Re: Ukistaajabu ya Mussa...
Huyo Mama amenishangaza sana jana kwenye TV, nadhani ameingilia majukumu ya Wizara ya Jinsia na Maendeleo ya Jamii (Maendeleo ya Jamii). Sasa kama anataka Wanahabari wageuze CD kwenda kwenye masuala ya unyanyasaji, hiyo CD ikielekezwa huko Waziri Sitta naye akisema geuzeni CD andikeni kuhusu Migomo ya Walimu itakuwaje?
Kwa kifupi ajue kuwa WaTanzania kwa sasa priority ni EPA, Elimu (Migomo ya Walimu na Wanafunzi) na baada ya hapo tutataka kujua kuhusu Meremeta, Tangold, Deep Green Finance na ubadhirifu mwingine. Ajue kuwa jukumu la kuandika habari ni la Wanahabari wenyewe na jukmu la habari ipi ipewe kipau mbele ni la Wahariri na Waziri.
__________________
"Then you will know the truth, and the truth will set you free; I am the way, the truth and the life." Jn 8:32; 14:6
|