JamiiForums |The Home of Great Thinkers - View Single Post - Naomba maana ya maneno haya...
View Single Post
  #278  
Old 22nd November 2008, 08:46 AM
Mzee Mwanakijiji's Avatar
Mzee Mwanakijiji Mzee Mwanakijiji is online now
Mzee Mwanakijiji anawashangaa wanaoitetea sheria mbovu
JF Premium Member
Points: 12,991,661, Level: 100 Points: 12,991,661, Level: 100 Points: 12,991,661, Level: 100
Activity: 95% Activity: 95% Activity: 95%
 
Join Date: Fri Mar 2006
Location: Kijijini
Posts: 18,485
Thanks: 8,529
Thanked 4,697 Times in 1,324 Posts
Rep Power: 44
Mzee Mwanakijiji is on a distinguished roadMzee Mwanakijiji is on a distinguished road
Send a message via MSN to Mzee Mwanakijiji Send a message via Skype™ to Mzee Mwanakijiji
Default Re: Maana ya neno "Venture"

mhanga - inatumiwa vibaya sana. Mhanga kimsingi ni "victim" yaani mtu aliyekutwa na jambo baya SIYO mtu alinayefanya jambo ambalo ambalo laweza kuwa baya au zuri.

hivyo: tuna "Mhanga wa mafuriko ya Tsunami" - Victim of the Tsunami"

Walioharibu matumizi ya neno hilo naamini ni BBC ambao walianza kutafsiri neno "waliojitoa mhanga" wakifikiri wanamaanisha aliyejitolea kuua!

Kujitoa mhanga ni kuwa kujitolea ili wawe yakukute yale mabaya ambayo yalikuwa yawakute watu wengine; you become a victim. Kwa wale waliowahi kuiona filamu ya "War Bus" watakumbuka askari mmoja mlevi mlevi aliwaokoa wenzake liliporushwa bomu la mkono kwa yeye kujirusha juu ya bomu hilo na hivyo likamlipua yeye na kumuua na kuwanusuru wale wengine (waliokuwa wanahangaika kwenye basi kuondoka eneo hilo). HIvyo yule askari "alijitoa mhanga" kuwaokoa wengine, he became a victim.

Hivyo basi, "mhanga" ni mtu ambaye anakutwa na jambo ambalo ni baya (huwezi kuwa mhanga wa jambo zuri) aidha alilolitarajia (kwa kuweka maslahi yake nyuma) au pasipo kulitarajia (kwa bahati mbaya).



Naamini mhanga anaweza akawa aliyenusurika (siyo lazima afe) na pia anaweza kufa katika kujitahidi kuokoa au kufanya jambo ambalo linanusuru, kuokoa maisha ya watu wengine.
__________________
Nchi hii imewahi kung' oa masultani wa kila aina. Tukianza kuvumilia masultani wakuchaguliwa tutapanda mbegu ya masultani wa kuzaliwa. - Nyerere katika "Uongozi wetu na Hatima ya Tanzania"
Reply With Quote