CRDB Visa Card: Utata wa matumizi yake mtandaoni - Page 5 - JamiiForums |The Home of Great Thinkers

Go Back   JamiiForums |The Home of Great Thinkers > Public Forums > Business & Economic Forum


Business & Economic Forum This' a place where contributors with an interest in business or economics can "meet" and discuss issues of importance to the business and economics matters. Register to comment here!


Reply
 
LinkBack Thread Tools Rate Thread Display Modes
Old 19th January 2009, 11:05 AM  
CRDB Visa Card: Utata wa matumizi yake mtandaoni
Manitoba Manitoba is offline 19th January 2009, 11:05 AM

Kama una CRDB Visa Card, na ulikuwa unafikiria kuitumia kwenye internet, basi usithubutu kutia sahihi kuiwezesha kutumika mtandaoni (ila kama tu unajua unachokifanya).

CRDB wametoa card mpya zenye nembo ya visa, ambayo wanatangaza kwamba unaweza kununulia vitu mtandaoni. Inaonekana kama ni bonge la wazo mpaka pale utakapogundua jinsi gani zisivyo salama hata kiduchu.

Mtu yeyote mwenye namba ya kadi yako, pamoja na vile vinamba vitatu vya "usalama" vilivyo nyuma, anaweza kuitumia hiyo kadi yako kwenye mtandao bila tatizo lolote. Kwa hiyo ukiitumia kwenye tovuti ambayo si salama, basi ni kama umegawa namba yako kwa watu wengine kujihudumia.

Pia ukiisahau kadi yako mezani, na mtu/rafiki yako/mtoto wako mtukutu/mpenzi wako/secretary wako akapata mda wa kunakili pembeni hizo namba zako, basi pia inakuwa imekula kwako.

Kama ulikuwa unafikiria ile pin yako, basi sahau maana haina kazi kwenye mtandao.

Address Verification
Unaweza ukawa unajiuliza mbona kuna watumiaji wengi tu wa credit cards duniani na wasiwe na wasiwasi hivyo?

Moja ya njia ambayo huwa inatumika kupunguza wizi wa kutumia kadi za wengine ni kufanya uhakiki wa anuani. Kiasi kwamba mtu akiweka oda ya kitu basi oda yake itakubaliwa na kadi kutumika ikiwa tu anuani ya ambapo vitu vya kwenye oda hiyo vitatumwa ni sawa na anuani ya mwenye kadi.

Kwa CRDB hii feature wameifinya, kiasi kwamba mtu yeyote duniani anaweza kutumia kadi yako na kununua na kutuma vitu vyake sehemu yoyote duniani anavyotaka.

Paypal
Kutumia site kama www.paypal.com inaweza kusaidia kuondoa uwezekano wa mtu kukuibia namba za kadi yako online.

Kujiunga kadi yako na paypal sio tatizo, tatizo ni jinsi ya paypal kuihakiki kwamba kweli ni ya kwako.

Paypal wanachofanya ni kukuchaji fedha kidogo (wastani wa 2,000TZS), halafa katika muamala huo wanaweka namba ya siri fulani. Sasa wewe inabidi uangalie statement yako kutoka benki, uione hiyo namba, halafu uwape paypal. Assumption hapo ni kwamba hakuna mtu mwingine anaweza kuona statement yako zaidi ya wewe.

Sasa ndani ya paypal unaweza ukakamilisha taratibu. Ukija CRDB ili kupata tu details za hiyo transaction, jasho litakutoka. Inaweza ukadhani ni kitu simple tu kupata details za transaction (hata mimi nilifikiria hivyo), lakini amini usiamini utashangazwa ... Nimefanya si chini ya trip 10 kwenda CRDB kwa ishu hiii, usihesabu simu, na nimetoka kupiga nyingine sasa hivi ... lol ...

Ningetakiwa niwe nimeshakata tamaa ila tu nataka tu nifuatilie mpaka mwisho waniambie inawezekana au haiwezekani.

Ila kama huu ndio utaratibu, sioni ni jinsi gani wataweza kuwahudumia wateja hata 100 tu wanaotaka kujiunga na paypal. Achilia mbali kwamba hawa watu 100 inabidi wapige kwata CRDB more that 10 times, halafu wawe wanapiga simu mara kwa mara kuwakumbushia CRDB case zao. Na mara nyingi watu unaoongea nao CRDB hata hawaelewi unazungumzia nini.

Makubaliano yako na CRDB ni soo
Ili kuiruhusu kadi yako kutumika online, itabidi utie saini makubaliano yako na CRDB, ambayo yanavipengele ambavyo vinaiondolea CRDB jukumu lolote la kukuhakikishia usalama wako unpotumia kadi yako kwenye mtandao. Kwa hiyo ukiwa online na kadi yako, jua you are on your own.

Kwa watumiaji wengine duniani kuna taratibu za jinsi ya mtu kupinga kuchajiwa transaction ambazo hujazifanya wewe. Na kuna taratibu za jinsi gani utarudishiwa pesa zako.

Mpkataba wa CRDB hauoneshi kama kuna kitu kama hicho. Kwa hiyo mtu akipata details za kadi yako, siku zote itakuwa inakula upande wako.

Kwa hiyo baada ya kuutia saini tu nimehakikisha kadi yangu haiondoki machoni pangu, na pia nahakikisha akaunti hiyo ya CRDB haina vijisenti vingi ... mpaka ntakapomaliza hii exercise.

Hitimisho
Sasa hivi unaweza kutumia kadi yako ya CRDB kwenye mtandao, lakini you do it at your own risk, tena risk kubwa tu.

Kinachonitisha ni kwamba kama kadi yako imewezeshwa kutumika kwenye internet, mtu hana haja ya kukuibia kadi nzima kwa sababu utashtuka, utaripoti, na kadi itafungwa. Anachotakiwa kufanya ni kupata namba za kadi zilizopo mbele, na vile vijinamba vitatu vilivyopo nyuma ya kadi, na inakula upande wako kimya kimya.

Kama umeiwezesha kadi yako kutumika kwenye mtandao, na kama vijinsenti vyako kwenye akaunti yako sio vidogo, na kama huwezi kuitunza details za kadi kiasi hicho, ni vyema ungewaambia waizibe isitumike kwenye mtandao ... or u may have to learn the hard way.
__________________
There are only 10 types of people in the world. Those that understand binary, and those that don't.

Manitoba
Senior Member
Points: 108,272, Level: 100 Points: 108,272, Level: 100 Points: 108,272, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
Join Date: Tue Jul 2008
Posts: 244
Thanks: 17
Thanked 10 Times in 7 Posts
Views: 4886
Reply With Quote
  #41  
Old 14th February 2009, 10:46 PM
Obhusegwe's Avatar
Obhusegwe Obhusegwe is offline
Obhusegwe is a Milo Rambaldi follower
Senior Member
Points: 96,417, Level: 100 Points: 96,417, Level: 100 Points: 96,417, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Sun Dec 2008
Posts: 161
Thanks: 43
Thanked 12 Times in 9 Posts
Rep Power: 22
Obhusegwe will become famous soon enoughObhusegwe will become famous soon enoughObhusegwe will become famous soon enoughObhusegwe will become famous soon enoughObhusegwe will become famous soon enoughObhusegwe will become famous soon enoughObhusegwe will become famous soon enoughObhusegwe will become famous soon enough
Default Re: CRDB Visa Card: Usithubutu kuitumia kwenye Mtandao

Quote:
View Post
Kaka hapo kama bado unahamu ya kutumia hiyo kadi ya CRDB inabidi uwe mvumilivu kwel kweli. Uwezokano mkubwa hapo tatizo lipo CRDB. My guess itakuwa kwamba hiyo kadi haijawa activated kwa ajili ya internate. Unauhakika kwamba iko activated? Na ulijaza kale kamkataba?

Nenda CRDB, hasa pale Azikiwe, waelezee Tatizo. Ukiona hamuelewani, waambie wakuunganishe na jamaa wa Card Center. Ukiongea na jamaa wa card center wasisitizie hiyo message, maana saa nyingine hata wao wanakuwa hawaelewi. Jibu watakalokupa, lipost hapa tafadhali.

Hatimaye mimi nimefanikiwa baada ya miezi kadhaa ya kupiga kwata na kupiga simu CRDB. Na tatizo lilikuwa kwamba system zao zilijikoroga, transaction ile ya paypal yenye verification code haikufanyika automatically, ikabidi ifanywe manually. Na mtu aliyefanya manually hakuona kwamba zile zina umuhimu wowote, akaziachilia mbali. Kwa hiyo hata kama ningekuwa natumia online account, nisingeweza kuona chochote.

Chakushangaza ni kwamba mtu wa mwisho niliyeongea naye aliyenitatulia tatizo haikumchukua hata masaa mawili kutrace hizo information kwenye intermediate servers. Sasa sijui siku zote nilikuwa naongea na vilaza ama nilikuwa nawakuta kwenye bad-mood, au nilitakiwa niwahonge ... sijui. Inawezekana mimi ndio mwenye mkosi ...
Aaaaghhhh!! Nilishajikatia tamaa zamaaaani!
Reply With Quote
  #42  
Old 15th February 2009, 12:11 AM
Chibidu's Avatar
Chibidu Chibidu is offline
Chibidu has no status.
Senior Member
Points: 68,863, Level: 100 Points: 68,863, Level: 100 Points: 68,863, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Fri Dec 2008
Posts: 81
Thanks: 1
Thanked 0 Times in 0 Posts
Rep Power: 22
Chibidu will become famous soon enoughChibidu will become famous soon enoughChibidu will become famous soon enoughChibidu will become famous soon enoughChibidu will become famous soon enoughChibidu will become famous soon enoughChibidu will become famous soon enoughChibidu will become famous soon enough
Default Re: CRDB Visa Card: Usithubutu kuitumia kwenye Mtandao

Quote:
View Post
Mimi nimetumia huduma hii kwa miezi sita na mpaka sasa sijapata matatizo na ukweli inarahisisha sana transactions zako. Zaidi ya kununua, unaweza pia ku-transfer pesa kwenda kwa mtu mwingine.
Cha muhimu angalau ukumbuke kila siku kuingia mtandaoni na kuangalia salio lako.
Mwanzo mgumu ila am confident "we" are progressing.
Sasa mkuu wangu kuangalia salio lako kila siku itakusaidia nini kama mtu alishaweka disclaimer kuwa ukiibiwa huko mtandaooni utajiju? Je ukishagundua kuwa kuna transaction huitambui inakuaje? Wewe shukuru Mungu kuwa mpaka sasa bado hujagongwa na huyo nyoka. Najua benki zote duniani huwa zinamtaka mteja awe mwangalifu na hela yake. Lakini linapoingilia suala la tekinolojia hapo mteja wakati mwingine anakuwa hana ujanja zaidi ya kupata ushirikiano toka kwa banker.Mimi hao CRDB kwanza nilishasumbuana nao mpaka nikaamua kufunga akanunti yangu na za watoto wangu wote. Kibaya zaidi walikuwa wananiboa kwenye customer care (hawajali kabisa). Najua kuna baadhi ya matawi wanajitahidi, lakini matawi mengine wanajiona kama miungu fulani hivi. Just imagine hata suala la bank statement mtu anakudengulia ku print wakati ni haki yako.Utadhani tuko enzi zile za benki moja tu NBC. Kwakweli hiyo benk inabidi watu wabadirike.
Reply With Quote
  #43  
Old 15th February 2009, 07:15 AM
Mdadisi Mdadisi is offline
Mdadisi has no status.
Member
Points: 82,364, Level: 100 Points: 82,364, Level: 100 Points: 82,364, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Wed Aug 2007
Posts: 32
Thanks: 0
Thanked 0 Times in 0 Posts
Rep Power: 0
Mdadisi will become famous soon enoughMdadisi will become famous soon enoughMdadisi will become famous soon enoughMdadisi will become famous soon enoughMdadisi will become famous soon enoughMdadisi will become famous soon enoughMdadisi will become famous soon enoughMdadisi will become famous soon enough
Default Re: CRDB Visa Card: Usithubutu kuitumia kwenye Mtandao

pole sana. hatua katika perfection ya system zetu itachukua muda. tuvute subira wakati tukiendelea na mapambano
Reply With Quote
  #44  
Old 15th February 2009, 10:01 AM
Kasharu Kasharu is offline
Kasharu has no status.
Junior Member
Points: 61,337, Level: 100 Points: 61,337, Level: 100 Points: 61,337, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Fri Feb 2009
Posts: 4
Thanks: 0
Thanked 0 Times in 0 Posts
Rep Power: 0
Kasharu will become famous soon enoughKasharu will become famous soon enoughKasharu will become famous soon enoughKasharu will become famous soon enoughKasharu will become famous soon enoughKasharu will become famous soon enoughKasharu will become famous soon enoughKasharu will become famous soon enough
Default Re: CRDB Visa Card: Usithubutu kuitumia kwenye Mtandao

Tunashukuru kwa kutufungua macho sisi tulioachwa na technologia
Reply With Quote
  #45  
Old 15th February 2009, 10:58 AM
Manitoba Manitoba is offline
Manitoba has no status.
Senior Member
Points: 108,272, Level: 100 Points: 108,272, Level: 100 Points: 108,272, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Tue Jul 2008
Posts: 244
Thanks: 17
Thanked 10 Times in 7 Posts
Rep Power: 22
Manitoba will become famous soon enoughManitoba will become famous soon enoughManitoba will become famous soon enoughManitoba will become famous soon enoughManitoba will become famous soon enoughManitoba will become famous soon enoughManitoba will become famous soon enoughManitoba will become famous soon enough
Default Re: CRDB Visa Card: Usithubutu kuitumia kwenye Mtandao

Quote:
View Post
What if nikikariri zile namba 3 za nyuma kisha nikazifuta kutoka kwenye kadi yangu, inaweza kunilinda kidogo?
Wewe jamaa ni bonge la jiniasi ...

Kama unaona kuitunza kadi isiingie kwenye mikono ambayo si sawa ni ngumu, basi wazo lako ni bomba sana kama inawezekana ku kwangua pale bila kuiharibu sana kadi.

Kumbuka mikono ambayo si sawa inaweza kuwa ni kipenzi chako chenye tamaa, mtoto wako mtukutu, au ndugu yako aliyeshindikana ... Sio lazima awe mwizi, maana at least kama imeibiwa utagundua imeibiwa na utatoa taarifa. Soo ni pale mtu anachukua namba anakuachia kadi kama ilivyo.
__________________
There are only 10 types of people in the world. Those that understand binary, and those that don't.
Reply With Quote
  #46  
Old 15th February 2009, 01:44 PM
The Invincible The Invincible is offline
The Invincible is not compromising with mafisadi
JF Premium Member
Points: 154,228, Level: 100 Points: 154,228, Level: 100 Points: 154,228, Level: 100
Activity: 3% Activity: 3% Activity: 3%
 
Join Date: Sat May 2006
Location: Online
Posts: 1,054
Thanks: 0
Thanked 79 Times in 47 Posts
Rep Power: 26
The Invincible will become famous soon enoughThe Invincible will become famous soon enoughThe Invincible will become famous soon enoughThe Invincible will become famous soon enoughThe Invincible will become famous soon enoughThe Invincible will become famous soon enoughThe Invincible will become famous soon enoughThe Invincible will become famous soon enough
Default Re: CRDB Visa Card: Usithubutu kuitumia kwenye Mtandao

Asante Manitoba kwa kuleta hili. Binafsi sijawahi kuiona CRDB kuwa benki bora. Kuna wengi wanaipigia debe kunishawishi nijiunge. Moyo unasita.

Ila karibuni hapa nilipata wazo la kuwa mteja wao, baada ya kuona mambo ya visa card ambayo unaweza kuitumia mtandaoni. I am out!
__________________
Watanzania vilaza watamchagua Kikwete aendeleze ubabaishaji ikulu kwa awamu nyingine - Tafakari
Reply With Quote
  #47  
Old 15th February 2009, 03:16 PM
Manitoba Manitoba is offline
Manitoba has no status.
Senior Member
Points: 108,272, Level: 100 Points: 108,272, Level: 100 Points: 108,272, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Tue Jul 2008
Posts: 244
Thanks: 17
Thanked 10 Times in 7 Posts
Rep Power: 22
Manitoba will become famous soon enoughManitoba will become famous soon enoughManitoba will become famous soon enoughManitoba will become famous soon enoughManitoba will become famous soon enoughManitoba will become famous soon enoughManitoba will become famous soon enoughManitoba will become famous soon enough
Default Re: CRDB Visa Card: Usithubutu kuitumia kwenye Mtandao

Mimi mwenye kusema kweli nilikuwa nimeshaitosa CRDB long time, nikaacha akaunti sijafunga just incase ikitokea ninaiitaji.

Kilichonikera wakati ule ni pale kadi yangu inaexpire kila mwaka halafu wananikata 8,000 kwa ku-renew bila hata kuniambia. Ukienda kuwauliza hii hela ya nini hapa ndio wanakwambia.

Sasa mwaka jana niliposikia hiyo Visa Card nikaona pengine muda umefika wa ku-renew hiyo kadi. Sasa baada ya hapo ndio chamoto nkakiona. tehetehe Ikafika mahali nikadhani mimi ndio nina mkosi mwanawane ... Saa nyingine nafika kaunter naanza kucheka kwanza nikiimagine yatakayonikuta dakika kadhaa zinazofuata.

Unajua jana nimekaa nikawa nacheka mwenyewe, nikakumbuka kipindi hicho hicho nasumbuana na CRDB, nikawa na kimeo cha TTCL. Yaani toka mwaka jana mwezi kama wanane nilipojaza fomu ya kwanza wiki iliyopita ndio line inafanya kazi. Mara fomu imepotea jaza nyingine (baadaye wakagundua ilikuwa missplaced), mara haiwezekani maana line zenu hazijafika huko, mara anakuja engineer kufanya survey, halafu husikii jibu ukienda kuwauliza wala hawajui kama kuna engineer amefika kwako, ... yaani ilimradi tu. Kuna mshkaji wangu akaniambia wape kitu kidogo tu utashangaa jinsi line itakavyofungwa faster, maana yeye yalimkuta kama hayo akarekebisha hivyo, bahati mbaya hata sijui jinsi ya kuanza. Huwa naonaga kumhonga mtu ni kama kumtukana, na sipendi kutukana watu

Pengine matatizo kama haya ni ya watendaji, lakini kampuni inabidi ilaumiwe kwa kushindwa kuweka jinsi ya kuhakikisha watendaji wanatenda inavyotakiwa, na watambua pale inapokuwa visivyo. Wengeweka jinsi ya wateja ku-complain kwa mfano wanapokuwa wanapewa huduma mbaya ...

Kwa mfano kwenye ile issue ya kupata verification code ya paypal. Nilienda pale mlimani CRDB nikamwambia yule dada wa reception kwamba nahitaji details za transaction moja ya mwezi wa kumi. Harakaharaka akaniambia inabidi uombe statement. Nikamwambia ni transaction moja tu, akasisitiza tena statement huku akienda kwa mteja anayefuata. Kichwani ilikuwa wazi huyu dada either amechoka, ama kuna kitu wameboana huko, yaani psychologically hakuwa ametualia. Nikamuonea huruma tu.

Akabidi niwe mpole, niombe statement. Ilikuwa jtano akaniambia nije ijumaa maana inabidi ziwe-printed kwenye tawi langu (AZIKIWE ). Nikaongeza siku moja, just in case, nikaenda jmosi. Akaniambia bado hazijaja. Nikawasha moto kidogo na kuwakumbusha nimelipia 5,000TZS hiyo kazi ya kutoa statement, na sio bure, halafu nikamwabia dada mwenzake pale kwamba ninachotaka ni details za transaction moja tu. Unajua akasemaje "Sasa si ungesema?". Na kweli akanichekia, ingawa tukakuta hakuna details za paypal na kulikuwa na tatizo lingine, lakini kumbe inawezekana kuchekiwa transaction moja bila kuomba statement yote na kusubiri siku kadhaa. Sasa nimepoteza siku nyingine kusafiri mpaka pale, halafu nimepoteza siku kadhaa kusubiri jibu la kitu kidogo tu kwa sababu kuna muungwana mmoja amechoka, au yuko in bad-mood, au yuko kwenye siku zake.

Au labda wanaona raha watu mkiwa mnakujakuja pale mnaunga msururu mpaka nje waonekane wako busy sana.
__________________
There are only 10 types of people in the world. Those that understand binary, and those that don't.
Reply With Quote
  #48  
Old 16th February 2009, 06:30 AM
Ogah Ogah is offline
Ogah is Omnipotent
JF Premium Member
Points: 5,280,536, Level: 100 Points: 5,280,536, Level: 100 Points: 5,280,536, Level: 100
Activity: 12% Activity: 12% Activity: 12%
 
Join Date: Fri Mar 2006
Posts: 3,409
Thanks: 1,374
Thanked 381 Times in 210 Posts
Rep Power: 2031
Ogah is one of most respected JF members!Ogah is one of most respected JF members!Ogah is one of most respected JF members!Ogah is one of most respected JF members!Ogah is one of most respected JF members!Ogah is one of most respected JF members!Ogah is one of most respected JF members!Ogah is one of most respected JF members!Ogah is one of most respected JF members!Ogah is one of most respected JF members!Ogah is one of most respected JF members!
Default Re: CRDB Visa Card: Usithubutu kuitumia kwenye Mtandao

nilishawishika sana kujiunga na CRDB baada ya kuambiwa mambo ya tanzanite account............dah nilipotaka kufungua hiyo account ilkuwa kasheshe mpaka basi......si unajua jamaa mpaka sijui wakuone umevaa kimamtoni mtoni ndio wanajua unatoka nje........pamoja na kuonyesha docs zangu bado nilisumbuka mpaka nikakata tamaa kabisaaa...........sitaki hata kuisikia tena.........very very poor customer service
Reply With Quote
  #49  
Old 16th February 2009, 08:36 AM
scorpiomama scorpiomama is offline
scorpiomama has no status.
Junior Member
Points: 62,476, Level: 100 Points: 62,476, Level: 100 Points: 62,476, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Tue Nov 2008
Posts: 2
Thanks: 0
Thanked 0 Times in 0 Posts
Rep Power: 0
scorpiomama will become famous soon enoughscorpiomama will become famous soon enoughscorpiomama will become famous soon enoughscorpiomama will become famous soon enoughscorpiomama will become famous soon enoughscorpiomama will become famous soon enoughscorpiomama will become famous soon enoughscorpiomama will become famous soon enough
Default Re: CRDB Visa Card: Usithubutu kuitumia kwenye Mtandao

Thanks
Reply With Quote
  #50  
Old 16th February 2009, 10:46 AM
Shapu's Avatar
Shapu Shapu is offline
Shapu a Citizen of the World
JF Senior Expert Member
Points: 151,031, Level: 100 Points: 151,031, Level: 100 Points: 151,031, Level: 100
Activity: 5% Activity: 5% Activity: 5%
 
Join Date: Thu Jan 2008
Location: Citizen of the World
Posts: 764
Thanks: 209
Thanked 67 Times in 49 Posts
Rep Power: 24
Shapu will become famous soon enoughShapu will become famous soon enoughShapu will become famous soon enoughShapu will become famous soon enoughShapu will become famous soon enoughShapu will become famous soon enoughShapu will become famous soon enoughShapu will become famous soon enough
Default Re: CRDB Visa Card: Usithubutu kuitumia kwenye Mtandao

Hawa jamaa wa CRDB pia nao wananikera sana kwenye hizi ATMS zao. Utatoa hela then hazitoki ukiangalia salio wameshakula. Ukiwasiliana nao wanakuambi usihofu zitarudishwa. Now inachukua mpaka a month kurudishwa hizo hela. Ukilalamika wanakuangalia kama vile we sijui vipi. Sasa kweli if you deduct my money from my account and you return it one month later hawajui kwa mtu kama mimi kipato changu ameharibu every thing on my budget. sasa sijui kwa nini hawan systeme ya kuhakikisha hiyo hela inarudi instantly????
__________________
"If silence is golden,speech is platinum.It dispels ignorance,ventilates grievances,stimulates curiosity and lessens the fundamental loneliness of the soul."
Reply With Quote
Reply

Bookmarks

Tags
card, crdb, kuitumia, kwenye, matumizi, mtandao, mtandaoni, usithubutu, utata, visa, yake


Currently Active Users Viewing This Thread: 1 (0 members and 1 guests)
 
Thread Tools
Display Modes Rate This Thread
Rate This Thread:

Posting Rules
You may not post new threads
You may not post replies
You may not post attachments
You may not edit your posts

BB code is On
Smilies are On
[IMG] code is On
HTML code is Off
Trackbacks are Off
Pingbacks are Off
Refbacks are On


Similar Threads
Thread Thread Starter Forum Replies Last Post
BoT Scandal: Tulikotoka, Tulipo, Tunakoelekea Maxence Melo Jamii Intelligence 3079 12th November 2009 08:12 AM
Muafaka CCM na CUF, pande mbili za shilingi! MwanaCCM Jukwaa la Siasa 148 13th July 2009 10:13 AM
Hotuba Mbadala TAMISEMI: Slaa ataka Balali ajiuzulu; ambana Lowassa kuhusu Richmond John Mnyika Jukwaa la Siasa 13 16th December 2008 02:21 PM

Tuma Ukurasa huu kwa rafiki yako!


All times are GMT +3. The time now is 10:33 PM.

Powered by JamiiForums.com
Copyrights reserved to JamiiForums.com