Jamani naomba niulize kwa wana JF ambao ni wataalamu wa ujenzi.
Naomba wanipatie bajeti ya kujenga nyumba ya kawaida yenye vyumba 5, sebule, kitchen, dinning na sitting room ina cost kwa makisio shilingi ngapi?
Naomba nielimishwe,
Asanteni.
Jamani naomba niulize kwa wana JF ambao ni wataalamu wa ujenzi.
Naomba wanipatie bajeti ya kujenga nyumba ya kawaida yenye vyumba 5, sebule, kitchen, dinning na sitting room ina cost kwa makisio shilingi ngapi?
Naomba nielimishwe,
Asanteni.
Nakushauri jenga nyumba yenye vyumba 3 vya kulala, sebule, jiko inatosha sana ukipata mgeni mwenye jinsia ya kike atalala na watoto wa kike na mwenye jinsia ya kiume atalala na watoto wa kiume huna haja ya kujenga vyumba vingi gharama itakuwa kubwa
Wakubwa, nimekuwa nikifuatilia swala zima la unjenzi humu, na sasa umefika muda wangu wa kujenga kasehemu ka kulala. Pesa zangu ni za kudundurisa hivyo najenga kwa speed ya kinyonga, tunapiga zege tunapumzika, tunasimamisha tofali mpaka dirishani tunapumzika... slow motion... Hivyo nina maswali yangu kadhaa.
Nina kiwanja Tegeta Mivumoni, Kimepimwa, Ukubwa wa kiwanja ni sqrm 600, ukubwa wa nyumba ni sqrm 450 (225 ground flow, 225 top flow) ina four bedrooms, mbili ziko up stairs mbili zipo down stairs, ina two living rooms, dining room, kitchen, pray room and four and half bathrooms. Plan yangu kuijenga ni 24 month project. Kwa sasa nina focus kwenye msingi, hivyo nataka kujua jee gharama zangu za msingi zitakuwaje?
Maana Kokoto niandae tani ngapi? Mchanga Tani Ngapi? Nondo Tani Ngapi? Cement Tani Ngapi? Mbao za zege kiasi gani? water Membrane Sheet Ngapi? Tofali za aina gani na ngapi? Kisha ufundi shillingi ngapi?
Nakubaliana na hesabu za Lakini tano kwa sqrm, lakini nadhani analysis yake hainipi full picture. So, nimeamua kuhire contractor lakini nitamlipa kwenye labor hour and I will control material. and if necessary I will hire consultant every now then. Lakini kwa sasa nataka kujua gharama hizo hapo juu.
If a free society cannot help the many who are poor, it cannot save the few who are rich.
Mtanganyika km una mchoro sioni sababu ya kutomshirikisha mkadiriaji...maswali yako hapa yatajibiwa kwa mazoea tu...kwa mfano depth ya foundation yako haiko wazi,aina ya foundation kwa maana ya strip,pad,raft au pile & beam,...uzito utakatarajiwa kukaa juu ya msingi huo n.k...kwanini usichukue hatua kumwona mshauri badala ya kufanya kazi kwa mazoea? Maana mwishowe hutakua umesave sana sana utaingia gharama zinazoweza kuepukika!
We are what we think. With our thoughts we make the world.
Horseshoe, nataka kwanza kupata estimate kutoka kwa watu kabla sijamuona mkandarasi. Concrete Slab ni kama ifuatavyo, Pile and Beam is my plan kwa sasa, urefu wa nguzo kwenda chini ni one meter, nina nguzo 23 zote zinabidi ziungwe na nondo across then zege limwagwe. I just need rough number kisha nikae chini nifanye my own analysis kabla sijaenda kukaa na building economist
If a free society cannot help the many who are poor, it cannot save the few who are rich.
Mimi naweza kukujibu kama ifuatavyo:
Ujenzi wa nyumba yako umekuwa si wa kama sisi waswahili bali wa kitaalamu. Kwa kuwa nyumba yako ni two floors na ina ramani tayari, kwa kawaida wachoraji wazuri wa ramani hufanya makadirio ya ujenzi, ingawa gharama hupanda kila wakati, hata hivyo katika makadirio ya mchoro huo wamekuorodheshea idadi ya vifaa vitakavyotumika kwa kila stage kuanzia msingi hadi kufikia second floor. Kujua bei yake nenda kenye maduka ya vifaa vya ujenzi kujua bei ya kila kifaa zidisha kwa idadi inayotakiwa utajua bei yake.
Kwa mfumo wa nyumba yako unatakiwa kufuata makadirio ya ramani ya mchoraji, pia ujue kwa kuwa inabeba uzito mkubwa kutokana na kuwa na second floor unatakiwa kuwa makini sana katika kufuata ushauri wa wataalamu wa fani hiyo, vinginevyo ukifanya njia ya mkato majuto ni mjukuu.
Njia nyepesi tunazoshauri mara nyingi hapa ni kwa ajili ya nyumba za kawaida ambazo ni single floor ambazo hazibebi uzito wa pekee isipokuwa paa na ceiling board. Kama ingekuwa nyumba ya aina hiyo tungekusaidia lakini kwa hiyo ushauri wangu tumia tu makadirio ya mchora ramani ndio msingi mzuri wa kujua gharama yake. Kumbuka utahitaji mbao nyingi pamoja na magome mengi kutokana na complications nyingi za ujenzi wa ghorofa pamoja na mbao kadhaa za uandaaji wa mtembele wa wabeba nzege kwa ajili ya second floor. Hayo tu nakushauri. Thanks.
Mkuu nitafite am a quantity surveyor, I can work that out, nipate mchoro Nita quantify, +255712833135
If a free society cannot help the many who are poor, it cannot save the few who are rich.
Mkuu nakupa matumizi ya nyumba ambayo ground floor ina ni square meter 210. Gharama za msingi ilikuwa kama ifuatavyo:-
1. Nondo 8 mm = 79 pcs, 12mm = 70 pcs, 16 mm = 53 pcs (tani moja).
2. Mchanga = Lori 8 za Tani 18
3. Kokoto = Lori 12 za Tani 18
4. Tofali (za chipping i.e zenye kokoto ndani) = 2000
5. Mbao za zenge (record haikuwekwa vizuri ila ziligharimu 2.2 milioni in August 2011)
6. Damp Proof Membrane sheet 46
7. Simenti = mifuko 347
8. Mawe (for hard core) (ulitumika mchanga badala ya mawe, lori 25 za Tani 18).
9. Ufundi = 6 milioni (walitumika mafundi wa mitaani).
Pamoja na vikorombwezo vya hapa na pale around Tshs. 35.5 mil zimetumika kujenga msingi tu.
Nakutakia kila la kheri mkuu katika project hiyo.
Last edited by rmashauri; 18th January 2012 at 08:20. Reason: spelling
Haki huinua taifa bali dhambi ni aibu ya watu wote (Mithali 14:34)
Nataka kujenga Nyumba yenye paa la Zege ili miaka ijayo niuze juu au baadae niongeze kujenga ghorofa moja tu hapo gharama zinakuwaje Wataalam
alichoseam manyusi ni sawa ila ulichoandika hapa sio sio sahihi , kitaaluma huwezi kujenga vyumba vitano kwenye jengo la 50 m2 au kwa kiswahili mita 50 za mraba kama sijakosea kila kila kitu kina kiwango chake ukitaka kujenga vhumba 5 unatakiwa kuwa na jengo lisilopunua 100-120m2 kama hueliwi ni mita 10 kwa 10 , hivi sasa bongo hutaweza kujenga nyumba yenye kiwango kwa vhini ya sh 500,000 kwa m2
Wakubwa nimeongea na mmoja wa marafiki zangu, yeye ni architecture na amefanya kazi na tanroad kwa muda. Nimempeleka kwenye site na amashauri yafuatayo. Ameshauri kupiga Beam chini ambazo zitaunganisha na column, kisha tutajaza mawe mwisho tufunge mkanda.
Nimesikia wengi hapa wanasema ni muhimu kupiga concrete slab chini. Jee lipi ni lipi?
If a free society cannot help the many who are poor, it cannot save the few who are rich.
Hapa inategemea unaposema "chini" unazungumzia kitu gani hasa (msingi au jamvi?). Kwa hiyo unaposema "kupiga Beam chini" inaweza kuwa ndio huo huo msingi ambao wengine wanaweza kuuita "slab". Au pengine kwa kusema slab walikuwa wanamaanisha 'jamvi'. Kwa hiyo ili kupata majibu mazuri pengine ungesema ni chini ipi unayoizungumzia - level ya msingi au jamvi?
"Rather than love, than money, than fame, give me truth" ----Thoreau
SMU asante sana kwa response mkuu. Ninapozungumzia level ya msingi. Engineer wangu amesema kwamba kwa nyumba ya ghorofa moja kinacho itajika kwa msingi ni kuweka nguzo, nyumba ina nguzo 23, kuziunga nguzo kwa nguzo na Concrete Beam. Kisha kupandisha tofali la msingi. Then kujaza mawe na kuweka kifusi. then tunapiga jamvi la 3 inch. Amesema Nondo tani mbili za Mil 12 zinatosha au tani moja na nusu za Mil 16. Kama zikitumia Mil 12 then zinafungwa sita kwenye beam na column kama ni 16 zinafungwa 4.
Swali langu jee huu mkeka wa chini hauitaji kulaza nondo kama ule wa juu? Kutoka na ujuzi wangu mdogo wa engineer, kama akifanya kama nilivyozungumzia hapo juu. Kisha tukalaza tofali na sababu nina nguzo nyingi jee hii haitotosha kusupport slab ya juu? Sababu nimesoma watu wanaeleza nondo tani tatu au zaidi kwenye msingi? Jee hizi zote zilitumika katika nyanja gani?
Ujenzi sio mchezo nimekubali.
If a free society cannot help the many who are poor, it cannot save the few who are rich.
Garama ya Milioni 500, tuangalie living standard ya mtanzania, income then mention hiyo bei; Watanzania Wezi kabisa, Nenda Nairobi angalia majumba yaliyojengwa, then waulize construction cost, almost 1/4 ya bei ya Tanzania; Pili Nyumba ya milioni 500 ni approx.= $340,000.00 Ingia kwenye Internet tafuta hiyo nyumba kwa nchi yoyote duniani, amabo vipato vyao still ni kubwa kuliko Tanzania, angalia structure utakayo ona, ni gorofa nzuri tena inayo basement, garage lenye automatic door, hao watu waambie wakujengee kama hiyo na bei ipungue. Tusidanganyane, garama za nyumba inakadiriwa kulingana na pale unapo jenga, ata ukitaka kuuza nyumba ya vyumba vitatu manzese the same nyumba Osterbay cost more. Mambo kama haya ndo maana tuko nyuma east Africa and we can not compete. ujenzi wa nyumba ya kawaida iwe $330000, hiyo nyumba ya $33000 hata in west only few people can afford it. Ukienda Texas hiyo nyumba ni $150,000 tu - Je tutafika???
Follow Us Here