Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Gwajima wa kanisa la Ufufuo na ving'ora barabarani

    Report Post
    Page 6 of 10 FirstFirst ... 45678 ... LastLast
    Results 101 to 120 of 186
    1. #1
      mfianchi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st July 2009
      Location : Likulufusi
      Posts : 3,574
      Rep Power : 1222
      Likes Received
      580
      Likes Given
      1209

      Default Gwajima wa kanisa la Ufufuo na ving'ora barabarani

      Niko Old Bagamoyo road nasikia ving'ora vinapigwa kutoka kwenye gari inabidi kuweka gari pembeni nikihisi ni Mheshimiwa au mgonjwa anapita nashangaa kuona Hummer nyekundu na msururu wa magari ukipita kwa kasi na hayo magari yamebandikwa Picha ya mheshimiwa askofu anakaribishwa nyumbani.

      Sijui huyu bwana karuhusiwa na nani kwa kutupigia ving'ora na kupita kwa kasi kama kiongozi wa nchi. Sasa hata matapeli wanajidai hii nchi sijui tunaenda wapi?

      3D. likes this.

    2. RukaaJuu Final

    3. #101
      kaburunye's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th May 2010
      Location : pandagisiza sogwinaminzi
      Posts : 679
      Rep Power : 599
      Likes Received
      57
      Likes Given
      13

      Default Re: Gwajima wa kanisa la Ufufuo na ving'ora barabarani

      Jamani kwani Gwajima ana jeshi la polisi? ebu msilete za kuleta hapa. Mnamlaumu Gwajima kana kwamba aliamrisha aje apokelewe airport na kupewa escort ya police. Shida mnakurupuka tu bila kujua ilikuwaje. Na mkitaka details kwa nini Gwajima alipewa escort si mkamwone IGP Mwema au kamanda Kova.

      Hakuna mtu anayeweza kujiamulia tu kuwa police wampe escort. Kama jambo hili halijawafurahisha basi msimlaumu Gwajima. Yeye alikuwa Japan akihubiri injili, karudi kafika airport kakuta washirika wake (watoto wake wa kiroho) wamekuja kumpokea. Sasa ni kipi kinachowakera? Hebu leteni mada za maana hapa na si mambo ya majungu yasiyo na maana. Tabia za udaku usio na maana hautusaidii chochote.

      Na kwa taarifa yenu bado muda kidogo sana Gwajima atakuwa anatembea na escort ya police kama mwana wa mfalme. Mbona Yesu siku moja aliingia Yerusalemu akiwa juu ya mwanapunda na tena mwanapunda akatandikiwa kanga (kwa mara ya kwanza). Gwajima ni mtumishi wa Mungu na anastahili heshima yake. Maandiko yanasema mtu akimtumikia Mungu, Mungu atamweshimu. Na sasa kam Mungu anamweshimu wewe ni nani umdharau.

      Hongera sana IGP Mwema kwa kumpa huyu mtumishi wa Mungu escort ili awahi kufika kanisani ambako maelefu ya washirika walikuwa wanamsubiri. Keep it up and God bless you.

    4. #102
      kaburunye's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th May 2010
      Location : pandagisiza sogwinaminzi
      Posts : 679
      Rep Power : 599
      Likes Received
      57
      Likes Given
      13

      Default Re: Gwajima wa kanisa la Ufufuo na ving'ora barabarani

      Quote By sabra
      Siku hizi wahubiri wengi wanafanya biashara na waumini, Wanauza injili kwa sadaka. Wanawakamua kondoo (washirika) bila aibu. Hata Benny Hinn ana kashfa kubwa ya kuwa nabii wa uongo. Kwa maoni yangu, watu wasome maandiko yanavyosema na kuyafuata na sio kuwafuata wahubiri matapeli. Ni maoni tu.

      We Sabra acha kuongea mambo usiyoyajua. Unawafahamu wahubiri wangapi wanaofanya biashara na washirika? Ni wajibu wa washirika kutoa sadaka na hili ni agizo la Mungu. We unafikiri watumishi wa Mungu hawahitaji pesa za kujikimu wao na familia zao. Mnajitafutia laana za bure kufanya generalization zisizo na ukweli wala maana yeyote. Kazi ya Mungu ili iende mbele LAZIMA washirika watoe pesa zao kama sadaka. Na mimi nashangaa sana watu wanaolalamika kuwa washirika wanakamuliwa wala sio washirika wa kanisa lolote ni watu wa vijiweni tu. Hata kama ni kweli washirika wanakamuliwa wewe kinakuuma nini kama pesa si za kwako. Unajifanya una huruma sana. Je hao wanaokamuliwa wao hawaoni kama wanakamuliwa mpaka waendelee kukubali kukamuliwa. Usiwafanye watu wanaotoa pesa zao kwa kazi ya Mungu kuwa hawana akili. They know what they are doing and you can stop them by your malicious words.
      FuturePresident likes this.

    5. #103
      Mpeni sifa Yesu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd May 2010
      Location : Dar es Salaam
      Posts : 472
      Rep Power : 551
      Likes Received
      18
      Likes Given
      1

      Default Re: Gwajima wa kanisa la Ufufuo na ving'ora barabarani

      ni kitu kibaya sana kuongea jambo usilolijuwa kwa kujifanya unalijua sana, unakuwa unampaka mtu matope pasipo hata na sababu. kitu cha muhimu kuelewa ni kwamba, ukimgusa mtumishi wa Mungu kama ninyi wengine mnavyofanya hivi, unagusa mboni ya jicho la Mungu...ni rehema za Mungu tu lakini Mungu anachukia mnachofanya......Mungu awasaidie.
      Hakuna lisilowezekana kwa Mungu, anaponya, anaokoa. kwa ushauri na maombi, tuwasiliane ([email protected]). karibu kwa Yesu.

    6. #104
      Anyisile Obheli's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th December 2009
      Location : Rohoni
      Posts : 3,261
      Rep Power : 1125
      Likes Received
      68
      Likes Given
      82

      Default Re: Gwajima wa kanisa la Ufufuo na ving'ora barabarani

      wafuasi wa ibilisi huwa hawapendi maendeleo ya mtumishi wa Mungu maana INJILI kama kawaida ni moto
      kwa watoto na wana wa pepo, sasa shetani ameuvaa mwili na kuanza kazi lasimi, lakini wapiganaji wa neno hatuko nyuma kuhakikisha tunapiga majeshi mpaka shetani na vimalaika vyake vikome, kazi ya Mungu haitosimama kwa sababu ya nani kasema nini, ama yupi kafanya nini
      ........................HAKUNA TIBA YA KIFO............
      HESHIMU WATU NA PIA JIHESHIMU, KISHA, MPENDE MUNGU

    7. #105
      Drifter's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th January 2010
      Posts : 634
      Rep Power : 603
      Likes Received
      93
      Likes Given
      63

      Default Re: Gwajima wa kanisa la Ufufuo na ving'ora barabarani

      Kama kweli mhubiri huyo alipewa escort ya Polisi na vin'gora ili kumuwahisha tu anakokwenda basi kuna mushkeli katika jeshi la Polisi. Na hii haina uhusiano kabisa na hoja ya kwamba ni mtumishi wa Mungu. Huko nako ni kwingine kabisa; labda ianzishwe thread yake nyingine. Kama itabidi wahubiri wote wapatiwe huduma ya aina hiyo basi huo mtafaruku katika barabara zetu sijui utakuwaje. Anayefahamu kadhia ya ma-VIP wa Lagos na Abuja na ving'ora barabarani anaweza kuipata picha kidogo. Sidhani kama sisi tunataka kuwa namna hiyo. Aidha, ni dalili ya kukwama kimaendeleo.
      The sources of our fears reside within our depths

    8. Miaka 50

    9. #106
      kaburunye's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th May 2010
      Location : pandagisiza sogwinaminzi
      Posts : 679
      Rep Power : 599
      Likes Received
      57
      Likes Given
      13

      Default Re: Gwajima wa kanisa la Ufufuo na ving'ora barabarani

      Quote By anyisile obheli
      wafuasi wa ibilisi huwa hawapendi maendeleo ya mtumishi wa Mungu maana INJILI kama kawaida ni moto
      kwa watoto na wana wa pepo, sasa shetani ameuvaa mwili na kuanza kazi lasimi, lakini wapiganaji wa neno hatuko nyuma kuhakikisha tunapiga majeshi mpaka shetani na vimalaika vyake vikome, kazi ya Mungu haitosimama kwa sababu ya nani kasema nini, ama yupi kafanya nini
      Utukufu. Nadhani wewe ni shepherd au potential shepherd. Hahahahaaaaaaa. Piga majeshi na usonge mbele.

    10. #107
      mfianchi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st July 2009
      Location : Likulufusi
      Posts : 3,574
      Rep Power : 1222
      Likes Received
      580
      Likes Given
      1209

      Default Re: Gwajima wa kanisa la Ufufuo na ving'ora barabarani

      Kikolo Anyisile,kulalamikia ving'ora sio ushetani ,bali mimi nafikiri ufahari anaonyesha huyo mchungaji ,sijui mfufuaji ndio ushetani,kwa kutaka yeye tu ndie apite kwanza barabarani na wengine wakae pembeni huo ni ubinafsi na ubinafsi ni dhambi ,angekuwa ni kiongozi wa kiserikali isingekuwa nongwa kwa maana naamini analindwa na sheria na utaratibu wa nchi .Ndugu zanguni tusipofushwa na manabii wa uongo na tusitumie dini kuwaona wengine ni outcast!

    11. #108
      Ubungoubungo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th July 2008
      Posts : 2,024
      Rep Power : 956
      Likes Received
      334
      Likes Given
      33

      Default Re: Gwajima wa kanisa la Ufufuo na ving'ora barabarani

      watu wanahangaika kupigana na watumishi wa Mungu...hawajui kama hao ndo wanawaweka mjini kwa maombi hadi tunapata amani ya kuweza kufanya kazi zetu bila matatizo...wakinyamaza kimya hao tz hapa patakuwa pamoto.
      Haya yote ni ubatili mtupu, hakuna jipya hapa duniani!

    12. #109
      Mpeni sifa Yesu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd May 2010
      Location : Dar es Salaam
      Posts : 472
      Rep Power : 551
      Likes Received
      18
      Likes Given
      1

      Default Re: Gwajima wa kanisa la Ufufuo na ving'ora barabarani

      Quote By kaburunye
      Utukufu. Nadhani wewe ni shepherd au potential shepherd. Hahahahaaaaaaa. Piga majeshi na usonge mbele.
      umenikumbusha mbali na huu usemi wa "utukufu" bila shaka anyisile ni more than a sherphard au potential sherphad....nimesikia mmehamia kawe, nikirudi tu bongo nitashinda church mwezi mzima nipigwe msasa wa Bible school, nimemiss hakika mashambulizi niliyokuwa nayafanya.....

      Piga majeshi..hahaha, majeshi majeshiiii, Majeshi ya Bwana, wamepigwa wamepigwaaaaaaaaaa, wamekoma kabisaaaa...

      wameshindwa vita vya rohoni, wamehamia vita vya mwilini,ukiona adui anaanza kuonekana kupiga vita vya mwilini, ujue alishashindwa muda mrefu kwenye vita vya rohoni na hapo imebaki tu udhihirisho kimwili wa adui kuaibishwa na kusurrender kabisa...Tanzania nzima imetekwa kwa nguvu ya Jina la Yesu, wachawi waganga, washirikina wasoma nyota, wakuu wa anga, wakuu wa giza falme na mamlaka za nchi mkoa wilaya hadi kijiji zinahangaika...ukombozi wa wengi umekaribia, na siku ya kuaibishwa kwa shetani na wafuasi wake imewadia....
      FuturePresident likes this.
      Hakuna lisilowezekana kwa Mungu, anaponya, anaokoa. kwa ushauri na maombi, tuwasiliane ([email protected]). karibu kwa Yesu.

    13. #110
      Shadow's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th May 2008
      Posts : 2,017
      Rep Power : 965
      Likes Received
      156
      Likes Given
      104

      Default Mchungaji Josephat Gwajima anapolindwa kama rais

      Jani Jioni nilikutana na hiki kipindi katika luninga ya SIBUKA, ' Saa ya ufufuo na uzima' cha Pastor Josephat Gwajima [http://www.ufufuonauzimaministries.or g/]. Suala lililonishangaza ni ulinzi aliyokuwa akipewa na walinzi wake waliovalia kama walinzi wa maraisi (walkie talkie radio et cetera). Je hawa 'wachungaji' wa kileo hawana imani na mazingira yao ya kazi? Naomba kueleweshwa katika hili.
      Hasta ala victoria, siempré

      "Forever, Until Victory"

    14. #111
      Bujibuji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th February 2009
      Location : NYUMBANI PANONO
      Posts : 13,912
      Rep Power : 11208
      Likes Received
      7067
      Likes Given
      5296

      Default Re: Mchungaji Josephat Gwajima anapolindwa kama rais

      Biblia inatueleza kuwa amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, amfanyaye kuwa ngao na kinga ya maisha yake.
      Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa.
      Bwana asipoulinda mji waulindao wakesha bure.
      KAZI NDIO MSINGI WA MAENDELEO. NCHI MASIKINI HAIWEZI KUENDELEA KWA MSINGI WA FEDHA. NCHI MASIKINI HAIWEZI KUJITAWALA KAMA INATEGEMEA MSAADA KUTOKA NCHI ZA NJE- J. K. NYERERE

    15. #112
      Utingo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th December 2009
      Location : Lyazumbi
      Posts : 4,435
      Rep Power : 1385
      Likes Received
      596
      Likes Given
      405

      Default Re: Mchungaji Josephat Gwajima anapolindwa kama rais

      Quote By Bujibuji
      Biblia inatueleza kuwa amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, amfanyaye kuwa ngao na kinga ya maisha yake.
      Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa.
      Bwana asipoulinda mji waulindao wakesha bure.
      Wala usishangae, haya yote Yesu aliyasema, ni dalili za mwisho wa nyakati. People have turned Jesus to big profitable businesses.
      Without justice – Government is nothing but a band of robbers

    16. #113
      Shadow's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th May 2008
      Posts : 2,017
      Rep Power : 965
      Likes Received
      156
      Likes Given
      104

      Default Re: Mchungaji Josephat Gwajima anapolindwa kama rais

      Quote By Utingo
      Wala usishangae, haya yote Yesu aliyasema, ni dalili za mwisho wa nyakati. People have turned Jesus to big profitable businesses.
      Kweli tena, nilishangaa sana jamaa kama 'presidaa' na jamaa wanaonekana wamebeba 'miguu ya kuku'
      Hasta ala victoria, siempré

      "Forever, Until Victory"

    17. #114
      Pearl's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th November 2009
      Location : banda la kuku
      Posts : 3,043
      Rep Power : 1095
      Likes Received
      224
      Likes Given
      238

      Default Re: Mchungaji Josephat Gwajima anapolindwa kama rais

      Buji jamani duh!mbn wknd yangu inaanza kwa mibaraka?ubarikiwe sana uncle chelulute
      Quote By Bujibuji
      Biblia inatueleza kuwa amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, amfanyaye kuwa ngao na kinga ya maisha yake.
      Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa.
      Bwana asipoulinda mji waulindao wakesha bure.
      Forever young!I wanna be!
      SINGO AND NOT SEARCHING!

    18. #115
      Michelle's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th November 2010
      Location : Empire State of Mind
      Posts : 6,926
      Rep Power : 8703
      Likes Received
      1867
      Likes Given
      2692

      Default Re: Mchungaji Josephat Gwajima anapolindwa kama rais

      Muache alindwe,yule mchungaji anamtegemea Mungu sana ukisikiliza mahubiri yake utajua hivyo.Ana vita yake anayopigana na Ibilisi,watabiri na wanasiasa anaowapinga kila siku........usisahau pia ana Hummer yake .....lol na mara nyingi watu ni wengi wanaotaka kumuona wale walinzi ni wakuweka taratibu tu za kuonana nae na kuhakikisha yu salama na anatupiga injili kama kawaida as well as kutoa mapepo yanayotutesa.Basi we usiweke geti kwa kuwa Mungu atakulinda kwako???wala kule benki ulikoweka hela zako,ziombee tu lakini kusiwe na ulinzi?????
      FuturePresident likes this.

    19. #116
      pierre's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 3rd September 2010
      Posts : 211
      Rep Power : 485
      Likes Received
      1
      Likes Given
      0

      Default Re: Mchungaji Josephat Gwajima anapolindwa kama rais

      Kwani ni mchungaji yupi halindwi?.Kuna mambo ya rohoni,hufanywa kiroho,kuna mambo ya mwilini hufanywa kimwili.Paroko huwa na timu ya vijana kama wawili au wanne,mchungaji wa kilutheri huwa na wazee wa kanisa,hawa ndio walinzi.Kwa upande wa mchungaji Gwajima ni kutokana na huduma yake,anapambana na wazito waliochukua wenzao misukule,wengi wao ni vingozi wa siasa na wafanyabiashara.Hivyo kupewa ulinzi kama raisi ni sawa.Kwanini raisi alindwe?Hali kadhalika kiongozi yeyote anapaswa kuwa na ulinzi.Wala sio kusema amtumainie mwanadamu....hiyo sio sahihi.Ni haki yake kupewa ulinzi.
      FuturePresident likes this.
      Watu hawa ni watu walioibiwa na kutekwa na ccm wala hapana asemaye rudisha.Ungana na Dr.Slaa kusema RUDISHA

    20. #117
      Safari_ni_Safari's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th October 2007
      Location : Kibaruani
      Posts : 12,014
      Rep Power : 24158
      Likes Received
      4736
      Likes Given
      2652

      Default Re: Mchungaji Josephat Gwajima anapolindwa kama rais

      Wanalinda SADAKA zao zisiibiwe

      Soki Ozali Mwasi Yaka, Soki Ozali Mobali Koya Te


    21. #118
      Safari_ni_Safari's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th October 2007
      Location : Kibaruani
      Posts : 12,014
      Rep Power : 24158
      Likes Received
      4736
      Likes Given
      2652

      Default Re: Mchungaji Josephat Gwajima anapolindwa kama rais

      Quote By pierre
      Kwani ni mchungaji yupi halindwi?.Kuna mambo ya rohoni,hufanywa kiroho,kuna mambo ya mwilini hufanywa kimwili.Paroko huwa na timu ya vijana kama wawili au wanne,mchungaji wa kilutheri huwa na wazee wa kanisa,hawa ndio walinzi.Kwa upande wa mchungaji Gwajima ni kutokana na huduma yake,anapambana na wazito waliochukua wenzao misukule,wengi wao ni vingozi wa siasa na wafanyabiashara.Hivyo kupewa ulinzi kama raisi ni sawa.Kwanini raisi alindwe?Hali kadhalika kiongozi yeyote anapaswa kuwa na ulinzi.Wala sio kusema amtumainie mwanadamu....hiyo sio sahihi.Ni haki yake kupewa ulinzi.
      Uinzi dhidi ya nani?
      Rais analindwa kwa sababu ana mabaya anayoyafanya kwa watu wake...huyu mchungaji kafanya mabaya gani kwa waumini wake?

      Soki Ozali Mwasi Yaka, Soki Ozali Mobali Koya Te


    22. #119
      Humphnicky's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st December 2010
      Posts : 847
      Rep Power : 601
      Likes Received
      133
      Likes Given
      25

      Default Re: Mchungaji Josephat Gwajima anapolindwa kama rais

      Yesu alikuwa anafuatwa na watu wengi kuliko huyo Gwajima, mbona hakuwa na mabodigadi?

    23. #120
      drphone's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th September 2009
      Posts : 3,515
      Rep Power : 1194
      Likes Received
      99
      Likes Given
      10

      Default Re: Mchungaji Josephat Gwajima anapolindwa kama rais

      jamani mambo ya rohoni ni ya rohoni na mambo ya mwilini yanaenda kimwili kama ww si mchungaji uwezikujua vita ya wachungaji binafsi sioni kosa kwa mtumishi wa mungu kulindwa kwani nimeona watu wenye mapepo wakiwavamia watumishi wengine wanatumwa kwakweli ulinzi ni lazima
      FuturePresident likes this.

    Page 6 of 10 FirstFirst ... 45678 ... LastLast

    Similar Topics

    1. Mbunge Godbless Lema awa mwana maombi ya ufufuo
      By NIMEKIMBIA CCM in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 34
      Last Post: 9th December 2011, 10:52
    2. Usalama barabarani isiwe ajali barabarani
      By Njowepo in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 2
      Last Post: 31st August 2011, 13:31
    3. Replies: 22
      Last Post: 16th April 2010, 17:07

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...