Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: mchango wenu wa mawazo jamani....

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 22
    1. #1
      Jestina's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th January 2011
      Posts : 3,620
      Rep Power : 1446
      Likes Received
      842
      Likes Given
      334

      Default mchango wenu wa mawazo jamani....

      wakuu nina milioni kumi,najiuliza nifungue biashara sijui biashara gani hapa mtaniadvise au niweke msingi kny kiwanja changu kule kibaha tatizo nikiweka msingi sijui nitamaliza lini kujenga as sina uhakika/regular income na b, nikianza biashara ni biashara gani itakayonirudishia hela yangu ili niweze kujenga? msaada kny tutazzz.....

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      KOMANDOO's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th March 2012
      Posts : 413
      Rep Power : 631
      Likes Received
      254
      Likes Given
      17

      Default Re: mchango wenu wa mawazo jamani....

      Hizi thread ni nyingi sana humu, Tatizo letu ni wavivu wa kusoma, pitia humu janvini ziko nyingi sana

    4. #3
      sweetlady's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 24th December 2010
      Location : Tanzania
      Posts : 15,307
      Rep Power : 36527
      Likes Received
      7468
      Likes Given
      4604

      Default Re: mchango wenu wa mawazo jamani....

      Tarlisha likes this.
      Life without problems never make a strong and good person!

    5. #4
      Jestina's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th January 2011
      Posts : 3,620
      Rep Power : 1446
      Likes Received
      842
      Likes Given
      334

      Default Re: mchango wenu wa mawazo jamani....

      Quote By sweetlady
      sweetlady utakuwa umeshiba sana,unasinzia tu lol

    6. #5
      Jestina's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th January 2011
      Posts : 3,620
      Rep Power : 1446
      Likes Received
      842
      Likes Given
      334

      Default Re: mchango wenu wa mawazo jamani....

      Quote By KOMANDOO
      Hizi thread ni nyingi sana humu, Tatizo letu ni wavivu wa kusoma, pitia humu janvini ziko nyingi sana
      leta mawazo mapya,sio wote tugombee kufanya wakala wa m-pesa...maana ndio biashara mnayoadvise kila siku....

    7. Study Abroad

    8. #6
      andybird314's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd January 2012
      Location : Tanzania
      Posts : 2,668
      Rep Power : 964
      Likes Received
      551
      Likes Given
      283

      Default Re: mchango wenu wa mawazo jamani....

      Tanzania biashara bado nyingi sana so ni wewe tu.
      waweza kuwa muuzaji wa bidhaa kwa retail.
      Hapa itategemea sasa na biashara waweza anzisha duka la retail hasa pale kkoo na ukawa unanunua vitu kwa wafanyabiashara wakubwa unauza kwa retail ukiwa mvumilivu utakula mbivu

    9. #7
      JATELO1's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st October 2011
      Posts : 1,014
      Rep Power : 899
      Likes Received
      81
      Likes Given
      39

      Default Re: mchango wenu wa mawazo jamani....

      Hiyo pesa yako iweke kwanza mpaka utakapopata au utakapojua nini majibu ya haya maswali:
      1. Biashara gani ambayo una uwezo wa kuifanya (hapa tunamaanisha capacity)
      2. Eneo gani unataka kuifanyia hiyo biashara-je wateja wanapatikana sehemu hiyo? na banda la kufanyia biashara, gharama ya banda?
      3. Soko la hiyo bidhaa ikoje? nina maana ya je ina soko mwaka mzima au kwa kipindi fulani tu.
      4. Bidhaa utakazouza zitapatikanaje?
      5. Je mzunguko wa pesa katika eneo hilo ukoje?
      6. Je wateja wako ni kundi gani au ni watu wa aina gani?
      7. Mtaji wa biashara huo ni kiasi gani?
      8. Je unataka kufanya biashara mwenyewe au kuna mtu au watu utawaajiri ili wakusaidie, kama ndivyo je ni watu wa aina gani na nini gharama zao?
      9. Je hiyo biashara itahitaji kiasi gani, na unategemea kuuza kiasi gani kwa siku au kwa mwezi? na je unategmea baada ya muda gani mtaji wako ulioweka kwenye biashara iweze kurudi?
      10. N.K

      Kama hauwezi kujibu hayo maswali au 80 asilimia ya hayo maswali vizuri, basi hiyo pesa yako nakushauri ukatafute kiwanja eneo zuri ukanunue na mara utakapokuwa tayari unajua biashara gani ya kufanya, ndipo ukauze hicho kiwanja ili hiyo pesa utumie kwenye hiyo biashara. Kiwanja ununue sehemu ambayo ni potential ili utakapohitaji kuuza usipate shida.

      Onyo.
      Kamwe usipoteze pesa zako kwa kutafuta akuandalie business plan kabla hujajua bado ni aina gani ya biashara una uwezo wa kuufanya. Kama unahitaji sehemu ya kwenda kujenga capacity kwanza ili ukimaliza uweze kujua nini biashara gani unaweza kufanya. Na naamini baada ya muda mfupi sana,tena masaa 3 kwa siku ya jmosi na jpili tu na ndani ya miezi 3 tayari utakuwa na uwezo wa kujua ni biashara gani una uwezo wa kufanya. Usihofu gharama, kwani katika kipindi hicho gharama haizidi 300,000(laki tatu tu).

      unaweza uni pm au tuwasiliane kwa [email protected]
      Tarlisha likes this.

    10. #8
      KOMANDOO's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th March 2012
      Posts : 413
      Rep Power : 631
      Likes Received
      254
      Likes Given
      17

      Default Re: mchango wenu wa mawazo jamani....

      Quote By Tarlisha
      leta mawazo mapya,sio wote tugombee kufanya wakala wa m-pesa...maana ndio biashara mnayoadvise kila siku....
      Wewe kweli ni punguwani, hizo thread zote zina zungumzia M-PESA TU? Kwani huwezi kuwa na mawazo yako mwenyewe? Hizi hudumu Nchi nyingine ni pesa, tusipende vya bure sana,

      Huko uliko kuna kampuni za Consultancy wafuate na uwape pesa wakushauri nini cha kufanya, Na by the way hutapata michango yoyote ya maana make watu walisha choka na marudio rudio ya vitu vile vile,

    11. #9
      KOMANDOO's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th March 2012
      Posts : 413
      Rep Power : 631
      Likes Received
      254
      Likes Given
      17

      Default Re: mchango wenu wa mawazo jamani....

      Quote By TELO
      Hiyo pesa yako iweke kwanza mpaka utakapopata au utakapojua nini majibu ya haya maswali:
      1. Biashara gani ambayo una uwezo wa kuifanya (hapa tunamaanisha capacity)
      2. Eneo gani unataka kuifanyia hiyo biashara-je wateja wanapatikana sehemu hiyo? na banda la kufanyia biashara, gharama ya banda?
      3. Soko la hiyo bidhaa ikoje? nina maana ya je ina soko mwaka mzima au kwa kipindi fulani tu.
      4. Bidhaa utakazouza zitapatikanaje?
      5. Je mzunguko wa pesa katika eneo hilo ukoje?
      6. Je wateja wako ni kundi gani au ni watu wa aina gani?
      7. Mtaji wa biashara huo ni kiasi gani?
      8. Je unataka kufanya biashara mwenyewe au kuna mtu au watu utawaajiri ili wakusaidie, kama ndivyo je ni watu wa aina gani na nini gharama zao?
      9. Je hiyo biashara itahitaji kiasi gani, na unategemea kuuza kiasi gani kwa siku au kwa mwezi? na je unategmea baada ya muda gani mtaji wako ulioweka kwenye biashara iweze kurudi?
      10. N.K

      Kama hauwezi kujibu hayo maswali au 80 asilimia ya hayo maswali vizuri, basi hiyo pesa yako nakushauri ukatafute kiwanja eneo zuri ukanunue na mara utakapokuwa tayari unajua biashara gani ya kufanya, ndipo ukauze hicho kiwanja ili hiyo pesa utumie kwenye hiyo biashara. Kiwanja ununue sehemu ambayo ni potential ili utakapohitaji kuuza usipate shida.

      Onyo.
      Kamwe usipoteze pesa zako kwa kutafuta akuandalie business plan kabla hujajua bado ni aina gani ya biashara una uwezo wa kuufanya. Kama unahitaji sehemu ya kwenda kujenga capacity kwanza ili ukimaliza uweze kujua nini biashara gani unaweza kufanya. Na naamini baada ya muda mfupi sana,tena masaa 3 kwa siku ya jmosi na jpili tu na ndani ya miezi 3 tayari utakuwa na uwezo wa kujua ni biashara gani una uwezo wa kufanya. Usihofu gharama, kwani katika kipindi hicho gharama haizidi 300,000(laki tatu tu).

      unaweza uni pm au tuwasiliane kwa [email protected]

      Mkuu unahangaika kushauri Mtu Asiye kuwa siriasi,

    12. #10
      Mgombezi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd March 2009
      Posts : 628
      Rep Power : 642
      Likes Received
      130
      Likes Given
      139

      Default Re: mchango wenu wa mawazo jamani....

      FURSA YA BIASHARA NI NINI?

      Watu wengi wamekuwa wakijiuliza biashara za kuanza kufanya, wakati mwingine kumekuwa na baadhi ya watu ambao huwa na kianzio cha biashara (mtaji), lakini hawafahamu ni biashara gani wataweza kufanya.

      Fursa ya Biashara (Business Oppurtunity) hutokana na mahitaji ya watu katika eneo husika; kwahiyo katika kutengeneza wazo la biashara (Business idea) huanza kwanza kwa kuchunuguza fursa zilizopo katika eneo husika. Baada ya hapo hufuata mpango wa biashara (Business Plan).

      Kwa hiyo unapofikiria ni biashara gani ya kufanya ni vyema kuchunguza mahitaji yaliyopo katika eneo husika (inaweza kuwa mtaani kwako, katika mji au hitaji la Taifa). Kwa kweli nchi yetu bado kuna mahitaji mengi ambayo yanaweza kutumika kama fursa ya biashara; hebu jiulize toka unapoamka ni mahitaji au shida kiasi gani umekutana nazo, naomba kuorodhesha baadhi ya maeneo ambayo tunaweza kuchunguza mahitaji:

      1. Unapotaka kwenda kuoga asubuhi nyumbani kwako, unapata maji kwa urahisi?
      2. Je unapotaka kupata kifungua kinywa, unapata kitafunio kwa urahisi?
      3. Je unapotaka kwenda kazini au kwenye shughuli zozote, usafiri kutoka eneo lako uko vipi?
      4. Unapofika katika eneo lako la kazi au shughuli yeyote kuna vitendea kazi vya kutosha?
      5. Vitu gani vinakufanya kushindwa kutekeleza majukumu yako ya kazi au shughuli za kila siku?
      6. Unapotaka kupata chakula cha mchana, je unapata katika mazingira gani?
      7. .............................
      8. .............................

      Wengine wanaweza kuendeleza, mambo ambayo tunaweza kuchunguza kutokana na mazingira husika.

      Jambo lolote ambalo utaliona ni hitaji kwa watu basi hiyo ndio fursa ya biashara, kwa hiyo unapaswa kutengeza wazo la biashara. Tuache kuyachukulia mazingira yanayotuzunguka na mambo yanayoendelea katika jamii kuwa ni kawaida, kwa mfano unaweza kuwa unakwenda kupanda daladala kila siku kwa kugombania na ukachukulia hiyo ndio hali ya kawaida, lakini tunaweza kutumia hiyo hali kama fursa ya biashara na kutengeneza wazo la biashara.

      Tunapoaangalia mahitaji ya watu na kugeuza kama fursa ya biashara, basi hapo tutakuwa tunafanya biashara lakini vile vile tutakuwa tumekutana na mahitaji ya jamii inayotuzunguka na taifa kwa ujumla, kwa kweli jamii yetu bado ina mahitaji mengi; itashangaza kusikia kwamba hatujui nini cha kufanya na jamii inayotuzunguka. Hebu tuige mfano wa Mjasiriamali Bakhresa na kampuni yake ya AZAM, kwamba amekuwa akichunguza mahitaji ya jamii na kuleta bidhaa ambayo itakutana na hitaji hilo, mfano; CHAPATI, MIKATE, TUI LA NAZI na nyinginezo.

      Vile vile tujifunze kutofautisha fursa za biashara katika nchi zilizoendelea na nchi zinazoendelea kama ya kwetu; kwani upatikanaji wa fursa za biashara ndani ya Marekani ni tofauti na Tanzania; ndio maana katika nchi zilizoendelea wamekuwa na biashara za mitandao na biashara nyinginezo ambazo zisikiri kama zinaweza kuwa na ufanisi mkubwa zaidi kutokana na mazingira yetu; kwani nimeshawahi kuona baadhi ya link zikielekeza jinsi ya kutengeza fedha ka jinsi ya mtandao n.k. Nafikiri bado jamii yetu ina mahitaji mengi ambayo yanahitaji mtu wa kuyatatua.

      Nawatakia kila la kheri wajasiriamali wenzangu, katika kukutana na mahitaji ya jamii inayotuzunguka na kupunguza hili wimbi kubwa la kutegemea bidhaa kutoka nje; yaani tumeshindwa hata vijiti vya kusafisha meno, miti ya kuchoma mishikaki n.k, vimekuwa vikitoka China; hawa watu wamekuwa wakitoka mbali na wakifika hapa wanabaini fursa za biashara na kurudi kwao kutendea kazi.
      TELO and Tarlisha like this.
      Ebenezer

    13. #11
      Jestina's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th January 2011
      Posts : 3,620
      Rep Power : 1446
      Likes Received
      842
      Likes Given
      334

      Default Re: mchango wenu wa mawazo jamani....

      Quote By KOMANDOO
      Wewe kweli ni punguwani, hizo thread zote zina zungumzia M-PESA TU? Kwani huwezi kuwa na mawazo yako mwenyewe? Hizi hudumu Nchi nyingine ni pesa, tusipende vya bure sana,

      Huko uliko kuna kampuni za Consultancy wafuate na uwape pesa wakushauri nini cha kufanya, Na by the way hutapata michango yoyote ya maana make watu walisha choka na marudio rudio ya vitu vile vile,
      ngoja nikupotezee kabla hujachafua mada yangu na ***** wako.

    14. #12
      Jestina's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th January 2011
      Posts : 3,620
      Rep Power : 1446
      Likes Received
      842
      Likes Given
      334

      Default Re: mchango wenu wa mawazo jamani....

      Thanks wakuu Telo,Mgombezi and Andybird kwa mawazo yenu mazuri,nitayafanyia kazi....
      TELO likes this.

    15. #13
      OGOPASANA's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 30th April 2009
      Posts : 207
      Rep Power : 553
      Likes Received
      65
      Likes Given
      121

      Default Re: mchango wenu wa mawazo jamani....

      Quote By Tarlisha
      wakuu nina milioni kumi,najiuliza nifungue biashara sijui biashara gani hapa mtaniadvise au niweke msingi kny kiwanja changu kule kibaha tatizo nikiweka msingi sijui nitamaliza lini kujenga as sina uhakika/regular income na b, nikianza biashara ni biashara gani itakayonirudishia hela yangu ili niweze kujenga? msaada kny tutazzz.....
      MISSION IMPOSSIBLE IDEA:

      1 - Tafuta frem moja ya biashara kisha lipia na uikarabati katika muonekano wa kiofisi ya kisasa.(weka mlango wa alluminium, air condition, meza, kiti, viti 2 vya wageni, kompyuta, printer, shelf / kabati nk ila usiweke tangazo lolote)
      2 - Watangazie watu waaminifu unaowafahamu (ambao wana uwezo wa kuingiza hela kila siku na walio na shughuli nzuri na kubwa zinazowaingizia kipato, mfano wafanyabiashara na wafanyakazi wenye mishahara mizuri) watangazie kuwa unatoa mikopo ya marejesho ya mwezi mmoja kwa riba ya 30%, kuanzia Tsh 100,000 hadi milioni moja.
      3- Weka lending policy and procedures ambazo zipo secured na sustainable katika utoaji wa huduma hiyo.
      4 -Anza kutoa mikopo kwa mtaji wa kiasi utakachokuwa nacho baada ya process hapo juu. Amini kuwa kama utakuwa serious na kufuatilia ipasavyo, basi baada ya miezi 12 (mwaka 1) tangu ufungue hiyo kijiofisi chako utaweza kupata return nzuri kama ifuatavyo: mfano ukaanza na mtaji wa milioni kumi (working capital)

      MWEZI MTAJI (TSH) RETURN (TSH)
      January 10,000,000 13,000,000
      February 13,000,000 16,900,000
      March 16,900,000 21,970,000
      April 21,970,000 28,561,000
      May 28,561,000 37,129,300
      June 37,129,300 48,268,090
      July 48,268,090 62,748,517
      August 62,748,517 81,573,072
      September 81,573,072 106,044,994
      October 106,044,994 137,858,492
      November 137,858,492 179,216,040
      December 179,216,040 232,980,851

      Hivyo baada ya miezi 12, unaweza kuisajiri biashara yako na kuwa kampuni na kuifanya kuwa ofisi kubwa. Najua kutakuwa na matumizi mfano, kulipa mshahara kama kuna mtu utakuwa umemwajiri, umeme nk. ila gharama zake hazitakuwa kubwa za kuweza kukushinda kulipia kwa kutafuta fedha mbadala kutoka katika vyanzo vingine ili mtaji ubaki vile vile.

      Ni wazo tu.
      Mgombezi, Marketer and Tarlisha like this.
      " Yesu ni Bwana"

    16. #14
      Jestina's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th January 2011
      Posts : 3,620
      Rep Power : 1446
      Likes Received
      842
      Likes Given
      334

      Default Re: mchango wenu wa mawazo jamani....

      Asante kwa hili wazo mkuu,ubarikiwe...nimelipenda.. will definately work on it....
      OGOPASANA likes this.

    17. #15
      Laigwanan76's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st November 2010
      Posts : 503
      Rep Power : 530
      Likes Received
      98
      Likes Given
      61

      Default Re: mchango wenu wa mawazo jamani....

      Quote By Tarlisha
      asante kwa hili wazo mkuu,ubarikiwe...nimelipenda.. will definately work on it....

      Hao ndio wabomgo na utajiri wa harakaharaka........kaazi kwelikweli

    18. #16
      Jestina's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th January 2011
      Posts : 3,620
      Rep Power : 1446
      Likes Received
      842
      Likes Given
      334

      Default Re: mchango wenu wa mawazo jamani....

      Quote By Laigwanan76
      Hao ndio wabomgo na utajiri wa harakaharaka........kaazi kwelikweli
      wacha tujaribu bana....

    19. #17
      Tuliwonda's Avatar
      Member Array
      Join Date : 29th June 2012
      Posts : 98
      Rep Power : 366
      Likes Received
      22
      Likes Given
      24

      Default Re: mchango wenu wa mawazo jamani....

      Ukishapata biashara ya kufanya, nakushauri usitumbukize hela yote huko. Weka pembeni angalau mil 3 itakusaidia kwenye + or -.

    20. #18
      exzavery's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 4th July 2012
      Posts : 1
      Rep Power : 0
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default

      Hello Tanzania!

    21. #19
      neggirl's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th July 2009
      Posts : 2,109
      Rep Power : 920
      Likes Received
      833
      Likes Given
      1204

      Default Re: mchango wenu wa mawazo jamani....

      Quote By OGOPASANA
      MISSION IMPOSSIBLE IDEA:

      1 - Tafuta frem moja ya biashara kisha lipia na uikarabati katika muonekano wa kiofisi ya kisasa.(weka mlango wa alluminium, air condition, meza, kiti, viti 2 vya wageni, kompyuta, printer, shelf / kabati nk ila usiweke tangazo lolote)
      2 - Watangazie watu waaminifu unaowafahamu (ambao wana uwezo wa kuingiza hela kila siku na walio na shughuli nzuri na kubwa zinazowaingizia kipato, mfano wafanyabiashara na wafanyakazi wenye mishahara mizuri) watangazie kuwa unatoa mikopo ya marejesho ya mwezi mmoja kwa riba ya 30%, kuanzia Tsh 100,000 hadi milioni moja.
      3- Weka lending policy and procedures ambazo zipo secured na sustainable katika utoaji wa huduma hiyo.
      4 -Anza kutoa mikopo kwa mtaji wa kiasi utakachokuwa nacho baada ya process hapo juu. Amini kuwa kama utakuwa serious na kufuatilia ipasavyo, basi baada ya miezi 12 (mwaka 1) tangu ufungue hiyo kijiofisi chako utaweza kupata return nzuri kama ifuatavyo: mfano ukaanza na mtaji wa milioni kumi (working capital)

      MWEZI MTAJI (TSH) RETURN (TSH)
      January 10,000,000 13,000,000
      February 13,000,000 16,900,000
      March 16,900,000 21,970,000
      April 21,970,000 28,561,000
      May 28,561,000 37,129,300
      June 37,129,300 48,268,090
      July 48,268,090 62,748,517
      August 62,748,517 81,573,072
      September 81,573,072 106,044,994
      October 106,044,994 137,858,492
      November 137,858,492 179,216,040
      December 179,216,040 232,980,851

      Hivyo baada ya miezi 12, unaweza kuisajiri biashara yako na kuwa kampuni na kuifanya kuwa ofisi kubwa. Najua kutakuwa na matumizi mfano, kulipa mshahara kama kuna mtu utakuwa umemwajiri, umeme nk. ila gharama zake hazitakuwa kubwa za kuweza kukushinda kulipia kwa kutafuta fedha mbadala kutoka katika vyanzo vingine ili mtaji ubaki vile vile.

      Ni wazo tu.
      wazo zuri.. but changamoto kubwa iko ktk kufuatilia waliokopa walipe.. na wakati mwingine wengine hushindwa kulipa

    22. #20
      mwajiri's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 17th February 2012
      Posts : 7
      Rep Power : 367
      Likes Received
      1
      Likes Given
      0

      Default Re: mchango wenu wa mawazo jamani....

      Quote By neggirl
      wazo zuri.. but changamoto kubwa iko ktk kufuatilia waliokopa walipe.. na wakati mwingine wengine hushindwa kulipa
      1. Kila jambo lenye mafanikio lina changamoto, hivyo ni muhimu kufahamu kwa mapana kitu unachokifanya, ukipende, utafute ujuzi, upate uzoefu kwa wengine wanaofanya au waliofanya. Nothing comes easy.
      2. Kila mkopo unapaswa kurejeshwa ama kulipwa kwa wakati na kama ilivyokubaliwa. Mkopeshaji na mkopaji wanapaswa wafahamu dhumuni la mkopo, umuhimu wa mkopo, athari zinazoweza kupatikana mkopo usiporejeshwa kwa wakati, usalama wa mkopo uliotolewa na yote muhimu yanayohusu mkopo ikiwemo kupanga namna za kuweza kufanya mikopo iliyotolewa kurejeshwa. Unaweza kupata msaada kwa hili kwa wanasheria, maafisa wa serikali za mitaa, maafisa watendaji wa kata, wajumbe wa nyumba kumikumi, wamiliki wa taasisi na asasi za kifedha na wafanyakazi wa mabenki ambao wanaweza kukusaidia kwa ushauri juu ya taratibu nzuri za kutumia katika biashara hii.
      3. Kabla ya kuanza biashara hii, mkopeshaji anapaswa kujua sababu zote zinazopelekea wateja kushindwa kulipa mikopo, kisha afanyie uchunguzi na kuweka mipango ya kuweza kukabiliana na changamoto hizo.
      4. Nimelipenda wazo hili, kama mtu akiwa serious anaweza kufanikiwa. Hasara na Faida ni sehemu ya biashara na hakuna biashara isyo na hasara ila kinachotakiwa ni hasara isiwe kubwa.
      neggirl likes this.

    23. Miaka 50
    Page 1 of 2 12 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...