Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Asilimia 80 ya wakazi Dar hawajui kutunza fedha

    Report Post
    Results 1 to 11 of 11
    1. #1
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,153
      Rep Power : 19203
      Likes Received
      8086
      Likes Given
      26557

      Default Asilimia 80 ya wakazi Dar hawajui kutunza fedha



      Florence Majani

      UTAFITI uliofanywa na Taasisi ya kifedha ya Finscope, umebaini kuwa, asilimia 21 tu ya wakazi wa Jiji la Dar es Salaam na vitongoji vyake ndiyo wenye elimu ya usimamizi wa fedha huku asilimia 48 tu, wakiwa na ufahamu wa jinsi ya kujiwekea akiba.

      Matokeo ya utafiti huo yanamaanisha kuwa, karibu asilimia 80 ya wakazi wa Dar es Salaam, hawana elimu hiyo muhimu kwa maendeleo ya kiuchumi.

      Aidha utafiti huo ulionyesha kuwa, wanawake ni asilimia 54 ya wakazi wa jiji ambao huchukua mikopo na ni kundi ambalo ni waathirika wa ukosefu wa elimu hiyo ya kifedha.
      Utafiti huo uliofanywa mwaka 2009 ulibaini kuwa idadi kubwa ya Watanzania wanashindwa kufikia malengo ya kimaendeleo kwa kukosa elimu hii ya usimamizi wa kifedha na wengine kudidimia zaidi katika umasikini kwa sababu hiyo.

      Akizungumza wakati wa semina kwa waandishi wa habari jana jijini, mtoa mada Ally Goronya alisema kutokana na hali hiyo, taasisi ya Nuebrand inatarajia kutoa elimu ya huduma ya kifedha na uwekezaji bure kwa muda wa siku nne kuanzia Oktoba 10 hadi 13, katika Viwanja vya Mnazi Mmoja.

      Kuhusu madhara ya ukosefu wa elimu hiyo kwa Watanzania, Goronya alisema wateja wengi wanaochukua mikopo wamekuwa wakidhulumiwa haki zao kwa sababu hawana elimu ya kutosha ya kifedha.


      “Watanzania wengi wanakwenda kuchukua mikopo, lakini wanashindwa kujua haki zao jambo linalosababisha mikopo hiyo kutowasaidia na badala yake kuwadidimiza katika lindi la umasIkini,” alisema Goronya
      Alisema wengi huchukua mikopo bila kupata elimu na kujua haki zao ili kuwalinda na kunufaika na mikopo hiyo akitolea mfano, riba kubwa, muda wa marejesho na haki ya kuvunja mkataba wa marejesho kama masuala yanayowatesa wakopaji.

      “Wakati mwingine watoaji wa mikopo huacha kwa makusudi kuwaelewesha vizuri au kuwapa elimu watumiaji wa huduma hiyo, ili wawadhulumu haki zao, hasa katika marejesho na riba,” alifafanua Goronya.

      Aliongeza zaidi na kusema kuwa ni vyema Watanzania wakapata elimu hiyo ili wajue uchaguzi sahihi wa taasisi za fedha za kupata huduma, kwa kuangalia kiasi cha riba kinachotozwa, muda wa marejesho, muda wa kupewa mkopo na usiri wa taarifa za mtumiaji.

      Ofisa Mawasiliano wa Kampuni hiyo, Deogratius Kishombo alisema katika kampeni hiyo ambayo imepewa jina la ‘Wiki ya Huduma za Kifedha na Uwekezaji’, Watanzania watapewa elimu ya kukabiliana na madeni, kuhifadhi fedha, bajeti na nidhamu ya mikopo.
      Asilimia 80 ya wakazi Dar hawajui kutunza fedha
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      Slave's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th December 2010
      Location : jamiiforums area
      Posts : 2,883
      Rep Power : 4892
      Likes Received
      872
      Likes Given
      690

      Default Re: Asilimia 80 ya wakazi Dar hawajui kutunza fedha

      Hii elimu ni muhimu sana katika jamii taasisi nyingi zinafundisha tu namna ufanye nini ili upate fedha lakini hawafundishi namna ya kumjengea nidhamu ya matumizi ya pesa,pengine post hii sasa iwe ni sehemu muhimu kwa wana jf wenye elimu na mambo haya kutoa elimu zao hapa.

    4. #3
      Father of All's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th February 2012
      Posts : 3,093
      Rep Power : 1044
      Likes Received
      1828
      Likes Given
      3343

      Default Re: Asilimia 80 ya wakazi Dar hawajui kutunza fedha

      Mtimkavu you are right. Umenikumbusha jinsi watu wengi Dar walivyoingizwa mjini na kampuni moja tapeli iliyojulikana kama Jaba. Iliwaletea migari iliyokwisha kuwa written off wakaipwakia na kula kwao. Tatizo pia linachangiwa na serikali kwa kuendekeza kuwalinda wezi wachache wanaoonekana kufanya vizuri kifedha wakati ni wezi na mbumbumbu wasiojua kutunza fedha. Jikumbushe maisha ya kibiashara ya Gulamali na wenzake.

    5. #4
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14621
      Likes Received
      2841
      Likes Given
      1961

      Default Re: Asilimia 80 ya wakazi Dar hawajui kutunza fedha

      Ni wakati muafaka wasome "Rich Dad Poor Dad".

      Wazo: Mtambuzi aanze na hii task ya kutafsiri hiki kitabu Kiswahili kinaweza kuwa big hit badala ya kututafsiria vile visa vya Hollywood pekee.
      Mtambuzi likes this.
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    6. #5
      Silicon Valley's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 6th March 2012
      Posts : 104
      Rep Power : 383
      Likes Received
      17
      Likes Given
      47

      Default Re: Asilimia 80 ya wakazi Dar hawajui kutunza fedha

      ni jambo jema sana lakini kumbukeni watanzania hawako mnazi mmoja tu its just 0.0000001% ya watanzania, nashauri mikakati mingine ifanyike na wale wa mikoani pia

    7. Miaka 50

    8. #6
      Mtambuzi's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 29th October 2008
      Location : Dar Es Salaam
      Posts : 6,094
      Rep Power : 27013
      Likes Received
      8227
      Likes Given
      17325

      Default Re: Asilimia 80 ya wakazi Dar hawajui kutunza fedha

      Quote By zomba
      Ni wakati muafaka wasome "Rich Dad Poor Dad".

      Wazo: Mtambuzi aanze na hii task ya kutafsiri hiki kitabu Kiswahili kinaweza kuwa big hit badala ya kututafsiria vile visa vya Hollywood pekee.
      Nianze lini hiyo kazi mkuu......................?

    9. #7
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14621
      Likes Received
      2841
      Likes Given
      1961

      Default Re: Asilimia 80 ya wakazi Dar hawajui kutunza fedha

      Quote By Mtambuzi
      Nianze lini hiyo kazi mkuu......................?
      Immediately.
      Mtambuzi likes this.
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    10. #8
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14621
      Likes Received
      2841
      Likes Given
      1961

      Default Re: Asilimia 80 ya wakazi Dar hawajui kutunza fedha

      Quote By Silicon Valley
      ni jambo jema sana lakini kumbukeni watanzania hawako mnazi mmoja tu its just 0.0000001% ya watanzania, nashauri mikakati mingine ifanyike na wale wa mikoani pia
      Ndio maana tumemuomba Mtambuzi atutafsirie kitabu kinachofundisha mambo ya fedha "Rich Dad Poor Dad".
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    11. #9
      rodrick alexander's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th February 2012
      Posts : 705
      Rep Power : 508
      Likes Received
      170
      Likes Given
      333

      Default Re: Asilimia 80 ya wakazi Dar hawajui kutunza fedha

      Swala si kuweka pesa bank zamani ukiweka pesa bank pesa yako inaongezeka sasa hivi nikiweka pesa bank zinapungua kwani kuna service charge wanakata kila mwezi,kila nikitoa pesa wanakata pesa ,sijawahi kupata faida kutokana na pesa ninayoweka bank ingawa pesa hizo hizo zinanunua dhamana,zinakopeshwa kwa hiyo nikajiuliza niweke pesa bank zipungue au niwekeze sehemu nyingine nimeamua siwezi kuwaruhusu bank waniibie pesa zangu kwa kisingizio cha service charge au upuuzi mwingine

    12. #10
      ZeMarcopolo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th May 2008
      Posts : 7,173
      Rep Power : 5034
      Likes Received
      2412
      Likes Given
      2224

      Default Re: Asilimia 80 ya wakazi Dar hawajui kutunza fedha

      Ili uweke akiba au uwe na interest ya kuweka akiba ni lazima kwanza pesa yenyewe uwe nayo. Asilimia 80 ya wakazi hawana uhakika wa milo mitatu, watafikiria vipi kuweka akiba. Huo utafiti ni void! walitakiwa kutafiti from among watu wenye kipato ambacho ni above the living average.
      jamiif likes this.
      "To greed, all nature is insufficient"

    13. #11
      Micha's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th September 2011
      Posts : 269
      Rep Power : 442
      Likes Received
      100
      Likes Given
      48

      Default Re: Asilimia 80 ya wakazi Dar hawajui kutunza fedha

      Hii ni kweli kabisa, ndiyo maana ukienda benki leo kama unataka mkopo utapewa maelezo ya ubabaishaji tu ili mwisho wa siku kama utaamua kukopa wakuchakachue. Benki nyingi za siku hizi hawatoi maelezo sahihi na zaidi wanafanya matangazo ambayo ni 'window dressing' kwa sababu hayafanani na ukweli wa huduma wanazotoa.

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...