Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Kikwete: Lowassa Ajiuzulu

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 26
    1. #1
      williams king's Avatar
      Member Array
      Join Date : 3rd December 2006
      Posts : 58
      Rep Power : 655
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Kikwete: Lowassa Ajiuzulu

      KWANZA KABISA POLE NA SAFARI MUH. LOWASA

      Inaonekana kasi mpya imegonga mwamba siamini waziri mkuu ameishiwa na maneno mwana siasa mahiri kama Lowasa au alikuwa amechoka na safari, ameshindwa kujibu swali la waandishi wa habari kuhusu janga la umeme linalo tukabili katika taifa letu imekuwa vichekesho katika vyombo vya habari hapa nchini vikiwemo radio ''eti Lowasa anazidi kuwakatisha mamilion ya watanzania tamaa'' kwa kusema kwamba tatizo la UMEME WAMELIRIDHI kutoka serikali ya awamu ya tatu (mbona Mkapa alikupenda sana )jamani wenzangu mnao lala giza mnakubaliana na kauli hiyo hii ni kauli ya kushindwa kazi .

      Ninaamini awamu iliyo pita walikuwa wamesha zaliwa na walikuwa kazini katika wizara nyeti wizari ya MTERA wiazri ya MAJI na KILIMO vyote hivi vinausiana na vimiminiko akulijua hilo au alikuwa anatumia REMOTE kama TV kuendesha wizara yake

      Sasa jamani tuangalie jinsi ambavyo tunaweza kuwapa wananchi matumaini ya kila kitu ni kweli JK kazi anaiweza lakini msimuangushe mimi nita mtetea Muh. Kikwete mpaka siku nitakapo ingi kaburini watu wake wana muaribia kama uwezi kujibu maswali usiongee na waandishi wa habari labda ukuonge hivyo lakini wame kutafsiri vibaya.

      Pia Muh. Lowasa anavyo penda sherehe atuwezi kusheherekea bila mwanga miaka 45 ya uhuru inakuja hizi sherehe za mabilion kwenye giza kwa nini tusishugulikie maswala ya muhimu sherehe tutazifanya tu tukiwa vizuri. hii ndiyo nchi ya kwanza duniani viongozi na wananchi wao wana fanya sherehe wakati wana matatizo kibao.

      Ninakumbuka gazeti la Tanzania Daima la wiki mbili zilizo pita kulikuwa na makala walimuandika mweshimiwa Lowasa ni NEWS EDITOR sasa hili imekuwaje akuliona au hawakukupigia simu?

      Muh. Lowasa mimi nina kupa ushauri siyo lazima kujibu kila swali utakalo ulizwa jibu la hili swali lilikuwa rahasi kabisa jibu lake ni ''Tunalishugulikia'' basi umemaliza ninaamini akuna viongozi wanaulizwa maswali magumu kama viongozi wa marekani lakini wanajibu kwa kifupi pili au unachukuwa maswali mengi jibu yale unayo yaweza

      Ninaomba nikuambie kuwa waandishi wa habari siyo rafiki zako ,hili unaju ndiyo walio wajenga na ndiyo wata kao wabomoa.

      Kwanza kabisa ungeliezea mafanikio ya safari yako kama ulivyo fanya pia umekuja na habari nzuri ya wa Canada kuwekeza katika UMEME basi inatupa sisi matumaini kuwa giza litaisha .

      hayo ndiyo maneno yangu kwa maziri husika wewe ni kiongizi mkubwa sana nchini neno lako moja linaweza kuadhiri watu wengi sana.

      Bado tuna wapenda kazi mnafanya msikate tamaa haya nimatatizo yanayo tatulika japo kuwa Mmepotea njia rudini njia panda muanza tena mtafika tu. mkiendelea hivi huko katikati mtapotea bado nguvu mnayo.

      Jingine Muh. kikwete wananchi wana Kapenda sana sana....... mimi pia nina kupenda sana kama nilivyo eleza mwanzo hata watanzania wakilala gizi wana fikiri Taa zina waka fanyeni haraka msingoje wakakurupushwa.
      asanteni
      Last edited by williams king; 5th December 2006 at 08:46.


    2. #2
      Mgumu's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 3rd November 2006
      Posts : 238
      Rep Power : 693
      Likes Received
      2
      Likes Given
      0

      Default

      Shy, EL hawezi kujiuzulu wametoka mbali na JK, hatakama ingekuwa wewe best wako atakama atakuwa anaboronga lazima utambeba, ila kama tungekuwa na maadili ya uongozi ingekuwa ni rahisi kumshikia bango kiongozi anayeboronga hata kama atakuwa mkuu wa nchi, Bongo hakuna maadili ya uongozi, kanyaga twende ndugu yangu.

      Kuhusu suala la sherehe wabongo tumeshindikana, inabidi tupate nabii atakaye tuokoa na hili, nilisikitika sana pale EL alipokuwa anapitisha bakuli kwenye TV kuomba mashirika na wafanya biashara kuchangia sherehe za Uhuru wa Tanganyika, hapa kuna swala la kisheria, kwani Tanganyika badi ipo? kwa mawazo yango baada ya muungano na Tanzania kuzaliwa uhuru wetu tuliutoa kafara, jambo la msingi si uhuru bali tuweke vipaumbele na kuhakikisha tunajipima ka tumefaniwa au la.

      Mfano, badala ya kuendekeza michango ya sherehe za Uhuru, EL angemshauri JK serikali imefanya nini na ilipanga kufanya nini, wakati huu ni wa kutafakari mapungufu na kuangalia njia mbadala za kuwakomboa wadanganyika

      wakati umefika viongozi wakawa na vipaumbele na kushughilika masuala ya msingi, PM anapogeuka na kuwa PR wa wizara haifai jamani

    3. #3
      JeiKei's Avatar
      Member Array
      Join Date : 29th September 2006
      Posts : 96
      Rep Power : 670
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default

      Lowassa ajisafisha matatizo ya umeme

      na Joseph Senga

      WAZIRI Mkuu, Edward Lowassa, amesema wanaoishutumu Serikali ya Awamu ya Nne kwa matatizo ya sasa ya umeme, hawaitendei haki, kwa kuwa suala hilo limerithiwa kutoka awamu zilizopita.

      Alisema ingawa matatizo hayo yamerithiwa kutoka Awamu ya Tatu, ukweli unabaki kuwa awamu zilizopita hazikuweka njia nyingine za kuzalisha umeme, zaidi ya kutegemea maji ya mvua katika mabwawa.

      Lowassa alisema hayo alipozungumza na waandishi wa habari baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, Dar es Salaam jana.
      Waziri Mkuu alikuwa nchini Canada na Mexico ambako alimwakilisha Rais Kikwete katika shughuli mbalimbali za kimataifa.

      “Serikali inakiri kuwa tatizo la umeme imekuwa kero kubwa sana, lakini ni muhimu wananchi wakafahamu kwamba, Rais Kikwete na serikali yake wamelirithi tatizo hilo kutoka Awamu ya Tatu, kwa hiyo nawaomba wananchi kuwa wavumilivu.

      “Serikali inafanya kila jitihada za kutatua tatizo hili na nina uhakika kuwa Serikali ya Awamu ya Nne itafanikiwa kulitatua,” alisema.

      Lowassa alijitetea kwa kusema kuwa matatizo ya umeme hayapo Tanzania pekee, bali nchi nyingine zikiwamo Uganda na Canada, nazo zinakabiliwa na uhaba wa umeme, ikiwa ni pamoja na kufungwa kwa mabwawa kadhaa.

      Lowassa anatoa kauli ya namna hiyo wakati historia ikionyesha kwamba yeye na Rais Kikwete waliingia katika Baraza la Mawaziri wakati wa Serikali ya Awamu ya Pili na pia kwa vipindi tofauti wakawa mawaziri katika Awamu ya Tatu.

      Mbali ya hilo, Kikwete ambaye Lowassa anataka aache kulaumiwa kwa sababu ya matatizo ya sasa ya umeme, aliingia serikalini mwaka 1988 akiwa Naibu Waziri wa Maji, Nishati na Madini na miaka miwili baadaye akateuliwa kuwa Waziri kamili katika wizara hiyo hiyo ambayo pamoja na mambo mengine ndiyo iliyokuwa na jukumu la kuelekeza taifa katika uwekezaji sahihi wa masuala yahusuyo nishati.

      Lowassa mwenyewe wakati wa serikali iliyopita alikuwa Waziri wa Maji na Mifugo, wizara ambayo pamoja na mambo mengine ilikuwa na dhamana ya kuangalia na kuendeleza hifadhi za vyanzo vya maji.

      Kwa upande mwingine, kauli hiyo ya Lowassa, imekuja huku hali ya umeme ikiwa mbaya, ingawa Kampuni ya Richmond, kwa mara nyingine, iliahidi kuwa wiki hii ingeanza kuzalisha megawati 20.

      Kupungua kwa maji katika mabwawa ya Mtera, Kidatu na mengine, ni matokeo ya uchafuzi wa mazingira kitaifa na kimataifa.
      Ukataji ovyo wa miti, uharibifu wa vyanzo vya maji, kilimo cha umwagiliaji kwa kutumia mbinu za kizamani na unyweshaji mifugo moja kwa moja katika mabwawa, vinaelezwa kama miongoni mwa vyanzo vya kupungua kwa maji katika mabwawa.

      Wakati kitaifa hayo ndiyo matatizo, kimataifa hali hiyo inachangiwa na uchafuzi wa mazingira uliosababisha kupasuka kwa ukanda wa ozoni, na hivyo joto kuanza kuongezeka duniani.

      Katika ziara hiyo Lowassa aliongozana na mawaziri, wabunge na viongozi wa taasisi za serikali.
      Mawaziri na viongozi wa taasisi hizo, walieleza mafanikio makubwa yaliyotokana na ziara hiyo.
      Viongozi hao, kwa maelekezo ya Waziri Mkuu, ndio waliojibu maswali yaliyoulizwa na wanahabari.

      Waziri wa Elimu ya Juu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Peter Msolla, alisema miongoni mwa mafanikio ni kuwapata wataalamu watakaoshiriki katika mradi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wa kutumia maziwa ya ng’ombe katika kupunguza makali ya ugonjwa wa UKIMWI. Majaribio yameanza kufanyika mkoani Mwanza.

      Mafanikio mengine ambayo yameelezwa kupatikana kutokana na ziara hiyo ni pamoja na kupatikana kwa mwekezaji ambaye anatarajiwa kuwekeza dola milioni 1.6 za Marekani. Haikuelezwa sehemu alizokusudia kuwekeza.

      Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Emmanuel ole Naiko, alisifu juhudi zinazofanywa na Rais Kikwete na Waziri Mkuu, Lowassa, za kuitangaza Tanzania kimataifa.

      Hata hivyo, Naiko alitumia neno ‘wanaiuza nchi’, kabla ya kusahihishwa na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Salome Joseph Mbatia, ambaye alimtaka aseme ‘wanaitangaza Tanzania’, badala ya ‘kuiuza Tanzania’.

      Baadhi ya mawaziri waliosafiri na Lowassa ni Profesa Msolla; Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi, na Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe.

      http://www.freemedia.co.tz/daima/2006/12/5/habari1.php

    4. #4
      williams king's Avatar
      Member Array
      Join Date : 3rd December 2006
      Posts : 58
      Rep Power : 655
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default

      PESA ZA KUSHEHEREJEA MIAKA 45 YA UHURU ZIKATOE MATOPE MTERA

      Kutokana na kauli ya muh. Lowassa kwamba tatizo la umeme ,serekali ya awamu ya nne imelirithi kutoka kwa rais mstafu benjameni william mkapa siyo la msingi.

      Tamko hili limetoka baada ya rais mstaafu kutoa sadaka kanisani kwa kumshukuru mungu kwa alimaliza kipindi chake cha uongozi wakitaifa kama rais wa jamuhuri ya muungano wa tanzania salama na kwa amani aliongoza kwa kipindi cha miaka kumi.

      Nijambo lisilo la kawaida kama viongozi hawa wataanza kutupiana lawama wakati mwingine anamshukuru mungu kumaliza kipindi kake salama. Rais mkapa aliku ng'ang'ari na mgumu pia alichukuwa nchi ikiwa katika hali baya kuli serekali ya awamu ya nne, kama kazi imewashinda anaanza kutupiana lawama sasa sisi wananchi tuwaeleweje?

      Mimi kwa kuwasaidia hizo pesa mlizo kusanya kwenye kapu kutoka kwa wafanyabiashara kwa ajili ya kusherehekea miaka 45 ya UHURU nibora zielekezwe kwenye kutoa matope katika bwawa la mtera ili tupate UMEME.


      Umahiri na Kasi mpya unaporomoka sasa wananchi tufuate na kuamini lipi?
      WANAFORUM WASAIDIENI HAWA VIONGOZI WETU MAWAZO BADO TUNAIPENDA CCM

    5. Dua is offline
      Dua
      #5
      Dua's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th November 2006
      Posts : 3,534
      Rep Power : 1369
      Likes Received
      9
      Likes Given
      0

      Default

      LOWASA LAZIMA UJIUZULU

      Lowasa wewe ndio ulikuwa mtu wa kwanza kuwaambia wabunge wasiongelee suala la Umeme, na leo hii unaanza kutaka kugeuza kibao; hivi ni kweli umefika wakati unafikiria watanzania wote ni wajinga?

      Jambo la muhimu kwako binafsi kama kiongozi ni kujiuzulu ndio tutaona ni kweli uko serious na nchi yetu, kuonyesha kwamba umeshindwa kutekeleza yale ambayo sisi kwa muda mrefu tumeyaona kwamba huyawezi.

      Lakini kabla ya kufanya hivyo tunakuomba uwawajibishe wale wote ambao kwa njia moja au nyingine wamekuwa wachangiaji wakubwa katika tatizo hili la umeme, na baada ya hapo ni wewe mwenyewe ingawaje utakuwa hukutimiza yale ambayo ulitarajia kufanya pamoja na kujibu maswali kadhaa ambayo uliulizwa baada ya kikao cha bunge kule Dodoma.
      Dua la kuku halimpati mwewe


    6. #6
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 29,613
      Rep Power : 46736
      Likes Received
      16712
      Likes Given
      8546

      Default

      Hivi, so ndo huyu huyu aliyejigamba kuwa viongozi hodari, majasiri, wanaojali watu wapo tena wamejaa tele?!!!
      [email protected]
      The Best of Tanzanian Socio-Political Blogging - http://www.mwanakijiji.com

    7. mTz is offline
      mTz
      #7
      mTz's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th August 2006
      Posts : 407
      Rep Power : 740
      Likes Received
      1
      Likes Given
      0

      Default

      Mwanakijiji,

      Hizo zilikuwa political rhetorics!
      "Be not afraid of growing slowly, be only afraid of standing still." Old Chinese Proverb

    8. #8
      Lunyungu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th August 2006
      Location : Malampaka
      Posts : 8,042
      Rep Power : 2570
      Likes Received
      793
      Likes Given
      29

      Default

      Lowasa ni kilaza mkubwa hata JK mwenyewe ni msanii .Leo issue ya umeme anaongea kama mhuni tu yaani hata hawezi kuwaza hata mara moja . Wote JK na Lowasa wako kweney serikali kuanzia JKN hadi sasa JK alikuwemo then akaja Lowasa wote wanajua kwa wamekuwa serikalini muda wote .Leo hii wanasema kwamba matatizo yako Duniani kalinganisha na issue ya tanzania na Canada ? Kweli jamaa anaropoka sana no wonder anakula na vyombo vya habari .

    9. #9
      williams king's Avatar
      Member Array
      Join Date : 3rd December 2006
      Posts : 58
      Rep Power : 655
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default

      Quote By Lunyungu View Post
      Lowasa ni kilaza mkubwa hata JK mwenyewe ni msanii .Leo issue ya umeme anaongea kama mhuni tu yaani hata hawezi kuwaza hata mara moja . Wote JK na Lowasa wako kweney serikali kuanzia JKN hadi sasa JK alikuwemo then akaja Lowasa wote wanajua kwa wamekuwa serikalini muda wote .Leo hii wanasema kwamba matatizo yako Duniani kalinganisha na issue ya tanzania na Canada ? Kweli jamaa anaropoka sana no wonder anakula na vyombo vya habari .
      LUNYUNGU

      Mimi ningelipenda kuelezea majukumu ya rais katika nchi lugha uliyo tumia kwamba JK ni msanii siyo nzuri ,JK ni raisi anawatendaji wake ambao ni Maziri Mkuu,

      na Mawaziri wa Wizara husika ,Makatibu wa Kuu,Ma- DC, Wakuu wa Mikoa na wengine wengi tu.

      Sasa ndugu yangu huyu bwana ana kazi nyingi sana awezi kufanya kila kitu mwenyewe watendaji wake lazima wa mletee taarifa ,tatizo ninalo liona mimi,

      wanamdanganya kwenye makaratasi kumuandikia ripoti nzuri nzuri kwa sababu wanajua wezi kwenda kuhakikisha kila kitu.

      ALIYE KUWA WAZIRI WA MALI ASILI NA UTALII ,MUH.DIALLO
      alimdanganya raisi JK kwamba watu wa mwanza awali MAPANKI ili

      lilimshangaza sana muheshimiwa JK kwa sababu raisi alisimama mbele ya mkutano wa hazara kupinga filamu ya mapanki kumbe kulikuwa na ukweli kidogo kuhusu mapanki .

      na wakazi wa mwanza walimshanga sana raisi kusema watu hawali mapanki
      raisi alionge kwa uchungu sana ,jinsi nchi yake ilivyo zalilishwa na mtu mmoja mjinga Bw. Sauper

      JK aliongea na viongozi wa mkoa wa mwanza faraga baada ya kumaliza mkutao kwa muda wa masaa matatu, kutaka kujua kwa nini waliruhu hayo yote yakatokea

      Sasa hatuwezi kumlaumu JK kuhusu swala la umeme hivyo hivyo waziri husika alikuwa anamdanganya raisi sasa jamani kichwa kimoja kinaweza kweli

      kufanya kazi zote, swala la maji mtera waziri husika kuto kuwajibika kisawasawa

      pia kuna wizara nyingi tu hawawajibiki kisawasawa hawaendi na kasi mpya sasa huu mtandao utawaondoa kazini,

      kwahiyo bwana .LUNYUNGU..kunaweza kukawa na mapungufu kwa upande wa JK lakini ni mapungufu ya kawaida tu kama maraisi wengine dunia, simtetei

      kwasababu ya sura yake mimi binafsi ninampenda kutoka moyoni kwangu,kama nikiwa bodigadi wake mimi niko tehari nife yeye apone pili amenipa kazi

      CCM DAIMA -Nina muomba Muh. Makamba humu

      BY KING
      Last edited by williams king; 5th December 2006 at 22:13.

    10. #10
      Jasusi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th May 2006
      Posts : 10,697
      Rep Power : 2911
      Likes Received
      3891
      Likes Given
      12464

      Default

      Bwana Mfalme (King)
      Kama Diallo alimdanganya na rais anafahamu hivyo mbona amemwacha serikalini? Huoni kuwa ndio huo usanii tunaozungumzia? Umeshajua fulani kakudanganya, unaendelea kumweka kwenye nafasi muhimu kwa sababu gani? He has to show he is serious ama sote tutaamini kuwa ni usanii tu.

    11. #11
      Tabasamu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2006
      Posts : 279
      Rep Power : 698
      Likes Received
      4
      Likes Given
      0

      Default

      Jasusi,
      Well said. Huo ndio usanii wenyewe. Yaani yeye hawezi hata kuhakikisha ukweli maadam tu Diallo kasema yeye anarudia kama kasuku? Alifanya juhudi gani kupata maelezo kutoka kwa source zake zingine? Suala kama hilo alipata wapi ujasiri wa ulizungumzia kwa jazba bila kufanya utafiti wa kina? Diallo hakumdanganya alimwambia anavyofahamu yeye. Diallo hajawahi kula mapanki, hajawahi kukuta watu wanakula mapanki, wananchi wa Mwanza hawajawahi kumweleza uchungu wao kuhusu kula mapanki sasa alijulia wapi kuhusu kula mapanki?

    12. #12
      Wacha's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd November 2006
      Posts : 798
      Rep Power : 802
      Likes Received
      82
      Likes Given
      142

      Default

      Kama huyu rais anamtegemea Diallo kwa maswala kama haya halafu haulizi kwa watu wake aliowaweka kule Mwanza basi njia ni moja tu naye hafai inabidi ajiuzulu mapema sana.

      Wacha

    13. mTz is offline
      mTz
      #13
      mTz's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th August 2006
      Posts : 407
      Rep Power : 740
      Likes Received
      1
      Likes Given
      0

      Default

      King!

      Hao watendaji wanawajibika kwa nani? kama wanamdanganya kwa nini asiwawajibishe? Kuna tendency ya kutaka kumfanya Rais kuwa ni mtakatifu na hakosei. Je mara ngapi tumeshasikia kuwa washauri wake wanamshauri vibaya. Je sisi tuliwachagua hao? sisi tulimchagua Rais, yeye ndio anawajibika kwetu moja kwa moja hao wengine sisi hatuwajui. Umeshasahau ule msemo wa mkubwa jalala?
      "Be not afraid of growing slowly, be only afraid of standing still." Old Chinese Proverb

    14. #14
      williams king's Avatar
      Member Array
      Join Date : 3rd December 2006
      Posts : 58
      Rep Power : 655
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default

      Quote By mTz View Post
      King!

      Hao watendaji wanawajibika kwa nani? kama wanamdanganya kwa nini asiwawajibishe? Kuna tendency ya kutaka kumfanya Rais kuwa ni mtakatifu na hakosei. Je mara ngapi tumeshasikia kuwa washauri wake wanamshauri vibaya. Je sisi tuliwachagua hao? sisi tulimchagua Rais, yeye ndio anawajibika kwetu moja kwa moja hao wengine sisi hatuwajui. Umeshasahau ule msemo wa mkubwa jalala?
      MTZ - MTOA HOJA

      Ninashukuru kusikia kwa mtoa HOJA, serekali au nchi Rais anauwezo mkubwa sana aswa nchi za Afrika, kwa mtazamo wangu mimi katika maisha yangu

      siwezi kufanya kazi na mtu ambaye siwezi kumkemea au mtu aliye nisaidia kwa shuguli fulani, ili pasiwe na sababu ya mimi kuto fanya kazi yangu ninavyo taka.

      mimi ninanukuu kauli ya Muh. Kikwete katika hutuba yake ya kwanza na wabunge kule Dodoma alisema hakuna chuo kinacho fundisha kuwa waziri,

      nitakuteuwa kuwa waziri kama nina imani na wewe na unaweza kuongoza wenzako.

      Nina kumbuka Rais wa Marekani G.BUSH kwa mara ya kwanza kuingia madarakani ali mu-apiinti jaji mkuu akakataliwa ikabidi apigiwe kura akashinda

      kwa kura moja tu,baada ya kukataliwa na bunge la marekani,
      pili alimu-apiinti IGP wa state ya New York akajiuzulu kwa kashifa alizokuwa

      nazo hii ni mifano michache sasa JK, Mimi nina kutetea lakini wenzangu wamenikataa tarehe 21 desemba 2006 unamaliza mwaka tangia uingie

      madarakani kama ni fadhila umesha walipa, sasa anza kuwatoa mmoja mmoja
      wanakuchezea ulivyosema ''usione nina tabasamu ninasimania mambo ya msingi'' kama nimekosea mnirekebishe.

      umewapa mwaka umewajua, kuwahamisha siyo hoja fukuza wanafikiri bila wao wewe uwezi kufanya kazi tupo wengi tu tumekaa benchi.

      jamani wenzangu katika forum hii tutoe ushauri kwa rais na viongozi wengine ni nini kifanyike tuweze kulijenga taifa letu.

      Naomba kutoa hoja

      BY KING
      Last edited by williams king; 6th December 2006 at 01:04.

    15. mTz is offline
      mTz
      #15
      mTz's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th August 2006
      Posts : 407
      Rep Power : 740
      Likes Received
      1
      Likes Given
      0

      Default

      King hapo umenena, swali kubwa ni kwamba je waTz tunautamaduni wa kumkoma nyani giladi kwa vitendo na sio longolongo? It is very unfortunate kuwa Mwalimu (RIP) kati ya vitu alivyoturithisha ni utamaduni "wrist slapping" badala ya kupiga rungu kabisa mtu akikosea. Ndio yale ya mtu anamesss sehemu, adhabu yake anahamishiwa sehemu nyingine akaharibu tena.

      JK needs to set up a new status quo, he commands a record mass support, the ball is on his side.
      "Be not afraid of growing slowly, be only afraid of standing still." Old Chinese Proverb

    16. #16
      Ogah's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Posts : 5,700
      Rep Power : 21825
      Likes Received
      750
      Likes Given
      3275

      Default

      Statement ya EL inaonyesha dalili za kushindwa kazi.

    17. #17
      Mkandara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd March 2006
      Location : T dot
      Posts : 13,768
      Rep Power : 7665
      Likes Received
      4930
      Likes Given
      4509

      Default

      Lowassa kaishiwa!
      Hivi kweli ameweza kusema mbele ya waandishi wa habari kuwa Canada ina matatizo ya Umeme?....Ama kweli Wagandanyika wanafungwa na mengi.
      Exploration of reality

    18. #18
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 29,613
      Rep Power : 46736
      Likes Received
      16712
      Likes Given
      8546

      Default

      Juzi, umeme ulikatika nilipofika kazini tu kwa karibu masaa 4! lakini twaweza kusema US kuna tatizo la umeme? labda maana ya neno "tatizo" imepotea!!
      [email protected]
      The Best of Tanzanian Socio-Political Blogging - http://www.mwanakijiji.com

    19. #19
      Mkuyuga's Avatar
      Member Array
      Join Date : 18th August 2006
      Posts : 92
      Rep Power : 675
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default

      Ni kwa sasabu alipkuwa canada kulitokea black out ya siku moja!!

      kwa sababu ya weather snow etc!!

      Hawa viongozi wanapokuwa wanaomba kura huwa wana solutions za matatizo yetu kibao!!!
      Lakini wanapochaguliwa huwa hawakaii kusema ohhh hata canada hakuna umeme, mara ujambazi uko katika kila nchi, etc, rushwa iko katika kila nchi etc.

      LAKINI WAKTI WA KAMPEN UKIFIKA TENA WANAKUJA NA SOLUTIONS KIBAO!!

      HADI MWISHO WA DUNIA UKIFIKA TANZANIA TUTABAKI PALE PALE KAMA VIONGOZI HAWATABADILIKA!!
      GRID YA TAIFA CHAKULA CHAKE UMEME UKICHEZA UTANATA

    20. #20
      Jafar's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd November 2006
      Location : Msoga, Chalinze
      Posts : 1,249
      Rep Power : 899
      Likes Received
      13
      Likes Given
      0

      Default

      Mwaka 1995, Mwl. Nyerere alisema kuwa E. Lowassa ni "Muhuni". Watu walikasirika sana, lakini cha kushangaza miaka kumi na moja baadaye bado ni "muhuni". Chakusikitisha huyu ndiye anaandaliwa 2015. Mweee Tanzania tunaendelea kuigiza. Ile kauli mbiu ya Ari nanihii, Nguvu sijuna na Kasi mpya sikuhizi JK ameisahau. HAISEMI KABISA.

    Page 1 of 2 12 LastLast

    Similar Topics

    1. Mwanza wamtaka Kikwete ajiuzulu
      By Rutashubanyuma in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 22
      Last Post: 12th January 2011, 17:16
    2. Replies: 10
      Last Post: 6th January 2011, 04:20
    3. Replies: 13
      Last Post: 16th December 2008, 14:21

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...