Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Baba Mzazi Wa Mwanamuziki Diamond Aibuka-Soma Mambo Mazito Aliyosema Hapo Chini

    Report Post
    Page 1 of 3 123 LastLast
    Results 1 to 20 of 44
    1. #1
      nngu007's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 2nd August 2010
      Posts : 11,669
      Rep Power : 3652
      Likes Received
      3204
      Likes Given
      473

      Default Baba Mzazi Wa Mwanamuziki Diamond Aibuka-Soma Mambo Mazito Aliyosema Hapo Chini





      BABA mzazi wa nyota wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul Juma ‘Diamond’, (pichani) Abdul Juma ameibuka ambapo mbali na tukio hilo pia amenena mambo mazito kuhusu mwanaye huyo huku akimsukumia tuhuma nzito mama mtu, Amani linaanika kila kitu.





      ASAKWA PANDE ZOTE ZA DAR
      Awali lilitangulia zoezi la kumsaka baba Diamond katika pande zote za Jiji la Dar es Salaam ili kumsikia alichonacho moyoni kuhusu mafanikio ya mwanaye huku taarifa za mahali anapoishi zikipotoshwa na watoa habari wetu.
      Wapo waliosema mzee huyo anaishi Kibamba, wengine Mbagala, pia wapo waliodai anakaa Manzese au Magomeni, jijini Dar es Salaam.
      Timu ya mapaparazi wa Amani ilizama kazini kikamilifu ikiapa kumnasa mzazi huyo popote alipo na hatimaye Julai 2, 2012 saa saba mchana ilifanikiwa kupabamba nyumbani kwake, Magomeni Kagera, jijini Dar es Salaam lakini mwenyewe hakuwepo.
      Ziliachwa salamu za utambulisho kwa jirani mmoja ili atakaporudi mzee huyo amtaarifu kuwa mapaparazi watarudi siku nyingine.
      Julai 7, 2012 saa tano asubuhi mapaparazi wetu walitinga nyumbani hapo na kumkuta mzee huyo akisema alipata salamu na alikuwa akisubiri ujio huo, hivyo akawa amejiibua mwenyewe.





      AANZA KWA KUANIKA HISTORIA KWA UFUPI
      Baada ya salamu na utambulisho, mzee huyo alianza kwa kukiri kwamba kweli yeye ni baba mzazi wa Nasibu (Diamond) na kuweka wazi kwamba aliachana na mama mzazi wa msanii huyo miaka 9 iliyopita.
      “Ni kweli mimi ndiye Abdul Juma, ni baba mzazi wa Nasibu au Diamond. Eee, mimi niliachana na mama Nasibu miaka tisa iliyopita, tena siku tunatengana niliondoka nyumbani saa tisa usiku, maana nilikuwa naishi kwao (ukweni).


      AMGEUKIA DIAMOND
      Kinyume na matarajio ya kuzungumzia mafanikio ya mwanaye kwa sasa, baada ya kuwekwa katikati na waandishi wetu, mzee Abdul ‘aliangusha’ kilio cha lawama kwa Diamond kuhusu matendo anayomfanyia kila kukicha.
      Mzee huyo anayeonekana ‘kisharobaro’ alisema mafanikio makubwa aliyonayo mwanaye yasimfanye ashindwe kumthamini yeye kama baba na mapenzi yake kuyaelekeza kwa mama yake tu.
      “Kuhusu Diamond, labda nimwambie huyu mtoto kuwa, amepata mafanikio ndiyo, lakini mafanikio hayo yasimfanye ashindwe kunithamini mimi kama baba yake na kupeleka mapenzi yote kwa mama yake tu,” alisema.


      NI KWANINI?
      “Nasema hivyo kwa sababu, zamani kabla jina lake halijawa kubwa, mawasiliano yetu yalikuwa mazuri sana, lakini nikaja kushangaa baada ya kuwa staa, akakata mawasiliano na mimi baba yake, aliangalie hilo.”
      Akaongeza: “Sisemi kwa sababu nataka awe ananiletea hizo fedha zake, la hasha! Ila mimi kama baba yake ajue kuniheshimu.
      “Diamond nampigia simu hapokei, namtumia meseji hajibu, maana yake nini? Naumizwa sana na kitendo cha kutopokea simu yangu kila ninapompigia kumjulia hali. Na hali hii ameanza mara baada ya kupata mafanikio.


      JARIBIO LAIVU Katika kuthibitisha hilo, paparazi wetu alimtaka mzee huyo kumwendea hewani mwanaye ili kujiridhisha kama kweli ‘hapokeagi’ simu yake, simu ikapigwa, ikaita wee mpaka ikakatika.
      Baba Diamond: “Si umeona, si nilikwambia ukawa huamini.”


      MARA YA MWISHO KUMUONA DIAMOND
      Mzee huyo aliendelea kutiririka kuwa, mara ya mwisho Diamond kufika nyumbani kwake ilikuwa mwezi wa tatu (Machi) mwaka huu baada ya hapo mawasiliano yakakatika.
      “Diamond alikuja nyumbani kwangu mwezi wa tatu ikiwa ni mfungo wa tatu katika dini yetu ya Kiislam, akanipa fedha. Baada ya hapo hatujaonana tena wala hanijulii hali,” alilalama mzee wa watu.


      SMS YA MWISHO KUIJIBU
      Alisema Aprili, mwaka huu, Diamond alipotwaa tuzo tatu za Kili Music Awards 2012, yeye alimtumia ujumbe mfupi wa maneno akimpa hongera naye akajibu asante baba. Lakini baada ya hapo ikawa imetoka.
      “Baada ya kufanikiwa kutwaa tuzo za Kili, mwaka huu nilimpigia simu mwanangu ili nimpongeze, hakupokea, nikamtumia SMS ndipo akajibu, ‘asante baba’, mchezo ukaishia hapo.
      “Namshukuru sana dada yake, Mwajuma Abdul (Queen Darleen) yeye ndiyo yupo karibu sana na mimi kwani mara kwa mara anakuja kunitembelea na wakati mwingine hunikumbuka kwa fedha, hata pale aliposhinda tuzo ya Wimbo Bora wa Dancehall alifika nyumbani kunionesha tuzo yake, binafsi nilijisikia furaha,” alisema mzee Abdul ambaye kwa sasa hana mke.


      HAJUI ANAPOISHI MWANAYE
      Mbali na msanii huyo kutopokea simu ya baba yake kila anapompigia, vile vile mzee huyo alidai hajamuonesha wapi anapoishi.
      “Huyu mtoto hajawahi kunionesha anapoishi, sijui anafikiri nikiwa karibu naye nitakuwa namuomba fedha. Mimi sina njaa ‘kihivyo’ na wala sitaki fedha zake, ila ninachotaka salamu tu, nasikiasikia anaishi Mwenge (usahihi ni Sinza Mori) lakini hataki kunionesha.
      “Ninachojua yote haya yana mwisho kwani nyota aliyonayo sasa kuna siku itazima. Simuombei mabaya lakini inaniuma sana kunifanyia hivyo.”


      DIAMOND APIGIWA SIMU MARA KUMI NA MBILI
      Baada ya kupata matamshi hayo ya baba mzazi wa Diamond, mwandishi wetu siku ya Jumanne alifanya jitihada za kumpata msanii huyo ili ajibu ‘mashitaka’ hayo lakini licha ya kupigiwa simu mara kumi na mbili hakupokea.
      Mbali na kupigiwa simu, paparazi wetu alimtumia ujumbe mfupi wa maneno kupitia simu yake ya mkononi, lakini pia hakujibu kitu. Juhudi za kumsaka zinaendelea.


      Source: GPL


    2. #2
      IGWE's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2011
      Location : Blue Plaza Building-Arusha
      Posts : 5,312
      Rep Power : 3307
      Likes Received
      1335
      Likes Given
      1240

      Default Re: Baba Mzazi Wa Mwanamuziki Diamond Aibuka-Soma Mambo Mazito Aliyosema Hapo Chini

      mbona sioni jambo zito hapo
      "We should learn to help others,not only in our prayer but also in daily life,if we cannot help them_then,the least thing we can do is to desist from harming them"

    3. #3
      Arvin sloane's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th July 2011
      Posts : 889
      Rep Power : 578
      Likes Received
      131
      Likes Given
      40

      Default Re: Baba Mzazi Wa Mwanamuziki Diamond Aibuka-Soma Mambo Mazito Aliyosema Hapo Chini

      Dingi hana lolote anataka mkwanja tuu.
      nngu007 likes this.

    4. #4
      Babuu Rogger's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 16th November 2011
      Posts : 244
      Rep Power : 431
      Likes Received
      36
      Likes Given
      2

      Default Re: Baba Mzazi Wa Mwanamuziki Diamond Aibuka-Soma Mambo Mazito Aliyosema Hapo Chini

      Baba ni baba hata ukiwa unamiliki Millioni Mia, Diamond arudi nyuma ana bahati sana baba yake yupo hai.
      Mamndenyi and Nawai like this.
      THERE AIN'T NO HIDING PLACE FROM THE FATHER OF CREATION.

    5. #5
      matumbo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th July 2011
      Posts : 2,430
      Rep Power : 1468
      Likes Received
      716
      Likes Given
      679

      Default

      Quote By IGWE
      mbona sioni jambo zito hapo
      jambo zito lipo mkuu,huu ni mwanzo tu wa hii tamthilia na itauza sana magazeti..watu wako kwenye biashara.
      St. Paka Mweusi and Nawai like this.


    6. #6
      Babuu Rogger's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 16th November 2011
      Posts : 244
      Rep Power : 431
      Likes Received
      36
      Likes Given
      2

      Default Re: Baba Mzazi Wa Mwanamuziki Diamond Aibuka-Soma Mambo Mazito Aliyosema Hapo Chini

      Quote By Arvin sloane
      Dingi hana lolote anataka mkwanja tuu.
      Usiseme hivyo ndugu yangu.
      Nawai likes this.
      THERE AIN'T NO HIDING PLACE FROM THE FATHER OF CREATION.

    7. #7
      ALEYN's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th November 2011
      Location : Dar es Salaam
      Posts : 1,065
      Rep Power : 597
      Likes Received
      134
      Likes Given
      17

      Default

      Quote By Babuu Rogger
      Baba ni baba hata ukiwa unamiliki Millioni Mia, Diamond arudi nyuma ana bahati sana baba yake yupo hai.
      Take 92%
      Nawai likes this.

    8. #8
      MVUMBUZI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th January 2011
      Posts : 2,713
      Rep Power : 1118
      Likes Received
      712
      Likes Given
      380

      Default Re: Baba Mzazi Wa Mwanamuziki Diamond Aibuka-Soma Mambo Mazito Aliyosema Hapo Chini

      Quote By Babuu Rogger
      Baba ni baba hata ukiwa unamiliki Millioni Mia, Diamond arudi nyuma ana bahati sana baba yake yupo hai.
      Ni kweli mkuu na pia ukitaka kujua umuhimu wa kitu ni pale utakapokikosa. Huyu baba akifa katika mahusiano mabaya namna hii na Diamond kuna uwezekano mkubwa wa nyota yake kupotea kabisa . Aelewe pasipo huyu baba asingekuwepo duniani leo na hiyo inatosha kuwa na THOUSANDS OF ASANTE NA HESHIMA KWA BABA
      Nawai likes this.

    9. #9
      Arvin sloane's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th July 2011
      Posts : 889
      Rep Power : 578
      Likes Received
      131
      Likes Given
      40

      Default Re: Baba Mzazi Wa Mwanamuziki Diamond Aibuka-Soma Mambo Mazito Aliyosema Hapo Chini

      Quote By Babuu Rogger
      Usiseme hivyo ndugu yangu.

      Unataka nisemaje?

    10. #10
      sawabho's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th February 2011
      Location : Miyakojima
      Posts : 1,835
      Rep Power : 788
      Likes Received
      430
      Likes Given
      121

      Default Re: Baba Mzazi Wa Mwanamuziki Diamond Aibuka-Soma Mambo Mazito Aliyosema Hapo Chini

      Quote By IGWE
      mbona sioni jambo zito hapo
      Weeee, kutopokea simu ya Baba mzazi sio jambo zito, je kama anaumwa anataka akwambie neno la mwisho !!!!
      mjasiria, Nawai and tara like this.
      INAWEZEKANA, TIMIZA WAJIBU WAKO

    11. #11
      idawa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th January 2012
      Posts : 4,940
      Rep Power : 3406
      Likes Received
      1333
      Likes Given
      492

      Default Re: Baba Mzazi Wa Mwanamuziki Diamond Aibuka-Soma Mambo Mazito Aliyosema Hapo Chini

      ya kanumba (r.i.p) ya hamia kwa Almasi na atauza sana magazeti ya shigongo.!

    12. #12
      Mzizi wa Mbuyu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th May 2009
      Posts : 3,375
      Rep Power : 1309
      Likes Received
      589
      Likes Given
      428

      Default Re: Baba Mzazi Wa Mwanamuziki Diamond Aibuka-Soma Mambo Mazito Aliyosema Hapo Chini

      Quote By nngu007

      BABA mzazi wa nyota wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul Juma ‘Diamond’, (pichani) Abdul Juma ameibuka ambapo mbali na tukio hilo pia amenena mambo mazito kuhusu mwanaye huyo huku akimsukumia tuhuma nzito mama mtu, Amani linaanika kila kitu.


      ASAKWA PANDE ZOTE ZA DAR
      Awali lilitangulia zoezi la kumsaka baba Diamond katika pande zote za Jiji la Dar es Salaam ili kumsikia alichonacho moyoni kuhusu mafanikio ya mwanaye huku taarifa za mahali anapoishi zikipotoshwa na watoa habari wetu.
      Wapo waliosema mzee huyo anaishi Kibamba, wengine Mbagala, pia wapo waliodai anakaa Manzese au Magomeni, jijini Dar es Salaam.
      Timu ya mapaparazi wa Amani ilizama kazini kikamilifu ikiapa kumnasa mzazi huyo popote alipo na hatimaye Julai 2, 2012 saa saba mchana ilifanikiwa kupabamba nyumbani kwake, Magomeni Kagera, jijini Dar es Salaam lakini mwenyewe hakuwepo.
      Ziliachwa salamu za utambulisho kwa jirani mmoja ili atakaporudi mzee huyo amtaarifu kuwa mapaparazi watarudi siku nyingine.
      Julai 7, 2012 saa tano asubuhi mapaparazi wetu walitinga nyumbani hapo na kumkuta mzee huyo akisema alipata salamu na alikuwa akisubiri ujio huo, hivyo akawa amejiibua mwenyewe.


      AANZA KWA KUANIKA HISTORIA KWA UFUPI
      Baada ya salamu na utambulisho, mzee huyo alianza kwa kukiri kwamba kweli yeye ni baba mzazi wa Nasibu (Diamond) na kuweka wazi kwamba aliachana na mama mzazi wa msanii huyo miaka 9 iliyopita.
      “Ni kweli mimi ndiye Abdul Juma, ni baba mzazi wa Nasibu au Diamond. Eee, mimi niliachana na mama Nasibu miaka tisa iliyopita, tena siku tunatengana niliondoka nyumbani saa tisa usiku, maana nilikuwa naishi kwao (ukweni).

      AMGEUKIA DIAMOND
      Kinyume na matarajio ya kuzungumzia mafanikio ya mwanaye kwa sasa, baada ya kuwekwa katikati na waandishi wetu, mzee Abdul ‘aliangusha’ kilio cha lawama kwa Diamond kuhusu matendo anayomfanyia kila kukicha.
      Mzee huyo anayeonekana ‘kisharobaro’ alisema mafanikio makubwa aliyonayo mwanaye yasimfanye ashindwe kumthamini yeye kama baba na mapenzi yake kuyaelekeza kwa mama yake tu.
      “Kuhusu Diamond, labda nimwambie huyu mtoto kuwa, amepata mafanikio ndiyo, lakini mafanikio hayo yasimfanye ashindwe kunithamini mimi kama baba yake na kupeleka mapenzi yote kwa mama yake tu,” alisema.

      NI KWANINI?
      “Nasema hivyo kwa sababu, zamani kabla jina lake halijawa kubwa, mawasiliano yetu yalikuwa mazuri sana, lakini nikaja kushangaa baada ya kuwa staa, akakata mawasiliano na mimi baba yake, aliangalie hilo.”
      Akaongeza: “Sisemi kwa sababu nataka awe ananiletea hizo fedha zake, la hasha! Ila mimi kama baba yake ajue kuniheshimu.
      “Diamond nampigia simu hapokei, namtumia meseji hajibu, maana yake nini? Naumizwa sana na kitendo cha kutopokea simu yangu kila ninapompigia kumjulia hali. Na hali hii ameanza mara baada ya kupata mafanikio.

      JARIBIO LAIVU Katika kuthibitisha hilo, paparazi wetu alimtaka mzee huyo kumwendea hewani mwanaye ili kujiridhisha kama kweli ‘hapokeagi’ simu yake, simu ikapigwa, ikaita wee mpaka ikakatika.
      Baba Diamond: “Si umeona, si nilikwambia ukawa huamini.”

      MARA YA MWISHO KUMUONA DIAMOND
      Mzee huyo aliendelea kutiririka kuwa, mara ya mwisho Diamond kufika nyumbani kwake ilikuwa mwezi wa tatu (Machi) mwaka huu baada ya hapo mawasiliano yakakatika.
      “Diamond alikuja nyumbani kwangu mwezi wa tatu ikiwa ni mfungo wa tatu katika dini yetu ya Kiislam, akanipa fedha. Baada ya hapo hatujaonana tena wala hanijulii hali,” alilalama mzee wa watu.

      SMS YA MWISHO KUIJIBU
      Alisema Aprili, mwaka huu, Diamond alipotwaa tuzo tatu za Kili Music Awards 2012, yeye alimtumia ujumbe mfupi wa maneno akimpa hongera naye akajibu asante baba. Lakini baada ya hapo ikawa imetoka.
      “Baada ya kufanikiwa kutwaa tuzo za Kili, mwaka huu nilimpigia simu mwanangu ili nimpongeze, hakupokea, nikamtumia SMS ndipo akajibu, ‘asante baba’, mchezo ukaishia hapo.
      “Namshukuru sana dada yake, Mwajuma Abdul (Queen Darleen) yeye ndiyo yupo karibu sana na mimi kwani mara kwa mara anakuja kunitembelea na wakati mwingine hunikumbuka kwa fedha, hata pale aliposhinda tuzo ya Wimbo Bora wa Dancehall alifika nyumbani kunionesha tuzo yake, binafsi nilijisikia furaha,” alisema mzee Abdul ambaye kwa sasa hana mke.

      HAJUI ANAPOISHI MWANAYE
      Mbali na msanii huyo kutopokea simu ya baba yake kila anapompigia, vile vile mzee huyo alidai hajamuonesha wapi anapoishi.
      “Huyu mtoto hajawahi kunionesha anapoishi, sijui anafikiri nikiwa karibu naye nitakuwa namuomba fedha. Mimi sina njaa ‘kihivyo’ na wala sitaki fedha zake, ila ninachotaka salamu tu, nasikiasikia anaishi Mwenge (usahihi ni Sinza Mori) lakini hataki kunionesha.
      “Ninachojua yote haya yana mwisho kwani nyota aliyonayo sasa kuna siku itazima. Simuombei mabaya lakini inaniuma sana kunifanyia hivyo.”

      DIAMOND APIGIWA SIMU MARA KUMI NA MBILI
      Baada ya kupata matamshi hayo ya baba mzazi wa Diamond, mwandishi wetu siku ya Jumanne alifanya jitihada za kumpata msanii huyo ili ajibu ‘mashitaka’ hayo lakini licha ya kupigiwa simu mara kumi na mbili hakupokea.
      Mbali na kupigiwa simu, paparazi wetu alimtumia ujumbe mfupi wa maneno kupitia simu yake ya mkononi, lakini pia hakujibu kitu. Juhudi za kumsaka zinaendelea.


      Source: GPL

      ...


      Mzee anafana na mwanae kichwa!!



      .........
      Ukweli ni maji ya chumvi unayotakiwa kuyaoga, ukiona mahali panawasha usiyachukie hayo maji....jua hapo pana jeraha pafanyie kazi.

    13. #13
      Safari_ni_Safari's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th October 2007
      Location : Kibaruani
      Posts : 12,431
      Rep Power : 24245
      Likes Received
      5084
      Likes Given
      2734

      Default Re: Baba Mzazi Wa Mwanamuziki Diamond Aibuka-Soma Mambo Mazito Aliyosema Hapo Chini

      Quote By IGWE
      mbona sioni jambo zito hapo
      Kutakuwa na aidha baba wa kambo au baba wa kufikia

      Zogolo Dangu Dawika Miye!


    14. #14
      samora10's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st July 2010
      Location : Kwa-Gude
      Posts : 3,270
      Rep Power : 1110
      Likes Received
      732
      Likes Given
      1167

      Default Re: Baba Mzazi Wa Mwanamuziki Diamond Aibuka-Soma Mambo Mazito Aliyosema Hapo Chini

      Hao waandishi nao yanawahusu nini?
      ''Mipango na Mikakati imekamilika na sasa tuko kwenye mchakato wa mazungumzo na wafadhili"- M Pinda

    15. #15
      sikafunje.N's Avatar
      Member Array
      Join Date : 10th July 2012
      Posts : 86
      Rep Power : 366
      Likes Received
      15
      Likes Given
      14

      Default Re: Baba Mzazi Wa Mwanamuziki Diamond Aibuka-Soma Mambo Mazito Aliyosema Hapo Chini

      Like father like son ... 'masharobaro'
      It's time for money to work for me.

    16. #16
      Ukwaju's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 19th October 2010
      Location : Dodoma
      Posts : 3,573
      Rep Power : 1153
      Likes Received
      672
      Likes Given
      884

      Default Re: Baba Mzazi Wa Mwanamuziki Diamond Aibuka-Soma Mambo Mazito Aliyosema Hapo Chini

      Du hapa mama atafutwe aseme ukweli huenda Diamond keshampata Baba mwingine mbona naona mdomo hawafanani?
      Hata hivyo bado inaniuma kwani inaonyesha hata km aliimlea hata kumjali hataki, watoto wa kiswahili atadai Baba yake ana Harrier, Scania au yuko YUROP
      nngu007 likes this.
      Sending by: BlackBerry 8100 Smartphone using JamiiForum

    17. #17
      Money stunna's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th August 2011
      Location : BeechGrove City,Indianapolis
      Posts : 2,907
      Rep Power : 979
      Likes Received
      840
      Likes Given
      564

      Default Re: Baba Mzazi Wa Mwanamuziki Diamond Aibuka-Soma Mambo Mazito Aliyosema Hapo Chini

      inakuaje baba anapotelekeza family pamoja na watoto,mama apate shida peke yake kulea watoto peke yake,ccha ajabu watoto wakikua na kuwa na pesa,baba ndio anajileta? visa kama diamond,kanumba etc vinatukuta wengi,mu uwa sielewi baba wengine inakuaje atelekeza familia harafu mkifanikiwa baadaye ndio anajileta
      Helios likes this.

    18. #18
      Jaguar's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th March 2011
      Location : IRINGA
      Posts : 3,000
      Rep Power : 1089
      Likes Received
      679
      Likes Given
      256

      Default

      Quote By Babuu Rogger
      Usiseme hivyo ndugu yangu.
      Hebu mwambie huyo,mzazi ni mzazi tu,no matter what!

    19. #19
      Jaguar's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th March 2011
      Location : IRINGA
      Posts : 3,000
      Rep Power : 1089
      Likes Received
      679
      Likes Given
      256

      Default Re: Baba Mzazi Wa Mwanamuziki Diamond Aibuka-Soma Mambo Mazito Aliyosema Hapo Chini

      Kuna kitu nimepata hapa,kumbe QUEEN DARLEEN na DIAMOND ni ndugu!,hii inathibitisha ule msemo wa wengi kwamba watoto wa kiume hupenda kuwa karibu na mama zao na watoto wa kike kama QUEEN DARLEEN kamwe hawawatupi baba zao.

    20. #20
      shosti's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st December 2010
      Location : M'nyamala
      Posts : 4,959
      Rep Power : 1527
      Likes Received
      1425
      Likes Given
      1830

      Default Re: Baba Mzazi Wa Mwanamuziki Diamond Aibuka-Soma Mambo Mazito Aliyosema Hapo Chini

      si kila baba ni baba wengine wana majina yao

    Page 1 of 3 123 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...