Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Sweden yaipa Tanzania Sh. bilioni 44 kusambazia umeme vijijini

    Report Post
    Results 1 to 9 of 9
    1. #1
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,113
      Rep Power : 19194
      Likes Received
      8047
      Likes Given
      26489

      Default Sweden yaipa Tanzania Sh. bilioni 44 kusambazia umeme vijijini

      Serikali ya Sweden imesaini mkataba wa kuipatia Serikali ya Tanzania Sh.bilioni 44 kwa ajili ya mradi wa usambazaji wa umeme vijijini.
      Akizungumza wakati wa kusaini mkataba huo jana na Serikali ya Sweden, Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Ramadhani Khijjah, alisema msaada huo utasaidia kuondoa umaskini kwa wananchi vijijini pamoja na kuendeleza uchumi wao.
      Alisema ni asilimia moja tu ya wananchi wa vijijini wanaofaidika na umeme unaozalishwa nchini.
      Alisema lengo la msaada huo ambao umetolewa kupitia mfuko wa Uendelezaji wa Nishati ya Umeme Vijijini (Rea) ni kufanikisha Mpango wa Kukuza Uchumi na Kuondoa Umaskini (Mkukuta) na kuendeleza Kilimo Kwanza sehemu za vijijini.
      Khijjah alisema umeme huo utawezesha pia kuanzisha viwanda vidogovidogo kwa ajili ya utengenezaji wa mazao ya wakulima vijijini pamoja na kuongeza ajira. Khijjah aliongeza kuwa uanzishwaji wa viwanda sehemu za vijijini utasaidia pia kuongeza thamani ya mazao.
      Alisema malengo ya kufanikisha Kilimo Kwanza hayawezi kufikiwa endapo hakutakuwepo mpango madhubuti wa kufanikisha umeme vijijini na kuanzisha viwanda vidogovidogo kwa wakulima. Aidha, alisema jambo kubwa ambalo limekuwa likichangia wakulima vijijini kutofikia maendeleo ni ukosefu wa umeme. Alisema mikoa 16 ya Tanzania bara ndio inatarajia kunufaika na mradi huo.



      CHANZO: NIPASHE

      Je Serikali itasambaza umeme vijijini? kama huo msaada Serikali ya Tanzania iliyopewa na Sweden? au ndio hizo pesa zitwafikia Mafisadi? Nawaombeni mnijibu Wakuu wenzangu.
      Last edited by MziziMkavu; 10th November 2010 at 00:11.
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    2. Study Abroad

    3. #2
      Alaigwanani's Avatar
      Member Array
      Join Date : 9th November 2010
      Posts : 15
      Rep Power : 435
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Sweden yaipa Tanzania Sh. bilioni 44 kusambazia umeme vijijini

      Tatizo sio fedha. Tatizo ni TANESCO inahitaji mabadiliko makubwa ya kimfumo na ya kiutendaji. umeme haugawanjwi bure, tunalipia wanashindwa nini kusambaza umeme. Tanesco imefikia ilipo kutokana na ufisadi, mawazo mgando ya uongozi wake.Hizo fedha watazichakachua hazitafanya chochote!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

    4. #3
      Masikini_Jeuri's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th January 2010
      Location : Igangidung'u
      Posts : 5,953
      Rep Power : 2078
      Likes Received
      698
      Likes Given
      5029

      Default Re: Sweden yaipa Tanzania Sh. bilioni 44 kusambazia umeme vijijini

      Rai yangu kwa Serikali ya Kifalme ya Sweden; Chonde simamieni wenyewe zoezi zima la sivyo zitachachuliwa na walengwa hawatafikishiwa huduma!
      24 hours in a day! 24 beers in a case, Coincidence? I think not!

    5. #4
      Henge's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th May 2009
      Posts : 5,440
      Rep Power : 1674
      Likes Received
      918
      Likes Given
      1673

      Default Re: Sweden yaipa Tanzania Sh. bilioni 44 kusambazia umeme vijijini


    6. #5
      Chapakazi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th April 2009
      Location : Kathmandu
      Posts : 2,910
      Rep Power : 1095
      Likes Received
      256
      Likes Given
      272

      Default Re: Sweden yaipa Tanzania Sh. bilioni 44 kusambazia umeme vijijini

      ohh no! pesa zote zitaishia kwenye administration hizo! africa ni laana tupu!
      Change begins with YOU

    7. FemaTV & Radio

    8. #6
      genekai's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th February 2010
      Location : Loitering!
      Posts : 7,493
      Rep Power : 2077
      Likes Received
      1056
      Likes Given
      1568

      Default Re: Sweden yaipa Tanzania Sh. bilioni 44 kusambazia umeme vijijini

      Vijiji vipi? Wasahau si ajabu zishaingia kwenye accounts za mafisadi. Mara ngapi tumeambiwa hayo?
      The future of this country is being jeopardized by the intellectual slavery of our top leaders

    9. #7
      Masikini_Jeuri's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th January 2010
      Location : Igangidung'u
      Posts : 5,953
      Rep Power : 2078
      Likes Received
      698
      Likes Given
      5029

      Default Re: Sweden yaipa Tanzania Sh. bilioni 44 kusambazia umeme vijijini

      waombe kupewa ripoti ya matumizi na wakahakiki!
      24 hours in a day! 24 beers in a case, Coincidence? I think not!

    10. #8
      QUALITY's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th September 2010
      Posts : 844
      Rep Power : 606
      Likes Received
      109
      Likes Given
      343

      Default Re: Sweden yaipa Tanzania Sh. bilioni 44 kusambazia umeme vijijini

      Quote By MziziMkavu
      Serikali ya Sweden imesaini mkataba wa kuipatia Serikali ya Tanzania Sh.bilioni 44 kwa ajili ya mradi wa usambazaji wa umeme vijijini.
      Akizungumza wakati wa kusaini mkataba huo jana na Serikali ya Sweden, Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Ramadhani Khijjah, alisema msaada huo utasaidia kuondoa umaskini kwa wananchi vijijini pamoja na kuendeleza uchumi wao.
      Alisema ni asilimia moja tu ya wananchi wa vijijini wanaofaidika na umeme unaozalishwa nchini.
      Alisema lengo la msaada huo ambao umetolewa kupitia mfuko wa Uendelezaji wa Nishati ya Umeme Vijijini (Rea) ni kufanikisha Mpango wa Kukuza Uchumi na Kuondoa Umaskini (Mkukuta) na kuendeleza Kilimo Kwanza sehemu za vijijini.
      Khijjah alisema umeme huo utawezesha pia kuanzisha viwanda vidogovidogo kwa ajili ya utengenezaji wa mazao ya wakulima vijijini pamoja na kuongeza ajira. Khijjah aliongeza kuwa uanzishwaji wa viwanda sehemu za vijijini utasaidia pia kuongeza thamani ya mazao.
      Alisema malengo ya kufanikisha Kilimo Kwanza hayawezi kufikiwa endapo hakutakuwepo mpango madhubuti wa kufanikisha umeme vijijini na kuanzisha viwanda vidogovidogo kwa wakulima. Aidha, alisema jambo kubwa ambalo limekuwa likichangia wakulima vijijini kutofikia maendeleo ni ukosefu wa umeme. Alisema mikoa 16 ya Tanzania bara ndio inatarajia kunufaika na mradi huo.



      CHANZO: NIPASHE

      Je Serikali itasambaza umeme vijijini? kama huo msaada Serikali ya Tanzania iliyopewa na Sweden? au ndio hizo pesa zitwafikia Mafisadi? Nawaombeni mnijibu Wakuu wenzangu.
      Hizo fedha zitatafunwa tu. Unaona hela ni za kusambaza umeme vijijini inakuwaje ziende kuendeleza kilimo kwanza? Ina maana Kilimo kwanza ni umeme? Tunahitaji kujua idadi ya viji na kaya zilizopata umeme kutokana na fedha hiyo. Zisije ishia katika Per Diem kwa wakuu wakifanya upembuzi yakinifu.
      HONGERENI SANA WOTE MLIOMPA KURA DR. SLAA (PhD) ILI AIKOMBOE TANZANIA. MAPAMBANO YANAENDELEA

    11. #9
      mwanaharakati2's Avatar
      Member Array
      Join Date : 5th November 2010
      Posts : 17
      Rep Power : 436
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default

      Kwa kweli hizo pesa wakipewa TANESCO zitaishia mifukoni
      Mwa vigogo wachache. TANESCO kwa muda mrefu sasa imekuwa haitumii
      Gharama zake gharama zake kusambaza umeme lakini cha kushangaza
      Unapokwenda kutaka kusambaziwa umeme ukienda pale utazungushwa
      Mwisho wake wanataka pesa. Utakuta kuna eneo lina wakazi wa kutosha
      Wanaomba umeme na wanaambiwa watapelekewa kama project,
      Na ili kufanikisha hili wanataka uwape rushwa ya atleast 6M.
      Mfano pale ilala kuna mtu anaitwa MUSHI, huyu ni kinara wa rushwa.
      Yuko idara ya planning. TAKUKURU inabidi iingilie kati suala hili.
      Ikasafishe pale.

    12. Miaka 50

    Similar Topics

    1. Iran yaipa Tanzania trekta 100
      By mdau wetu in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 4
      Last Post: 14th October 2011, 21:43
    2. Iran yaipa tanzania dola milioni 1.2 kusaidia kilimo kwanza
      By mdau wetu in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 9
      Last Post: 2nd May 2011, 11:19
    3. Replies: 2
      Last Post: 18th April 2011, 13:07
    4. Mabilioni ya Sweden ya umeme vijijini yako wapi?
      By Owuocha in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 1
      Last Post: 28th March 2011, 11:56
    5. Japan yaipa Tanzania mabilioni ya chakula
      By MziziMkavu in forum Business & Economic Forum
      Replies: 1
      Last Post: 25th May 2010, 14:06

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...