Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Uchakajuaji wa pembejeo za Kilimo

    Report Post
    Results 1 to 2 of 2
    1. #1
      luvara's Avatar
      Member Array
      Join Date : 9th April 2011
      Posts : 58
      Rep Power : 422
      Likes Received
      10
      Likes Given
      10

      Cool Uchakachuaji wa pembejeo za Kilimo

      Ni zipi sababu za msingi zinazoifanya serikali iendelee kuwalea wachakachaji wa pembejeo za kilimo? Mchakachuaji wa pembejeo za kilimo kwangu mimi ni mhujumu uchumi namba moja na anastahili kutupwa gerezani mara moja anapobainika na si kunyang'anjwa leseni ambayo anaweza kuomba na kupata nyingine hata kwa kupitia kwa rafiki yake. Kimsingi kumyanyang'a leseni mhujumu uchumi sio adhabu ni upuuzi mtupu. Nisaidieni kiwazo ndugu zangu na hapohapo muishauri serikali yetu namna bora ya kuwashughulikia wahujumu uchumi kupitia pembejeo za kilimo ambao wengi wao walituhujumu msimu ulipita wanafahamika.
      Last edited by luvara; 8th August 2012 at 13:35. Reason: Makosa ya kimaandishi

    2. Study Abroad

    3. #2
      Malila's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd December 2007
      Posts : 2,601
      Rep Power : 10970
      Likes Received
      826
      Likes Given
      444

      Default Re: Uchakajuaji wa pembejeo za Kilimo

      Suala hili ni gumu sana, sio jepesi kama unavyodhani. Kuna mtu serikalini aliwaambia viongozi wenzake wamwage ugali na yy atamwaga mboga, habari ikaishia pale. Katika hili nani atamfunga au kumshitaki mwenzake?

      Pembejeo zinaibiwa kwa mfumo maalumu tokea juu mpaka chini kwa wakala. Wanaokamatwa ni wale walioshindwa kupeleka kidogodogo kwa wahusika. Wale jamaa wanaovaa nguo nyeupe jinsi wanavyopokea kitu kidogo na kukipeleka kwa bosi wake na bosi huyu naye hupeleka kwa bosi wake naye hupeleka kwa bosi wake, sasa huyu wa chini ukimkamata na kumpeleka kwa bosi wake, utaambiwa andika maelezo kisha uje kesho saa nne. kinachofuata jamaa anapewa likizo au transfer kituo/mkoa mwingine.

      Msimu uliopita walipeleka mbolea feki wilaya fulani, hakuna aliyeshitakiwa, kwingine walipeleka mbolea baada ya msimu kupita, jamaa bado yuko ofisini na cheo juu, huko kwa Wasukuma walipeleka mbegu bomu za pamba, mbona kuko kimyaaaaaaaaa.

      Dawa ni kuwatoa hawa Magamba madarakani kwanza ili tusuke upya mfumo wetu baada ya kuufumua kabisa.
      kasopa likes this.
      Mtu mwema huacha urithi kwa wana wa wanawe.

    4. Miaka 50

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...