzo? Kulikuwa na ulazima?

      Bruce Lee,

      ..ungeisaidia sana jamii forums kwa ku-post paper uliyoandika kuhusu vita vya Kagera.

      ..nadhani sasa hivi kutakuwepo na a lot of de-classified documents toka mashirika ya kijasusi ya nchi za magharibi zinazoweza kutoa mwangaza kuhusu nini kiliendelea.

    Page 1 of 25 12311 ... LastLast

    Similar Topics

    1. Video za Vita vya Kagera
      By Black Uhuru in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 3
      Last Post: 19th September 2011, 01:23
    2. Vita vya Kagera tulipigana na Libya (Gadafi)
      By Mwana wa Mungu in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 123
      Last Post: 22nd March 2011, 07:22
    3. Mashujaa wetu wa vita vya Kagera
      By MaxShimba in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 1
      Last Post: 27th July 2009, 02:22
    4. Miaka 30 Ya Vita Vya Kagera
      By X-PASTER in forum Jukwaa la Elimu (Education Forum)
      Replies: 1
      Last Post: 2nd November 2008, 00:36

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...