Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: NSSF kumwaga mikopo Saccos kuanzia Julai

    Report Post
    Results 1 to 6 of 6
    1. #1
      BabuK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th July 2008
      Posts : 927
      Rep Power : 736
      Likes Received
      110
      Likes Given
      42

      Talking NSSF kumwaga mikopo Saccos kuanzia Julai

      WANACHAMA wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) nchini kupitia vyama vya Akiba na Mikopo (Saccos) wataanza kupata mikopo ya nyumba na masuala mengine ya maendeleo kuanzia Julai mwaka huu, ilifahamika jana.

      Ofisa Mipango Mkuu wa NSSF , Gerald Sondo alisema hayo jana alipoeleza mikakati mbalimbali ya mfuko huo katika kuboresha maisha ya wanachama.

      Sondo alisema NSSF imejipanga kuwakopesha wanachama fedha nyingi kwa ajili ya ujenzi wa nyumba zao, elimu na hata biashara na kwamba mkopo huo utapitia Saccos za wanachama mahali pa kazi.

      “Kima cha chini kuikopesha Saccos kitakuwa Sh 50 milioni, lakini cha juu kinafikia hadi Sh 1 bilioni’’ alisema opfisa huyo akiwa kwenye Viwanja vya Maonyesho vya Mwalimu Nyerere maarufu kwa jina la Sabasaba mtaa wa Barabara ya Kilwa.

      Alisema maandalizi ya kuanza kutoa mikopo imekamilika na kwamba NSSF inatarajia kuanza kutoa fedha kuanzia Julai Mosi na kwamba taarifa kuhusu mpango huo zilishatyolewa kwa wadau wakati wa mkutano uliofanyika Arusha mapema mwaka huu.

      Kuhusu masuala ya riba, Sondo alisema NSSF itahakikisha inatoa riba ndogo kwa Saccos na kwamba ni martarajio yake kwamba wanachama nao watapata fedha hizo bila ya kuwa na riba kubwa kama za vyombo vingine vya fedha.

      Alitoa wito kwa wanachama NSSF kuunza Saccos mahali pa kazi na kujiwekea akiba nyingi ili waweze kukopa fedha hizo ambazo malengo ni kuwasaidia wanachama ili kuboresha maisha yao.
      Chanzo: Mwananchi

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      Mr.Mak's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd February 2011
      Posts : 1,146
      Rep Power : 650
      Likes Received
      156
      Likes Given
      84

      Default Re: NSSF kumwaga mikopo Saccos kuanzia Julai

      Nauliza ivi hiyo mikopo itakuwa na riba? Na kama ndio kwanini wanitoze riba kwenye pesa niliyovujia jasho?

    4. #3
      ndetichia's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 18th March 2011
      Location : Mwime - Buswangili
      Posts : 18,196
      Rep Power : 5100
      Likes Received
      2776
      Likes Given
      231

      Default Re: NSSF kumwaga mikopo Saccos kuanzia Julai

      itabidi JE SACCOS nao wapeleke maombi kama kuna memba wenu ambaye ni memba NSSF..
      Mkeshahoi likes this.

    5. #4
      Mwita Maranya's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st July 2008
      Location : Ikorongo Game Reserve
      Posts : 7,955
      Rep Power : 12003
      Likes Received
      5275
      Likes Given
      5119

      Default Re: NSSF kumwaga mikopo Saccos kuanzia Julai

      Ni mpango mzuri kwa kuanzia kwni hizo fedha zetu tumekuwa tukizililia siku nyingi ili ziweze kutunufaisha.
      Ningewashauri wafikirie na kuweka utaratibu wa kuwakopesha wanachama mmoja mmoja (individually) kwakuwa si maeneo yote ya kazi yana saccos na mahali pengine zipo lakini si endelevu.
      Mkeshahoi likes this.
      Honesty is a very expensive GIFT. Do not expect it from cheap people.

    6. #5
      Mkeshahoi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th January 2009
      Posts : 2,251
      Rep Power : 983
      Likes Received
      200
      Likes Given
      786

      Default Re: NSSF kumwaga mikopo Saccos kuanzia Julai

      Quote By ndetichia
      itabidi JE SACCOS nao wapeleke maombi kama kuna memba wenu ambaye ni memba NSSF..
      kama nimisoma vizuri wanalenga SACCOS za mahala a kazi.. JE ni muunganiko wa watu wenye fani mbalimbali na inasimama yenyewe.... welwdi watusaidie katika hili..
      Hela silaha... Kisu Mzigo

    7. Miaka 50

    8. #6
      FemaraFe's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 17th April 2012
      Location : Kenya
      Posts : 8
      Rep Power : 358
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default buy famciclovir online

      buy famvir uk is an anti-viral medication which after transformation in human organism turns into penciclovir which is active against such viruses as Herpes simplex (types I and II), Varicella zoster, and the Epstein-Barr virus (EBV). Penciclovir penetrates into the cells infected by virus where being subjected to treatment by viral ferments it turns into penciclovir-triphosphate which inhibits replication of viral DNA. The medication has not effect on the non-infected cells. buy famciclovir no prescription is active against certain strains of Herpes simplex with changed DNA polymerase which are resistant to Acyclovir (Zovirax).

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...