Re: Kikwete amkubalia Mwanyika kung'oka
Sioni ubaya wowote kustaafu. Kwanza keshatimiza miaka 60 ambao ni umri wa lazima wa mtumishi wa serikali kustaafu. Ingawa inaweza kuonekana ni kulea maovu lakini watumishi wa serikali wafanyapo makosa (ingawa makosa mengine hayatangazwi) na kuwajibika kuadhibiwa, na hasa suala la kufukuzwa kazi, mara nyingi umri wao huangaliwa kabla ya adhabu kutolewa. Hii haiko kisheria lakini ni suala la ubinadamu tu. Hata mahakamani inatokea adhabu kupunguzwa kwa sababu ya umri.
Wakati mwingine lazima Serikali ionekane imara kuwa haishurutishwi na chombo chochote. Bunge litakapokaa mwezi November itatolewa taarifa kuwa Mwanasheria Mkuu kastaafu kwa lazima. Azimio la bunge litakuwa limetekelezwa.
Wakianza kufukuzana kwa kila kosa linalotokea habaki mtu serikalini. Kastaafu mwacheni aende. Mengine baadae.
Halafu kama ni suala la kuwajibishana kuhusu Richmond wa kuondoka ni wengi.
|