Jamani naomba niulize kwa wana JF ambao ni wataalamu wa ujenzi.
Naomba wanipatie bajeti ya kujenga nyumba ya kawaida yenye vyumba 5, sebule, kitchen, dinning na sitting room ina cost kwa makisio shilingi ngapi?
Naomba nielimishwe,
Asanteni.
Jamani naomba niulize kwa wana JF ambao ni wataalamu wa ujenzi.
Naomba wanipatie bajeti ya kujenga nyumba ya kawaida yenye vyumba 5, sebule, kitchen, dinning na sitting room ina cost kwa makisio shilingi ngapi?
Naomba nielimishwe,
Asanteni.
Tuko pamoja mkubwa ukipata muda na kusimamia mwenyewe au mtu unae muamini Vyumba vitatu vya kulala, sebule na other rooms ka za choo,bafu etc gharama yaweza kuwa ndogo around 20m unahamia kwako ndani ya miezi michache tu. Hao wa 100m, 200m and abovu ni wakinga na wachaga wanaokwepa ushuru kariakoo na mafisadi wa TZ sie watumishi wasafi wa Serikali na vimshahara mbuzi we have to use common sense.
tuacheni kudanganyana hapa ... mfanyakazi gani wa kawaida (awe wa serikali au binafsi) mwenye uwezo wa kujenga nyumba ya mil 100+?? Labda ni makatibu wakuu na wakuregenzi tena kwa kupata mikopo ya riba nafuu benki!! vinginevyo ni wizi ndo utakufanya upate mil 100+ za kujengea nyumba! tunafurahisha baraza kwa kusema nyumba za m15+ sio realistic wakati wengi humu tumepanga kwenye nyumba za namna hiyo na wengine wazazi wetu walijenga nyumba za namna hiyo na tumekulia humo tukiwa angalau part ya middle-class families. No wonder nchi yetu inaibiwa sana kwa wanaojiita professionals ..... mfano mdogo ... barabara ya 1km inagharimu 2.5 bil - 10 bil?? nyumba ya gavana wa benki ... 1 bil?? Kwa kweli .... ni wizi tu!! Mungu atusamehe!!
I hope Guantanamo, you have gotten an answer and thank you for contributing such a open end question. I have learned a lot.
Wakuu asanteni. nimenufaika na discussion yetu.
Hapa nadhani ishu kubwa ni aina na kiwango cha nyumba. Ni kweli unaweza kujenga nyumba kwa mil 15 au chini ya hapo lakini swali ni ya kiwango gani? Actually huko vijijini watu wanajenga 'nyumba' kwa hata laki moja tu (ya miti na udongo, juu nyasi, nk ambavyo almost vyote anavipata bure tu) anachohitaji ni nguvu zake mwenyewe au kwa kushirikiana na ndugu na jamaa (hiyo laki moja ni ya kunuua mabaki ya ya madebe kwa ajili ya milango na madirisha na pombe ya watu kunywa wakati wakifanya kazi!).
"Rather than love, than money, than fame, give me truth" ----Thoreau
Hakuna mtu anayesema kuwa lazima ujenge nyumba ya milioni 100. Makosa ambayo wengi tunafanya ni kwanza kuchagua nyumba halafu kuulizia gharama za kuijenga! Ni kama vile mtu kuchagua suti ya Armani halafu kulalamika unapoambiwa ulipe maelfu ya dola. Kitu cha busara ni kuangalia kwanza uwezo wako, chagua mtaalamu kwa makini (yule ambaye unadhani atakuelewa na kujitahidi kutimiza mahitaji yako kwa uaminifu), kaa naye halafu muangalie kwa pamoja nini mnachoweza kupata kutokana na fedha ulizonazo. Ukweli ni kuwa kwa mfanyakazi wa kawaida hata nyumba ya milioni 10 inahitaji kujinyima sana. Lakini ukipata mchoraji creative, anaweza kukubunia kitu ndani ya bajeti hiyo ambacho utaridhika nacho. Kama uwezo wako ni sh. 100,000 kuna mafundi vyerehani kibao wanaoweza kukutengenezea suti isiyo na label ambayo unaweza kuolea bila matatizo. Kama uwezo ni 10000 basi itabidi ukaazime au ukabahatishe kwenye mitumba. Nyumba ni hivyo hivyo. Kama uwezo wako ni 10000 kwa mwezi itabidi ukubali kupanga au ujenge nyumba isiyo na msingi, kuta za nchi 4, bila siling, madirisha, milango na choo na bafu nje. Hauwezi kutaka nyumba yenye self container na jacuzzi, gereji ya magari mawili, maktaba, jiko la nguvu, chumba cha kuoshea nguo n.k. halafu ukagwaya unapoambiwa mamia ya mamilioni! Wengi wetu hatuko realistic yanapokuja maswala ya nyumba.
Amandla......
Fundi Utumbo
Usiwanyime watu mema yaliyo haki yao, ikiwa katika uwezo wa mkono wako kuyatenda (Mithali 3:27)
Yes huyo huenda alitaka kupata faida kubwa zaidi hiyo 500,000 ni material and labor na kwa kuwatumia wataalamu wa ujenzi waliosajiliwa na bodi kabisa.Ila angalizo ukienda kwenye kampuni kubwa kama Holtan,Noremco utakuta the same sqm wanacharge 700,000 overhead cost zao ni kubwa na kampuni kama hizo hazichukui miradi chini ya 1bn
Usiwanyime watu mema yaliyo haki yao, ikiwa katika uwezo wa mkono wako kuyatenda (Mithali 3:27)
Nyumba ya kawaidda ya vyumba 5,jiko,dinning na sitting ambayo haina tiles,haina ceiling board na ina madirisha ya nondo na mbao tu inagharimu 20,000,000/=milion. hapa kiwanja unacho na maji yapo kalibu.sema tena kamanda!
Kwa kukupa picha kidogo:
Mimi nina ongoing project, imefika kwenye linter, (Nyumba ya kawaida): 1 Masterbedroom moja, 1 Guest Room with attached toilet, 2 other Bedrooms, Study room 1, Laundry, Kitchen, Public Toilet & Bath, Dinning Room na Sitting Room...hadi sasa tayari $65,000 zimekatika! I just received estimates ya kupauwa (Kwa bati pana) ni kama $18,000..hapo ni mbao, mabati na ufundi etc. Sasa nikianza kufikiria finishing nahaisi nitapaswa kuwa na kama $30,000 nyingine (total kuanzia kuezeka)! Hapo sijaweka hesabu ya fence.....
Kwa mantiki hiyo bosi waliosema uwe na kama 100,000,000/= kwa uchache hawajakosea (ingawa mimi nashauri uwe na kama 160,000,000/=
jamani hapa mmenigusa sana kuna nyumba inauzwa ipo kimara mwisho ghorofani - njia ya kwenda bonyokwa mill 25 tu.kama kuna mhitaji jamani tuwasiliane
Humble One
Mimi nahitaji ya chini tu:
- 4 bedrooms (2 of which en-suite,one of which is adjacent to two ordinary one and the other as a guest room far from the three),plus a largely ventilated kitchen with store-cum-laundry room,Living room,dinning room,study
- Plot iko Mivumoni ya size 35mX55m slanting westwards (mteremko kimagharibi),main road towards south
Wenye design ideas please
Soki Ozali Mwasi Yaka, Soki Ozali Mobali Koya Te
Take it from me with not more than 50,000,000/= unajenga nyumba hiyo pamoja na uzio usiogopeshwe na watu. Mie nina nyumba ya vyumba vitatu, Master, choo na bafu la public ipo Makongo Juu DSM bado sijamalizia finishingi kama tiles na kuweka madirisha ya aluminium ila ina magrill na ni ya bati la kawaida ina upana na urefu ni almost futi 40 hadi sasa imekula kama 20 hivi.
An Eye for an Eye Makes the whole World Blind
Inategemea ni nyumba ya aina gani!kwa mfano unaweza kujenga nyumba ukapaua kwa kutumia bati za kawaida, na mwingine akatumia vigae. in this case,it is defenitely cost shall deffer,the former will pay less and the later will pay more!
kweli kutumia wataalam ni kitu mhimu sana,awa mafundi uswazi ni headache na utalizwa!
A 'parliament' is not only made up of our dear politicians,but is also a group of owls.
The greedy people are the victims to the evil people.
Follow Us Here