KUFUATIA mafanikio alinayoyapata hivi sasa kwenye anga ya muziki wa kizazi kipya Bongo, staa wa muziki huo Naseeb Abdul ‘Diamond’ ndiye mkali aneingiza mkwanja mrefu zaidi kuliko nyota wote wanaotamba hivi sasa hapa nchini.
Uchunguzi uliofanywa na Teentz.com umebaini kuwa Diamond anaingiza kiasi cha shilingi za kibongo Milioni 16 kwa kila shoo mbili anazofanya akiwa ndani na nje ya jiji la Bongo.
Katika kuhakikisha kuwa ukweli unapatikana Teentz ilimsaka Diamond na baada ya kufanikiwa kumpata alikiri kufikia kiwango hicho .
“Nashukuru Mungu kwa kufika hapa na ukweli ni kuwa nalipwa mkwanja huo na hii imekuja kufuatia kuweka nguvu zangu katika muziki na kufanya vitu vizuri kwa kuwa gemu ndiyo maisha yangu” alisema Diamond.
Akiendelea zaidi nyota huyo wa ‘Songi’ la ‘Mawazo’ alianika kuwa mafanikko haya yanakuja pia kutokana na sapoti anayoipata kutoka kwa watu wake wa karibu akiwemo Mama yake mzazi na wengine kibao.
Hapa chini ni mkataba ambao amelamba kutoka kampuni ya Emilates Hall kupiga shoo huko pande za Mtwara
re: Baada ya Wema kumwaga, Diamond nae amwaga haya...
Kwani kulikuwa na ulazima wa kumuandika WEMA katika habari yako au na wewe nawe ndio walewale gazeti haliwezi uzika mpaka liwe na kichwa cha kinoko noko??
re: Baada ya Wema kumwaga, Diamond nae amwaga haya...
Kama kuna mtu wa TRA humu na ni mzalendo afuatilie tupate chetu kwa njia ya kodi tafadhali.Si sahihi kuvuna pesa za wananchi bila kulipa kodi.Moja ya mambo yanayowasumbua TRA kwenye kukusanya kodi ni watu/taasisi/makampuni kuficha mapato yao halisi .Sasa huyu amekuwa muwazi kuweka kipato chake ,TRA mpo wapi ?ama mnasubiri mkusanye kodi kwenye beer na sigara!!!?
re: Baada ya Wema kumwaga, Diamond nae amwaga haya...
By LEGE
Kwani kulikuwa na ulazima wa kumuandika WEMA katika habari yako au na wewe nawe ndio walewale gazeti haliwezi uzika mpaka liwe na kichwa cha kinoko noko??
huwezi jua, labda yeye ni intern wa gl0bal publ1shers,
re: Baada ya Wema kumwaga, Diamond nae amwaga haya...
mkataba mbovu ajabu, hivi tuhela take huto hanaga wanasheria wa kumsaidia kuingia mikataba, au anasubiri hadi apate tatizo kubwa ndo awe nao....manake mkataba huo umeeandikwa na mtu lay man mno....
Kama huna meno,usile bisi, kula Bwimbwi yaani kimbugi. Uongozi ukikushinda waachie wanaoweza!
Follow Us Here