Re: Stars yalipa kisasi kwa Msumbiji
Kwa sababu hawa Nyoka weusi walitukandamiza kwenye mechi ya kimashindano na kutuharibia safari (kama ilikuwepo) yetu ya kwenda Bondeni 2010 (na Angola), basi hatuwezi kusema tumelipiza kwa kuwafunga kwenye mechi ya kirafiki.
Tusubiri tukutane nao kwenye mechi ya kimashindano.
BTW: Viva Stars kwa ushindi, yaweza kutusaidia kupanda kidogo (labda hadi kwenye top 100) kwenye chati ya FIFA.
|