Wanabodi,
Mimi ni miongoni mwa wanabodi ambao hupenda kupongeza pale panapo stahili pongezi as "encouragement" ili kuendeleza mazuri, na hukosoa pale panapo stahili critique kama mambo hayaendi yanavyopaswa kwa lengo la kujenga yaani "contractive cricticisim.
Nachukua fursa hii kuipongeza Televisheni ya Taifa TBC-1 kwa kitu kinachoitwa "Live News interactive" ambayo sina tafsiri sahihi kwa Kiswahili sanifu " Habari Shirikirishi za Moja kwa Moja " Live!.
Pongezi hizi zimefuatia jinsi TBC-1 ilivyotumia "Live News interactive" katika kuripoti tukio la ajali ya meli ya Zanzibar compared to ITV.
Kwa kuanzia habari ya ajali hiyo ya meli huko Zanzibar, ndio lead story kwa taarifa zote za habari usiku huu, na ndivyo itakavyokuwa kwenye magazeti ya kesho. ITV na TBC zote zimeitangaza hii habari ya kuzama kwa meli kama lead story. Habari inapokuwa ni lead story, inategemewa habari hiyo ndio itakuwa ni habari ya kwanza yaani "1st news item" kwa ITV baada ya kuitangaza kama lead story, habari yenyewe ndio ilikuwa "last News Item" huku ikisema hakuna taarifa yoyote rasmi ya serikali!. Kwa TBC-1 taarifa ya habari hiyo ndio ilikuwa lead story na habari ya kwanza, na ikaanza kwa taarifa rasmi ya serikali!. Hii inamaana reporter wa ITV ili file story mapema kabla ya taarifa rasmi ya serikali haijatoka!.
Baada ya TBC kutuletea taarifa rasmi, wakafuatia na taarifa ya kilichotokea Bungeni Dodoma ambapo kwa ITV hii ndio ilikuwa lead story yao. Baada ya kumaliza na kilichotokea Bungeni, wakamtafuta Waziri wa Mambo ya Ndani, akasungumza live ndani ya taarifa ya habari na kumalizia na katibu wa Bunge nae live nda ni ya taarifa ya habari kuhusu bunge linajipangaje!.
Kitendo cha kumuita mtu "live" ndani ya taarifa ya habari hii ndio hiyo "live News Interactive" kama CCN na BBC!.
Hivyo kwa Tanzania, TBC-1 ndio wamekuwa pioneers wa "Live News Anchors" vs " News Readers". News Reader ni msomaji wa habari, ambaye anakuwa anasoma habari alizoandikiwa!, sifa kuu ya news reader ni kuwa na "sauti nzuri", (news voice) na "kuonekana vyema", (photogenic). Kila sauti, ni sauti nzuri, na kila sauti inaweza kutangaza, ila sio kila sauti, ni sauti nzuri kwa kusomea habari. Ukishakuwa na sauti nzuri kwa kusomea habari, wewe unakuwa msoma habari!. Na kila mtu ana sura nzuri na muonekano mzuri,ila sio kila muonekano mzuri ni photogenic, wako wengi wenye sura nzuri, na muonekano mzuri, lakini bado hawawezi kuonekana vizuri kwenye screen, lakini ikitokea mtu ukawa na sauti nzuri ya kusomea habari, na muonekano mzuri wa kuonekanika kwenye screen (photogenic), basi wewe unatosha kabisa kuwa mtangazaji, news reader, hata kama kichwani hamna kitu!, ndio maana kuna watangazaji kibao kwenye TV ni wauza sura tuu au watangazaji kibao maredioni ni vilaza tuu wa kutupwa kwa sababu kigezo ni sura na sauti na sio intelect!.
Lakini kuwa 'news anchor', zaidi ya kuwa na sauti nzuri na sura ya kutazamika vizuri, lazima uwe knowlegable na intelligent kuweza kufanya mahojiano live inside the news!, kitu ambacho mpaka sasa ni TBC pekee wameonyesha uwezo huo!.
ITV, Channel Ten na Star TV, zote wanazo "Live Interactive Srudio" lakini hawaitumii kwenye news bali huitumia kwenye kusoma magazeti na vile vipindi vya mahojiano ya asubuhi!. Hii ni changamoto kwa TV nyingine, kunapotokea habari kubwa, unawatafuta ma specialist na kuwahoji live inside the news.
Hii inamaanisha Tanzania sasa na sisi tunaingia kwenye TV News revolution kwa kuachana na makasuku wasoma habari, kuelekea kwenye specialization zaidi kwa 'anchorman' ambaye ni mtangazaji aliyebobea, hivyo kuijengea heshima zaidi hii tasnia ya habari za Radio na TV.
ITV, Channel Ten na Star TV zilitangulia ujio wa TBC kwa takriban miaka 6 kabla, na TVZ iliyotangulia tangu mwaka 1972, lakini sasa ndio inachechemea kana kwamba inasubiria kujifia!.
Ama kweli, kutangulia sii kufika!, Hongera sana TBC-1 kwa Kuonyesha njia ili wengine wafuatie!.
Hata hivyo, TBC inatakiwa iji redifine its role, wengi wanaidhania TBC kuwa ni TV ya serikali!, kiukweli, TBC japo serikali imeihodhi kama TV yake, TBC sio TV ya serikali, ni public Television Broadcasting, ambayo is paid by taxpayers money!, inabidi iwatumikie watu na sio kuitumikia serikali!. Kwa hali ilivyo sasa, TBC inajikomba komba sana kwab serikali. Viongozi wa TBC wanapaswa kuwatumikia wananchi na ikibidi kuweka vipindi critical kwa serikali, na huko ndiko kuisaidia serikali kiukweli.
Na nyinyi waserikali, msiitumie TBC as if ni TV yenu, TBC ni TV yetu sote, natayarisha maoni yangu kwenye katiba mpya kuhakikisha Watanzania wote, tunapata excess ya kuitumia TBC kwa manufaa ya taifa na sio kama ilivyo sasa, kutumika zaidi kwa manufaa ya serikali mpaka wengi wakiidhania TBC ni TV ya Serikali, kitu ambacho sio cha kweli!.
Wasalaam.
Pascal Mayalla
NB. Pascal Mayalla aliwahi kuwa Mtayarishaji/Mtangazaji Mwandamizi Grade I wa TVT.


Reply With Quote

Follow Us Here