Re: Kitu gani kinamfikisha mtu kwenye ufanisi katka maisha
Wazee naomba nichangie kidodo hapa.
Mimi nafikiria mafanikio ya mtu kwanza kabisa yanapimwa na namna anavyoweza kukidhi mahitaji ya msingi kikamilifu. utakuwa umefanikiwa endapo mkono unaenda kinywani bila wasiwasi, watoto wanaenda shule bila mikwaruzo, ukiugua na familia yako uhakika wa matibabu ya maana upo, malazi safi na salama, usafiri na mavazi na mengine anayotakiwa kuwa nayo binadamu. zaidi ya hayo, mahusiano yako na jamii inayokuzunguka kama vile kushriki katika shida na raha bila kunata ni muhimu. na mwisho kwa maoni yangu, utakuwa umefanikiwa endapo utaweza kutumia uwezo wako ulionao kusaidia jamii yako kielimu, kiutamaduni, kifikra nk. lakini kujilimbikizia mali na kujiona mungu mtu katika jamii si mafanikio.
|