LATEST ENTRIES

Wanawake watakiwa kujitokeza kutibiwa ugonjwa wa fistula

February 27th, 2013 | by Gordon Kalulunga

WITO umetolewa kwa wanawake wanaosumbuliwa na tatizo la kutokwa na haja ndogo mfululizo na haja kubwa katika sehemu zao za siri kujitokeza kupata matibabu yanayotolewa bure katika hospitali teule ya wilaya ya Mbeya Mbalizi-Ifisi iliyopo wilaya ya Mbeya Vijijini.

Sababu 5 hatari kwa watoto chini ya miaka mitano zinazosababisha vifo hizi hapa

February 27th, 2013 | by Gordon Kalulunga

1. Upungufu mkubwa wa damu.
2. Upungufu wa maji mwilini.
3. Dege dege.
4. Homa kali (Maralia).

Mhudumu wa Bar anyofolewa kizazi na Daktari…!

February 26th, 2013 | by Gordon Kalulunga

JESHI la polisi wilayani Bunda linamshikilia afisa tabibu Michael Msimu 43 kwa tuhuma za kudaiwa kumtoa mimba mhudumu wa Club ya pombe za kisasa (bar) ijuliknayo kwa jina la Savana iliyopo mtaa wa benki katikati ya mji mdogo wa Bunda mkoani Mara.

Mahabusu yenye umri wa miaka 68

February 26th, 2013 | by Kulwa Magwa

UNAPOFIKA kwenye ofisi ya kijiji cha Mwadui-Lohumbo, kilichopo mashariki mwa mji mdogo wa Maganzo, wilayani Kishapu, mkoani Shinyanga, utakutana na  majengo yenye yaliyojengwa enzi za ukoloni wa Waingereza.

Safari yangu kuelekea kijiji cha Nyaminywiri

February 26th, 2013 | by Stella Mwaikusa

Safari yangu kuelekea Mkoa wa Pwani Wilaya ya Rufiji kata ya Kipugira katika kijiji cha Nyaminywiri, nikitokea Dar es salaam naweza kuiita ni safari ya tofauti si utofauti wa eneo ila ni namna nilivyoweza kusafiri.

Uchimbaji wa Dhahabu kwenye Hifadhi unavyoharibu Mazingira

February 26th, 2013 | by David Azaria

SHUGHULI za uchimbaji wa madini katika hifadhi ya Taifa ya Moyowosi wilayani Biharamulo Mkoani Kagera,zinadaiwa kusababisha uharibifu mkubwa wa mazingira unaotokana na ukataji wa miti katika hifadhi hiyo.

Daraja linalowawasumbua wakazi wa kata ya Subira (Songea) kwa miaka 30

February 26th, 2013 | by Mariam Mkumbaru

Wakazi wa kata ya Subira katika Manispaa ya Songea  Mkoani Ruvuma,  wako katika hatari ya kusombwa na maji wakati wa kuvuka katika daraJa la kisiwani kitongoji cha Lihwena.

Rufiji: Wajawazito wakosa huduma ya Choo

February 26th, 2013 | by Stella Mwaikusa

Zahanati za Ndundunyikanza na Mtanza  zinazopatikana katika kata ya Kipugira wilayani Rufiji hazina huduma za vyoo.

Hali  hiyo  inawalazimu  wajawazito  wanaofika  kwenye zahanati  hizo kwa ajili ya kupima na wengine kuja kujifungua, kwenda nyumba za...

Choo cha muuguzi na vichaka vya nyasi

February 26th, 2013 | by Kulwa Magwa

Unaweza usiamini kuwa unaingia kwenye choo kinachotumiwa na mtu anayejua nini maana ya neno ‘afya bora’. Hata hivyo, katika hali halisi, choo kinachotumiwa na muuguzi, Ester Malangwa, hakifai kutumiwa na binadamu kutokana na kuzingirwa na nyasi. Choo hicho kiko katika nyumba ya serikali...

Serikali yatakiwa kutimiza wajibu wake wajawazito wapate huduma bure

February 24th, 2013 | by Frank Leonard

UONGOZI wa Hospitali Teule ya Ilembula, wilayani Wanging’ombe mkoani Njombe umeiomba serikali kutekeleza vifungu vyote vya makubaliano ya uendeshaji wa pamoja wa hospitali hiyo ili huduma kwa makundi maalumu wakiwemo wajawazito na watoto chini ya miaka mitano zitolewe...

Hizi ndizo pilikapilika za Mto Rufiji

February 23rd, 2013 | by Stella Mwaikusa

Unapozungumzia shilingi 100 katika jiji la Dar es salaam thamani yake ni ndogo sana kutokana na hali halisi ya kupanda kwa gharama za maisha, kwani ukiwa na kiasi hicho cha pesa huwezi hata kupanda daladala kutoka kituo kimoja mpaka kingine.