MSANII wa filamu ambaye pia anang’ara kwenye muziki kwa sasa, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ ameuanza mwaka 2012 kwa kulinadi penzi lake akidai, anayetaka kuwa mume wake awe na mkwanja wa kutosha.SHILOLE: Wa kufaidi penzi langu awe nazo - Global Publishers
Tamko hilo amelitoa mbele ya paparazi wa Ijumaa hivi karibuni Mwananyamala jijini, Dar alipokuwa akizungumzia mikakati yake ya kikazi kwa mwaka mpya.
“Mwaka jana sikuutendea haki sana katika kazi hivyo mambo yangu mengi hayakwenda sawa kiivyo lakini sasa nimekuja kivingine kwani mkwanja siyo tatizo hivyo hata huyo mwanaume atakayetaka kulifaidi penzi langu kama mke wake lazima awe nazo la sivyo bora nibaki peke yangu.
“Nimegundua wanaume wengi wanapenda mteremko kwa wanawake hivyo mwaka huu huyo anayejiita mume basi ajipange kweli kweli maana na mimi si mlaini bila fedha,” alisema Shilole.

Reply With Quote




Follow Us Here