Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Ushauri kuanzisha dry cleaner

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 21
    1. #1
      Mayu's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 11th May 2010
      Posts : 239
      Rep Power : 505
      Likes Received
      31
      Likes Given
      38

      Default Ushauri kuanzisha dry cleaner

      Wadau naombeni msaada wenu wa mawazo kwani naamini yupo mwenye kujua kuhusu hili.
      Nini capital kama 7milion nataka kuanzisha dry cleaner katika sehemu ambayo hakuna kabisa hiyo kitu.
      je capital hiyo inaweza kutosha, pia sijui ni mashine gani nzuri ya kufulia bei ya wastani.
      pia nahitaji kujua nahitaji washing machine kama ngapi kuanzia labda ya kufulia nguo za kawaida suti, na kusafisha macarpet.
      Nawasilisha

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      Lambardi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th February 2008
      Location : KITAANI ZAIDI
      Posts : 4,499
      Rep Power : 1791
      Likes Received
      653
      Likes Given
      0

      Default Re: Ushauri kuanzisha dry cleaner

      Labda ungeongeza hiyo capital maana hapo pango bado...machines ni bei kidogo...kama ukiagizaa...kuna watu wanagiza au kama unaweza uagize mwenyewe ila kwa 7m nakushauri uongeze kama 7m zingine....la sivyo badilisha biashara! Nunua bajaj 2 ndio size yako...kwa pesa hiyo....ni ushauri wangu tuu...nami nilifanya research 2yrs back....

    4. #3
      Nyumbu-'s Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th May 2009
      Posts : 666
      Rep Power : 641
      Likes Received
      65
      Likes Given
      204

      Default Re: Ushauri kuanzisha dry cleaner

      Quote By Skills4Ever
      Labda ungeongeza hiyo capital maana hapo pango bado...machines ni bei kidogo...kama ukiagizaa...kuna watu wanagiza au kama unaweza uagize mwenyewe ila kwa 7m nakushauri uongeze kama 7m zingine....la sivyo badilisha biashara! Nunua bajaj 2 ndio size yako...kwa pesa hiyo....ni ushauri wangu tuu...nami nilifanya research 2yrs back....
      Thanks,
      Hata mie nina wazo la hiyo biashara. Sasa ni vizuri umesema umefanya research miaka miwili iliyopita....unaweza tumegea mchanganuo wake japo roughly?
      Thanks

    5. #4
      Mayu's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 11th May 2010
      Posts : 239
      Rep Power : 505
      Likes Received
      31
      Likes Given
      38

      Default

      Quote By Nyumbu-
      Thanks,
      Hata mie nina wazo la hiyo biashara. Sasa ni vizuri umesema umefanya research miaka miwili iliyopita....unaweza tumegea mchanganuo wake japo roughly?
      Thanks
      Asante mkuu namimi nilitaka kujua hivyo.
      Mimi yangu nataka kufungulia mkoani na haswa kinacho nitatiza ni suti, siitaji kubwa sana kama za huku dar siunajua tena mambo ya mkoa

    6. #5
      Lambardi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th February 2008
      Location : KITAANI ZAIDI
      Posts : 4,499
      Rep Power : 1791
      Likes Received
      653
      Likes Given
      0

      Default Re: Ushauri kuanzisha dry cleaner

      Wana JF wajasirimali...kwanza unatakiwa ujue kuwa kila dry cleaner machines zina kilo tofauti bei yake inatokana na hizo kilo kuanzia 10kg and above....

      Kama unataka ziwe mbili ina maana utaagiza set hizo 2 na machine za kusuuza...kunyooshea...pia...

      Nawapa link kwanza msome mjue hata zina hitaji nini...pia umeme lazima uwe 3phase line...

      Dry Cleaning Machine (Series CBC-4) - China Dry Cleaning Machine, Washing Machine, Dryer Machine in Washing & Drying Machine

      Dry Cleaning Machine (22kg) - China dry cleaning machine, industrial dry cleaning machine, industrial washing machine in Cleaning Machine

      Sasa anzia pango la sehemu..vibalii...umeme na kuagiza kutoa bandarini....na kuzifunga....then cost za ndani sasa....sabuni etc...

      Jipange sawa sawa....all the best$
      Uliza bei kwa hizo link watakupa....haraka sana ila FOB ni kama 5,000 hivi dola

    7. Miaka 50

    8. #6
      Nyumbu-'s Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th May 2009
      Posts : 666
      Rep Power : 641
      Likes Received
      65
      Likes Given
      204

      Default Re: Ushauri kuanzisha dry cleaner

      Quote By Skills4Ever
      Wana JF wajasirimali...kwanza unatakiwa ujue kuwa kila dry cleaner machines zina kilo tofauti bei yake inatokana na hizo kilo kuanzia 10kg and above....

      Kama unataka ziwe mbili ina maana utaagiza set hizo 2 na machine za kusuuza...kunyooshea...pia...

      Nawapa link kwanza msome mjue hata zina hitaji nini...pia umeme lazima uwe 3phase line...

      Dry Cleaning Machine (Series CBC-4) - China Dry Cleaning Machine, Washing Machine, Dryer Machine in Washing & Drying Machine

      Dry Cleaning Machine (22kg) - China dry cleaning machine, industrial dry cleaning machine, industrial washing machine in Cleaning Machine

      Sasa anzia pango la sehemu..vibalii...umeme na kuagiza kutoa bandarini....na kuzifunga....then cost za ndani sasa....sabuni etc...

      Jipange sawa sawa....all the best$
      Uliza bei kwa hizo link watakupa....haraka sana ila FOB ni kama 5,000 hivi dola
      Good info:
      Hebu saidia zaidi
      1) Hii machine inanyoosha nguo automatically? Naona kwenye hiyo ya 22Kg inaonyesha hivyo.
      2) Ina hitaji chumba cha ukubwa gani kwa mujibu wa utafiti wako?
      3) Nini conditions zingine ambapo hiyo machine inatakiwa iwekwe?

      Thanks

    9. #7
      Lambardi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th February 2008
      Location : KITAANI ZAIDI
      Posts : 4,499
      Rep Power : 1791
      Likes Received
      653
      Likes Given
      0

      Default

      Quote By Nyumbu-
      Good info:
      Hebu saidia zaidi
      1) Hii machine inanyoosha nguo automatically? Naona kwenye hiyo ya 22Kg inaonyesha hivyo.
      2) Ina hitaji chumba cha ukubwa gani kwa mujibu wa utafiti wako?
      3) Nini conditions zingine ambapo hiyo machine inatakiwa iwekwe?

      Thanks
      1.Ukubwa unategemea na unataka machine ngapi...na pia machine huwa zinakaa kwa nyuma...kumbuka mbele si mapokezi...unaweka partition...ili wakati mchakato(usiku) unafua..wateja hawaoni....pia lazima kunakuwa sehemu kutolea mvuke...

      Hiyo machine ni ya kisasa zaidi...na ndio ya katikati...kwa kuanzia sio mbaya..

      Wakati mwingine unahitaji generator(onana watalam wa umeme na size hizo ujue ukubwa wa generator)...kama umeme unasumbuaa maana kazi za watuu zitalala...

    10. #8
      Mayu's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 11th May 2010
      Posts : 239
      Rep Power : 505
      Likes Received
      31
      Likes Given
      38

      Default"display:none" id="progress_1439643" style="display:none;visibility:hidden;" data-cfsrc="template/JamiV1/default/misc/quote_icon.png" alt="Quote" /> By Skills4Ever

      1.Ukubwa unategemea na unataka machine ngapi...na pia machine huwa zinakaa kwa nyuma...kumbuka mbele si mapokezi...unaweka partition...ili wakati mchakato(usiku) unafua..wateja hawaoni....pia lazima kunakuwa sehemu kutolea mvuke...

      Hiyo machine ni ya kisasa zaidi...na ndio ya katikati...kwa kuanzia sio mbaya..

      Wakati mwingine unahitaji generator(onana watalam wa umeme na size hizo ujue ukubwa wa generator)...kama umeme unasumbuaa maana kazi za watuu zitalala...
    Mkuu asante kwa info nzuri sasa umenipa mwangaza zaidi, nadhani nimepata pa kuanzia.
    ingawa bei inaonekana kama imesimama, vipi uliwahi kujaribu kucheck amazon na ebay kwa used mashine?
    Reply With Quote

  • #9
    The Finest's Avatar
    JF Senior Expert Member Array
    Join Date : 14th July 2010
    Posts : 21,682
    Rep Power : 6123
    Likes Received
    5861
    Likes Given
    4947

    Default Re: Ushauri kuanzisha dry cleaner

    Hii biashara ya dry cleaner inabidi uwe umejipanga kisawasawa hasa kwenye suala la generator maana umeme wa bongo ni kama ugonjwa wa moyo at any time you get screwed so namshauri angalie genrator zinaoendana na capacity ya hizo mashine anazotaka kuagiza all in i think for 7 million capital bado ni ndogo sana unless kama target ya biashara yake iko tofauti
    "What is legal, but not logical, logical, but not legal, and neither logical, nor legal?"


  • #10
    Ikimita's Avatar
    JF Senior Expert Member Array
    Join Date : 23rd October 2010
    Posts : 299
    Rep Power : 493
    Likes Received
    12
    Likes Given
    15

    Default Re: Ushauri kuanzisha dry cleaner

    Bado unaweza kuanza, kimkakati - mkoani sidhani kama italipa.

    Kama upo Dar chagua eneo moja la kuhudumia kwa mfano vyuoni ukaanzania Mlimani ukaunganisha na vyuo vya jirani au nenda kwenye hostels kubwa kubwa. Hauhitaji kufungua duka ila unatakiwa kununua bajaj moja kuifanya kuwa duka la kutembea. Bajaj yako jaribu kuijengea ka-body and then tenga sehemu mbili; upande mmoja ya kuchukulia nguo chafu na upande wa pili kuchukulia nguo safi zinazorudishwa.

    Kwa kuanza huhitaji mashine, ili kukupunguzia gharama za uendeshaji. Ajiri watu wawili wa kufua na mmoja wa kunyoosha na ku-pack nguo vizuri. Kazi hizi unaweza kuzifanya kutokea nyumbani (kama haukupanga chumba). Maji Dar ni mgao itakubidi kununua tank la kuhifadhia maji, ukipata ya kubeba lita 5000 itafaa sana. Ajiri mlinzi mmoja kukuangalizia nguo zilizoanikwa.

    Hii ni biashara kama zingine hakikisha unapata vibali na kujitambulisha kama mlipa kodi ili kuhalalisha shughuli zako. Tafuta label yako ya kukutambulisha eg DOWANS Laundry Services. Label na contact zako zote ziweke kwenye bajaj, zing'arishe kadri utakavyoweza. Kazi kubwa utakayofanya mwanzo mwanzo ni kutambulisha biashara (promotion) na kazi hii itabidi uifanye bila kuona aibu. Kwa huo mtaji nakushauri kazi ya promotion ufanye mwenyewe na jinsi hiyo itakubidi pia uwe dereva bajaj.

    Nakutakia mafanikio mema.

  • #11
    Lambardi's Avatar
    JF Senior Expert Member Array
    Join Date : 7th February 2008
    Location : KITAANI ZAIDI
    Posts : 4,499
    Rep Power : 1791
    Likes Received
    653
    Likes Given
    0

    Default

    Quote By Mayu
    Mkuu asante kwa info nzuri sasa umenipa mwangaza zaidi, nadhani nimepata pa kuanzia.
    ingawa bei inaonekana kama imesimama, vipi uliwahi kujaribu kucheck amazon na ebay kwa used mashine?
    Kama unataka used ones nenda www.alibaba.com hapoo dubai utapat*....all the best...mimi nilipata wazimu...na biashara upate sehemnu nzuri ya kuiweka...utashangaa..baada mwezi linatokeaa jitu lenye pesa...halikujuaa,..wapi aka invest utakoma jibu lake next 2 doors balaa ndio linaanzia hapo

  • #12
    Mayu's Avatar
    Senior Member Array
    Join Date : 11th May 2010
    Posts : 239
    Rep Power : 505
    Likes Received
    31
    Likes Given
    38

    Default

    Quote By The Finest
    Hii biashara ya dry cleaner inabidi uwe umejipanga kisawasawa hasa kwenye suala la generator maana umeme wa bongo ni kama ugonjwa wa moyo at any time you get screwed so namshauri angalie genrator zinaoendana na capacity ya hizo mashine anazotaka kuagiza all in i think for 7 million capital bado ni ndogo sana unless kama target ya biashara yake iko tofauti
    Hii mitaji itatuua jamani.
    Mkuu mfano kama unaanzisha na mashine moja tu na ikitokea umeme hamna unafua manual tabu ipo kwa makoti ya suti,
    target yangu ni mikoa ya singida au tabora najua wateja sio wengi sana, just kuanzia. hii imekaaje?

  • #13
    Mayu's Avatar
    Senior Member Array
    Join Date : 11th May 2010
    Posts : 239
    Rep Power : 505
    Likes Received
    31
    Likes Given
    38

    Default

    Quote By Ikimita
    Bado unaweza kuanza, kimkakati - mkoani sidhani kama italipa.

    Kama upo Dar chagua eneo moja la kuhudumia kwa mfano vyuoni ukaanzania Mlimani ukaunganisha na vyuo vya jirani au nenda kwenye hostels kubwa kubwa. Hauhitaji kufungua duka ila unatakiwa kununua bajaj moja kuifanya kuwa duka la kutembea. Bajaj yako jaribu kuijengea ka-body and then tenga sehemu mbili; upande mmoja ya kuchukulia nguo chafu na upande wa pili kuchukulia nguo safi zinazorudishwa.

    Kwa kuanza huhitaji mashine, ili kukupunguzia gharama za uendeshaji. Ajiri watu wawili wa kufua na mmoja wa kunyoosha na ku-pack nguo vizuri. Kazi hizi unaweza kuzifanya kutokea nyumbani (kama haukupanga chumba). Maji Dar ni mgao itakubidi kununua tank la kuhifadhia maji, ukipata ya kubeba lita 5000 itafaa sana. Ajiri mlinzi mmoja kukuangalizia nguo zilizoanikwa.

    Hii ni biashara kama zingine hakikisha unapata vibali na kujitambulisha kama mlipa kodi ili kuhalalisha shughuli zako. Tafuta label yako ya kukutambulisha eg DOWANS Laundry Services. Label na contact zako zote ziweke kwenye bajaj, zing'arishe kadri utakavyoweza. Kazi kubwa utakayofanya mwanzo mwanzo ni kutambulisha biashara (promotion) na kazi hii itabidi uifanye bila kuona aibu. Kwa huo mtaji nakushauri kazi ya promotion ufanye mwenyewe na jinsi hiyo itakubidi pia uwe dereva bajaj.

    Nakutakia mafanikio mema.
    Mkuu wazo lako angalau limenitia moyo.
    Mimi nimehamishiwa mkoa kikazi hivyo baada ya kutafiti nikaona biashara hii hakuna ndio maana nikaona nitumie nafasi hii kuanzisha.
    Tatizo wanasema kufua makoti ya suti mashine ni lazima

  • #14
    Mayu's Avatar
    Senior Member Array
    Join Date : 11th May 2010
    Posts : 239
    Rep Power : 505
    Likes Received
    31
    Likes Given
    38

    Default

    Quote By Skills4Ever
    Kama unataka used ones nenda www.alibaba.com hapoo dubai utapat*....all the best...mimi nilipata wazimu...na biashara upate sehemnu nzuri ya kuiweka...utashangaa..baada mwezi linatokeaa jitu lenye pesa...halikujuaa,..wapi aka invest utakoma jibu lake next 2 doors balaa ndio linaanzia hapo
    Mkuu kweli huo ni mtihani mgumu, unaangaika kuanzisha kitu, ukianza tu from no where wenye mihela yao wanakuja hivyo hivyo.
    Lakini ndio hivyo tunaambiwa wajasiriamali sikuzote ni ma risk taker

  • #15
    Nyumbu-'s Avatar
    JF Senior Expert Member Array
    Join Date : 26th May 2009
    Posts : 666
    Rep Power : 641
    Likes Received
    65
    Likes Given
    204

    Default Re: Ushauri kuanzisha dry cleaner

    Quote By Skills4Ever
    Kama unataka used ones nenda Manufacturers, Suppliers, Exporters & Importers from the world's largest online B2B marketplace-Alibaba.com hapoo dubai utapat*....all the best...mimi nilipata wazimu...na biashara upate sehemnu nzuri ya kuiweka...utashangaa..baada mwezi linatokeaa jitu lenye pesa...halikujuaa,..wapi aka invest utakoma jibu lake next 2 doors balaa ndio linaanzia hapo


    Interesting, though painfully true!
    Hata hivyo, ndivyo law of demand and supply in a perfect competion market inavyotuonya. Mnapouza bidhaa zinazofanana kunatokea price war, na hiyo hushusha bei ya vitu. Lakini linapokuja jamaa lenye mtaji mkubwa, litashusha bellow economic level, na litakuwipe out kutoka kwenye soko.
    Hata hivyo, unaweza survive na kamtaji kako kwa njia nyingi, na ya juu zaidi ni customer care na uaminifu. Kama una jina zuri, hata kama akaja mtu mwenye pesa pale, watu wataendelea kuwa Royal kwako bila kujali ukisasa wa machine ya rival wako.
    Mfano mzuri, ni Salon za kunyolea nywele mijini, zipo zingine za kisasa kabisa, lakini hazina wateja na zingine ndogo zinafurika: Sababu ni kwamba custors wameshaipenda kazi yako hivyo wamejenga bond iliyo zaidi ya biashara !
    So jirushe tu kama unaweza, na jitu likija na mipesa yake we unaweza ku-relocate au kubuni biashara mbadala......au kuingia naye ubia kama yuko tayari!

  • #16
    Baiskeli's Avatar
    JF Senior Expert Member Array
    Join Date : 8th December 2010
    Posts : 267
    Rep Power : 481
    Likes Received
    33
    Likes Given
    1

    Default Re: Ushauri kuanzisha dry cleaner

    sikiza mkuu usikate tamaa 7m unaweza kabisa anzisha hiyo kazi, tafuta machne ndogo tu ya kawaida kama hizi za majumba unapata machine nzuri tu kwa 1m inayofua na kukausha. haitaji 3phase. inauwezo wa kufua jeans 20 kwa saa. Muhimu ni sehemu ya biashara na matangazo. tengeneza office kali sana especially mapokezi fenicha zilizoenda shule, print bango moja kali sana liwe na picha ya mrembo mkali, bango liwe kubwa lijae pote kwa nje usiku liwake taa kali. usisahau kuandika unafua kwa machine za kisasa na wataalamu kutoka dar. tafuta mtu wa kunyoosha nguo mzuri asiwe wa hapo singida. usiruhusu watu kujua siri ya urembo wa ndani we wacha wababaike na urembo wa nje. weka na mfuaji 1 Wa mikono standby umeme ukikatika anacover. print vipeperushi vikali sambaza maotelini na maofisini. toa muda kwa mteja unaowezeka. mkuu mwanzo mgumu 7m kwa style hii utaweza. mwaka 1 utakuwa ushafunga hizo mashne.

  • #17
    Ikimita's Avatar
    JF Senior Expert Member Array
    Join Date : 23rd October 2010
    Posts : 299
    Rep Power : 493
    Likes Received
    12
    Likes Given
    15

    Default Re: Ushauri kuanzisha dry cleaner

    Quote By Mayu
    Mkuu wazo lako angalau limenitia moyo.
    Mimi nimehamishiwa mkoa kikazi hivyo baada ya kutafiti nikaona biashara hii hakuna ndio maana nikaona nitumie nafasi hii kuanzisha.
    Tatizo wanasema kufua makoti ya suti mashine ni lazima
    Mkuu, mkoa suti si nyingi sana labda Arusha, Mwanza, Kilimanjaro, Dodoma - zipotezee kwanza. Mkakati ni ule ule, badala ya kwenda vyuoni au kwenye hostels zungusha bajaj mtaa kwa mtaa na nyumba kwa nyumba huko ulipo utafanikiwa. Anza kwanza, utajiimarisha kadri siku zinavyoenda.

  • #18
    Lambardi's Avatar
    JF Senior Expert Member Array
    Join Date : 7th February 2008
    Location : KITAANI ZAIDI
    Posts : 4,499
    Rep Power : 1791
    Likes Received
    653
    Likes Given
    0

    Default Re: Ushauri kuanzisha dry cleaner

    Mkuu nakushaurii pia angaliaa hata biashara zingine hapo vipi car wash...??nayo ni nzurii tafuta bar maarufu,,......fungua kwa pembeni...utapata hata gari 5 tu kwa siku za kawaida na hata 10 kwa kila week end inatosha kwa 7m unapata machine na kujenga /tank lako la maji na pump machine..saafii kabisaa........fikiriaa na hii piaa dry cleaner inasum bua kidogo kwa vimitaji vyetu.....maana ukikwama utashindwa kuuza....kirahisi hizo machine
    "No matter how far down the wrong road you've gone,TURN BACK"

  • #19
    paulss's Avatar
    JF Senior Expert Member Array
    Join Date : 27th August 2009
    Posts : 3,610
    Rep Power : 4402
    Likes Received
    1086
    Likes Given
    977

    Default Re: Ushauri kuanzisha dry cleaner

    Mayu nataka nikutie moyo kuwa unaweza kabisa kufungua hiyo biashara kwa huo mtaji wako wa m7 (nahisi ni hela yako ya uhamisho ).
    Chakufanya kwanza anza na mashine ndogo ya wastani najua mkoani wateja mwanzo hawatakuwa wengi kivile, nunua washing mashine ya kama m1 hadi m2, inatosha sana kwa kufulia nguo za kawaida kama mashati, suruali, magauni, sketi, bauzi.pia mashuka, mapazia,nk.
    Makoti hayafuliwi na washing mashine yana utaratibu wake wa ku dry clean, waweza tafuta kuna dry cleaner simple kwa aajili ya kusafishia makoti manual.
    Pia tafuta mshine ya kusafishia makarpet ya kama lk5 inatosha sana nahii unaweza kuwafuata wateja hata majumbani si lazima walete ofisini.
    Cha umuhimu tengeneza ofisi kali inayovutia nje na ndani, weka muudumu smati hakikisha unatoa muda sahihi kwa mteja kuja kuchukua nguo zake.
    Hakikisha unapata mifuko ya plastiki na enga simple kuwekea nguo za wateja.
    Siku za mwanzo uwe kipromotion zaidi kwa kutoa viofa vya hapa na pale mfano, mteja kaleta nguo kumi basi mbili mwambie unamfanyia free.
    Mikoani kuna tv cable zinafanya matangazo bei powa sana, peleka matangazo,tengeneza vipeperushi vizuri jisifie sana kuwa unafua kutumia mashine na utaalamu wa kisasa zaidi.
    Kaunta ukiweza weka ka pc pale, feed kila kitu ili uwe unatoa risiti nk utaonekana makini na smati zaidi.
    Hakikisha at start zoezi unalisimamia wewe mwenyewe na hakikisha customer care ndio silaha yako no moja.
    Jitahidi upate ofisi sehemu nzuri kama katikati ya mji, unahitaji ofisi kwa maana ya sehemu ya kupokelea na kutoa nguo, hii ndio inayohitajika iwe ya viwango.
    pia unahitaji sehemu ya kufulia na kuanikia hii inaitwa factor, hapa inaweza kuwa hata nyumbani kwako kama utakosa sehemu utakayoshindwa kuigawa ofisi na factory.
    Pia kuwa mjanja si kila mara uwe unatumia washing mashine wakati mwingine tumia watu wako kufua kawaida labda kwa nguo maalum.
    Google namna mbali mbali za kufua aina mbali mbali na kupiga basi even how to dry clean suit nk jifunze mwenyewe kisha wafundishe watu wako na wasimamie.
    Mwisho nakutakia kila la heri ndugu yangu na usisite kurudi ukumbini kutujuza yaliyojiri
    Last edited by paulss; 4th January 2011 at 08:46.

  • #20
    funzadume's Avatar
    JF Senior Expert Member Array
    Join Date : 28th January 2010
    Location : Kwenye Uchafu/Uozo
    Posts : 3,465
    Rep Power : 1171
    Likes Received
    547
    Likes Given
    591

    Default Re: Ushauri kuanzisha dry cleaner

    Quote By BAISKELI
    sikiza mkuu usikate tamaa 7m unaweza kabisa anzisha hiyo kazi, tafuta machne ndogo tu ya kawaida kama hizi za majumba unapata machine nzuri tu kwa 1m inayofua na kukausha. haitaji 3phase. inauwezo wa kufua jeans 20 kwa saa. Muhimu ni sehemu ya biashara na matangazo. tengeneza office kali sana especially mapokezi fenicha zilizoenda shule, print bango moja kali sana liwe na picha ya mrembo mkali, bango liwe kubwa lijae pote kwa nje usiku liwake taa kali. usisahau kuandika unafua kwa machine za kisasa na wataalamu kutoka dar. tafuta mtu wa kunyoosha nguo mzuri asiwe wa hapo singida. usiruhusu watu kujua siri ya urembo wa ndani we wacha wababaike na urembo wa nje. weka na mfuaji 1 Wa mikono standby umeme ukikatika anacover. print vipeperushi vikali sambaza maotelini na maofisini. toa muda kwa mteja unaowezeka. mkuu mwanzo mgumu 7m kwa style hii utaweza. mwaka 1 utakuwa ushafunga hizo mashne.
    ulichoongea ni sahihi kabisa hata mimi nilitaka kumpa ushauri huu huu, Milioni 7 inatosha kabisa kuanzisha biashara ya Dry Cleaner ndogo ya kawaida tu kwani kwa mkoa uliopo nina uhakika kodi za vyumba vya biashara si kubwa kama DSM na pia kwa kuanzia nunua mashine za kawaida tu kama tunazotumia majumbani ila ziwe zenye capacity kubwa kidogo ambazo bei yake ni kuanzia laki 6 mpk milioni 1 nunua kama 3 hivi moja ya milioni na nyingine say za laki 8 na 6. Hakikisha mojawapo iwe inafua na kukausha kwa ajili ya wateja wenye haraka na hizo nyingine unatumia wakati mtu hana haraka kwa mfano akileta suti leo unamwambia aje kuchukua kesho kutwa

    pia uwe na mtu (dobi) ambaye atakuwa anafua kawaida nguo za kawaida na kuzianika na kupiga pasi vizuri kisha kuzihifadhi kwenye mifuko maalum yenye nembo ya Dry Cleaner yako.

    Mtaji ulionao ni mkubwa sana wala watu wasikukatishe tamaa ila cha muhimu ni kuangalia demand ya hiyo huduma ktk sehemu uliyopo ndio itakayokuahakikishia kuendelea kwa biashara yako

    Kwa kuanzia jaribu kuwa na mashine moja ya milioni yenye kufua na kukausha halafu ukiona soko ni zuri ongeza nyingine mbili kama nilivyokushauri hapo juu na kama ikichanganya zaidi ndipo ufikirie kuagiza mashine kubwa kutoka nje kama wengine walivyoshauri ila kwa sasa anza na mashine za kawaida za majumbani ambazo bei yake ni nafuu na zinafanya kazi vizuri tu maana mie nina mashine nilinunua laki 5 Mlimani City wakati ndio imeanzishwa na inatumika mpk leo na inafua vizuri tu na nina uhakika hata ningeitumia kwa biashara ingemudu vizuri tu kwani inafanya kazi poa sana

    Pia ukishaanza hiyo kazi tafuta tender kwenye mahospitali ya kufua mashuka na nguo zingine zinazotumika hospitali unaweza kutoka ila anza kidogo usiweke hizo hela zote mpaka usome soko kwenye ndio uweke hiyo M7 yote

    Wengi humu wanakuchuuza kwa kufikiria maofisi makubwa kwa zile dry cleaner za Shoppers Plaza au Namanga wakati mikoani wala hmna wateja kihivo

    Kwa ushauri wa kibiashara: [email protected]
    All good things in the World are not things

  • Study Abroad
    Page 1 of 2 12 LastLast

    Similar Topics

    1. Wataalamu wa DRY CLEANER
      By fikirini in forum Matangazo madogo
      Replies: 0
      Last Post: 8th October 2011, 10:57
    2. Ushauri Kuanzisha Bakery
      By Evmem in forum Business & Economic Forum
      Replies: 4
      Last Post: 30th May 2011, 12:51
    3. registry cleaner
      By PingPong in forum Tech, Gadgets & Science Forum
      Replies: 1
      Last Post: 16th February 2011, 14:20
    4. New vacuum cleaner - hahaha
      By Blue_Face in forum Jokes/Utani + Udaku/Gossips
      Replies: 0
      Last Post: 9th February 2011, 05:38

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...