Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Live News Interactive!-TBC-1 Yastahili Pongezi!. ''Hongera TBC-1" Keep it Up!

    Report Post
    Page 3 of 3 FirstFirst 123
    Results 41 to 60 of 60
    1. #1
      Pascal Mayalla's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 2nd August 2009
      Posts : 210
      Rep Power : 3207
      Likes Received
      231
      Likes Given
      1531

      Default Live News Interactive!-TBC-1 Yastahili Pongezi!. ''Hongera TBC-1" Keep it Up!

      Wanabodi,

      Mimi ni miongoni mwa wanabodi ambao hupenda kupongeza pale panapo stahili pongezi as "encouragement" ili kuendeleza mazuri, na hukosoa pale panapo stahili critique kama mambo hayaendi yanavyopaswa kwa lengo la kujenga yaani "contractive cricticisim.

      Nachukua fursa hii kuipongeza Televisheni ya Taifa TBC-1 kwa kitu kinachoitwa "Live News interactive" ambayo sina tafsiri sahihi kwa Kiswahili sanifu " Habari Shirikirishi za Moja kwa Moja " Live!.

      Pongezi hizi zimefuatia jinsi TBC-1 ilivyotumia "Live News interactive" katika kuripoti tukio la ajali ya meli ya Zanzibar compared to ITV.

      Kwa kuanzia habari ya ajali hiyo ya meli huko Zanzibar, ndio lead story kwa taarifa zote za habari usiku huu, na ndivyo itakavyokuwa kwenye magazeti ya kesho. ITV na TBC zote zimeitangaza hii habari ya kuzama kwa meli kama lead story. Habari inapokuwa ni lead story, inategemewa habari hiyo ndio itakuwa ni habari ya kwanza yaani "1st news item" kwa ITV baada ya kuitangaza kama lead story, habari yenyewe ndio ilikuwa "last News Item" huku ikisema hakuna taarifa yoyote rasmi ya serikali!. Kwa TBC-1 taarifa ya habari hiyo ndio ilikuwa lead story na habari ya kwanza, na ikaanza kwa taarifa rasmi ya serikali!. Hii inamaana reporter wa ITV ili file story mapema kabla ya taarifa rasmi ya serikali haijatoka!.

      Baada ya TBC kutuletea taarifa rasmi, wakafuatia na taarifa ya kilichotokea Bungeni Dodoma ambapo kwa ITV hii ndio ilikuwa lead story yao. Baada ya kumaliza na kilichotokea Bungeni, wakamtafuta Waziri wa Mambo ya Ndani, akasungumza live ndani ya taarifa ya habari na kumalizia na katibu wa Bunge nae live nda ni ya taarifa ya habari kuhusu bunge linajipangaje!.

      Kitendo cha kumuita mtu "live" ndani ya taarifa ya habari hii ndio hiyo "live News Interactive" kama CCN na BBC!.
      Hivyo kwa Tanzania, TBC-1 ndio wamekuwa pioneers wa "Live News Anchors" vs " News Readers". News Reader ni msomaji wa habari, ambaye anakuwa anasoma habari alizoandikiwa!, sifa kuu ya news reader ni kuwa na "sauti nzuri", (news voice) na "kuonekana vyema", (photogenic). Kila sauti, ni sauti nzuri, na kila sauti inaweza kutangaza, ila sio kila sauti, ni sauti nzuri kwa kusomea habari. Ukishakuwa na sauti nzuri kwa kusomea habari, wewe unakuwa msoma habari!. Na kila mtu ana sura nzuri na muonekano mzuri,ila sio kila muonekano mzuri ni photogenic, wako wengi wenye sura nzuri, na muonekano mzuri, lakini bado hawawezi kuonekana vizuri kwenye screen, lakini ikitokea mtu ukawa na sauti nzuri ya kusomea habari, na muonekano mzuri wa kuonekanika kwenye screen (photogenic), basi wewe unatosha kabisa kuwa mtangazaji, news reader, hata kama kichwani hamna kitu!, ndio maana kuna watangazaji kibao kwenye TV ni wauza sura tuu au watangazaji kibao maredioni ni vilaza tuu wa kutupwa kwa sababu kigezo ni sura na sauti na sio intelect!.

      Lakini kuwa 'news anchor', zaidi ya kuwa na sauti nzuri na sura ya kutazamika vizuri, lazima uwe knowlegable na intelligent kuweza kufanya mahojiano live inside the news!, kitu ambacho mpaka sasa ni TBC pekee wameonyesha uwezo huo!.

      ITV, Channel Ten na Star TV, zote wanazo "Live Interactive Srudio" lakini hawaitumii kwenye news bali huitumia kwenye kusoma magazeti na vile vipindi vya mahojiano ya asubuhi!. Hii ni changamoto kwa TV nyingine, kunapotokea habari kubwa, unawatafuta ma specialist na kuwahoji live inside the news.

      Hii inamaanisha Tanzania sasa na sisi tunaingia kwenye TV News revolution kwa kuachana na makasuku wasoma habari, kuelekea kwenye specialization zaidi kwa 'anchorman' ambaye ni mtangazaji aliyebobea, hivyo kuijengea heshima zaidi hii tasnia ya habari za Radio na TV.

      ITV, Channel Ten na Star TV zilitangulia ujio wa TBC kwa takriban miaka 6 kabla, na TVZ iliyotangulia tangu mwaka 1972, lakini sasa ndio inachechemea kana kwamba inasubiria kujifia!.

      Ama kweli, kutangulia sii kufika!, Hongera sana TBC-1 kwa Kuonyesha njia ili wengine wafuatie!.

      Hata hivyo, TBC inatakiwa iji redifine its role, wengi wanaidhania TBC kuwa ni TV ya serikali!, kiukweli, TBC japo serikali imeihodhi kama TV yake, TBC sio TV ya serikali, ni public Television Broadcasting, ambayo is paid by taxpayers money!, inabidi iwatumikie watu na sio kuitumikia serikali!. Kwa hali ilivyo sasa, TBC inajikomba komba sana kwab serikali. Viongozi wa TBC wanapaswa kuwatumikia wananchi na ikibidi kuweka vipindi critical kwa serikali, na huko ndiko kuisaidia serikali kiukweli.

      Na nyinyi waserikali, msiitumie TBC as if ni TV yenu, TBC ni TV yetu sote, natayarisha maoni yangu kwenye katiba mpya kuhakikisha Watanzania wote, tunapata excess ya kuitumia TBC kwa manufaa ya taifa na sio kama ilivyo sasa, kutumika zaidi kwa manufaa ya serikali mpaka wengi wakiidhania TBC ni TV ya Serikali, kitu ambacho sio cha kweli!.

      Wasalaam.

      Pascal Mayalla

      NB. Pascal Mayalla aliwahi kuwa Mtayarishaji/Mtangazaji Mwandamizi Grade I wa TVT.
      Last edited by Pascal Mayalla; 21st July 2012 at 10:24.

    2. RukaaJuu Final

    3. #41
      Pascal Mayalla's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 2nd August 2009
      Posts : 210
      Rep Power : 3207
      Likes Received
      231
      Likes Given
      1531

      Default Re: Live News Interactive!-TBC-1 Yastahili Pongezi!. ''Hongera TBC-1" Keep it Up!

      Quote By Inkoskaz
      Kaka sikubaliani nawe...labda ungesema wameileta ili kuficha aibu ya makinda...sijaona hata kipande kilichoonyesha ajali...japo ITV wameonyesha still pics.hata mahojiano na majeruhi,mashuhuda hamna...halafu masaa 7 baada ya ajali bado wanaripoti watu waliofariki ni 12 wakati BBC na VOA na taarifa sahihi tulizonazo hata humu JF zinathibitisha miili 62 Kuopolewa,,,am sorry Pascal kwa hili hapana!
      Mkuu Inkoskazi, (jina lako linanikumbusha Alan Quaterman), nakubaliana na wewe kwenye hili na pia naheshimu kutokubaliana. Pongezi zangu ni za kitu kiitwachwo "Live TV News Interactive", kukatisha taarifa ya habari na kujiunga na mtu live yuko studio nyingine"!. =TBC imefungua milango ya kuondoka toka new readers kuelekea kwenye news anchors!.

    4. #42
      Pascal Mayalla's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 2nd August 2009
      Posts : 210
      Rep Power : 3207
      Likes Received
      231
      Likes Given
      1531

      Default Re: Live News Interactive!-TBC-1 Yastahili Pongezi!. ''Hongera TBC-1" Keep it Up!

      Quote By Mohamedi Mtoi
      Kwanza hakuna tv station inaitwa tbc1 kwa sasa! Natambua kuwa ipo TBCCM kituo cha mapoyoyo ambacho kazi yake kubwa ni kuwapumbaza wananchi kwa kuilinda ccm kwa habari nzuri tu huku wakificha uozo hata ulioko wazi machoni mwa watoto. Kuitetea Tbccm unatakiwa kuwa na akili za maiti. Ndiyo.
      Mkuu Mohamed Mtoi, kitendo cha kukanusha kitu ambacho kipo na kina exist in reality, kinaitwa "denial" na hiyo ni hali ya matatizo ya kisaikolojia ya kuukana ukweli ili kujifariji nafsi temporalily kama wafanywavyo wanywa pombe kupunguza mawazo wakati wana tatizo, atalewa atasahau na atalala, akiamka tatizo atalikuta!. Hivyo endelea kujifariji TBC-1 haipo, na iliyopo ni TBCCM, na jee ndio tuisubirie na TBCDM ile 2015?.

      Quote By Mohamedi Mtoi
      Kwanza wameonyesha dharau kubwa kwa watu wa Zanzibar. Tukio limetokea zanzibar waache kumhoji waziri mwenye dhamana hata ya usafirishaji/uchukuzi alieko karibu na tukio mumhoji mtu alieko Dodoma tena kwa takwimu za tangu mchana? Nafasi ya mawaziri wa Zanzibar iko wapi?
      Wa kwanza kwenye news ya TBC ni msemaji wa SMZ!. Ila kwenye hili la "Live TV news Interactive", linaweza kufanyika mahali kwenye live TV transmission only!, hii inamaana "live news interactive" inaweza au kufanyika studio, au mahali kwenye OB (Outside Broadcast). TBC wana OB Dodoma kwa ajili ya bunge live, hawana OB Zanzibar, ama mahali pengine popote!.

      Quote By Mohamedi Mtoi
      KPili tuwasifu tbccm kwa kipi? Kurusha habari si ndio jukumu lao na wanatimiza wajibu wao? Yaani wawatende wapenda habari kwa upendeleo wao wakianza kuiona njia wasifiwe?

      Kituo bora mpaka sasa kwa upande wangu ni jf. Period
      Kama una watoto, umewaandikisha shule, kusoma kwa bidii si ni wajibu wao?, hivi mwanao akifanya vizuri darasani na kuwa wa kwanza, wewe humpongezi?!. Lengo la pongezi hizo sio kutoa sifa kuwa "mwanangu ana akili!. bali "appreciation ya kazi nzuri" mwanao aliyofanya na encouragement wazidi kufanya vizuri!.

      Mimi nina watoto 6, watano kati yao wanasoma. Nimeweka prize money kwa kila scores za A, B na C na kila mtoto anayeshika nafasi ya kwanza, anakula bingo nene!. Wanangu wanashindana kushika nafasi ya za juu madarasani mwao due to appreciation and ancouragement!.

      TBC inalaumiwa sana kwa madudu chungu mzima, lakini inapofanya zuri hata moja tuu hivi haistahili pongezi?!. Au kwa vile kwako ni TBCCM then ni lawama mtindo mmoja, na pongezi zitaanza kumiminika pale itakapokuwa TBCDM baada ya 2015?!.
      Last edited by Pascal Mayalla; 21st July 2012 at 12:27.

    5. #43
      Pascal Mayalla's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 2nd August 2009
      Posts : 210
      Rep Power : 3207
      Likes Received
      231
      Likes Given
      1531

      Default Re: Live News Interactive!-TBC-1 Yastahili Pongezi!. ''Hongera TBC-1" Keep it Up!

      Quote By luluka
      taarifa yako imekaa ya kujipendekeza pendekeza flani hivi!
      Mkuu Luluka, kuna tofauti kati ya kutoa pongezi ili kujipendekeza na kujikomba komba, na kutoa pongezi kwa encouragement!. Wanaotoa pongezi ili kujipendekeza pendekeza wao watasifu tuu, mwanzo mwisho, au fagilia tuu!. Wanaotoa pongezi for encouragement, watasifu panapostahili sifa, na ku criticize pale wanapoboronga!. Hi umenisoma kule niliposema TBC ni TV ya taifa na sio TV ya serikali?. Mtu anayejikomba komba mahali, anaweza kurusha na madongo?.

    6. #44
      Pascal Mayalla's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 2nd August 2009
      Posts : 210
      Rep Power : 3207
      Likes Received
      231
      Likes Given
      1531

      Default Re: Live News Interactive!-TBC-1 Yastahili Pongezi!. ''Hongera TBC-1" Keep it Up!

      Quote By Mfamaji
      BTW ulikuwa unamaanisha encouragement ...hapo ulipoandika "incouragement"? NA hii "contractive criticisim'' ulimaanisha constructive criticism? Kaazi kweli kweli.
      Mkuu Mfamaji, excatly ndicho nilichomaanisha, hizi ni lugha za watu, mimi ni product ya UPE na wanangu wanasoma shule za kata!.

    7. #45
      Lokissa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th November 2010
      Location : Goba
      Posts : 4,092
      Rep Power : 5807
      Likes Received
      1026
      Likes Given
      2876

      Default Re: Live News Interactive!-TBC-1 Yastahili Pongezi!. ''Hongera TBC-1" Keep it Up!

      pasco TBC itabaki kuwa TBCCM1 siku zote labda itakaporudishwa mikononi
      mwa umma na sii kuwa chini ya umiliki wa serikali ka ailivo sasa.
      Tofautisha kati ya KBC,BBC na TBC kiuongozi,
      TBC haiko huru,mkurugenzi kuteuliwa na rais, lazima atangaze habari zinazowapendeza viongozi na kutoiudhi serikali, lazima iwabebe CCM huku kodi zetu zikitumika
      hata baba yangu kijijini haangalii TBC wakati wa news imeshapoteza weledi wake tangu aondoke TIDO

      sitaiamini TBC hadi hapo itakapokuwa huru na uongozi wake uwe huru labda mkurugenzi awajibike kwa bunge na sio waziri.
      Pascal Mayalla likes this.
      You may know me but you have no Idea who I am !

    8. Miaka 50

    9. #46
      Pascal Mayalla's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 2nd August 2009
      Posts : 210
      Rep Power : 3207
      Likes Received
      231
      Likes Given
      1531

      Default Re: Live News Interactive!-TBC-1 Yastahili Pongezi!. ''Hongera TBC-1" Keep it Up!

      Quote By Lokissa
      pasco TBC itabaki kuwa TBCCM1 siku zote labda itakaporudishwa mikononi
      mwa umma na sii kuwa chini ya umiliki wa serikali ka ailivo sasa.
      Tofautisha kati ya KBC,BBC na TBC kiuongozi,
      TBC haiko huru,mkurugenzi kuteuliwa na rais, lazima atangaze habari zinazowapendeza viongozi na kutoiudhi serikali, lazima iwabebe CCM huku kodi zetu zikitumika
      hata baba yangu kijijini haangalii TBC wakati wa news imeshapoteza weledi wake tangu aondoke TIDO

      sitaiamini TBC hadi hapo itakapokuwa huru na uongozi wake uwe huru labda mkurugenzi awajibike kwa bunge na sio waziri.
      Mkuu Lokissa, kwani Tido aliteuliwa na nani?. Kama Tido aliveza ku maitain TBC independence dhidi ya serikali, Mshana atashindwa nini?. Baada ya pongezi zangu nimetoa angalizo kuwa TBC sio TV ya serikali ni TV ya umma. Tena katika miaka hii mitatu iliyobakia,nitautumia ushawishi nilionao kwa uongozi wa TBC uruhusu vipindi analitical na critical vitakavyokosoa serikali, ili kuuthibitishia umma kuwa TBC ni ya umma na sio ya serikali.
      Lokissa likes this.

    10. #47
      simplemind's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th April 2009
      Posts : 2,850
      Rep Power : 1157
      Likes Received
      509
      Likes Given
      0

      Default Re: Live News Interactive!-TBC-1 Yastahili Pongezi!. ''Hongera TBC-1" Keep it Up!

      Best kama wangetupa shuguli ya ukoaji live kutoka sehemu ya tukio via setellite link. Majirani wetu wanayo uwezo huu.
      Pascal Mayalla likes this.

    11. #48
      Al Zagawi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th March 2009
      Location : Tabora
      Posts : 832
      Rep Power : 685
      Likes Received
      160
      Likes Given
      51

      Default Re: Live News Interactive!-TBC-1 Yastahili Pongezi!. ''Hongera TBC-1" Keep it Up!

      TBC naangalia vipindi viwili tu....Ze Komedi na Mziki...at least hapo kuna ukweli kidogo, kwengine ni ujinga mtupu.

      Najiskia kichefuchefu nnapoendelea kuiona TBC ikiwa hewani, natamani ife leo na kisha tuanzishe mchakato mpya wa kuanzisha new Television ya Taifa.
      Pascal Mayalla likes this.
      ...........Uwanja wa siasa katika nchi karibu zote za Kiafrika, ni uwanja uliotekwa na majambazi ambao wanafanya wanachotaka, vile wanavyotaka..........Jenerali Ulimwengu, Raia Mwema Namba 278.

    12. #49
      Al Zagawi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th March 2009
      Location : Tabora
      Posts : 832
      Rep Power : 685
      Likes Received
      160
      Likes Given
      51

      Default Re: Live News Interactive!-TBC-1 Yastahili Pongezi!. ''Hongera TBC-1" Keep it Up!

      Quote By Pascal Mayalla
      Baada ya pongezi zangu nimetoa angalizo kuwa TBC sio TV ya serikali ni TV ya umma.
      ni kweli kwa kuangalia makaratasi.....lakini utendaji unaonyesha vinginevyo. Ngoma inapigwa kipemba watu wanacheza kinyamwezi.


      Quote By Pascal Mayalla
      Tena katika miaka hii mitatu iliyobakia,nitautumia ushawishi nilionao kwa uongozi wa TBC uruhusu vipindi analitical na critical vitakavyokosoa serikali, ili kuuthibitishia umma kuwa TBC ni ya umma na sio ya serikali.
      miaka mitatu iliyobakia kufanya nini????

      Quote By Pascal Mayalla
      Tena katika miaka hii mitatu iliyobakia,nitautumia ushawishi nilionao kwa uongozi wa TBC uruhusu vipindi analitical na critical vitakavyokosoa serikali, ili kuuthibitishia umma kuwa TBC ni ya umma na sio ya serikali.
      ushawishi gani mkuu....kwani wewe peke yako ndiye mwenye kulipa kodi inayoendesha TBC??? ikiwa TBC hawaoni kasoro yoyote katika ujinga wao, wewe ndiye utaweza kuwashawishi hao akina Mshana???

      Najua ungependa na ungetamani TBC iwe hivyo unavyotaka(chombo cha uma na si serikali)...bahati mbaya hilo halitoweza kutokea, TBC na CCM ni kama Lila na Fila..havitengemani.
      Pascal Mayalla likes this.
      ...........Uwanja wa siasa katika nchi karibu zote za Kiafrika, ni uwanja uliotekwa na majambazi ambao wanafanya wanachotaka, vile wanavyotaka..........Jenerali Ulimwengu, Raia Mwema Namba 278.

    13. #50
      Pascal Mayalla's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 2nd August 2009
      Posts : 210
      Rep Power : 3207
      Likes Received
      231
      Likes Given
      1531

      Default Re: Live News Interactive!-TBC-1 Yastahili Pongezi!. ''Hongera TBC-1" Keep it Up!

      Quote By simplemind
      Best kama wangetupa shuguli ya ukoaji live kutoka sehemu ya tukio via setellite link. Majirani wetu wanayo uwezo huu.
      Mkuu Simplemind, Tanzania hatuna TV yoyote yenye uwezo wa kurusha live kupitia mobile satellite link!. Live zote za bongo unazoziona zinapitia microwave link!. Star TV wanayo satellite link ila sio mobile, ni fixed!. Ila pale nje ya mjengo wa Clouds, nimeona wana OB van yao ndogo na juu ina ka satelite dish, tatizo Clouds hawana Chanell kwenye Satellite, wanaitumia satellite ya Startimes, hivyo in short kwenye mambo ya kutangaza live kupitia Satillite, kwa Tanzania, safari bado ni ndefu!.

    14. #51
      Pascal Mayalla's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 2nd August 2009
      Posts : 210
      Rep Power : 3207
      Likes Received
      231
      Likes Given
      1531

      Default Re: Live News Interactive!-TBC-1 Yastahili Pongezi!. ''Hongera TBC-1" Keep it Up!

      Quote By Al Zagawi
      ni kweli kwa kuangalia makaratasi.....lakini utendaji unaonyesha vinginevyo. Ngoma inapigwa kipemba watu wanacheza kinyamwezi.

      miaka mitatu iliyobakia kufanya nini????

      ushawishi gani mkuu....kwani wewe peke yako ndiye mwenye kulipa kodi inayoendesha TBC??? ikiwa TBC hawaoni kasoro yoyote katika ujinga wao, wewe ndiye utaweza kuwashawishi hao akina Mshana???

      Najua ungependa na ungetamani TBC iwe hivyo unavyotaka(chombo cha uma na si serikali)...bahati mbaya hilo halitoweza kutokea, TBC na CCM ni kama Lila na Fila..havitengemani.
      Mkuu Al Zagawi, ni miaka mitatu kufikia 2015!, au wewe hujui kitakachotokea?.

      Kama ulinisoma mwisho, nimesema niliwahi kufanya kazi TVT, kwa sasa mimi ni independent producer, kila mwaka napeleka program zangu zaidi ya 100 hapo TBC na zinarushwa.

      Ushawishi wangu ni kama wanavyoruhusu vipindi kutoka nje vya non political issues, sasa waruhusu na political programs kutoka nje ambazo zitakuwa analytical na kuikosoa serikali!. Hili nitajaribu!.

      Kuna uwezekano mkubwa, baadhi ya shutuma kwa TBC ni za asumptions tuu, kuwa wanaitetea sana serikali, kuna vipindi very critical kama kile cha This Week in Prespective" kinachoendeshwa na Adam Simbeye, sometimes kiko very critical ila wengi hamkioni.

      Watanzania wengi tuna tatizo la kutojaribu!. Kwa vile TBC ni TV yetu, tuitumie, tusiiogope!. Inawezekana uoga wetu ni kama uoga wa baadhi yetu kwa mtu lofa kama mimi unapomuona mrembo very striking, unasita kumtokea, kwa kujifikiria, utampa nini?!. Kumbe ni uoga wa bure tuu, kwani huyo mrembo tayari anacho kila kitu cha dunia hii na alichokosa ndicho hicho hicho nilichonacho liofa mimi!. Kumbe ningemtokea tuu ningekubaliwa!. Sasa ndio naahidi TBC nitaitokea!.

    15. #52
      Lokissa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th November 2010
      Location : Goba
      Posts : 4,092
      Rep Power : 5807
      Likes Received
      1026
      Likes Given
      2876

      Default Re: Live News Interactive!-TBC-1 Yastahili Pongezi!. ''Hongera TBC-1" Keep it Up!

      paschal umma hauna sauti juu YA TBC bali serikali
      hata kiutendaji nsahsema haiko huru,sidhani kama iko independent kama ilivo KBC
      kama serikali ndio inahusika kuteuwa mkurugenzi na uongozi mzima itafanya kazi kwa maslahi ya serikali ilikoko madarakani
      na sio vinginevyo.
      tafiti KBC inajiendeshaje afu ndio useme TBC inamilikiwa na umma.
      Tido hakupewa nafasi kurenew mkataba na siku mda wake unaisha alipewa treatment ambazo hakustahili.
      Pascal Mayalla likes this.
      You may know me but you have no Idea who I am !

    16. #53
      Codon's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th December 2011
      Posts : 553
      Rep Power : 486
      Likes Received
      75
      Likes Given
      20

      Default Re: Live News Interactive!-TBC-1 Yastahili Pongezi!. ''Hongera TBC-1" Keep it Up!

      Pole sana Pascal,naona kama unauwinda ukuu wawilaya incase mmoja akiteleza?
      Pascal Mayalla likes this.

    17. #54
      Pascal Mayalla's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 2nd August 2009
      Posts : 210
      Rep Power : 3207
      Likes Received
      231
      Likes Given
      1531

      Default Re: Live News Interactive!-TBC-1 Yastahili Pongezi!. ''Hongera TBC-1" Keep it Up!

      Quote By Lokissa
      paschal umma hauna sauti juu YA TBC bali serikali
      hata kiutendaji nsahsema haiko huru,sidhani kama iko independent kama ilivo KBC
      kama serikali ndio inahusika kuteuwa mkurugenzi na uongozi mzima itafanya kazi kwa maslahi ya serikali ilikoko madarakani
      na sio vinginevyo.
      tafiti KBC inajiendeshaje afu ndio useme TBC inamilikiwa na umma.
      Tido hakupewa nafasi kurenew mkataba na siku mda wake unaisha alipewa treatment ambazo hakustahili.
      Mkuu Likissa, mwanzo nilikuuliza kwani Tido aliteuliwa na nani?!, kama Tido aliweza, kwanini aliyepo asiweze?!. Kama Mkataba wa Tido ulisema wazi ni wa muda gani, na muda uliisha, kwanini waurenew?. Renewer ya mkataba wowote ni discretional ya muajiri, kama kuna wengine wenye uwezo, kwa nini wale wale warudishwe?!.

      Nilikuwa TVT hii ndio ilikuwa ya serikali, sasa ilipogeuka TBC, iko independent ina menejiment yake na bodi yake. Hoja kuwa TBC haiko huru ni dhana tuu na labda inahalalishwa kwa upron strings ambazo ziko attached kama kwa mama na mtoto!.

      Wakuu wa taasisi ngapi wanateuliwa na rais na bado taasisi hizo zinamaitain their independence?. Uendeshaji wa TBC ni kama KBC na kama BBC, zote ziko paid by taxpayers money, zina independent body, na editorial independence, sasa kama waliopo wanaiendesha kwa (jikombaring style) kwa serikali kwa imani kuwa huko ndiko kuisaidia serikali, hiyo ni individual initiative, na kama serikali makini kamwe haiwezi kuogopa kuambiwa ukweli, ndio maana nikasema, TBC ni yetu na tuitumie.

      Kwanza zifanyike efforts za kuitumia tukataliwe ndipo tulalamike!.
      Lokissa likes this.

    18. #55
      Lokissa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th November 2010
      Location : Goba
      Posts : 4,092
      Rep Power : 5807
      Likes Received
      1026
      Likes Given
      2876

      Default Re: Live News Interactive!-TBC-1 Yastahili Pongezi!. ''Hongera TBC-1" Keep it Up!

      paschal nadhani bado una kipaji nlikuwa nakuangalia sana wakati wa sabasaba na PPR.
      nakusahuri ingia ITV au Star tv ndiko kuna watazamaji makini ukirudi TBC jihesabu kupoteza umahiri wako.
      wengi tunajua TBC ilishakufa na wengi wetu hata frequency zake tulishadelete ktk vi receiver vyetu.

      Quote By Pascal Mayalla

      Mkuu Likissa, mwanzo nilikuuliza kwani Tido aliteuliwa na nani?!, kama Tido aliweza, kwanini aliyepo asiweze?!. Kama Mkataba wa Tido ulisema wazi ni wa muda gani, na muda uliisha, kwanini waurenew?. Renewer ya mkataba wowote ni discretional ya muajiri, kama kuna wengine wenye uwezo, kwa nini wale wale warudishwe?!.

      Nilikuwa TVT hii ndio ilikuwa ya serikali, sasa ilipogeuka TBC, iko independent ina menejiment yake na bodi yake. Hoja kuwa TBC haiko huru ni dhana tuu na labda inahalalishwa kwa upron strings ambazo ziko attached kama kwa mama na mtoto!.


      KBC na kama BBC, zote ziko paid by taxpayers money, zina independent body, na editorial independence, sasa kama waliopo wanaiendesha kwa (jikombaring style) kwa serikali kwa imani kuwa huko ndiko kuisaidia serikali, hiyo ni individual initiative, na kama serikali makini kamwe haiwezi kuogopa kuambiwa ukweli, ndio maana nikasema, TBC ni yetu na tuitumie.

      Kwanza zifanyike efforts za kuitumia tukataliwe ndipo tulalamike!.
      Pascal Mayalla likes this.
      You may know me but you have no Idea who I am !

    19. #56
      Mwalufunamba's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 12th June 2012
      Posts : 151
      Rep Power : 380
      Likes Received
      61
      Likes Given
      26

      Default Re: Live News Interactive!-TBC-1 Yastahili Pongezi!. ''Hongera TBC-1" Keep it Up!

      Quote By Pascal Mayalla
      Mkuu Mfamaji, excatly ndicho nilichomaanisha, hizi ni lugha za watu, mimi ni product ya UPE na wanangu wanasoma shule za kata!.
      Wenye akili tu ndiyo watakaoelewa uzito wa sentesi hii!!
      Pascal Mayalla likes this.

    20. #57
      ha ha ha's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th December 2011
      Location : Hapahapa
      Posts : 456
      Rep Power : 466
      Likes Received
      45
      Likes Given
      71

      Default Re: Live News Interactive!-TBC-1 Yastahili Pongezi!. ''Hongera TBC-1" Keep it Up!

      Huwa naangalia ki/vipindi vya wakata mauno tu ndo wanawezea habari ilishawashinda. Kwa ufupi wako bias kutoa sura kamili ya tukio.
      Pascal Mayalla likes this.
      "If you find yourself in ahole, the first thing to do is stop digging"



    21. #58
      Pascal Mayalla's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 2nd August 2009
      Posts : 210
      Rep Power : 3207
      Likes Received
      231
      Likes Given
      1531

      Default Re: Live News Interactive!-TBC-1 Yastahili Pongezi!. ''Hongera TBC-1" Keep it Up!

      Quote By Codon
      Pole sana Pascal,naona kama unauwinda ukuu wawilaya incase mmoja akiteleza?
      Mkuu Codon, ulijuaje?. Kiukweli ukuu wa wilaya ni deal kubwa sana!. Yaani nimeutafuta kwa nguvu zangu zote, haswa baada ya kuisoma job description yake na mshahara wake mnono sana, huku ukitembelea gari la bendera, kwa kuzingatia usafiri wangu ni pikipiki huku nikiishi nyumba ya kupanga upande hapa Tandale.

      Kuupata U-DC ndio njia pekee iliyobakia ambayo inaweza kunitoa kimaisha!. Tena ndio maana hata ile kazi ya "political advisor" mahali, niliacha kwa mategemeo ya kuwa DC!. Kule nilikuwa nalipwa kamshahara ka tujisent tuu, ili kufuata mshahara wa milioni 2 za U-DC!.

      Na kupitia hapa natangaza rasmi kuifuatilia ile kadi yangu ya Chama, nilio katiwa kwa lazima wakati ule nikiwa JKT kwa mujibu wa sheria, sasa naifuatilia kwa ridhaa yangu na nitailipia miaka yote iliyopita bila kuilipia na kusubiria kwa hamu, awamu nyingine ya 2015 wakati wa uteuzi mwingine!. Wana jf niingizeni kwenye sala zenu, mwenzenu naupenda sana U-DC!.

    22. #59
      Pascal Mayalla's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 2nd August 2009
      Posts : 210
      Rep Power : 3207
      Likes Received
      231
      Likes Given
      1531

      Default Re: Live News Interactive!-TBC-1 Yastahili Pongezi!. ''Hongera TBC-1" Keep it Up!

      Quote By Lokissa
      paschal nadhani bado una kipaji nlikuwa nakuangalia sana wakati wa sabasaba na PPR.
      nakusahuri ingia ITV au Star tv ndiko kuna watazamaji makini ukirudi TBC jihesabu kupoteza umahiri wako.
      wengi tunajua TBC ilishakufa na wengi wetu hata frequency zake tulishadelete ktk vi receiver vyetu.
      Mkuu Lokissa, "Saba Saba na PPR" na sasa zinakuja "Nane Nane na PPR", kuanzia 01/08/ hadi 09/08, zinaruka pia ITV, Star TV na Channel Ten ila sio kweli kuwa TBC ilishakufa, ila nakiri, imepunguza mvuto!. Kwa vile hii ni TV yetu na tunaigharimia kwa kodi zetu, nadhani ni busara kuisaidia pale inapowezekana kwa kuipa 1st priority ya program zangu, ndipo niende vituo hivyo vingine.

    23. #60
      Al Zagawi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th March 2009
      Location : Tabora
      Posts : 832
      Rep Power : 685
      Likes Received
      160
      Likes Given
      51

      Default Re: Live News Interactive!-TBC-1 Yastahili Pongezi!. ''Hongera TBC-1" Keep it Up!

      Quote By Pascal Mayalla
      Mkuu Al Zagawi, ni miaka mitatu kufikia 2015!, au wewe hujui kitakachotokea?.

      Kama ulinisoma mwisho, nimesema niliwahi kufanya kazi TVT, kwa sasa mimi ni independent producer, kila mwaka napeleka program zangu zaidi ya 100 hapo TBC na zinarushwa.

      Ushawishi wangu ni kama wanavyoruhusu vipindi kutoka nje vya non political issues, sasa waruhusu na political programs kutoka nje ambazo zitakuwa analytical na kuikosoa serikali!. Hili nitajaribu!.

      Kuna uwezekano mkubwa, baadhi ya shutuma kwa TBC ni za asumptions tuu, kuwa wanaitetea sana serikali, kuna vipindi very critical kama kile cha This Week in Prespective" kinachoendeshwa na Adam Simbeye, sometimes kiko very critical ila wengi hamkioni.

      Watanzania wengi tuna tatizo la kutojaribu!. Kwa vile TBC ni TV yetu, tuitumie, tusiiogope!. Inawezekana uoga wetu ni kama uoga wa baadhi yetu kwa mtu lofa kama mimi unapomuona mrembo very striking, unasita kumtokea, kwa kujifikiria, utampa nini?!. Kumbe ni uoga wa bure tuu, kwani huyo mrembo tayari anacho kila kitu cha dunia hii na alichokosa ndicho hicho hicho nilichonacho liofa mimi!. Kumbe ningemtokea tuu ningekubaliwa!. Sasa ndio naahidi TBC nitaitokea!.
      Mkuu Pascal...good luck!!!
      Pascal Mayalla likes this.
      ...........Uwanja wa siasa katika nchi karibu zote za Kiafrika, ni uwanja uliotekwa na majambazi ambao wanafanya wanachotaka, vile wanavyotaka..........Jenerali Ulimwengu, Raia Mwema Namba 278.

    Page 3 of 3 FirstFirst 123

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...