Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Kwa nini Chidumule kawachana waimbaji wa bongo flavor pamoja na wale wa dini?

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 24
    1. #1
      Johnsecond's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th May 2010
      Posts : 949
      Rep Power : 657
      Likes Received
      156
      Likes Given
      68

      Default Kwa nini Chidumule kawachana waimbaji wa bongo flavor pamoja na wale wa dini?

      Wakati nikisikiliza taarifa ya habari ITV Chidumule akiwa msibani kwa Dr. Remi Ongala alipewa nafasi ya kuongea chochote. Alisema kuwa marehemu alikuwa mwanamuziki mahili lakini alikuwa hatembei mabega juu ila anashangaa wanamuziki wa bongo flavor ambao kwanza wamepanga kwenye mabanda ya uani harafu wanatembea mabega juu na wale wa dini kasema wakitoa kasingle kamoja basi wanamsahau hata askofu.

      My take: Wanamuziki wa zamani hawawapendi vijana wa bongo flavor maana nilishamsikia ngurumo pia akiwachana kuwa wanaimbia juu, hivyo hawana maana.

      ebu nisikie views zenu nanyi pia wana jf.


    2. #2
      Pakawa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th March 2009
      Posts : 1,172
      Rep Power : 758
      Likes Received
      173
      Likes Given
      185

      Default Re: Kwa nini Chidumule kawachana waimbaji wa bongo flavor pamoja na wale wa dini?

      Kasema kweli kabisa.
      Hata itakuwa kwa kila mtu atakayeliita jina la bwana atampokea roho wa mungu' 'Niiteni nami nitaitika anasema bwana wa majeshi.'

    3. #3
      Gang Chomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th February 2008
      Location : hell
      Posts : 5,264
      Rep Power : 1772
      Likes Received
      1042
      Likes Given
      0

      Default Re: Kwa nini Chidumule kawachana waimbaji wa bongo flavor pamoja na wale wa dini?

      ''neno ya Muzee, ukabisha
      Mwisho utapata shida''....Quotes from Hayati Dakta.


      Sasa nirudi kwenye mada yako.
      Alichokisema Cosmas ni cha kweli kabisa kwani tumeshashuhudia wasanii kadhaa wa kizazi kipya waliokuwa ndani ya makundi then baada ya kung'aa ktk single moja basi anatoka ktk kundi then akishapewa kagari ''vilts'' na Muhindi anayemnyonya basi nyodo zinaanza.

      Au ukija kwenye medani ya muziki wa Dini mambo ni yaleyale, mtu akipata kaujiko basi hata tuzo zinazoitwa na kudhaminiwa na kilevi yeye atataka aende tu ili mradi keshajiona star.

      Tuliona kwaya kama Makongoro, kwaya ya mtakatifu Cecilia Mwenge, kwaya ya Nkinga, kwaya ya Ulyankulu barabara ya 13, kwaya ya Mabibo walioimba ''sauti ikatoka'' Maranatha, New life Band...tuliwaona watu kama kina Nyambele, Mzungu Four, Faustin Munishi na wengine weeengi ambao ulikuwa ukisikiliza nyimbo zao ni sawa na kusoma Bilble au kusikiliza mahubiri.


      Mfano hii kwaya ya mtakatifu cecilia Mwenge walitamba sana na albam yao inayomsifu Mama Maria mwanzoni mwa miaka ya 90 na mpaka leo ikipigwa utakubali kweli ujumbe unaupata.

      Tuje kwa ulyankulu:
      Hawa jamaa waliimba nyimbo kama
      Nuhu, Samson, na nyingine nyingi zenye ujumbe.
      Albam hii iliimbwa kwa ustadi wa hali ya juu sana. Kwani kila nyimbo iliyomo humu ni Mstari ktk Bible.
      Kwa mfano kuna nyimbo inayosema ''mtu mkubwa mmoja aliuliza akisema mwalimu, nifanye nini ili nipate kuurithi uzima wa Milele?''...huu ni mstari ndani ya Bible na umezungumziwa ktk nyimbo. So ina maana hata kama hujui kinachozungumziwa ktk Bible basi utakielewa ktk nyimbo.


      Sasa rudi uje uwasikilize hao wanakwaya wenu wa siku hizi nyimbo zao utasikia ''nibebe'' mara huyo Frola Mbasha ana wimbo unaSema ''mwanamke simama imara'' kauimba kama mchiliku...lool

      Ni ushuzi mtupu.

    4. #4
      Masanilo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd October 2007
      Location : Swat valley, Keta Keta
      Posts : 19,261
      Rep Power : 5512
      Likes Received
      3581
      Likes Given
      1995

      Default Re: Kwa nini Chidumule kawachana waimbaji wa bongo flavor pamoja na wale wa dini?

      Quote By Gang Chomba View Post
      ''neno ya Muzee, ukabisha
      Mwisho utapata shida''....Quotes from Hayati Dakta.


      Sasa nirudi kwenye mada yako.
      Alichokisema Cosmas ni cha kweli kabisa kwani tumeshashuhudia wasanii kadhaa wa kizazi kipya waliokuwa ndani ya makundi then baada ya kung'aa ktk single moja basi anatoka ktk kundi then akishapewa kagari ''vilts'' na Muhindi anayemnyonya basi nyodo zinaanza.

      Au ukija kwenye medani ya muziki wa Dini mambo ni yaleyale, mtu akipata kaujiko basi hata tuzo zinazoitwa na kudhaminiwa na kilevi yeye atataka aende tu ili mradi keshajiona star.

      Tuliona kwaya kama Makongoro, kwaya ya mtakatifu Cecilia Mwenge, kwaya ya Nkinga, kwaya ya Ulyankulu barabara ya 13, kwaya ya Mabibo walioimba ''sauti ikatoka'' Maranatha, New life Band...tuliwaona watu kama kina Nyambele, Mzungu Four, Faustin Munishi na wengine weeengi ambao ulikuwa ukisikiliza nyimbo zao ni sawa na kusoma Bilble au kusikiliza mahubiri.


      Mfano hii kwaya ya mtakatifu cecilia Mwenge walitamba sana na albam yao inayomsifu Mama Maria mwanzoni mwa miaka ya 90 na mpaka leo ikipigwa utakubali kweli ujumbe unaupata.

      Tuje kwa ulyankulu:
      Hawa jamaa waliimba nyimbo kama
      Nuhu, Samson, na nyingine nyingi zenye ujumbe.
      Albam hii iliimbwa kwa ustadi wa hali ya juu sana. Kwani kila nyimbo iliyomo humu ni Mstari ktk Bible.
      Kwa mfano kuna nyimbo inayosema ''mtu mkubwa mmoja aliuliza akisema mwalimu, nifanye nini ili nipate kuurithi uzima wa Milele?''...huu ni mstari ndani ya Bible na umezungumziwa ktk nyimbo. So ina maana hata kama hujui kinachozungumziwa ktk Bible basi utakielewa ktk nyimbo.


      Sasa rudi uje uwasikilize hao wanakwaya wenu wa siku hizi nyimbo zao utasikia ''nibebe'' mara huyo Frola Mbasha ana wimbo unaSema ''mwanamke simama imara'' kauimba kama mchiliku...lool

      Ni ushuzi mtupu.
      Wachungaji tunapata shida sana kutumia nyimbo za enjili za sasa kuhubiri neno!

      Kindness is the language which the deaf can hear and the blind can see - Mark Twain
      CCM is enemy of GOD

    5. #5
      Mess's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd March 2009
      Location : Ukonga
      Posts : 625
      Rep Power : 654
      Likes Received
      123
      Likes Given
      36

      Default Re: Kwa nini Chidumule kawachana waimbaji wa bongo flavor pamoja na wale wa dini?

      Sina tatizo na waimbaji wale wasiokuwa na dini maana wenyewe ni ile free style tu. Ila wale sasa wa dini wanaharibu sana na ndo maana hata wa miziki mingine wanawapaka. Angalieni muziki wa shaggy church heathen


    6. 3D. is offline
      3D.
      #6
      3D.'s Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th September 2010
      Location : DSM, Tanzania
      Posts : 1,025
      Rep Power : 651
      Likes Received
      258
      Likes Given
      1465

      Default Re: Kwa nini Chidumule kawachana waimbaji wa bongo flavor pamoja na wale wa dini?

      Wa-Bongo flavour si wanamuziki ni waimbaji. Ni wachache wanaweza kuwa na hadhi ya uanamuziki. Kijana akiwa na sauti ya kuimba basi ni kuandaa single tu, ndiyo maana karibu wanafunzi wote wa kiume wa sekondari wanaigiza uanamuziki. Mob psychology!!! Wao hawajijui, umri bwana!!!

    7. #7
      Mchaka Mchaka's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 20th July 2010
      Location : Ashmore and Cartier Islands
      Posts : 3,702
      Rep Power : 1218
      Likes Received
      929
      Likes Given
      470

      Default Re: Kwa nini Chidumule kawachana waimbaji wa bongo flavor pamoja na wale wa dini?

      flora mbasha ndio anachefua kabisaaaaaa! Hafai kabisa kumwimbia bwana.

    8. #8
      Tausi Mzalendo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd May 2010
      Location : Solomon Island
      Posts : 1,457
      Rep Power : 891
      Likes Received
      681
      Likes Given
      865

      Default Re: Kwa nini Chidumule kawachana waimbaji wa bongo flavor pamoja na wale wa dini?

      Hivi Bongo fleva nao ni wanamuziki?
      Mi huwa siwafagilii hata chembe..namfagiliaga prodyuza siku zote kwa ku copy, cut and paste mirindimo na mautamu ya nyimbo za watu na kuwawekea mabongo fleva!

      Mnakumbuka prodyuza alivyoiba wimbo wa watu akamuwekea TID... TID akajiona yuko juu hadi alipoteremshwa kwa aibu kwa kuwekewa wimbo original sambamba na ule wake feki?

      AIBU!
      "You were born an original. Don't die a copy." —John Mason

    9. #9
      Mess's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd March 2009
      Location : Ukonga
      Posts : 625
      Rep Power : 654
      Likes Received
      123
      Likes Given
      36

      Default Re: Kwa nini Chidumule kawachana waimbaji wa bongo flavor pamoja na wale wa dini?

      Quote By Tausi Mzalendo View Post
      Hivi Bongo fleva nao ni wanamuziki?
      Mi huwa siwafagilii hata chembe..namfagiliaga prodyuza siku zote kwa ku copy, cut and paste mirindimo na mautamu ya nyimbo za watu na kuwawekea mabongo fleva!

      Mnakumbuka prodyuza alivyoiba wimbo wa watu akamuwekea TID... TID akajiona yuko juu hadi alipoteremshwa kwa aibu kwa kuwekewa wimbo original sambamba na ule wake feki?

      AIBU!
      Kwa hiyo unawapongeza jamaa kwa ku copy and paste? lakini wanazikamata saana pesa za watz. Ila ndo hivyo mimi pia nimekuwa nikifuatilia nyimbo nyingi za wa bongo wana copy kwenye olds za siku nyingi sana.

    10. #10
      Chipukizi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th March 2009
      Location : Manzese
      Posts : 1,065
      Rep Power : 736
      Likes Received
      265
      Likes Given
      31

      Default Re: Kwa nini Chidumule kawachana waimbaji wa bongo flavor pamoja na wale wa dini?

      Hawa wana mziki wa Ubongo wa fleva,ni sawa kabisa alivyosema Cosmas-DUDU BAYA ni upi wimbo weake ambao mtu anaweza pata fundisho?
      Ni kweli awa wakitoa singo tu wanajiona madona au Michael Jackson
      Yupo wp Mr Nice?,Pig black,etc.
      Wanalewa masifa tena sana na kusahau wametoka wapi

    11. #11
      Chimunguru's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd May 2009
      Posts : 7,887
      Rep Power : 2171
      Likes Received
      1258
      Likes Given
      561

      Default Re: Kwa nini Chidumule kawachana waimbaji wa bongo flavor pamoja na wale wa dini?

      chidumule wewe mwisho. unanikuna sana kwenye usitumie pesa km fimbo, barua toka kwa mama.

    12. #12
      NDOFU's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd February 2009
      Posts : 651
      Rep Power : 656
      Likes Received
      131
      Likes Given
      10

      Default Re: Kwa nini Chidumule kawachana waimbaji wa bongo flavor pamoja na wale wa dini?

      Wabana pua wanaridhika haraka af wanajiona wamemaliza safari ya muziki..wakati wanaimba tungo nyepesi tena kama Big G zina heat leo,kesho kapuni...........Naunga mkono hoja.

    13. #13
      NGULI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st March 2008
      Location : HOME
      Posts : 4,441
      Rep Power : 1461
      Likes Received
      214
      Likes Given
      1

      Default Re: Kwa nini Chidumule kawachana waimbaji wa bongo flavor pamoja na wale wa dini?

      Quote By Mess View Post
      Sina tatizo na waimbaji wale wasiokuwa na dini maana wenyewe ni ile free style tu. Ila wale sasa wa dini wanaharibu sana na ndo maana hata wa miziki mingine wanawapaka. Angalieni muziki wa shaggy church heathen
      Some sweet hearts are bitter than chloroquine packed in a sweet paper

    14. #14
      Baba_Enock's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st August 2008
      Location : Bunju "B"
      Posts : 5,857
      Rep Power : 1911
      Likes Received
      1182
      Likes Given
      1010

      Default Re: Kwa nini Chidumule kawachana waimbaji wa bongo flavor pamoja na wale wa dini?

      Very True

      - Bongo Flavours siyo wanaMUZIKI ni waimbaji wa MUZIKI

      - Ni Kweli Bongo Flavours "akitoa single" utadhani amepata "Platinum" :: Haishi baa na vibinti na ujinga ujinga mwingi!
      Ad Majorem Dei Gloriam - "For the greater glory of God"

    15. #15
      Mubii's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 24th July 2008
      Posts : 129
      Rep Power : 581
      Likes Received
      8
      Likes Given
      52

      Default Re: Kwa nini Chidumule kawachana waimbaji wa bongo flavor pamoja na wale wa dini?

      Kwa mtazamo wangu naona wanamuziki wa zamani hawakufaidika kimaslahi kama hawa wa bongo flavour wanavyofaidika nyakati hizi. Huenda hii imeleta msuguano kwa kuwa wale wa zamani walitunga nyimbo nzuri za kitanzania, walipiga kwa kutumia vyombo kama gitaa, saxaphone nk. Licha ya kufanya hivyo wengi wamekuwa na hali ya umasikini. Angalia vijana wa bongo flavour. Hajui kupiga hata aina moja ya muziki, hajui nota, lakini akiingia studio anatoka na nyimbo na michuzi zaidi kuliko wana muziki wa zamani. Katika hali ya ubinadamu, lazima utaona uchungu fulani kwamba wewe uli 'toil' sana hukupata mafanikio ya hali na mali ya kutosha na sasa wanakuja vijana wadogo wana 'toil' kidogo na anatoka na nyumba, ka-saloon n.k. Nashukuru Mwenyezi MUNGU yupo na anaona haya yote. Tumuachie kwani yeye anatawala vitu vyote ulimwenguni.

    16. #16
      Ngongo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th September 2008
      Location : Mlima Meru
      Posts : 4,972
      Rep Power : 6859
      Likes Received
      2415
      Likes Given
      3175

      Default Re: Kwa nini Chidumule kawachana waimbaji wa bongo flavor pamoja na wale wa dini?

      Wanamuziki wa zamani walifanyakazi zao kwenye mazingira magumu ukilinganisha na wanamuziki wa Bongo flavor.
      Enzi za Chidumule na wanamuziki wa zamani hawakuwa na fursa nyingi kama ilivyo kipindi hiki cha wanamuziki wa kizazi kpya.studio za kurekodi ilikuwa moja hapa Tanzania RTD kuliwa pia masharti ya nyimbo kurekodiwa mashairi yalifanyiwa uhariri kabla nyimbo haijaruhusiwa kurekodiwa.Wanamuziki wa Tanzania walilazimika kwenda nchi jirani ya Kenya kurekodi muziki kwenye santuri mahandalizi ya safari pamoja na gharama kubwa zilihitajika kabla ya Bendi ya muziki kwenda Kenya.Muziki wa zamani ulitumia vyombo [hala] za muziki hivyo ujuzi wa ulihitajika zaidi.Vipaji vya wanamuziki ilikuwa ni jambo lisilokwepeke hata kidogo.

      Muziki wa kizazi kipya ni vurugu kubwa hakuna wataalamu wa kupiga hala za muziki eg Solo guita,Rhyzim,Bass,Saxphone,Dru m,Tumba na kinanda.Wapo waimbaji wa mashairi ambao ukiwapa hata kinanda hawawezi kutumia.hawana ujuzi wa muziki hata kidogo mara kadha nimehudhuria maonyesho ya muziki wa kizazi kipya nimegundua wameathiria sana na utamaduni wa wanamuziki wa Marekani na Ulaya.Utakuta mwanamuziki wa Kizazi kipya anashusha suruali chini ya makalio,katoboa masikio,kasuka nywele,kajichubua na upuuzi mwingine mwingi unaoufahamu.

      Wanamuziki wa Injili wa siku hizi tofauti na wa zamani hawana ujuzi wa muziki mbaya zaidi hawatumii neno la Mungu kwenye muziki wao maneno ya mitaani yamejaa kwenye muziki wanaouita muziki wa Injili.Muziki wa Injili unapaswa kwa namna yoyote ujikite kwenye maandiko matakatifu na si vinginevyo.Muziki wa Injili unapaswa kutumia tune ya kanisa na si Sebene au Rhumba na nk.Sebene na Rhumba hazina nafasi kwenye muziki wa Injili [Kanisa].Uchezajiwa wa wanamuziki wanaojiita wanamuziki wa Injili hauna tofauti na wanamuziki wa bendi za muziki wa dansi kabisa wakati mwingine nalazimika kubadiluisha chanel kukwepa kuangalia wanamuziki wa Injili wanvyodhalilisha kanisa na ukristo.Uvaaji wa wanamuziki wa Injili unatia kichefu chefu.

      Wapo wanamuziki wa Injili na kwanya mbali mbali zinazojitahidi kufuata njia sahihi ya uimbaji wa muziki wa Injili lakini hazipewi umuhimu wa kipekee kwenye TV station zetu pengine uelewa wa mdogo wa muziki wa Injili ndani ya vyombo vyetu vya habari umechagia kuporomosha muziki wa Injili.

    17. #17
      Kabota's Avatar
      Member Array
      Join Date : 15th August 2009
      Posts : 39
      Rep Power : 508
      Likes Received
      1
      Likes Given
      0

      Default Re: Kwa nini Chidumule kawachana waimbaji wa bongo flavor pamoja na wale wa dini?

      Ni kweli waimbaji wengi wa kizazi si wanamuziki kama wengi wanavyosema siku zote. Lakini hata hivyo katika biashara ya muziki hicho si kitu cha ajabu. Najua wengi wenu mnaosoma maoni haya ni wasomi na mnafahamu namna muziki kwa wenzetu unavyohusisha watu wengi mpaka wimbo ukausikia hewani.

      Kuna wanamuziki wengi wa nje ambao ni waimbaji tu(kutoa sauti basi) ambao hawahusiki katika kutunga, kuandaa melody, kupiga chombo chochote cha muziki na zoezi zima la utayarishaji. Kila kitu kinafanywa na mtu mwingine. Lakni niambie jinsi albam zao zinavyouza! Mwimbaji asipoweza kucheza chombo chochote cha muziki haimanishi kuwa hawezi kabisa kupewa heshima yake. Sababu kubwa inayowafanya wanamuziki wa zamani wawadharau wale wa bongo flava ni wivu tu. Walikuwa na nyimbo nzuri sana katu sikatai lakini hazikuwapa chochote.

      Leo hii vijana wanaodharauliwa kuwa si wanamuziki bali wababaishaji tu ndo ambao wamefanikiwa hata kuiweka kdg Tanzania kwenye ramani ya muziki duniani. Ni bendi gani ama mwanamuziki gani wa zamani ambaye amewashawahi kutajwa kuwania tuzo yoyote kubwa duniani? Kwa wengine yaweza kuwa ni sababu ndogo lakini hivyo ndo vigezo vya kutambua kama wanamuziki wetu wanatambuliwa nje ya mipaka. Wanamuziki wa zamani waache wivu kwani kulalama hadharani juu ya vijana wa sasa hv hakutasaidia chochote kama ujumbe wao wanautoa kwa dharau.

      Pengine hawafurahishwi na maisha wanayoishi vijana wa sasa yaani jinsi wanavyovaa, wanavyoongea, maudhui katika nyimbo zao lakni watambue kuwa hao ni vijana sio wazee. Namheshimu sana mwanamuziki anayeipa heshima kazi ama style ya mwenzie hata kama haipendi.

      Michael Jackson kabla ya kufa alikuwa ameshafanya kazi na wasanii wa sasa kama Akon, 50 Cent. Wil.iam kuonesha heshima katika mabadiliko ya muziki na pia kuwavutia mashabiki ambao muziki wa zamani hawaujui. Hayo ni maoni tu.

    18. #18
      NGULI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st March 2008
      Location : HOME
      Posts : 4,441
      Rep Power : 1461
      Likes Received
      214
      Likes Given
      1

      Default Re: Kwa nini Chidumule kawachana waimbaji wa bongo flavor pamoja na wale wa dini?

      Quote By Ngongo View Post
      Wanamuziki wa zamani walifanyakazi zao kwenye mazingira magumu ukilinganisha na wanamuziki wa Bongo flavor.
      Enzi za Chidumule na wanamuziki wa zamani hawakuwa na fursa nyingi kama ilivyo kipindi hiki cha wanamuziki wa kizazi kpya.studio za kurekodi ilikuwa moja hapa Tanzania RTD kuliwa pia masharti ya nyimbo kurekodiwa mashairi yalifanyiwa uhariri kabla nyimbo haijaruhusiwa kurekodiwa.Wanamuziki wa Tanzania walilazimika kwenda nchi jirani ya Kenya kurekodi muziki kwenye santuri mahandalizi ya safari pamoja na gharama kubwa zilihitajika kabla ya Bendi ya muziki kwenda Kenya.Muziki wa zamani ulitumia vyombo [hala] za muziki hivyo ujuzi wa ulihitajika zaidi.Vipaji vya wanamuziki ilikuwa ni jambo lisilokwepeke hata kidogo.

      Muziki wa kizazi kipya ni vurugu kubwa hakuna wataalamu wa kupiga hala za muziki eg Solo guita,Rhyzim,Bass,Saxphone,Dru m,Tumba na kinanda.Wapo waimbaji wa mashairi ambao ukiwapa hata kinanda hawawezi kutumia.hawana ujuzi wa muziki hata kidogo mara kadha nimehudhuria maonyesho ya muziki wa kizazi kipya nimegundua wameathiria sana na utamaduni wa wanamuziki wa Marekani na Ulaya.Utakuta mwanamuziki wa Kizazi kipya anashusha suruali chini ya makalio,katoboa masikio,kasuka nywele,kajichubua na upuuzi mwingine mwingi unaoufahamu.

      Wanamuziki wa Injili wa siku hizi tofauti na wa zamani hawana ujuzi wa muziki mbaya zaidi hawatumii neno la Mungu kwenye muziki wao maneno ya mitaani yamejaa kwenye muziki wanaouita muziki wa Injili.Muziki wa Injili unapaswa kwa namna yoyote ujikite kwenye maandiko matakatifu na si vinginevyo.Muziki wa Injili unapaswa kutumia tune ya kanisa na si Sebene au Rhumba na nk.Sebene na Rhumba hazina nafasi kwenye muziki wa Injili [Kanisa].Uchezajiwa wa wanamuziki wanaojiita wanamuziki wa Injili hauna tofauti na wanamuziki wa bendi za muziki wa dansi kabisa wakati mwingine nalazimika kubadiluisha chanel kukwepa kuangalia wanamuziki wa Injili wanvyodhalilisha kanisa na ukristo.Uvaaji wa wanamuziki wa Injili unatia kichefu chefu.

      Wapo wanamuziki wa Injili na kwanya mbali mbali zinazojitahidi kufuata njia sahihi ya uimbaji wa muziki wa Injili lakini hazipewi umuhimu wa kipekee kwenye TV station zetu pengine uelewa wa mdogo wa muziki wa Injili ndani ya vyombo vyetu vya habari umechagia kuporomosha muziki wa Injili.
      Mkubwa hakika nimekupata maelezo mazuri sana,
      Some sweet hearts are bitter than chloroquine packed in a sweet paper

    19. #19
      FirstLady1's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th July 2009
      Location : Mama Mwenye Nyumba
      Posts : 15,052
      Rep Power : 3723
      Likes Received
      3621
      Likes Given
      5885

      Default Re: Kwa nini Chidumule kawachana waimbaji wa bongo flavor pamoja na wale wa dini?

      anachokiona ndicho alichokisema na ni klweli usiopingika
      No one is in charge of your happiness except you...
      God time is the best..
      Hadi tufike 2015 tutakuwa tumekoma

    20. #20
      The Finest's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th July 2010
      Posts : 21,682
      Rep Power : 6128
      Likes Received
      5861
      Likes Given
      4948

      Default Re: Kwa nini Chidumule kawachana waimbaji wa bongo flavor pamoja na wale wa dini?

      Hawa wa bongo fleva wanajulikana tu, ila hawa wa muziki wa injili ndio huwa nawashangaa hawana tofauti na wa bongo flava
      "What is legal, but not logical, logical, but not legal, and neither logical, nor legal?"


    Page 1 of 2 12 LastLast

    Similar Topics

    1. Viongozi wa dini na wale vingozi wastaafu wanamaanisha nini?
      By Ndallo in forum Tanzania 2010-2015
      Replies: 3
      Last Post: 19th October 2010, 22:50
    2. Waimbaji wa makundi ya dini kushiriki kampeni
      By Anfaal in forum Tanzania 2010-2015
      Replies: 98
      Last Post: 27th August 2010, 01:45
    3. JF Bongo Flavor duh!
      By Tripo9 in forum Entertainment
      Replies: 1
      Last Post: 22nd April 2010, 16:27

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...