Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Hivi kweli TRA wana nia njema na nchi yetu?

    Report Post
    Results 1 to 7 of 7
    1. #1
      Kaduguda's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st August 2008
      Posts : 261
      Rep Power : 604
      Likes Received
      33
      Likes Given
      5

      Default Hivi kweli TRA wana nia njema na nchi yetu?

      Kampuni za mizigo bandarini Dar zalalamikia ushuru mpya

      Na Leon Bahati

      KAMPUNI zinazotoa huduma ya kupakua na kupakia mizigo (forwarding and Clearing) Bandari ya Dar es Salaam zimegoma na kusababisha hofu ya kuzuka kwa mkanganyiko wa uchumi nchini

      Pamoja na kugoma, kampuni hizo zimedai zinafikiria kuitumia Bandari ya Mombasa nchini Kenya katika kupakua na kupakia mizigo ya kibiashara.

      Habari zilizolifikia gazeti hili zilisema baadhi ya kampuni hizo zinatishia kuondoka Dar es Salaam baada ya Serikali kupandisha ushuru kwa karibu asilimia 50 tangu Jumatano iliyopita.

      Baadhi ya wamiliki wa kampuni hizo , waliliambia Mwananchi Jumapili kuwa serikali imebadili mfumo wake wa kutoza ushuru wa forodha ambapo kila kontena linatozwa kati ya Sh20 milioni na 40 milioni, bila kujali aina ya mzigo uliopo ndani.

      Lakini mchumi mmoja , alisema jana kwamba wakati wote mfanyabiashara akiongezewa gharama, basi atakayeumia ni mlaji (wananchi).

      Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Hamfrey Mushi alisema katika mazingira hayo, ni vigumu kupambana na mfumuko wa bei.

      Wakizungumza kwa masharti ya kutotajwa jina gazetini, baadhi ya wenye kampuni walidai, awali walikuwa wanalipa ushuru kulingana na thamani ya bidhaa zilizopo ndani ya kontena.

      Lakini mfumo mpya, uliobuniwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) unatoza Sh 20 milioni kwa kila kontena lenye urefu wa futi 20 na Sh.40 milioni kwa kila kontena lenye futi 40.

      Bila kuangalia thamani.

      Mwananchi Jumapili lilipowasiliana na Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo alisema kuwa yupo safari ya kikazi, Kilosa Morogoro, na kushauri kuwasiliana na Katibu Mkuu wa Wizara, Ramadhan Kijja.

      Hata hivyo, Kijja hakupatikana kupitia simu yake ya mkononi na hata ile ya ofisini kwake iliita kwa muda mrefu bila kupokelewa.

      Mkurugenzi wa Elimu kwa walipa Kodi na Uhusiano wa TRA, Protas Mmanda naye hakupatikana ili kufafanua juu ya jambo hilo baada ya simu yake nayo kutopokelewa.

      Pamoja na hali hiyo, habari zilizolifikia gazeti hili zilieleza kuwa baadhi ya watendaji wakuu wa TRA walikuwa kwenye vikao mwishoni mwa wiki ili kujadili hatma ya mgogoro huo.

      Bandari ya Dar es Salaam imekuwa ikishutumiwa kutokana na utendaji usioridhisha wa Ticts, ambao unasababisha foleni kubwa ya meli zinazosubiri kupakuliwa.

      Waziri wa Miundombinu, Dk. Shukuru Kawamba alisema kuwa hali hiyo imekuwa ikisababishia serikali hasara ya Sh20, milioni kila siku kwa kila meli.

      Wakizungumzia juu ya utendaji mbovu wa bandari hiyo pamoja na kuongezeka kwa gharama pamoja na ushuru wa forodha, wataalam kadhaa wa uchumi walisema athari zake ni kubwa kwa uchumi na kwamba zitaongeza ugumu wa maisha hasa kwa wananchi wa kipato cha chini.

      Aliitaka serikali kuchukua hatua za haraka za kupambana na hali hiyo vingionevyo, hali ya uchumi wa nchi itaendele kudorora na hali ya maisha itazidi kuwaendea vibaya watu wa kipato cha chini.


      SOURCE: MWANANCHI - 2/21/2009

      My take: Naomba wadau mnieleweshe hivi inakuwaje container lilipiwe ushuru flat rate, maana hata maji ya DAWASCO siku hizi kuna meter unalipa kwa kadri unavyotumia. Sasa mtu kaleta container kisha unasema ni flat rate hii wadau imekaaje? JF kuna wadau wa aina zote hebu ,lio TRA mtuambie kulikoni hata mkafikia maamuzi hayo?
      He walked on water; he turned water to wine; Healed the sick, Raised the dead and now he wants to be your candidate for president.

    2. Miaka 50

    3. #2
      bm21's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th May 2008
      Location : Britain
      Posts : 777
      Rep Power : 718
      Likes Received
      2
      Likes Given
      15

      Default Re: Hivi kweli TRA wana nia njema na nchi yetu?

      Kaduguda, ukisikia hii ni serikali ya vihio ndio hiyo. Mi nadhani wakapimwe akili tunaweza walaumu kumbe baadha ya fyuzi vichwani mwao zilishakatika. Nimeshawahi changia sana juu ya mfumuko wa bei Tanzania, malengo na mikakati ya kufanikisha malengo hayo. Serikali hii inalengo la kushusha mfumko wa bei kuwa 7.5% by jun 2009 pia malengo yaliyopo ni kwamba uchumi utakuwa (of course najua wanafanya finacial engineering hatakama mambo hayapo hivyo basi dada tutakazo pewa ni kwamba uchumi umekua hata kama kuna recession).

      Kwakifupi hii inaitwa 'import tariff restriction', hata hivyo haina basis (crazily done). Kama tunataka kuzuia uagizaji bidhaa nje ya nchi tunatakiwa kuwa na alternative domestic supply ya bidhaa hizo. Hata hivyo huwezi kuwa na flat rate bali kupandisha rate kwa kiasi fulani kwa aina fulani ya bidhaa unazotaka kuzuia uagizaji wake toka nji ili kulinda soko la ndani. Sasa sisi tunabidhaa gani hapo kama mbadala?. Au ndio wanatekeleza agizo la mwanye nyumba sikasha watembelea hao au bado?.

    4. #3
      Boney E.M.'s Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd January 2007
      Posts : 392
      Rep Power : 709
      Likes Received
      7
      Likes Given
      3

      Default Re: Hivi kweli TRA wana nia njema na nchi yetu?

      Mara nyingi tasisi zetu huususan TRA huwa wanatangaza viwango vipya kupitia kwenye bajeti sasa hii mbona haiko sawa? Kuweka tarifss haphazard namna hii ni uvurugaji wa uchumi. Hakika lazima TRA na Wizara ya Fedha iwaeleze wananchi kuhusu hali hii. Mimi inanipa wasiwasi kuwa uchaguzi unakuja mambo kama haya utayasikia sana. Ingawa kweli ataumia mlaji wa mwisho lakini "wao" watakuwa wamepata wanachokitaka irrespective of the fact anaeumia ni mwananchi wa hali ya chini. Hakuna mantiki ni WIZI MTUPU!!!!!

    5. #4
      Mfamaji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th November 2007
      Posts : 2,884
      Rep Power : 1161
      Likes Received
      286
      Likes Given
      158

      Default Re: Hivi kweli TRA wana nia njema na nchi yetu?

      Walipa kodi wakubwa Tz ni walewale wakianzia wafanyakazi ambao hutozwa kodi kubwa kuliko. TRA wanajidai eti wanajiwekea malengo ya ukusanyaji wa kodi kumbe wanachokifanya ni kuwabambikia watu kodi . Hawana tofauti sana na baadhi ya Polisi . Wakesha kubambikia wanakuamuru ulipe 1/3 ya hiyo amount kwanza ndio maelezo au makubaliano yafuate. Wanaangalia upande mmoja tu kama nyati wakasahau efeect yake kwa uchumi in general.

      Halafu nijuavyo mimi kodi nyingi huongezwa wakati wa bajeti. Je kuweka viwango vipya bandarini imezingatia hilo? Nani ana aprove mambo hayo. Kama ni bunge basi linapaswa kuact.

    6. #5
      TIMING's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th April 2008
      Location : Roaming...
      Posts : 20,091
      Rep Power : 12253
      Likes Received
      6015
      Likes Given
      6854

      Default Re: Hivi kweli TRA wana nia njema na nchi yetu?

      Jamani;

      Kabla ya kulaumu tuangalie sana... Yawezekana haya ni maagizo ya wakubwa kutokana na hali ya uchumi au maandalizi ya uchaguzi

      The bottom line ni kwamba - kuna viazi katika level zote hapa nchini ambao wanaweza kuamua chochote popote bila kujali yeyote... hadi yaharibike ndio watengue maamuzi

      Watch this one
      .....Ana sifa zote, nzuri na mbaya!!!

    7. RukaaJuu Final

    8. #6
      TIMING's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th April 2008
      Location : Roaming...
      Posts : 20,091
      Rep Power : 12253
      Likes Received
      6015
      Likes Given
      6854

      Default Re: Hivi kweli TRA wana nia njema na nchi yetu?

      Jamani;

      Kabla ya kulaumu tuangalie sana... Yawezekana haya ni maagizo ya wakubwa kutokana na hali ya uchumi au maandalizi ya uchaguzi

      The bottom line ni kwamba - kuna viazi katika level zote hapa nchini ambao wanaweza kuamua chochote popote bila kujali yeyote... hadi yaharibike ndio watengue maamuzi

      Watch this one
      .....Ana sifa zote, nzuri na mbaya!!!

    9. #7
      Hofstede's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th July 2007
      Posts : 3,604
      Rep Power : 21341
      Likes Received
      981
      Likes Given
      988

      Default Re: Hivi kweli TRA wana nia njema na nchi yetu?

      Kama ni kweli basi Tanzania sasa inaendeshwa kama Somalia(kwa style ya ransom), hawa watu wanaojiita wachumi na wamebobea katika masula haya inakuwaje leo hawazingatii kanuni walizojifunza darasani?.

      Unapofanya flat rate katika kulipia container kwanza ni kinyume cha sheria za kodi zilizopo kwa sasa, labda watuambie kuna sheria mpya imepitishwa na bunge. Japo sheria zinampa uwezo Commissioner of Domestic revenue kutumia uwezo wake katika kufikia kadirio analodhani yeye kuwa ni thamani ya mzigo, bado flat rate ni misuse of that clause na anatakiwa kupimwa akili kama kweli ana sound mind katika kufikia maamuzi.

      Mtu amekaa marekani miaka 20 anaamua kurudi nyumbani na kuchukua container anaweka makochi yake, jiko na gari alilotumia miaka kumi vyote havizidi $10,000 unamwambia alipe million 40? kweli wewe unaakili kweli?. Ok utasema ni returning resident atakuwa na exemption ila kama anataka kuja na mitambo yake ya kuanzisha biashara atafikiria hilo?. Huku ni kudidimiza uchumi mchana kweupe.

      Nafikiri kuweka malengo isiwe ni kwa cost ya wananchi, waweke mazingira mazuri ya kukuza biashara na uchumi kwani ng'ombe usipomlisha hatatoa maziwa, sasa hawa jamaa wao wanataka kukamua tu kulisha hawataki sasa si wataua?. Hii ndiyo Bongo "on your own"

    Similar Topics

    1. Hivi rage anaweza kumwona obama kirahisi hivi??hii nchi kweli imeuzwa
      By Pdidy in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 14
      Last Post: 22nd June 2011, 12:53
    2. weekend ilikuwa hivi j3 njema wana jf
      By Viper in forum Jamii Photos
      Replies: 19
      Last Post: 18th April 2011, 13:03
    3. Hivi ni kweli kazi yetu ni kunung'unika tu?
      By mapambano in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 1
      Last Post: 20th April 2008, 19:34
    4. Hivi ni kweli serikali yetu haipo makini hivi ??
      By KadaMpinzani in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 1
      Last Post: 13th August 2007, 21:08

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...