HIVI HUYU MZEE BADO YUKO SERIKALINI TUU?
inamaana hakuna damu changa ambayo inawez akufanya hiyo kazi anaifanya?
HIVI HUYU MZEE BADO YUKO SERIKALINI TUU?
inamaana hakuna damu changa ambayo inawez akufanya hiyo kazi anaifanya?
drWHO,
Hivi anafanya kazi gani? Nijuavyo alikuwa kwenye bodi ya Vodacom. Unakumbuka alivyotukebehi kwa wivu wa kike?
Mhe, Jasusi!
Katibu Mkuu huyo wa kwanza wa CCM,bado yupo kwenye Board mbalimbali.Hivi karibuni alikuwa huko Japan,Holland na Germany kutangaza mambo ya Hifadhi ya Ngorongoro.Yeye ni Mwenyekiti wa Hifadhi ya Ngorongoro na pia ni Mjumbe kwenye kamisheni ya Ustawi wa makao makuu (Dodoma) ni Mjumbe kwenye kamati ya Ustawi wa kisiwa cha saa nane na pia mjumbe kwenye Board ya kampuni ya simu (Vodacom) ukiacha wadhifa wake wa Ujumbe wa Halmashauri kuu ya CCM,wanaomjua kwa karibu wanasema yeye ni CCM asilia pamoja na watu wengine wachache kama Mzee Kawawa Mzee Jumanne na Pius Ngeze bila kumsahau Athuman Kabongo.Ikumbukwe kuwa Mama pia bado yupo kwenye chart,kwani baada ya kuondoka kwenye serikali amejikita zaidi kwenye UWT (Mwenyekiti).Mzee Msekwa muda mwingi anautumia akiwa Dodoma,ambako haswa ndio makazi yake na sio Ukerewe!
Mwawado,
Thanks. Kwa mtaji huu angekuwa Marekani angekuwa tayari millionaire. Kwa sababu Marekani influence pays.
katika ile miaka ya sabini na mwanzoni mwa miaka ya themanini Msekwa alikuwa akifanya mambo yake kiakaili kweli kweli. Alikuwa ni kiongozi aliyekuwa na sifa mbili: (a) alikuwa akijiamini (b) alikuwa hababishi. Ni wachache sana kama Sokoine, Salim, Msuya, Amil Jamal na Mtei ambao pia walikuwa sifa kama hizo katika madaraka yao. Kuanzia Azimio la Zanzibar kuzaliwa na kuzuka kwa dira tofauti ya uongozi wa nchi, Mzee huyu aligeuka na kuwa mtu wa ajabu kweli kweli. Nashangaa kuwa bado yuko katika politiksi za nchi: Labda Jasusi na Mkandara wananaweza kumchambua huyu Mzee vizuri zaidi kuhusu kile kilichomkumba baada ya mabadiliko yale kwani kuanzia hapo hayuko tena kama yule Vice Chancellor wa UDSM wa enzi hizo au yule Principal wa Kivukoni College.
Last edited by Kichuguu; 19th March 2007 at 08:13.
Kichuguuu: Nyumba inayohifadhi mchwa na nguchiro kwa pamoja bila mkwaruzo
Jasusi,
kwani huyo muheshimiwa sasa hivi sio millionaire???
Jemba,
No, he is not. He is a billionaire.
Anazilipia kodi?
Vodacom alishapigwa chini looong time, baada ya kuukosa uspika tu jamaa wakamwandikia barua kumjulisha kipindi chake katika bodi kilishakwisha. Kwi kwi kwi.
Mafuchila,
Hawa hawalipi kodi. EL halipi kodi mali zote alizo nazo. Lakini Kichuguu, umegusa swala muhimu. Watu kama Msekwa na Kingunge walikuwa mstari wa mbele katika sera za ujamaa lakini baada ya Zanzibar ndio wamekuwa vigeugeu wa kupindukia.
Magazeti ya last week kila mmoja alisoma kwamba sasa Serikalio haina kazi 1milioni kama walivyosema wakati wa kampeni na wakati JK anachukua Nchi. They have backed down hadi 300,000 jobs to be created kila mwaka . Je ni sera ya CCM kusema uongp ili kuopata kura ? Kwa nini JK alikuwa anaahidi na kusisitiza jambo hili bila ya kulijua kwa undani ? Au nimekosea mimi kuelewa kwamba walisema kazi kila mwaka 1milioni ? Je kama wamekuja hadi kwenye 300,000 mwaka wameyajua lini ? Je kauli zao na akiwemo rais zichukuliwe vipi na watanzania ?
Je tumemwamini Rais na kauli zake ?
Je watanzania tumedanganywa tukawapa kura leo wanasema ukweli ?
Je kama tumedanganywa twende mahakamani kumshitaki Rais kusema uongo kabla wakat wa kampeni na baada yaa kiapo cha Urais ?
ana nini kinachomfanya haonekane billioner biashara,majumba,wake. tuambieni siri yake,sio kuandika kiujumla tu.
kuna thread ilianzishwa hapa juu ya mali za viongozi lakini imepita bila kuona baadha ya mali za hawa viongozi wetu zaidi ya porojo tu.hii ni sehemu ya ukweli na uwazi.
Follow Us Here