CRDB Visa Card: Utata wa matumizi yake mtandaoni - JamiiForums |The Home of Great Thinkers

Go Back   JamiiForums |The Home of Great Thinkers > Public Forums > Business & Economic Forum


Business & Economic Forum This' a place where contributors with an interest in business or economics can "meet" and discuss issues of importance to the business and economics matters. Register to comment here!


Reply
 
LinkBack Thread Tools Rate Thread Display Modes
Old 19th January 2009, 11:05 AM   #1
CRDB Visa Card: Utata wa matumizi yake mtandaoni
Manitoba Manitoba is offline 19th January 2009, 11:05 AM

Kama una CRDB Visa Card, na ulikuwa unafikiria kuitumia kwenye internet, basi usithubutu kutia sahihi kuiwezesha kutumika mtandaoni (ila kama tu unajua unachokifanya).

CRDB wametoa card mpya zenye nembo ya visa, ambayo wanatangaza kwamba unaweza kununulia vitu mtandaoni. Inaonekana kama ni bonge la wazo mpaka pale utakapogundua jinsi gani zisivyo salama hata kiduchu.

Mtu yeyote mwenye namba ya kadi yako, pamoja na vile vinamba vitatu vya "usalama" vilivyo nyuma, anaweza kuitumia hiyo kadi yako kwenye mtandao bila tatizo lolote. Kwa hiyo ukiitumia kwenye tovuti ambayo si salama, basi ni kama umegawa namba yako kwa watu wengine kujihudumia.

Pia ukiisahau kadi yako mezani, na mtu/rafiki yako/mtoto wako mtukutu/mpenzi wako/secretary wako akapata mda wa kunakili pembeni hizo namba zako, basi pia inakuwa imekula kwako.

Kama ulikuwa unafikiria ile pin yako, basi sahau maana haina kazi kwenye mtandao.

Address Verification
Unaweza ukawa unajiuliza mbona kuna watumiaji wengi tu wa credit cards duniani na wasiwe na wasiwasi hivyo?

Moja ya njia ambayo huwa inatumika kupunguza wizi wa kutumia kadi za wengine ni kufanya uhakiki wa anuani. Kiasi kwamba mtu akiweka oda ya kitu basi oda yake itakubaliwa na kadi kutumika ikiwa tu anuani ya ambapo vitu vya kwenye oda hiyo vitatumwa ni sawa na anuani ya mwenye kadi.

Kwa CRDB hii feature wameifinya, kiasi kwamba mtu yeyote duniani anaweza kutumia kadi yako na kununua na kutuma vitu vyake sehemu yoyote duniani anavyotaka.

Paypal
Kutumia site kama www.paypal.com inaweza kusaidia kuondoa uwezekano wa mtu kukuibia namba za kadi yako online.

Kujiunga kadi yako na paypal sio tatizo, tatizo ni jinsi ya paypal kuihakiki kwamba kweli ni ya kwako.

Paypal wanachofanya ni kukuchaji fedha kidogo (wastani wa 2,000TZS), halafa katika muamala huo wanaweka namba ya siri fulani. Sasa wewe inabidi uangalie statement yako kutoka benki, uione hiyo namba, halafu uwape paypal. Assumption hapo ni kwamba hakuna mtu mwingine anaweza kuona statement yako zaidi ya wewe.

Sasa ndani ya paypal unaweza ukakamilisha taratibu. Ukija CRDB ili kupata tu details za hiyo transaction, jasho litakutoka. Inaweza ukadhani ni kitu simple tu kupata details za transaction (hata mimi nilifikiria hivyo), lakini amini usiamini utashangazwa ... Nimefanya si chini ya trip 10 kwenda CRDB kwa ishu hiii, usihesabu simu, na nimetoka kupiga nyingine sasa hivi ... lol ...

Ningetakiwa niwe nimeshakata tamaa ila tu nataka tu nifuatilie mpaka mwisho waniambie inawezekana au haiwezekani.

Ila kama huu ndio utaratibu, sioni ni jinsi gani wataweza kuwahudumia wateja hata 100 tu wanaotaka kujiunga na paypal. Achilia mbali kwamba hawa watu 100 inabidi wapige kwata CRDB more that 10 times, halafu wawe wanapiga simu mara kwa mara kuwakumbushia CRDB case zao. Na mara nyingi watu unaoongea nao CRDB hata hawaelewi unazungumzia nini.

Makubaliano yako na CRDB ni soo
Ili kuiruhusu kadi yako kutumika online, itabidi utie saini makubaliano yako na CRDB, ambayo yanavipengele ambavyo vinaiondolea CRDB jukumu lolote la kukuhakikishia usalama wako unpotumia kadi yako kwenye mtandao. Kwa hiyo ukiwa online na kadi yako, jua you are on your own.

Kwa watumiaji wengine duniani kuna taratibu za jinsi ya mtu kupinga kuchajiwa transaction ambazo hujazifanya wewe. Na kuna taratibu za jinsi gani utarudishiwa pesa zako.

Mpkataba wa CRDB hauoneshi kama kuna kitu kama hicho. Kwa hiyo mtu akipata details za kadi yako, siku zote itakuwa inakula upande wako.

Kwa hiyo baada ya kuutia saini tu nimehakikisha kadi yangu haiondoki machoni pangu, na pia nahakikisha akaunti hiyo ya CRDB haina vijisenti vingi ... mpaka ntakapomaliza hii exercise.

Hitimisho
Sasa hivi unaweza kutumia kadi yako ya CRDB kwenye mtandao, lakini you do it at your own risk, tena risk kubwa tu.

Kinachonitisha ni kwamba kama kadi yako imewezeshwa kutumika kwenye internet, mtu hana haja ya kukuibia kadi nzima kwa sababu utashtuka, utaripoti, na kadi itafungwa. Anachotakiwa kufanya ni kupata namba za kadi zilizopo mbele, na vile vijinamba vitatu vilivyopo nyuma ya kadi, na inakula upande wako kimya kimya.

Kama umeiwezesha kadi yako kutumika kwenye mtandao, na kama vijinsenti vyako kwenye akaunti yako sio vidogo, na kama huwezi kuitunza details za kadi kiasi hicho, ni vyema ungewaambia waizibe isitumike kwenye mtandao ... or u may have to learn the hard way.
__________________
There are only 10 types of people in the world. Those that understand binary, and those that don't.

Manitoba
Senior Member
Points: 108,272, Level: 100 Points: 108,272, Level: 100 Points: 108,272, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
Join Date: Tue Jul 2008
Posts: 244
Thanks: 17
Thanked 10 Times in 7 Posts
Views: 4892
Reply With Quote
  #2  
Old 19th January 2009, 11:22 AM
Boney E.M. Boney E.M. is offline
Boney E.M. has no status.
Senior Member
Points: 98,992, Level: 100 Points: 98,992, Level: 100 Points: 98,992, Level: 100
Activity: 3% Activity: 3% Activity: 3%
 
Join Date: Mon Jan 2007
Posts: 233
Thanks: 0
Thanked 11 Times in 9 Posts
Rep Power: 24
Boney E.M. will become famous soon enoughBoney E.M. will become famous soon enoughBoney E.M. will become famous soon enoughBoney E.M. will become famous soon enoughBoney E.M. will become famous soon enoughBoney E.M. will become famous soon enoughBoney E.M. will become famous soon enoughBoney E.M. will become famous soon enough
Default Re: CRDB Visa Card: Usithubutu kuitumia kwenye Mtandao

Katika hali kama hii ni vipi wadau watahamasika kununua hisa za CRDB wakati ikiingizwa katika soko la hisa? Hizi ni weaknesses ambazo bila ya kutafutiwa ufumbuzi zita-cast a shadow of doubt kwa customers kama pesa yao iko safe. Can U please educate me on this?
Reply With Quote
  #3  
Old 19th January 2009, 11:31 AM
Shy Shy is offline
Shy is yours
Banned
Points: 2,380,404, Level: 100 Points: 2,380,404, Level: 100 Points: 2,380,404, Level: 100
Activity: 9% Activity: 9% Activity: 9%
 
Join Date: Thu Nov 2006
Posts: 4,258
Thanks: 0
Thanked 170 Times in 112 Posts
Rep Power: 0
Shy will become famous soon enoughShy will become famous soon enoughShy will become famous soon enoughShy will become famous soon enoughShy will become famous soon enoughShy will become famous soon enoughShy will become famous soon enoughShy will become famous soon enough
Send a message via Yahoo to Shy
Default Re: CRDB Visa Card: Usithubutu kuitumia kwenye Mtandao

Kuna wakati server ya crdb inayohusiana na hiyo ili crash watu wa nchi nyingi za asia walikuwa wanatoa pesa tu kwa wale waliokuwa wanajua jamaa walikaa kama siku 4 hivi mpaka mtaalamu wao walipokuja toka majuu

walahi kazi ipo nakwambia
Reply With Quote
  #4  
Old 19th January 2009, 11:35 AM
tonge nyama tonge nyama is offline
tonge nyama has no status.
Member
Points: 69,724, Level: 100 Points: 69,724, Level: 100 Points: 69,724, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Mon Jul 2008
Posts: 29
Thanks: 0
Thanked 0 Times in 0 Posts
Rep Power: 0
tonge nyama will become famous soon enoughtonge nyama will become famous soon enoughtonge nyama will become famous soon enoughtonge nyama will become famous soon enoughtonge nyama will become famous soon enoughtonge nyama will become famous soon enoughtonge nyama will become famous soon enoughtonge nyama will become famous soon enough
Default Re: CRDB Visa Card: Usithubutu kuitumia kwenye Mtandao

Wadau naomba mtufahamishe vizuri, je ni wakati gani unapoweza ama kuruhusu au kuzuia kadi yako kuweza kutumika mtandaoni je nipale unapo apply for the new card au wakati wa kuichukua? nimeomba kadi crdb baada ya niliyokuwa nayo ku-expire.
Reply With Quote
  #5  
Old 19th January 2009, 11:35 AM
Manitoba Manitoba is offline
Manitoba has no status.
Senior Member
Points: 108,272, Level: 100 Points: 108,272, Level: 100 Points: 108,272, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Tue Jul 2008
Posts: 244
Thanks: 17
Thanked 10 Times in 7 Posts
Rep Power: 22
Manitoba will become famous soon enoughManitoba will become famous soon enoughManitoba will become famous soon enoughManitoba will become famous soon enoughManitoba will become famous soon enoughManitoba will become famous soon enoughManitoba will become famous soon enoughManitoba will become famous soon enough
Default Re: CRDB Visa Card: Usithubutu kuitumia kwenye Mtandao

Quote:
View Post
Katika hali kama hii ni vipi wadau watahamasika kununua hisa za CRDB wakati ikiingizwa katika soko la hisa? Hizi ni weaknesses ambazo bila ya kutafutiwa ufumbuzi zita-cast a shadow of doubt kwa customers kama pesa yao iko safe. Can U please educate me on this?
Wanaangalia kama benki inapata faida mwanawane. Na inapata faida. Kumbuka pesa zikiibwa hapo, ni zako ndio zimeubwa, wewe ndio umepata hasara sio wao ... tena wao watakuwa wametengeneza mapata kidogo kwa transaction hiyo ya wizi ... sasa sioni kwa nini hata wewe usiende wekeza huko :-)
__________________
There are only 10 types of people in the world. Those that understand binary, and those that don't.
Reply With Quote
  #6  
Old 19th January 2009, 11:42 AM
Manitoba Manitoba is offline
Manitoba has no status.
Senior Member
Points: 108,272, Level: 100 Points: 108,272, Level: 100 Points: 108,272, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Tue Jul 2008
Posts: 244
Thanks: 17
Thanked 10 Times in 7 Posts
Rep Power: 22
Manitoba will become famous soon enoughManitoba will become famous soon enoughManitoba will become famous soon enoughManitoba will become famous soon enoughManitoba will become famous soon enoughManitoba will become famous soon enoughManitoba will become famous soon enoughManitoba will become famous soon enough
Default Re: CRDB Visa Card: Usithubutu kuitumia kwenye Mtandao

Quote:
View Post
Wadau naomba mtufahamishe vizuri, je ni wakati gani unapoweza ama kuruhusu au kuzuia kadi yako kuweza kutumika mtandaoni je nipale unapo apply for the new card au wakati wa kuichukua? nimeomba kadi crdb baada ya niliyokuwa nayo ku-expire.
Walipoanza haya mambo ya kadi kutumika mtandaoni, ilikuwa kwamba unapewa kadi ikiwa tayari kutumika mtandaoni.

Nadhani baada ya kugundua hizo loopholes ndio wakaweka utaratibu wa kukusainishe wewe makubaliano ambayo yanaiondolea CRDB wajibu wowote wa kukuhakikishia usalama wako, na hivyo hata ukiibiwa ni juu yako.

Kwa hiyo ukipata kadi yako mpya hutaweza kuitumia mtandaoni mpaka usaini kale kamkataba kao. Kwa hiyo uko salama mpaka pale utakapotia saini kale kamkataba kalikokaa upande.
__________________
There are only 10 types of people in the world. Those that understand binary, and those that don't.
Reply With Quote
  #7  
Old 19th January 2009, 12:43 PM
Mwanjelwa Mwanjelwa is offline
Mwanjelwa Msema kweli kulingana na muda uliopo.
JF Senior Expert Member
Points: 136,339, Level: 100 Points: 136,339, Level: 100 Points: 136,339, Level: 100
Activity: 1% Activity: 1% Activity: 1%
 
Join Date: Sun Jul 2007
Location: Chenorbly
Posts: 520
Thanks: 17
Thanked 25 Times in 17 Posts
Rep Power: 24
Mwanjelwa will become famous soon enoughMwanjelwa will become famous soon enoughMwanjelwa will become famous soon enoughMwanjelwa will become famous soon enoughMwanjelwa will become famous soon enoughMwanjelwa will become famous soon enoughMwanjelwa will become famous soon enoughMwanjelwa will become famous soon enough
Default Re: CRDB Visa Card: Usithubutu kuitumia kwenye Mtandao

Quote:
View Post
Kama una CRDB Visa Card, na ulikuwa unafikiria kuitumia kwenye internet, basi usithubutu kutia sahihi kuiwezesha kutumika mtandaoni (ila kama tu unajua unachokifanya).

CRDB wametoa card mpya zenye nembo ya visa, ambayo wanatangaza kwamba unaweza kununulia vitu mtandaoni. Inaonekana kama ni bonge la wazo mpaka pale utakapogundua jinsi gani zisivyo salama hata kiduchu.

Mtu yeyote mwenye namba ya kadi yako, pamoja na vile vinamba vitatu vya "usalama" vilivyo nyuma, anaweza kuitumia hiyo kadi yako kwenye mtandao bila tatizo lolote. Kwa hiyo ukiitumia kwenye tovuti ambayo si salama, basi ni kama umegawa namba yako kwa watu wengine kujihudumia.

Pia ukiisahau kadi yako mezani, na mtu/rafiki yako/mtoto wako mtukutu/mpenzi wako/secretary wako akapata mda wa kunakili pembeni hizo namba zako, basi pia inakuwa imekula kwako.

Kama ulikuwa unafikiria ile pin yako, basi sahau maana haina kazi kwenye mtandao.

Address Verification
Unaweza ukawa unajiuliza mbona kuna watumiaji wengi tu wa credit cards duniani na wasiwe na wasiwasi hivyo?

Moja ya njia ambayo huwa inatumika kupunguza wizi wa kutumia kadi za wengine ni kufanya uhakiki wa anuani. Kiasi kwamba mtu akiweka oda ya kitu basi oda yake itakubaliwa na kadi kutumika ikiwa tu anuani ya ambapo vitu vya kwenye oda hiyo vitatumwa ni sawa na anuani ya mwenye kadi.

Kwa CRDB hii feature wameifinya, kiasi kwamba mtu yeyote duniani anaweza kutumia kadi yako na kununua na kutuma vitu vyake sehemu yoyote duniani anavyotaka.

Paypal
Kutumia site kama www.paypal.com inaweza kusaidia kuondoa uwezekano wa mtu kukuibia namba za kadi yako online.

Kujiunga kadi yako na paypal sio tatizo, tatizo ni jinsi ya paypal kuihakiki kwamba kweli ni ya kwako.

Paypal wanachofanya ni kukuchaji fedha kidogo (wastani wa 2,000TZS), halafa katika muamala huo wanaweka namba ya siri fulani. Sasa wewe inabidi uangalie statement yako kutoka benki, uione hiyo namba, halafu uwape paypal. Assumption hapo ni kwamba hakuna mtu mwingine anaweza kuona statement yako zaidi ya wewe.

Sasa ndani ya paypal unaweza ukakamilisha taratibu. Ukija CRDB ili kupata tu details za hiyo transaction, jasho litakutoka. Inaweza ukadhani ni kitu simple tu kupata details za transaction (hata mimi nilifikiria hivyo), lakini amini usiamini utashangazwa ... Nimefanya si chini ya trip 10 kwenda CRDB kwa ishu hiii, usihesabu simu, na nimetoka kupiga nyingine sasa hivi ... lol ...

Ningetakiwa niwe nimeshakata tamaa ila tu nataka tu nifuatilie mpaka mwisho waniambie inawezekana au haiwezekani.

Ila kama huu ndio utaratibu, sioni ni jinsi gani wataweza kuwahudumia wateja hata 100 tu wanaotaka kujiunga na paypal. Achilia mbali kwamba hawa watu 100 inabidi wapige kwata CRDB more that 10 times, halafu wawe wanapiga simu mara kwa mara kuwakumbushia CRDB case zao. Na mara nyingi watu unaoongea nao CRDB hata hawaelewi unazungumzia nini.

Makubaliano yako na CRDB ni soo
Ili kuiruhusu kadi yako kutumika online, itabidi utie saini makubaliano yako na CRDB, ambayo yanavipengele ambavyo vinaiondolea CRDB jukumu lolote la kukuhakikishia usalama wako unpotumia kadi yako kwenye mtandao. Kwa hiyo ukiwa online na kadi yako, jua you are on your own.

Kwa watumiaji wengine duniani kuna taratibu za jinsi ya mtu kupinga kuchajiwa transaction ambazo hujazifanya wewe. Na kuna taratibu za jinsi gani utarudishiwa pesa zako.

Mpkataba wa CRDB hauoneshi kama kuna kitu kama hicho. Kwa hiyo mtu akipata details za kadi yako, siku zote itakuwa inakula upande wako.

Kwa hiyo baada ya kuutia saini tu nimehakikisha kadi yangu haiondoki machoni pangu, na pia nahakikisha akaunti hiyo ya CRDB haina vijisenti vingi ... mpaka ntakapomaliza hii exercise.

Hitimisho
Sasa hivi unaweza kutumia kadi yako ya CRDB kwenye mtandao, lakini you do it at your own risk, tena risk kubwa tu.

Kinachonitisha ni kwamba kama kadi yako imewezeshwa kutumika kwenye internet, mtu hana haja ya kukuibia kadi nzima kwa sababu utashtuka, utaripoti, na kadi itafungwa. Anachotakiwa kufanya ni kupata namba za kadi zilizopo mbele, na vile vijinamba vitatu vilivyopo nyuma ya kadi, na inakula upande wako kimya kimya.

Kama umeiwezesha kadi yako kutumika kwenye mtandao, na kama vijinsenti vyako kwenye akaunti yako sio vidogo, na kama huwezi kuitunza details za kadi kiasi hicho, ni vyema ungewaambia waizibe isitumike kwenye mtandao ... or u may have to learn the hard way.
Nafikiri inategemea. Nimetumia mara kadhaa na hakuna shaka, na jamaa wengi nawajua wanatumia bila shaka. Kwa kufananisha, nimewahi ona mtu hapo Norway kapata kwenye account yake 6 billions NKR ikiwa inatoka na makosa ya Kibenki na vivyo hivyo kule Sweden kuna jamaa wa Moscow (Mrusi) alilamba zaidi ya SKR equivalent to USD 2 ml bila wenyewe kushtuka kwa mwaka mzima kwa kucheza na Credit Cards. Huyu Mrusi mpaka leo anatafutwa huku akiendeleza huo uzandiki. Zingine nyingi zinafahamika.

CRDB VISA CARD haiwezi kuwa tofauti na hizi incidences. Ni pro and cons za technology. technology Inaweza kukubamiza au kukunyanyua.
Reply With Quote
  #8  
Old 19th January 2009, 12:45 PM
Lole Gwakisa's Avatar
Lole Gwakisa Lole Gwakisa is offline
Lole Gwakisa has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 225,228, Level: 100 Points: 225,228, Level: 100 Points: 225,228, Level: 100
Activity: 3% Activity: 3% Activity: 3%
 
Join Date: Wed Nov 2008
Posts: 1,180
Thanks: 289
Thanked 282 Times in 139 Posts
Rep Power: 24
Lole Gwakisa will become famous soon enoughLole Gwakisa will become famous soon enoughLole Gwakisa will become famous soon enoughLole Gwakisa will become famous soon enoughLole Gwakisa will become famous soon enoughLole Gwakisa will become famous soon enoughLole Gwakisa will become famous soon enoughLole Gwakisa will become famous soon enough
Default Re: CRDB Visa Card: Usithubutu kuitumia kwenye Mtandao

Thanks Manitoba, itakuwaje kutumia kadi yako kwa single transactions-yaani ukitaka kununua kitu kwenye mtandao unacharge akaunti yako na fedha zile tu zinazohitajika?
Nimeona wengine wanatumia mtindo huu, imekaaje hapo mkuu!
Reply With Quote
  #9  
Old 19th January 2009, 02:42 PM
Manitoba Manitoba is offline
Manitoba has no status.
Senior Member
Points: 108,272, Level: 100 Points: 108,272, Level: 100 Points: 108,272, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Tue Jul 2008
Posts: 244
Thanks: 17
Thanked 10 Times in 7 Posts
Rep Power: 22
Manitoba will become famous soon enoughManitoba will become famous soon enoughManitoba will become famous soon enoughManitoba will become famous soon enoughManitoba will become famous soon enoughManitoba will become famous soon enoughManitoba will become famous soon enoughManitoba will become famous soon enough
Default Re: CRDB Visa Card: Usithubutu kuitumia kwenye Mtandao

Quote:
View Post
Nafikiri inategemea. Nimetumia mara kadhaa na hakuna shaka, na jamaa wengi nawajua wanatumia bila shaka. Kwa kufananisha, nimewahi ona mtu hapo Norway kapata kwenye account yake 6 billions NKR ikiwa inatoka na makosa ya Kibenki na vivyo hivyo kule Sweden kuna jamaa wa Moscow (Mrusi) alilamba zaidi ya SKR equivalent to USD 2 ml bila wenyewe kushtuka kwa mwaka mzima kwa kucheza na Credit Cards. Huyu Mrusi mpaka leo anatafutwa huku akiendeleza huo uzandiki. Zingine nyingi zinafahamika.

CRDB VISA CARD haiwezi kuwa tofauti na hizi incidences. Ni pro and cons za technology. technology Inaweza kukubamiza au kukunyanyua.
Mzee mimi nadhani wanao-design hizi technologies huwa wanashirikisha sana akili. Kama tungekuwa sisi basi ndio tungesema hivyo kirahisi tu kwamba "Inaweza kukubamiza au kukunyanyua". Lakini wenzetu wanashirikisha akili na kujitahidi kuhakikisha kuwa technolojia inasaidia zaidi kuliko inavoumiza.

Sasa naomba nikupe fact mbili tatu ambazo pengine zitakubadili mawazo.

Kwa wenzetu interests za mwenye kadi zinakuwa protected. Kwengine kunakuwa na jinsi ambayo mwenye kadi anaweza kuilalamikia transaction ambayo hakufanya yeye, na issuer wa card yake akaissue kitu chaitwa "charge back" ambapo mwenye kadi anarudishiwa pesa yake, na mtua huduma anakatwa hiyo pesa.

Kwenye sehemu zenye utaratibu huu, anayeumia ni mtoa huduma na si mwenye kadi. Kwa hiyo hayo mabilioni unayoyatolea macho ni hasara zaidi kwa mtoa huduma kuliko kwa mwenye kadi.

Utaratibu huo unahakikisha kwamba mtoa huduma anajiridhisha kwamba hiyo kadi ni halali na mtumiaji wake ni halali. Na njia za kufanya hivyo kwa kutumia technolojia hiyo hiyo zipo, na zinatumika huku duniani: si mapambo.

Tofauti ya CRDB card hapa nikwamba mtu akitumia card yako ya CRDB, na ukaona transaction ambayo hukuifanya wewe, huna pa kulalamika. Maana yake CRDB ni kama wanasema ukiibiwa ni shauri yako. Yaani inawezekana hata kumtafuta mwizi wasikusaidie. Wakati kwa wenzetu ukiibiwa aliyesaidia wizi ndio anabanwa.

Umeona hiyo tofauti?
__________________
There are only 10 types of people in the world. Those that understand binary, and those that don't.
Reply With Quote
  #10  
Old 19th January 2009, 02:51 PM
Manitoba Manitoba is offline
Manitoba has no status.
Senior Member
Points: 108,272, Level: 100 Points: 108,272, Level: 100 Points: 108,272, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Tue Jul 2008
Posts: 244
Thanks: 17
Thanked 10 Times in 7 Posts
Rep Power: 22
Manitoba will become famous soon enoughManitoba will become famous soon enoughManitoba will become famous soon enoughManitoba will become famous soon enoughManitoba will become famous soon enoughManitoba will become famous soon enoughManitoba will become famous soon enoughManitoba will become famous soon enough
Default Re: CRDB Visa Card: Usithubutu kuitumia kwenye Mtandao

Quote:
View Post
Thanks Manitoba, itakuwaje kutumia kadi yako kwa single transactions-yaani ukitaka kununua kitu kwenye mtandao unacharge akaunti yako na fedha zile tu zinazohitajika?
Nimeona wengine wanatumia mtindo huu, imekaaje hapo mkuu!
Kutumia card ya CRDB kwenye mtandao ni wazo zuri. Na CRDB inabidi wapongezwe kwa hatu hiyo.

Ninachosema hapa ni kwamba CRDB wamejitoa kwenye tatizo lolote litakalotokea kwa matumizi ya kadi yako. Kitu ambacho ni tofauti na kwa wenzetu kwa jinsi ninavyofahamu mimi.

Hiyo inafanya matumizi ya hii card yawe na risk zaidi. Yaani hata kama kosa ni lakwao bado hakuna wa kukusaidia.

Kwa mfano ukinunua kitu online halafu kwa bahati mbaya anayekuuzia akatoa fedha zaidi ya zile alizotakiwa kutoa. Halafu kwa bahati mbaya akawa anasuasua kukurudishia fedha zako. Hapo utakuwa huna jinsi ila kukubali umeliwa kimachomacho. Lakini kwa wenzetu kuna taratibu za kupinga transaction ambayo si sawa au si halali, na mwenye kadi waweza kurudishiwa pesa ambazo hukutakiwa kukatwa. Kwa CRDB inaonekana hakuna kitu kama hicho.

Sisemi kwamba CRDB wanatakiwa waweke utaratibu kama huo. Ila nasema wewe mtumiaji ujue hali ilivyo, usije ukang'atwa siku ndio ukaanza kutoa macho na kuwa mkali na CRDB.
__________________
There are only 10 types of people in the world. Those that understand binary, and those that don't.
Reply With Quote
Reply

Bookmarks

Tags
card, crdb, kuitumia, kwenye, matumizi, mtandao, mtandaoni, usithubutu, utata, visa, yake


Currently Active Users Viewing This Thread: 1 (0 members and 1 guests)
 
Thread Tools
Display Modes Rate This Thread
Rate This Thread:

Posting Rules
You may not post new threads
You may not post replies
You may not post attachments
You may not edit your posts

BB code is On
Smilies are On
[IMG] code is On
HTML code is Off
Trackbacks are Off
Pingbacks are Off
Refbacks are On


Similar Threads
Thread Thread Starter Forum Replies Last Post
BoT Scandal: Tulikotoka, Tulipo, Tunakoelekea Maxence Melo Jamii Intelligence 3079 12th November 2009 08:12 AM
Muafaka CCM na CUF, pande mbili za shilingi! MwanaCCM Jukwaa la Siasa 148 13th July 2009 10:13 AM
Hotuba Mbadala TAMISEMI: Slaa ataka Balali ajiuzulu; ambana Lowassa kuhusu Richmond John Mnyika Jukwaa la Siasa 13 16th December 2008 02:21 PM

Tuma Ukurasa huu kwa rafiki yako!


All times are GMT +3. The time now is 08:37 AM.

Powered by JamiiForums.com
Copyrights reserved to JamiiForums.com