 |
 |

20th July 2008, 10:00 PM
|
|
Senior Member
|
|
Join Date: Wed Jun 2008
Posts: 175
Rep Power: 61
Thanks: 21
Thanked 124 Times in 75 Posts
|
|
Re: Waziri wa Fedha atoka mikono mitupu kwa wafadhili
Chonde chonde wafadhili, msitoe pesa hizo hata kidogo. Msidanganywe na Serikali ya Tanzania kwamba eti hatuna pesa. Pesa tunazo lakini hatujui kupanga matumizi yetu (priority) na wizi umekithiri mno.
Viongozi wetu ni wezi wa kutisha, wamekuwa wakijunufaisha wao zaidi kuliko nchi ingawa wamekuwa wakitumia jina la Tanzania kuombea misaada hiyo.
Hii ni sawa na Baba kuomba mkopo ama msaada kwa jina la familia kwamba haina chakula ama ada za shule kumbe Baba huyo anamalizia mapesa ya msaada na mikopo kwenye kunywa pombe na kiti moto huku familia nyumbani haijui chochote kuhusu misaada na mikopo hiyo.
Ndugu wana JF tupige debe sana kuwaomba hawa wafadhili wasitoe pesa hizo kabisa.
|
|
The Following 2 Users Say Thank You to Kidatu For This Useful Post:
|
|

20th July 2008, 10:12 PM
|
 |
JF Senior & Premium Member
|
|
Join Date: Sun Feb 2007
Location: Buzwagi
Posts: 7,576
Rep Power: 2057
Thanks: 3,125
Thanked 3,602 Times in 2,051 Posts
|
|
Re: Waziri wa Fedha atoka mikono mitupu kwa wafadhili
Waungwana itakuwa si vibaya tukiandika barua kwa nchi zote za wafadhili kuwaunga mkono katika uamuzi wao wa kutotoa pesa ili kusupport budget ya 2008/2009 mpaka hapo wahusika wote na ufisadi wa EPA watakapotajwa hadharani na hatimaye kufunguliwa mashtaka.
__________________
I will die poor rather than stealing from Tanzanians through fake contracts and dubious ownership of Tanzanians' Natural Resources
|
|
The Following User Says Thank You to Bubu Ataka Kusema For This Useful Post:
|
|

22nd July 2008, 01:50 AM
|
|
Senior Member
|
|
Join Date: Wed Jun 2008
Posts: 175
Rep Power: 61
Thanks: 21
Thanked 124 Times in 75 Posts
|
|
Re: Waziri wa Fedha atoka mikono mitupu kwa wafadhili
Quote:
Originally Posted by Bubu ataka kusema
Waungwana itakuwa si vibaya tukiandika barua kwa nchi zote za wafadhili kuwaunga mkono katika uamuzi wao wa kutotoa pesa ili kusupport budget ya 2008/2009 mpaka hapo wahusika wote na ufisadi wa EPA watakapotajwa hadharani na hatimaye kufunguliwa mashtaka.
|
Hili ni wazo zuri sana. Wana JF kwa pamoja tunaweza kuandika barua na kuzifikisha kwa wafadhili ili kuomba ili suala lifanyike hivi tunavyotaka. (NO MISAADA KWA TANZANIA MPAKA PESA ZA EPA ZIRUDI NA WAHUSIKA KUCHUKULIWA HATUA ZA KISHERIA)
Mzee Mwanakijiji na Invisible mnasemaje kwa hili?
|
|
The Following User Says Thank You to Kidatu For This Useful Post:
|
|

18th September 2008, 08:12 PM
|
 |
JF Senior & Premium Member
|
|
Join Date: Sun Feb 2007
Location: Buzwagi
Posts: 7,576
Rep Power: 2057
Thanks: 3,125
Thanked 3,602 Times in 2,051 Posts
|
|
Hatimaye EU wakubali kutoa Sh. 860 billioni za maendeleo
Date::9/18/2008
Hatimaye EU wakubali kutoa Sh860bilioni za maendeleo
Boniface Meena
Mwananchi
NCHI 14 washirika wa maendeleo katika Mpango wa Kuchangia bajeti ya Tanzania (GBS) wamepanga kuipatia serikali Sh860bilioni (sawa na Dola 750milioni za Marekani) kwa ajili ya mwaka wa fedha 2008/09 ambayo ni sawa na asilimia 12 ya bajeti yote ya serikali.
Kiwango hicho ni pungufu kwa asilimia 22 ukilinganisha na asilimia 34 ambazo washirika hao waliahidi kutoa katika bajeti nzima ya serikali ambayo ni Sh7.2 trilioni.
Uamuzi wa kutoa msaada huu umetokana na mazungumzo ya karibu baina ya washirika wa maendeleo pamoja na Serikali ya Tanzania, mazungumzo yaliyochukua miezi tisa baada ya kashfa za ufisadi kuwafanya wasitishe kuanza kutoa fedha hizo za msaada kwenye bajeti ya Serikali ya Tanzania.
Balozi wa Denmark nchini, Bjarne H Sorensen, ambaye kwa sasa ni mwenyekiti wa kundi la nchi 14 washirika wa GBS, alisema jana kuwa washirika wote wa mpango huo wamethibitisha kutoa mchango wao kwa mwaka huu wa fedha.
"Hii inadhihirisha kuheshimu ahadi zetu kwa maendeleo ya Tanzania," alisema balozi huyo. "Serikali ya Tanzania imeimarisha usimamizi katika Benki Kuu pamoja na kuchukua hatua za kinidhamu dhidi ya maofisa wanaohusika.
"Uchunguzi juu ya suala la EPA umefikia hatua nzuri, ikiwa ni pamoja na kuweza kurejeshwa kwa baadhi ya fedha zilizochukuliwa na kuwagundua wahusika. Serikali imetuhakikishia kuwa uchunguzi utaendelea mpaka kufikiwa kwa hitimisho kamili.
"Tanzania imepata maendeleo muhimu. Lakini hakuna shaka kwamba changamoto bado zipo. Tutazitilia mkazo changamoto hizi wakati washirika wa GBS na serikali kwa pamoja tutakapotathmini maendeleo yaliyofikiwa katika mkutano utakaofanyika Novemba mwaka huu."
Aisema washirika hao wanataka kufanya kazi na serikali na asasi za kiraia ili kupata fursa za kukuza uchumi, na kuhakikisha kwamba Watanzania walio masikini zaidi wananufaika na mpango huo.
Pia alisema: "Uwajibikaji wa ndani ni kitu muhimu sana. Na katika jambo hili tumetiwa moyo na mchango unaotolewa na vyombo vya habari, asasi za kiraia na Bunge katika kuendeleza uwajibikaji.
“Mpango wa GBS unaipatia Serikali uwezo na motisha katika kuimarisha uwezo wake wa kubuni, kutekeleza na kufanikisha mipango yake ya maendeleo kwa muda mrefu na njia endelevu zaidi. Tutaendelea kufanya kazi pamoja na serikali kwa ukaribu ili kuhakikisha kuwa malengo na vipengele vya GBS vinaendelezwa,” aliongeza Sorensen.
Washirika wa maendeleo ambao wako kwenye mpango huo wa GBS ni Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB), Canada, Denmark, Kamisheni ya Nchi za Ulaya, Finland, Ujerumani, Ireland, Japan, Uholanzi, Norway, Sweden, Uswisi, Uingereza na Benki ya Dunia.
Wakati washirika hao wakiridhia kutoa fedha hizo, serikali jana ilipokea kiasi cha Sh216 bilioni kutoka serikali ya Uingereza, ikiwa ni sehemu ya mpango wa GBS.
Akizungumza na waandishi wa habari, waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo alisema serikali ya Uingereza ni moja ya nchi 14 washirika ambao husaidia bajeti kuu ya Tanzania kwa ajili ya kusaidia maendeleo.
Alisema misaada hiyo huenda moja kwa moja kwenye bajeti ya taifa na kuiwezesha serikali kutoa fedha katika sekta za maendeleo zilizopewa kipaumbele na kufanikisha Mkakati ya Kupunguza Umasikini na Kukuza Uchumi Tanzania (Mkukuta)
Taarifa ya maandishi kwa gazeti hili ya Julai 19 kutoka kwa Sorensen, ilithibitisha kwamba kundi la nchi hizo washirika lilifanya mkutano na Mkulo, ikiwa ni sehemu ya mikutano ya kawaida na mijadala wanayofanya na serikali hujadili na kuangalia maendeleo muhimu yatakayotoa fursa ya kuamua ni lini fedha hizo zianze kutolewa kwa bajeti ya mwaka 2008/09.
Katika taarifa hiyo, ilionekana kuwa washirika hao walikuwa wanasita kutoa fedha zao kusubiri hatua kuchukuliwa dhidi ya mafisadi, hasa katika sakata la wizi wa fedha za Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA), ufisadi ndani ya Benki Kuu ya Tanzania na taarifa ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Serikali (CAG).
Msimamo huu ulikwenda sambamba na kauli waliyotoa wakati wakiridhia kusaidia katika bajeti ya mwaka huu, waliposema: "Kabla ya kutoa fedha kusaidia bajeti hii, tunatazamia kupokea taarifa zaidi za utekelezaji wa namna serikali inavyopambana na tuhuma za rushwa, kuboresha utawala bora na utekelezaji wa mapendekezo ya CAG yaliyohusu ukaguzi wa hesabu za Benki Kuu ya Tanzania kwa mwaka wa fedha wa 2005/06."
Wafadhili hao waliahidi kuchangia asilimia 34 ya bajeti ya mwaka huu ya Sh7.2trilioni, hali ambayo iliiweka serikali kwenye wakati mgumu kama fedha hizo zisingetolewa kwa wakati kutokana na fedha hizo kutegemewa kwenye miradi mbalimbali ya maendeleo.
Mara ya mwisho washirika hao kuibana serikali katika bajeti yake ilikuwa wakati wa utawala wa serikali ya Awamu ya Pili iliyokuwa chini ya Rais Ali Hassan Mwinyi. Katika kipindi hicho, washirika hao walikataa kufadhili Tanzania kutokana na serikali kushindwa kukusanya kodi kiasi cha Sh70bilioni kwa wakati huo.
Wakati huohuo, serikali ya Marekani imesema Tanzania itahatarisha misaada yake kutoka nchini humo kama itagundulika kwamba misaada hiyo inatumika vibaya au kuishia katika mifuko ya viongozi mafisadi.
Akizungumza katika semina iliyoandaliwa na ubalozi wa Marekani nchini na kufanyika kwenye ukumbi wa hoteli ya Blue Pearl iliyo kwenye jengo la Ubungo Plaza, balozi wa Marekani nchini, Mark Green alisema wamarekani wanaisaidia sana Tanzania katika mambo mbalimbali, lakini iwapo watagundua kwamba misaada hiyo inatumika vibaya au kuishia katika mifuko ya viongozi mafisadi, watasitisha.
“Sisi ni wakarimu sana, lakini si wapumbavu kama Rais George Bush alivyosema wakati alipoitembelea Tanzania Februari mwaka huu kwamba 'hatutoi fedha zetu kwa mataifa ya kifisadi,'” alisema Green.
Alisema juhudi za Serikali ya Tanzania katika kupambana na ufisadi zinaonekana na imeifanya nchi kupata jina zuri katika jumuiya ya kimataifa, ikiwa kama mwanzilishi wa kweli wa vita dhidi ya ufisadi.
Alifafanua kuenea kwa programu za Mifumo ya Kufuatilia Matumizi ya Umma (PETS), kumesaidia sana katika kuipatia Tanzania jina zuri mbele ya jumuiya ya kimataifa.
“PETS inawafanya watumishi wa Umma kukumbuka kwamba kuna watu wanawaangalia na sio viongozi tu, bali watu wa kawaida na imewasaidia Watanzania wa kawaida kujiamini kwamba serikali yao inalinda maslahi ya walio wengi na si ya mtu mmoja mmoja,” alisema Green.
Alieleza kwamba katika hatua za awali za PETS wametoa mafunzo kwa zaidi ya waandishi 280 wa habari katika kuandika habari za uchunguzi, kutoa vifaa na mafunzo ya kupambana na ufisadi pamoja na kumsaidia mnunuzi mkuu wa vitu vya serikali katika kufanya ukaguzi wa manunuzi ndani ya mashirika mbalimbali ya kiserikali.
Katika hatua hiyo ya awali ambayo itamalizika mwishoni mwa mwezi huu alisema bila ya shaka kazi hiyo itaendelezwa na wale waliopatiwa mafunzo hayo.
__________________
I will die poor rather than stealing from Tanzanians through fake contracts and dubious ownership of Tanzanians' Natural Resources
|
|
The Following User Says Thank You to Bubu Ataka Kusema For This Useful Post:
|
|

19th September 2008, 02:59 AM
|
|
Senior Member
|
|
Join Date: Fri Mar 2008
Posts: 80
Rep Power: 21
Thanks: 0
Thanked 19 Times in 14 Posts
|
|
Re: Hatimaye EU wakubali kutoa Sh. 860 billioni za maendeleo
Hivi ndivyoninavyoipenda serekali yangu ya TANZANIA wamewezawapiga magoli wahisani na pesa zinatolewa kwa ulani hongera sasa kazi nikurudi kwa wananchi na kuwalaza chali tuendelee na mchakato wamaisha
|

19th September 2008, 11:48 AM
|
|
JF Senior Expert Member
|
|
Join Date: Wed Sep 2008
Location: Morogoro
Posts: 268
Rep Power: 21
Thanks: 23
Thanked 106 Times in 78 Posts
|
|
Re: Hatimaye EU wakubali kutoa Sh. 860 billioni za maendeleo
Narudia tena na tena na tena, hatuhitaji michango hii katika maendeleo yetu.Tunachohitaji ni kujipanga vizuri ili tu 'take off.'
|

22nd November 2008, 12:00 AM
|
 |
JF Senior & Premium Member
|
|
Join Date: Mon Jun 2007
Location: Mapinduzi - Iringa & Nyambiti - Mwanza
Posts: 3,087
Rep Power: 148
Thanks: 3,308
Thanked 1,814 Times in 1,021 Posts
|
|
Re: Hatimaye EU wakubali kutoa Sh. 860 billioni za maendeleo
Upokeaji wa misaada ni laana ya aina yake tuliyoshindwa kuipigia ramri, mwishowe kitafikia kizazi cha nne tokea uhuru laana hii ikiwa bado nasi!!
__________________
~*~ Happy New Year To You All !! ~*~
Fikra ni kitu kizuri, uzushi unatokana na fikra, fikra za uzushi ni kitu kibaya na ni uzushi, kutotenganisha uzushi na fikra ni kitu kibaya zaidi kwani mwisho wa fikra ni matendo pale fikra hazibakii kuwa fikra. SDD6-07.
|

22nd November 2008, 02:37 AM
|
 |
Senior Member
|
|
Join Date: Mon Mar 2008
Location: on planet earth
Posts: 2,535
Rep Power: 4026
Thanks: 1,409
Thanked 1,572 Times in 946 Posts
|
|
Re: Hatimaye EU wakubali kutoa Sh. 860 billioni za maendeleo
Nani alitulaani na tulimkosea nn hadi akatulaani kiasi hicho?
|
|
Currently Active Users Viewing This Thread: 1 (0 members and 1 guests)
|
|
|
| Thread Tools |
|
|
| Display Modes |
Linear Mode
|
Posting Rules
|
You may not post new threads
You may not post replies
You may not post attachments
You may not edit your posts
HTML code is Off
|
|
|
All times are GMT +3. The time now is 03:05 PM.
|
 |