Mkuu BAK,
Si kuwa wanataka kwa ajili ya kula ila wanataka kama BI-DIESEL.
Kuna hii kampuni Giant ya mafuta hapa Poland na hadi nje ya mikapa inaitwa PKN ORLEN (
PKN Orlen - Wikipedia, the free encyclopedia) ambao kipato chao (faida) kwa mwaka wanacheza na kitu kama US $ 1 Bilion.
Hawa jamaa si wazalishaji tu wa mafuta ila katika kutimiza masharti ya Umoja wa nchi za Ulaya, basi kila mafuta yanayouzwa, lazima yawe na Bio-Diesel kiasi fulani, kama sikosei kwenye 5% au zaidi. Sasa katika kujiandaa na masharti hayo, wanafanya utafiti wa mafuta mengi ya Bio-Disel.
Waliomba mafuta ya NAZI ila jamaa ambaye ndiyo anaongea nao moja kwa moja ambaye ni kutoka Msumbiji, kavutia kwao Msumbiji. Ila kwa sababu ni jamaa yangu karibu, nimefanya kulazimisha na mie awatafutie soko jamaa zangu kwa mafuta mawese. Ni kiwanda kikubwa sana na huwa wanaagiza mafuta machafu na kuanza kuyasafisha wenyewe kwenye mitambo yao. Hivyo basi technical know how wanayo na hapo huweza kwa urahisi sana kuchanganya na Bio-Diesel ili kupunguza hewa chafu duniani.
Tutaangalia bei na matatizo mengine yatakayozuka kama itawezekana kufanya biashara au lahh.
Kwa kuongezea tu: Mafuta ya JETROPHER haya nayo wanatafuta. Nafikiri wanatafuta ya aina tofauti na kuyafanyia utafiti kwenye magari
Follow Us Here